Elimu: Changamoto za utekelezaji wa kalenda ya mtaala

Elimu: Changamoto za utekelezaji wa kalenda ya mtaala

Kila mwanasiasa anakuja na lake.

Walimu walishaandaa mpango kazi wa MWAKA mzima kabla shule kufunguliwa January, ghafla wanaitwa wanaambiwa Kuna marekebisho, maana yake wakaanze tena kutengeneza scheme of work upya.
unajiuliza wakati wote tangu shule zilipofungwa walishindwa Nini kutoa huo mwongozo.

Nchi ngumu sana hii
 
Kila mwanasiasa anakuja na lake.

Walimu walishaandaa mpango kazi wa MWAKA mzima kabla shule kufunguliwa January, ghafla wanaitwa wanaambiwa Kuna marekebisho, maana yake wakaanze tena kutengeneza scheme of work upya.
unajiuliza wakati wote tangu shule zilipofungwa walishindwa Nini kutoa huo mwongozo.

Nchi ngumu sana hii
Tufanye nin sasa?? Kama tatizo tushaliona
 
Ila huu mpango umeonesha kufeli mapema sana
 
Kazi mnayo... Mnalazimishwa kufanya the imposible kua posible...
 
Katika kumoderate kazi ya ufundishaji na kuweka usawa kwa nchi nzima kalenda iko sahihi,changamoto ni kutokuwa na;

1. Muda wa mazoezi na majaribio

2. Muda wa kufanya marudio na masahihisho

3. Kuchelewa kwa umaliziaji wa mada, mfano, kidato cha NNE,kalenda inakutaka ufundishe hadi wiki moja au mbili kabla ya mtihani wa taifa,..huyu mwanafunzi kitu alichofundishwa wiki moja kabla atakisoma,kukifanyia mazoezi na kukirudia rudia ili kikae kichwani SAA ngapi?

4.Room ya kufidia magap kama mwalimu atapata dharura yoyote,means mwalimu anatakiwa kuwepo shule siku zote bila kujali ataumwa,atafiwa,atapata kazi maalum

Naungana na mdau aliesema ifanyiwe majaribio kidato cha kwanza tu kwa sekondari,vingnevyo walimu na wazazi wasipojiongeza mwaka huu matokeo yatakua mabaya.
 
Katika kumoderate kazi ya ufundishaji na kuweka usawa kwa nchi nzima kalenda iko sahihi,changamoto ni kutokuwa na;

1. Muda wa mazoezi na majaribio

2. Muda wa kufanya marudio na masahihisho

3. Kuchelewa kwa umaliziaji wa mada, mfano, kidato cha NNE,kalenda inakutaka ufundishe hadi wiki moja au mbili kabla ya mtihani wa taifa,..huyu mwanafunzi kitu alichofundishwa wiki moja kabla atakisoma,kukifanyia mazoezi na kukirudia rudia ili kikae kichwani SAA ngapi?

4.Room ya kufidia magap kama mwalimu atapata dharura yoyote,means mwalimu anatakiwa kuwepo shule siku zote bila kujali ataumwa,atafiwa,atapata kazi maalum

Naungana na mdau aliesema ifanyiwe majaribio kidato cha kwanza tu kwa sekondari,vingnevyo walimu na wazazi wasipojiongeza mwaka huu matokeo yatakua mabaya.
Umeongea madini sana mkuu
 
Nina imani wahusika wanausoma huu uzi na watafanyia kazi maoni yetu.
 
Hivi ni nani msimamizi wa elimu nchini Kati ya tamisemi na wizara ya elimu?
Huu mpango umetoka tamisemi na wizara husika ya elimu ipoipo TU kama haihusiki na masuala ya elimu vile!
Nijuavyo mtaaluma mkuu anatoka wizara ya elimu na ndiye mhusika mkuu wa masuala ya taaluma katika shule zote za nchi hii.
Tamisemi watuambie Kama na wao Wana mtaaluma mkuu na anahusika na shule za serikali pia! Kama hawana mtaaluma mkuu mamlaka ya kuwapangia walimu mambo ya kitaaluma wanayapata wapi?
Vingine serikali au mpanga wizara awaambie walimu ni nani hasa anayehusika na masuala ya taaluma na mwalimu anawajibika Kwa nani Kati ya wizara ya elimu na tamisemi?
 
Hivi ni nani msimamizi wa elimu nchini Kati ya tamisemi na wizara ya elimu?
Huu mpango umetoka tamisemi na wizara husika ya elimu ipoipo TU kama haihusiki na masuala ya elimu vile!
Nijuavyo mtaaluma mkuu anatoka wizara ya elimu na ndiye mhusika mkuu wa masuala ya taaluma katika shule zote za nchi hii.
Tamisemi watuambie Kama na wao Wana mtaaluma mkuu na anahusika na shule za serikali pia! Kama hawana mtaaluma mkuu mamlaka ya kuwapangia walimu mambo ya kitaaluma wanayapata wapi?
Vingine serikali au mpanga wizara awaambie walimu ni nani hasa anayehusika na masuala ya taaluma na mwalimu anawajibika Kwa nani Kati ya wizara ya elimu na tamisemi?
Kuna ombwe katikati. Walimu bosi wao ni mkurugenzi (mtamisemi), wizara ya elimu inaishia vuoni. Ni kama vile zahanati na vituo vya afya vipo chini ya halmashauri wakati wizara ya afya ipoipo tu kama ulivyosema. Wanaounda hii mifumo sometimes wawe wanaangalia basi. Kah!
 
Tuwe na Mfumo mpya wa Elimu ili vijana wengi wanapohitimu vyuo wasisubiri kuajiriwa bali wawe na uwezo MKUBWA sana wa kujiajiri,hizi kalenda wanazoleta kwenye Elimu ni aina nyingine ya upuuzi tunaoendelea nao ambao hauna tija yoyote kwa nchi hii.hapo tunawatafulia watu ulaji tu,watu wamekaa wakaandaa hilo li kalenda wamepiga mpunga na wamesepa.Ss tunajadili upuuzi wa wapiga deal.
 
Mpango huu nimeukubali kabisa kabisa, walimu wamefungiwa speed controller! wakuu wa shule walikuwa wanawakoromea walimu..'nataka kufikia mwezi mei mada zote ziwe zimeisha'.. kwa sasa hicho kitu hakipo tena, safi kabisa!
 
Nawasalimu kwa jina la JMT


Kazi iendelee.....

Nikiwa kama mdau wa Elimu nimebaini haya yafuatayo hasa baada ya kupitia maoni ya baadhi ya watu ambao wengi wao ni walimu juu ya utekelezaji wa kalenda mpya ya mtaala inayowataka walimu wote Tanzania kuwa sawa ktk ufundishaji. Kwa maana kama leo jumatatu ya tarehe 7/2/2022 Mwalimu wa Feza Boys akifundisha mada ya simultaneous equation na Mwalimu wa huko Maundo Tandahimba afundishe mada hiyo hiyo, wasitifautiane.

Bila shaka serikali ina nia njema juu ya hili; lakini hata hivyo sisi wadau tunalo la kuchangia huenda tukaisaidia serikali kufanya maboresho.

Changamoto hizo ni kama ifuatavyo;-

(1) Kutofautiana kwa idadi ya vipindi kati ya syllabus na kalenda katika baadhi ya masomo. Maeneo mengi yameonesha kwenye syllabus kuwa na vipindi vingi katika mada husika wakati kwenye kalenda mada hizo hizo zimewekewa vipindi vichache na hali muda wa vipindi ni ule ule

(2) Kalenda imechukua muda wote wa mwaka mzima kwa ajili ya kusoma darasani na siku chache kwa ajili ya upimaji na likizo. Hivyo kumfanya mwalimu akose muda wa kuwa na upimaji wa wiki (weekly test), upimaji wa mwezi (monthly test) na hata muda wa kufanya mtihani wa utimilifu (Mock exams). Kubwa zaidi mwalimu huyu huyu hakuwekewa muda wa kusahisha hiyo mitihani na kufanya marudio kama somo halikufahamika vizuri kwa wanafunzi

(3) Kalenda haikuzingatia uwepo wa shuguli za kitaifa zinazowahusisha walimu na wanafunzi pia kama vile Mwenge, Umiseta na Umitashunta, kazi maalumu nk.

(4) Kwa mujibu wa kalenda mitihani ya robo muhula imetengewa siku tatu tu jambo ambalo ni changamoto kwa shule zenye masomo zaidi ya 10 kumtahini mwanafunzi ndani ya siku tatu tu kwa mtihani wenye vigezo stahili/timilifu. Kwa kawaida shule hutumia siku 7 hadi 12 kwa ajili ya mitihani hiyo ya robo muhula.

(5) Kalenda haikuzingatia dharura mbalimbali zitakazomfanya mwalimu asiingie darasani siku husika kama vile maradhi, matatizo/shuguli za kijamii au za kiserikali nk. Ukizingatia baadhi ya shule (ambazo ni nyingi) zina uhaba wa walimu.

MAPENDEKEZO

Kwa kuwa huu mpango wa kalenda unaonyesha kuwa na mafanikio, na kwa sababu ndio kwa mara ya kwanza unaingizwa kwenye field kufanyiwa kazi ili kuwa na ufanisi mdau mimi ningependekeza, hii kalenda ingeanza na kidato cha kwanza wa mwaka huu wa 2022, ili madarasa mengine waendelee na utaratibu wa kawaida uliozoeleka. Kupitia hao wanafunzi wa kidato cha kwanza tungefanya tathimini mwisho wa mwaka na kubaini kama tuendelee nao au la.!! Na kama utaonekana hauna tija hasara ingekua kidogo. Lakini kwa hali ya sasa ya majaribio alafu tunafanya majaribio hayo na hata kwa madarasa ya mitihani nina hofu kama usipoleta ma
Hii ndio naisikia,Nani ameleta mpango huu,yaan ufundishaji uwe sawa?!ina maana walimu wapo wa kutosha mashule,niufuatilie Kwanza nijue undan wake
 
Iko hivyo..! Kalenda ipo ila haitekelezeki
 
Nawasalimu kwa jina la JMT


Kazi iendelee.....

Nikiwa kama mdau wa Elimu nimebaini haya yafuatayo hasa baada ya kupitia maoni ya baadhi ya watu ambao wengi wao ni walimu juu ya utekelezaji wa kalenda mpya ya mtaala inayowataka walimu wote Tanzania kuwa sawa ktk ufundishaji. Kwa maana kama leo jumatatu ya tarehe 7/2/2022 Mwalimu wa Feza Boys akifundisha mada ya simultaneous equation na Mwalimu wa huko Maundo Tandahimba afundishe mada hiyo hiyo, wasitifautiane.

Bila shaka serikali ina nia njema juu ya hili; lakini hata hivyo sisi wadau tunalo la kuchangia huenda tukaisaidia serikali kufanya maboresho.

Changamoto hizo ni kama ifuatavyo;-

(1) Kutofautiana kwa idadi ya vipindi kati ya syllabus na kalenda katika baadhi ya masomo. Maeneo mengi yameonesha kwenye syllabus kuwa na vipindi vingi katika mada husika wakati kwenye kalenda mada hizo hizo zimewekewa vipindi vichache na hali muda wa vipindi ni ule ule

(2) Kalenda imechukua muda wote wa mwaka mzima kwa ajili ya kusoma darasani na siku chache kwa ajili ya upimaji na likizo. Hivyo kumfanya mwalimu akose muda wa kuwa na upimaji wa wiki (weekly test), upimaji wa mwezi (monthly test) na hata muda wa kufanya mtihani wa utimilifu (Mock exams). Kubwa zaidi mwalimu huyu huyu hakuwekewa muda wa kusahisha hiyo mitihani na kufanya marudio kama somo halikufahamika vizuri kwa wanafunzi

(3) Kalenda haikuzingatia uwepo wa shuguli za kitaifa zinazowahusisha walimu na wanafunzi pia kama vile Mwenge, Umiseta na Umitashunta, kazi maalumu nk.

(4) Kwa mujibu wa kalenda mitihani ya robo muhula imetengewa siku tatu tu jambo ambalo ni changamoto kwa shule zenye masomo zaidi ya 10 kumtahini mwanafunzi ndani ya siku tatu tu kwa mtihani wenye vigezo stahili/timilifu. Kwa kawaida shule hutumia siku 7 hadi 12 kwa ajili ya mitihani hiyo ya robo muhula.

(5) Kalenda haikuzingatia dharura mbalimbali zitakazomfanya mwalimu asiingie darasani siku husika kama vile maradhi, matatizo/shuguli za kijamii au za kiserikali nk. Ukizingatia baadhi ya shule (ambazo ni nyingi) zina uhaba wa walimu.

MAPENDEKEZO

Kwa kuwa huu mpango wa kalenda unaonyesha kuwa na mafanikio, na kwa sababu ndio kwa mara ya kwanza unaingizwa kwenye field kufanyiwa kazi ili kuwa na ufanisi mdau mimi ningependekeza, hii kalenda ingeanza na kidato cha kwanza wa mwaka huu wa 2022, ili madarasa mengine waendelee na utaratibu wa kawaida uliozoeleka. Kupitia hao wanafunzi wa kidato cha kwanza tungefanya tathimini mwisho wa mwaka na kubaini kama tuendelee nao au la.!! Na kama utaonekana hauna tija hasara ingekua kidogo. Lakini kwa hali ya sasa ya majaribio alafu tunafanya majaribio hayo na hata kwa madarasa ya mitihani nina hofu kama usipoleta ma
Ukifuatilia kwa karibu unaweza kuona aliyetoa mwongozo hajawahi hata kufundisha kipindi kimoja darasani, ila ametengenezewa connection tu na jamaa fulani akapewa post
 
Naweza kuunganisha dots.
Kuna baadhi ya shule za serikali za msingi kwa sasa kumekuwa na ubunifu wa kuwataka watoto/wanafunzi kufika darasani saa 12 asubuhi na kutoka saa moja jioni. Pia weekend moja inapukusuliwa.

Pamoja na hii nia njema lakini kuna mambo hayajazingatiwa kama:

1: Usalama wa watoto(muda wa kufika na kuondoka ni hatarishi , unapoanza kuondoka na kufika nyumbani).

2: Afya za watoto/ muda mrefu wa kusoma bila kupumzika(muda ulioongezwa ni zaidi ya nusu ya muda wa kawaida).

3: Psychological toucher/watoto wanaweza kuona shule ni mzigo, wasifurahie uwepo wao shuleni.

NB: Ukikutana na mwalimu mkuu anakwambia tulishakaa kikao na kuamua, tunataka wafaulu.
Hilo la afya ya watoto tatizo sio muda mrefu tu wa kusoma bila kupumzika ni pamoja na watoto kukaa na njaa muda mrefu Kuna watoto wanatoka nyumbani bila kula chochote na wanashinda na njaa shule kutwa nzima kiafya ni tatizo kubwa
 
Siasa ikiingia kwenye taaluma ni hatari. Hili wazo liboreshwe kwa upande mwingine lina faida kubwa sana!!
 
Back
Top Bottom