Edward Lowassa Richmond kuibuliwa 2008 kama si mapenzi ya Mungu Israel na aseme

Baada ya aibu ya mwaka kumshukia waziri mkuu mstaafu bwana sumaye sasa kiwembe kinanolewa kumnyoa Lowassa kwenye uchaguzi wa kugombea ujumbe wa NEC kuwakilisha wilaya ya monduli.
Mpaka sasa Dr Salash Mokosyo anakubalika na wana monduli wengi na kama Takukuru watafanikiwa kuziba mianya ya rushwa basi uchaguzi huu utakuwa ndio mwisho wa siasa za lowassa nchi hii.
Nakutakia Heri Dr na nina amini mizengwe yote unayopigwa na mafisadi itashindwa na wewe kuibuka kidedea.
Wana Monduli twakutegemea
Nb
Nipo monduli na nitawajulisha yote yanatakayotokea huku.
 
Mimi naona FISADI mzuri ni yule ambaye ameiba na amewekeza hapa TZ kama EL kuliko yule wale ambao wameshatuibia na hatujui wamezificha wapi!

Hilo nalo neno iba nje leta ndani lakini hawa mafisadi wetu wanaiba ndani
 
Hapa kwa kweli aliniacha hoi.
PROB ya huyu mtu hakuwahi kukanusha tuhuma zilizokuwa zikimkabiri akaamua kukubali kwa kujiuzuru!
Kwa hilo hafai kwa TZ.


Habari zisizo thibitika zinasema JK alimwambia amuache yeye aendelee ili walindane maana anguko Hilo lilimhusu sana JK na ingekuwa balaa Kama JK angeanguka kwani serikali nzima ya JK ingeanguka na kuishia segerea ikabili lowasa akubali ili kulinda maslahi ya jk na ccm ndio maana mpaka Leo kawa bubu.
 
Najua Uko kwenye pay slip yake ila ndugu utafua kaniki mpaka itoboke ukidhani una gharisha. Kama Richmond ni JK mbona lowasa hasemi? ****
Wewe huielewi nchi hii unaongea tu bila fact zozote.
Je unaushahidi wa Richmond? Au unapayuka tu? Kwanini sasa usimshitaki? kwanini wengine wanashitakiwa?
Lowassa hana doa ni wewe tu Kipofu.
 
usihusishe Mungu na ujinga wa lowasa! hata wewe fikiria wazo lako upya! nchi hii haiwezi kuliwa na panya kiasi hiki. kama umepewa sabuni ya roho na lowasa, imekula kwake mazima! afadhali tumpe mtikila ambaye kila kesi anayoshtakiwa na serikali anashinda!
 
Tutajuta hafai ni mwizi mkubwa tena ni mroho kupindukia kumbuka kauli ya Nyerere alivyomumbua hakika, vibaraka vyake na wakome kutuandikia madudu ya huyu fisadi komeni kabisa, hafai kwa lolote.
E.lowassa ni GOOD FOR NOTHING VERY CORRUPTIVE OLD MAN.

Hivi kabla hujaandika haya maneno kwa wanaJF umejitizama kweli???,mbona inaonekana wewe na EL hamtofautiani lakini kwa nini unamshambulia sana?? Sikiliza nenda kajitizame kwenye kioo kwanza kisha ndo urejee hapa JF na maneno yako hayo machafu.

EL ni Rais 2015

Inawezekana kwa sababu ni mtu ambaye anawajibika,lakini pia ni Mjeshi na nchi hii ukizingatia hapa ilipofika sasa inahitaji mjeshi walau kuirejesha kwenye mstari kidogo.

Mkuu Labda Rais wa TFF au Laigwan wenzake huko masaini

Unakula MSUBA wewe!!!!!!!!!!!!!!!

Najua Uko kwenye pay slip yake ila ndugu utafua kaniki mpaka itoboke ukidhani una gharisha. Kama Richmond ni JK mbona lowasa hasemi? ****

Kaka mbona unajihami sana kuna nini au umetumwa?kwa nini usistulie upate comment kutoka kwa JF,naona kila comment unataka uijibu,au umetumwa na wabaya wa EL???!
 

Wezi wana roho ngumu sana ndugu yangu........kama ulikuwa hujui

 
Kumbe ndio maana TBC bado wanatulazimisha tuendelee kutumia akili za Nyerereeee!

Hayo ni mawazo yako Bwana,sio ya wote na hasa mimi,CCM,CDM,CUF,NCCR-MAGEUZI,Vyote havina lolote,kwani lazima rais atokane na chama,mi namsubiri mgombea binafsi.
 
Kichwa cha habari na yaliyoandikwa tofauti kwanini?
 

Hakuna sabuni inayoweza kumsafisha Lowa hasa na rich monduli yake
 

Ububu wake unamponza wa TZ hawamwelewi na zaidi wanajua anahusika na ndio maana alikubali kiulaini kuachia ngazi kuliko kwenda mahakanmani kujibu tuhuma.lol!
 
ka hujui nyamaza, huyu ni mwizi tena wa hali ya juu sana!
 
Nafikiri mtu pekee ndani ya ccm mwenye sifa ulizotitaja hapo juu ni John Pombe Magufuli, na sio mtu mwingene yeyote.Kwa ufupi ni kwamba mtu pekee ambae watz wanamkubali na kama anagombea urais hata leo anapita kwa 90% ni John Pombe Magufuli!
 
Kumjadili lowassa kwenye viongozi bora ni kupoteza muda. Poor Tanzanians
 
Wewe huielewi nchi hii unaongea tu bila fact zozote.
Je unaushahidi wa Richmond? Au unapayuka tu? Kwanini sasa usimshitaki? kwanini wengine wanashitakiwa?
Lowassa hana doa ni wewe tu Kipofu.


Asante Kama Mimi ni kipofu Sijui nchi inavokwenda lowasa msafi nk. Ila embu JIULIZE kwanza kwanini lowasa hamtaji Richmond ni nani? Anasema kaonewa Ina maana aliye muonea Yuko juu yake au chini yake? Kama ameweza kuficha maovu kwa maslahi ya wachache ndio mtu unayesema anafaa??? Anakufaa wewe Mkuu na ubarikiwe kwa kujua nchi hii Zaidi ya tuijuavo sisi..kifupi nikukumbushe usimdharau usiye mjua huenda Mimi baba yako Kama sio mzazi basi wa kambo Wacha kauli chafu
 
Mleta mada ameorodhesha takwimu wala hakutuambia zimetoka wapi na kwa vigezo gani!

Hsitoria ndio inamhukumu Lowasa.Sio wanaomchukia.
Mwizi ni yule aliyekamatwa na ngozi siyo aliyeiba Ng'ombe.

Midhali jina la Rostam Aziz li hai, Edward Hosea, Mwakyembe, Selelii, Karamagi, Mbuzi wa kafara Msabaha n.k ni kitu kigumu sana kumsafisha huyu bwana.
Midhali dini zipo ushahidi wa matumizi ya dini utajieleza wenyewe

Tatizo la Lowasa si mavazi au kuoga, ni uchafu wa Roho.
ENL ni mchafu wa roho kiasi kwamba anatoa matumaini kuwa akionekane peponi basi vibaka, majambazi n.k. watakuwa na nafasi kubwa tu katika ufalme wa mbinguni.
 
Ububu wake unamponza wa TZ hawamwelewi na zaidi wanajua anahusika na ndio maana alikubali kiulaini kuachia ngazi kuliko kwenda mahakanmani kujibu tuhuma.lol!

Ni kweli Mkuu angeweza kumtaja Richmond ni nani Na ikadhibitika hausiki ningerudisha Imani ila ningemkanya kutokuwa bubu kwenye maslahi ya taifa... Ila it's too late maana Hata akisema Leo Hatuta muelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…