Elimu inarudi ilikotokea... Ni hatari Sana Kwa Afrika

Elimu inarudi ilikotokea... Ni hatari Sana Kwa Afrika

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Ukiangalia kwa makini siasa za Afrika zinavyoendeshwa Kwa Sasa, unaweza kuona pasina shaka kuwa mserereko wa kurudi nyuma miaka 200 iliyopita ni mkubwa sana.

Kabla ya Mkutano wa Berlin ulioigawanya Afrika vipande vipande. Afrika yenyewe tayari ilikuwa imegawanyika kikabila na kiukoo.

Maarifa ambayo Kwa lugha nyepesi ndiyo Elimu, kwa upande wa Afrika yalikuwa chini Sana ukilinganisha na watu toka Asia, Arabuni ama ulaya..

Uduni wa Elimu yetu ndiyo uliosababisha tuwe na mifumo dhaifu ya kiutawala ambayo ilikuwa rahisi kushambuliwa na kutekwa/kuvunjwa na wavamizi toka Uarabuni, Asia na Ulaya.

Elimu yetu kuhusu Mungu na kuabudu ndiyo ilisababisha dini zetu kuonekana za "kishenzi" na mpaka leo athari na taathira zake zinaonekana kwenye maisha yetu ya Kila siku.

Kwa kuwa Elimu maana yake ni uwezo wa binadamu kutumia maarifa yake aliyonayo kutatua changamoto zinazomkabili, basi bila ya shaka Afrika imo hatarini kurudi utumwani.

Ukiwaangalia viongozi wa Afrika (pamoja na wale ambao hawakwenda Korea ya Kusini) jinsi wanavyojaribu kutatua matatizo ya nchi zao, unapata shaka kama wanayo Elimu inayohitajika kuwa viongozi.

Leo hii wakati mabara mengine yanasonga mbele kimaendeleo kwa kutumia maarifa mapya na ya zamani toka kwa watu wao, Afrika bado imeshikilia utambuzi wa Elimu kwa vyeti.

Mabara mengine mbali ya cheti ulichonacho cha kuthibitisha ulichosomea, kupata kazi ama kubakia kazini kunategemea zaidi tija unayoileta kwenye taasisi na siyo ukubwa wa cheti chako.

Mwenendo huu wa hali ya Mambo duniani, unaleta shaka kama Afrika tunayo Elimu ya kutosha kuzuia kuingizwa utumwani Kwa mara nyingine tena.

Uchaguzi wa Afrika ya Kusini ni ishara mojawapo kuwa Elimu ya Afrika ni duni Sana.

Waafrika ya kusini walipambana dhidi ya utawala wa wazungu walowezi wachache zama za ukaburu,. Leo wanapambana na waafrika weusi wenzao ili kuwarudisha wazungu madarakani.

Ukiwasikiliza Kwa makini wanaona waafrika wenzao hawana Elimu ya kuiongoza Afrika ya kusini kiufanisi. Lakini wao pia wananchi wa kawaida wameonekana hawana Elimu ya kutosha kuhusu umajumui (Pan Africanism) wa Afrika.

Elimu ni uwezo wa kutumia maarifa kutatua changamoto zinazokuzunguka na siyo uwezo wa kukariri ili kufaulu mitihani.

Kwa kuwa mabara mengine yanarudi kwenye msingi huu kuhusu Elimu, si ajabu kizazi hiki nacho kikaja kuzalisha kina Mangungo wa zama zetu.

Maana inawezekana tukawa na Rais Profesa lakini bado akawa anasaini mikataba uchwara kama alivyofanya Babu yetu Mangungo.
 
Mnawalalamika watu weupe kwani nyie nashindwa nini kuandaa Elimu yenu ,dini yenu na n.k so acha kulalamika be responsible for ur life .

Mmevunja sheria za ulimwemgu that is way mnashindwa Kupata revelation
 
Bara la Afrika limeathiriwa sana na ukoloni pamoja na utumwa, kiasi kwamba limepoteza kabisa radha halisi na vigezo vyote halisi vya thamani ya ustaarabu wake wa asili. Afrika ya sasa ni muhanga mkubwa wa ustaarabu mpya ulio chotara na wenye kuchagizwa na tamaduni za kimapokeo za mataifa ya kigeni.

Ustaarabu ni utamaduni wenye kujumuisha taratibu muhimu za kijamii, zikijumuisha maadili, urithi wa rasiilimali, utunzaji wa mazimgira, desturi, sheria, falsafa, imani za kiroho, siasa, sanaa, pamoja na matumizi mazuri ya sayansi na teknolojia.

Tabia ya asili ya ustaarabu wa eneo husika ni kujali mambo ya msingi na yenye tija kwa jamii pana ya watu badala ya kuwa na mitazamo ya jamii ndogo tu kibinafsi. Ustaarabu wenye kukubalika kwa vigezo vya kimataifa ni uwekezaji wa kutosha katika kustawisha akili za wanajamii na kupanua wigo wa mitazamo chanya ya kijamii katika mambo ya msingi kuendana na utamaduni wa asili wa eneo husika badala ya kuwa na "over-dependence" katika tamaduni za kigeni na kimapokeo.

Afrika na Waafrika hasa Kusini mwa Jangwa la Sahara ndiyo wahanga wakubwa zaidi. Kiasi kwamba wamevurugwa na kugalagazwa kabisa hata kufikia kiasi cha kila mtu kushika kivyake utamaduni ambao ameupokea kutokana na mapokeo ya mtu binafsi, familia, yake ukoo wake ama kabila lake.
 
Ukiangalia kwa makini siasa za Afrika zinavyoendeshwa Kwa Sasa, unaweza kuona pasina shaka kuwa mserereko wa kurudi nyuma miaka 200 iliyopita ni mkubwa sana.

Kabla ya Mkutano wa Berlin ulioigawanya Afrika vipande vipande. Afrika yenyewe tayari ilikuwa imegawanyika kikabila na kiukoo.

Maarifa ambayo Kwa lugha nyepesi ndiyo Elimu, kwa upande wa Afrika yalikuwa chini Sana ukilinganisha na watu toka Asia, Arabuni ama ulaya..

Uduni wa Elimu yetu ndiyo uliosababisha tuwe na mifumo dhaifu ya kiutawala ambayo ilikuwa rahisi kushambuliwa na kutekwa/kuvunjwa na wavamizi toka Uarabuni, Asia na Ulaya.

Elimu yetu kuhusu Mungu na kuabudu ndiyo ilisababisha dini zetu kuonekana za "kishenzi" na mpaka leo athari na taathira zake zinaonekana kwenye maisha yetu ya Kila siku.

Kwa kuwa Elimu maana yake ni uwezo wa binadamu kutumia maarifa yake aliyonayo kutatua changamoto zinazomkabili, basi bila ya shaka Afrika imo hatarini kurudi utumwani.

Ukiwaangalia viongozi wa Afrika (pamoja na wale ambao hawakwenda Korea ya Kusini) jinsi wanavyojaribu kutatua matatizo ya nchi zao, unapata shaka kama wanayo Elimu inayohitajika kuwa viongozi.

Leo hii wakati mabara mengine yanasonga mbele kimaendeleo kwa kutumia maarifa mapya na ya zamani toka kwa watu wao, Afrika bado imeshikilia utambuzi wa Elimu kwa vyeti.

Mabara mengine mbali ya cheti ulichonacho cha kutihibitisha ulichosomea, kupata kazi ama kubakia kazini kunategemea zaidi tija unayoileta kwenye taasisi na siyo ukubwa wa cheti chako.

Mwenendo huu wa hali ya Mambo duniani, unaleta shaka kama Afrika tunayo Elimu ya kutosha kuzuia kuingizwa utumwani Kwa mara nyingine tena.

Uchaguzi wa Afrika ya Kusini ni ishara mojawapo kuwa Elimu ya Afrika ni duni Sana.

Waafrika ya kusini walipambana dhidi ya utawala wa wazungu walowezi wachache zama za ukaburu,. Leo wanapambana na waafrika weusi wenzao ili kuwarudisha wazungu madarakani.

Ukiwasikiliza Kwa makini wanaona waafrika wenzao hawana Elimu ya kuiongoza Afrika ya kusini kiufanisi. Lakini wao pia wananchi wa kawaida wameonekana hawana Elimu ya kutosha kuhusu umajumui (Pan Africanism) wa Afrika.

Elimu n uwezo wa kutumiai maarifa kutatua changamoto zinazokuzunguka na siyo uwezo wa kukariri ili kufaulu mitihani.

Kwa kuwa mabara mengine yanarudi kwenye msingi huu kuhusu Elimu, si ajabu kizazi hiki nacho kikaja kuzalisha kina Mangungo wa zama zetu.

Maana inawezekana tukawa na Rais Profesa lakini bado akawa anasaini mikataba uchwara kama alivyofanya Babu yetu Mangungo.
Mama anaupiga mwingi na mara nyingine kaenda kukopa Trillion 2.5 za watanganyika mtazilipa kwa bakora au muuze bahari!
 
Tuwe wa kweli mnazunguka ila kuendeleza elimu hii tuliachiwa na wakoloni ni sawa ya kutawaliwa kiakili , itabidi tuondoe elimu hii kabisa maana ilitolewa maksudi ili kufanya waafrica wazdi kutawaliwa .

Bora sasa kwenda sehemu za mbali kutafuta elimu , kulinganisha ya ya kwetu ?

Kwa nn ndani ya nchi moja wengine wanasoma english medium , wengine international school na wengine hizi kajamba 8 ? Haya ni matabaka ya awali kabisa katika kuandaa makundi tofauti .

Je, wanaotunga sera za elimu wao mbona watoto wao wanasoma mitaala tofauti ?
 
Mkuu kwenye mikataba hivi leo ipo zaidi hata ya ile ya Magungo!
Angalia kwenye mikataba ya uchimbaji madini iliyosainiwa na awamu ya 3 haihitaji hata elimu kujuwa ilisainiwa na mtu asiyejua chochote kuhusu madini

Kidogo ilileta unafuu baada ya awamu ya 5 kuingilia kati lakini bado tu haina manufaa yoyote!

Magungo historia inamtumia kama sample study ya viongozi wabaya sana ila yote ni kwakuwa iliishi enzi dark age ila amini leo ipo mikataba mibovu mara mia zaidi ya hiyo ya akina Magungo na inasainiwa na kushangiliwa ka makofi na wanaotuongoza!
 
Mnawalalamika watu weupe kwani nyie nashindwa nini kuandaa Elimu yenu ,dini yenu na n.k so acha kulalamika be responsible for ur life .

Mmevunja sheria za ulimwemgu that is way mnashindwa Kupata revelation
Kuna mahali kwenye hili bandiko nimelalamika!?
 
Waafrika ya kusini walipambana dhidi ya utawala wa wazungu walowezi wachache zama za ukaburu,. Leo wanapambana na waafrika weusi wenzao ili kuwarudisha wazungu madarakani.

Ukiwasikiliza Kwa makini wanaona waafrika wenzao hawana Elimu ya kuiongoza Afrika ya kusini kiufanisi. Lakini wao pia wananchi wa kawaida wameonekana hawana Elimu ya kutosha kuhusu umajumui (Pan Africanism) wa Afrika.
Hapana mkuu, waafrika kusini wanapambana na ufisadi uliojikita mizizi ndani ya ANC huku ukijificha ndani ya koti la Umajumuhi na ukombozi.
 
Hapana mkuu, waafrika kusini wanapambana na ufisadi uliojikita mizizi ndani ya ANC huku ukijificha ndani ya koti la Umajumuhi na ukombozi.
Fuatilia kidogo... Umajumui ulikuwa unapigiwa upatu na Julius Malema wa chama cha Economic Freedom Fighters (EFF).

YES! ANC imegubikwa Kwa rushwa... Lakini tofauti yao na watawala wengine Afrika ikoje?

Elimu ni maarifa, jee viongozi wetu wa Afrika wanaonesha maarifa tukuka ya kiuongozi kwenye nyanja ya Elimu, sayansi, matumizi ya Teknolojia, kilimo,biashara za kimataifa,uchumi na maendeleo ya jamii!!??

Usione watu wanamshangilia Ibrahim Traore wa Bukina Faso ukadhani ameonesha maarifa ya kiongozi,la hasha.

Traore anashangiliwa Kwa kuwa anafanya mambo ya kawaida ambayo wananchi walitamani zamani Sana yafanywe na watawala waliomtangulia.
 
Fuatilia kidogo... Umajumui ulikuwa unapigiwa upatu na Julius Malema wa chama cha Economic Freedom Fighters (EFF).

YES! ANC imegubikwa Kwa rushwa... Lakini tofauti yao na watawala wengine Afrika ikoje?

Elimu ni maarifa, jee viongozi wetu wa Afrika wanaonesha maarifa tukuka kwenye nyanja ya Elimu, sayansi, matumizi ya Teknolojia, kilimo,biashara za kimataifa,uchumi na maendeleo ya jamii!!??

Usione watu wanamshangilia Ibrahim wa Traore wa Bukina Faso ukadhani ameonesha maarifa ya kiongozi,la hasha.

Traore anashangiliwa Kwa kuwa anafanya mambo ya kawaida ambayo wanananchi walitamani zamani Sana yafanywe na watawala waliomtangulia.
Waafrika kusini wamepigia kura kwa sababu za kiuchumi na kijamii zaidi, huo Umajumui uliokuwa unahubiriwa na kina Malema na Zuma hawauelewi.
 
Waafrika kusini wamepigia kura kwa sababu za kiuchumi na kijamii zaidi, huo Umajumui uliokuwa unahubiriwa na kina Malema na Zuma hawauelewi.
Hawataki siyo hawauelewi.... Zuma yeye mfanano wake na Malema ulikuwa kwenye kutaifisha migodi ya dhahabu na Platinum.

Hapa kwetu Mwalimu alitaifisha majumba ya watu, Leo hii wale waliotaifishiwa majumba yao ndiyo wamekuwa matajiri kama baba/Babu zao zamani.

Leo hii National Housing Corporation (NHC) shirika kubwa la umma Afrika lenye thamani ya shilingi Trilioni zaidi ya 6, hakuna jambo kubwa lililofanya Kwa miaka yote ya uhai wake.

Fikiria NHC lingekuwa ni shirika binafsi.
 
Hawataki siyo hawauelewi.... Zuma yeye mfanano wake na Malema ulikuwa kwenye kutaifisha migodi ya dhahabu na Platinum.

Hapa kwetu Mwalimu alitaifisha majumba ya watu, Leo hii wale waliotaifishiwa majumba yao ndiyo wamekuwa matajiri kama baba/Babu zao zamani.

Leo hii National Housing Corporation (NHC) shirika kubwa la umma Afrika lenye thamani ya shilingi Trilioni zaidi ya 6, hakuna jambo kubwa lililofanya Kwa miaka yote ya uhai wake.

Fikiria NHC lingekuwa ni shirika binafsi.
Mkuu hizo sera za utaifishaji hazijawahi kuleta tija hapa barani mfano mzuri huko Zimbabwe.

Kwa ufupi waafrika kusini wamegundua hilo ndio maana kina Zuma na Malema wamenyimwa kura.
 
Mkuu hizo sera za utaifishaji hazijawahi kuleta tija hapa barani mfano mzuri huko Zimbabwe.

Kwa ufupi waafrika kusini wamegundua hilo ndio maana kina Zuma na Malema wamenyimwa kura.
Kabisa... Kitendo Cha chama cha wazungu cha Democratic Alliance (DA) kupata kura nyingi kuliko chama vya Zuma au Malema, ni ushahidi tosha kuwa waafrika Kusini wamepoteza Imani na ANC lakini pia hawawaamini kina Zuma na Malema.
 
Mkuu hizo sera za utaifishaji hazijawahi kuleta tija hapa barani mfano mzuri huko Zimbabwe.

Kwa ufupi waafrika kusini wamegundua hilo ndio maana kina Zuma na Malema wamenyimwa kura.
Mkuu ukiangalia kwa umakini mkubwa Malema amepata ushindi mkubwa kwa sababu ameidhofisha ANC kwa kiasi kikubwa sana. Kwa kipindi hiki ANC haina uwezo wa kuunda serikali bila kuungana na vyama vingine.

Mkuu ukiwashindwa wamomonyoe!
 
"Ukiwaangalia viongozi wa Afrika (pamoja na wale ambao hawakwenda Korea ya Kusini)"

Inasikitisha sana.
 
....... sometimes unaweza kukubaliana na wanaosema black race is inferior in all aspects, najaribu kujiuliza ni Kwa nini wakati wenzetu wanaamka na kuanza kutafuta makoloni na natural wealthies sisi tulikuwa tunafanya nini, hii dhana ya kuwa umasikini wetu ni kwa sababu ya ukoloni huwa siikubali kabisa na inatudumaza......
.......upungufu wa akili ukijumlishwa na umasikini matokeo yake ni matatizo throughout the lifetime, mimi nashindwa kuwalaumu viongozi wa Africa tena hasa mbele ya mzungu coz they have nothing to offer, imagine una rasimali zote lakini huna technology ina maana hizo sio mali tena coz huwezi kutumia, na hapo ndo lazima ukubali mikataba ya kina mangungo.......
.......mchawi wa kila kitu Africa ni Akili, ukikosa akili huwezi pambana na umasikini wala maradhi, ukweli mchungu ni kwamba it will take us a very long time to reach ability and discipline ya mzungu, eti tunashindwa kuendesha mradi wa udart ambao ni mkoa mmoja tu, very sad........
........whitemen wametuaminisha sisi weusi kuwa tuna unatajiri mkubwa sana wa rasilimali na na kwamba dunia inatutegemea hivyo tumevimba kichwa, tukiitwa kusaini mikataba ya ushirikiano kiuchumi tunajiona matajiri tunajiona wa maana na kwamba tunanufaika, kumbe ni staili soft ya kutuibia, naamini baada ya mamia ya miaka tutajifunza lakini ni kwa njia ngumu, kwa mateso na majuto........
.........my take: tubadili mtazamo wa kudhani kuwa na rasiimali ndo ujanja bali kuwa na akili(elimu & technology), sio kuendekeza ujinga kila siku ooh! tuna mbuga tuna miti kwani nani hana, watu wanatunyanyasia akili au ujuzi.......
 
Back
Top Bottom