Elimu, Maarifa na Ujuzi vina Nafasi gani Katika Kuchangia Mafanikio ya Mjasiriamali?

Elimu, Maarifa na Ujuzi vina Nafasi gani Katika Kuchangia Mafanikio ya Mjasiriamali?

Entareyehirungu

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2006
Posts
488
Reaction score
471
Kuna kambi kuu mbili juu ya nadhari la chimbuko la ujasiriamali. Kambi ya kwanza inaamini ujasiriamali ni hali au sifa mtu anazaliwa nazo wakati kambi ya pili inaamini kwamba mtu yeyote anaweza kuwa mjasiriamali na hivyo ujasiriamali siyo jambo la lazima iwe hali au jambo la kuzaliwa nalo.

Katika mjadala wetu: Je, Kuna Umuhimu wa Kuandika Mchangamanuo/Mpango wa Biashara?hoja hii ya jasiriamali kama hali ya kuzaliwa nayo au kufundishika imejitokeza sana katika michango ya washiriki. Naomba kwa idhini yenu CONSULT, Kubota, Makirita Amani, Mrimi, Malila, Mvaa Tai, MILLIONS MOVEMENT, Mama Joe, Innocent Prince, Chasha, tuipe hii hoja mjadala wake rasmi hapa.

Mtagundua kwamba katika kichwa cha habari TABIA haijaorodheshwa. Nimefanya hivyo maksudi ili kupunguza upana wa eneo la mjadala na kutaka tujikite katika kuichambua nadharia ya kambi moja tu kwanza "UJASIRIAMALI KAMA JAMBO LINALOFUNDISHIKA"

Ili mtu afanikiwe katika nyanja yake ya Biashara kijasiriamali, anahitaji maarifa gani? Elimu kubwa kiasi gani inahitajika? na ni ujuzi upi ni muhimu kwake kufikia mafanikio?

AU kwa namna nyingine:

Elimu, Maarifa na Ujuzi vina nafasi gani katika kuchangia kumfanya mtu kuwa mjasiriamali mwenye mafanikio?

Karibuni kwa mjadala
 
Mkuu Tunachnganya vitu viwili hapa, Business skills na enteprenership,kinacho fundishwa na vyuo vyote na watoa semina za ujasiriamali ni Buiness skills ambazo sasa wewe kama mjasirimali unaeza zitumia kusonga mbele

Mjasirimali ambaye tiyali ameisha jitoa mhanga na ana spirit ya Ujasirimali anahitaji elimu ya biashara ambayo ndo inayo tolewa na vyuo vyote
- Marketing managment, sales, Pricing, mambo ya neotiation, Promotion, marketing planing, financial planing, Business planing, customer care, na kazalika, Hizi ndo kozi zinazo tolewa n hakuna zaidi ya hapa

SO HAKUNA MAHALI UNAPO WEZA PATA ELIMU YA WEWE KUWA MJASIRIMALI, HAKUNA, ILA KUNA SEHEMU YA WEWE MJASIRIMALI KUONGEZA ELIMU HASA ELIMU YA BIASHARA.

Ni kwa sababu hakuna Chuo chini ya Jua kinacho weza kufundisha haya, na aliye wahi kuhudhuria seina za Ujasirimal kama aisha wahi kufundishwa haya ajitokeza hapa

- Commitment,
- Confidance
- mambo ya risk taking
- Spirit nzima ya ujasiriamali

SO AMBAYE TIYALI NI MJASIRIAMALI ANAHITAJI ELIMU YA BIASHARA ILI AWEZE KUSONGA MBELE,

watu waache kuchangaya Madesa kwanza tukumbuke hakuna Mjasirimali mfanya kazi, make kuna watu ni full wafanya kazi then wanajiita wajasirimali, hakuna na hii iko Tanzania pekee ambapo wafanyakazi nao hujiita wajasirimali

Passion is something that people develop, not something that can be instilled through a series of lectures. It is possible to inspire through lecturing, but if someone isn't passionate about issue,
no amount of convincing or hard facts is going to change that.
Passion is what drives an entrepreneur-

Hapo kwenye Green ndo shida ilipo
 

Na Tutambue kwamba Elimu inayo tolewa nawashari wa Biashara ni elimu ya Biashar na si Elmu ya UJASIRIAMALI, Tatizo tunapotoshwa na wana siasa na sisi tunachukulia yale wanayo tamka wao
Mkuu nakufuatilia dot2dot na nukuu ya hapo juu imenukumbusha mbali. Kipindi neno "UJASIRIAMALI" lilipoanza kuvuma, TACAIDS walikuwa wanaendesha semina za "HIV and AIDS: Home Treatment and Care" lakini washiriki na mgeni rasmi (Kiongozi wa Kisiasa) walijua hayo ndiyo mafunzo ya Ujasiriamali!
 
MwanaJf yeyote alie karibu na Chuo chochote cha kilimo Tanzania, afanye mawasiliano, kwenye mtaala wa mafunzo (syllabus) kuna somo linalofundisha Entrepreneurship. Kwa hiyo hapo naondoa kabisa ile dhana kwamba hakuna chuo duniani kinachofundisha ujasiliamali. Elements zote za ujasilia mali zinafundishwa ikiwamo risk management! Katika mafundisho ya ujasilia mali inafundishwa kwamba masikini hawafaulu kwa kuwa hudai kwamba jambo hili haliwezekani, matajiri husema how can I do this! Moja ya sifa kubwa ya watu masikini na losers ni kusema this is impossible, au this can not be done!!
 
MwanaJf yeyote alie karibu na Chuo chochote cha kilimo Tanzania, afanye mawasiliano, kwenye mtaala wa mafunzo (syllabus) kuna somo la Entrepreneurship. Kwa hiyo hapo naondoa kabisa ile dhana kwamba hakuna chuo duniani kinachofundisha ujasiliamali. Elements zote za ujasilia mali zinafundishwa ikiwamo risk management! Katika mafundisho ya ujasilia mali inafundishwa kwamba masikini hawafaulu kwa kuwa hudai kwamba "jambo hili haliwezekani", matajiri husema "how can I do this"! Moja ya sifa kubwa ya watu masikini na losers ni kusema " this is impossible, au this can not be done!! "
 
Mkuu Tunachnganya vitu viwili hapa, Business skills na enteprenership,kinacho fundishwa na vyuo vyote na watoa semina za ujasiriamali ni Buiness skills ambazo sasa wewe kama mjasirimali unaeza zitumia kusonga mbele

Mjasirimali ambaye tiyali ameisha jitoa mhanga na ana spirit ya Ujasirimali anahitaji elimu ya biashara ambayo ndo inayo tolewa na vyuo vyote
- Marketing managment, sales, Pricing, mambo ya neotiation, Promotion, marketing planing, financial planing, Business planing, customer care, na kazalika, Hizi ndo kozi zinazo tolewa n hakuna zaidi ya hapa

SO HAKUNA MAHALI UNAPO WEZA PATA ELIMU YA WEWE KUWA MJASIRIMALI, HAKUNA, ILA KUNA SEHEMU YA WEWE MJASIRIMALI KUONGEZA ELIMU HASA ELIMU YA BIASHARA.

Ni kwa sababu hakuna Chuo chini ya Jua kinacho weza kufundisha haya, na aliye wahi kuhudhuria seina za Ujasirimal kama aisha wahi kufundishwa haya ajitokeza hapa

- Commitment,
- Confidance
- mambo ya risk taking
- Spirit nzima ya ujasiriamali

SO AMBAYE TIYALI NI MJASIRIAMALI ANAHITAJI ELIMU YA BIASHARA ILI AWEZE KUSONGA MBELE,

watu waache kuchangaya Madesa kwanza tukumbuke hakuna Mjasirimali mfanya kazi, make kuna watu ni full wafanya kazi then wanajiita wajasirimali, hakuna na hii iko Tanzania pekee ambapo wafanyakazi nao hujiita wajasirimali

Passion is something that people develop, not something that can be instilled through a series of lectures. It is possible to inspire through lecturing, but if someone isn’t passionate about issue,
no amount of convincing or hard facts is going to change that.
Passion is what drives an entrepreneur-

Hapo kwenye Green ndo shida ilipo

Well said, nakumbuka kama si wewe basi ni member mwingine alisema ujasiriamali ni kama mapenzi akiwa na maana huwezi kufundishwa true.
 
Well said, nakumbuka kama si wewe basi ni member mwingine alisema ujasiriamali ni kama mapenzi akiwa na maana huwezi kufundishwa true.

Mku tatizo watu wanachanganya mambo that is why inakuwa vigumu kuelewa
 
MwanaJf yeyote alie karibu na Chuo chochote cha kilimo Tanzania, afanye mawasiliano, kwenye mtaala wa mafunzo (syllabus) kuna somo la Entrepreneurship. Kwa hiyo hapo naondoa kabisa ile dhana kwamba hakuna chuo duniani kinachofundisha ujasiliamali. Elements zote za ujasilia mali zinafundishwa ikiwamo risk management! Katika mafundisho ya ujasilia mali inafundishwa kwamba masikini hawafaulu kwa kuwa hudai kwamba "jambo hili haliwezekani", matajiri husema "how can I do this"! Moja ya sifa kubwa ya watu masikini na losers ni kusema " this is impossible, au this can not be done!! "


Hapo Kwenye Red mku unazidi kujichanganya, na unazungumzia vitu vingine kabisa, na wala hicho hakina uhusiano na ,Unazungumzia ishu tofautiau au kwa sababau umesikia inaitwa risk managment basi umejua ni ishu za ujasiriamali?

Kuhusu Vyuo vya Kilimo, Huko ni Mbali Nenda kwenye website ya MZUMBE UNIVESITY kule tafuta kozi ya etreprenership Development, cheki kwenye hiyo Kozi masomo yanayofundishwa hapo,

Kuhusu Vyuo kutoa Kozi zenye kuitwa Entreprenership, Mkuu hiyo ni Biashara, ni sawa na Chuo cha Biashara Cha CBE kiitwe Collage of Entreprenership Education, hivyo hakuna tofauti kati ya mtu kutoa semina ya Biashara na seminan ujasiriamali,

Kinachofanyika hapo ni Kuvutia watu tu na mtu akisikia semina Ujasiriamali basi anajua hapo ndo penyewe na iitwe vyovyote vile haindoi dhana kwamba Ujasirimali haufundishwi,

NA NARUDIA KWA MARA NYINGINE TUACHE KUCHANGANYA VITU HAPA, NDO SHIDA KUBWA TULIYO NAYO,

Tuendele kudangnana kwamba unaweza jifunza Ujasirimali, na tatizo tunazania mtu akienda kufundishwa Jinsi ya Kuanzisha biashara ndo Ujasirimali wenyewe, tunapotoshwa, Business skills sio Ujasiriamali,
 
MwanaJf yeyote alie karibu na Chuo chochote cha kilimo Tanzania, afanye mawasiliano, kwenye mtaala wa mafunzo (syllabus) kuna somo la Entrepreneurship. Kwa hiyo hapo naondoa kabisa ile dhana kwamba hakuna chuo duniani kinachofundisha ujasiliamali. Elements zote za ujasilia mali zinafundishwa ikiwamo risk management! Katika mafundisho ya ujasilia mali inafundishwa kwamba masikini hawafaulu kwa kuwa hudai kwamba "jambo hili haliwezekani", matajiri husema "how can I do this"! Moja ya sifa kubwa ya watu masikini na losers ni kusema " this is impossible, au this can not be done!! "

maelezo yako ni theory ndio inafundishwa na practical hakuna ambayo ndio commitment pia kuna entreprenuer spirit.
 
Mkuu Tunachnganya vitu viwili hapa, Business skills na enteprenership,kinacho fundishwa na vyuo vyote na watoa semina za ujasiriamali ni Buiness skills ambazo sasa wewe kama mjasirimali unaeza zitumia kusonga mbele

Mjasirimali ambaye tiyali ameisha jitoa mhanga na ana spirit ya Ujasirimali anahitaji elimu ya biashara ambayo ndo inayo tolewa na vyuo vyote
- Marketing managment, sales, Pricing, mambo ya neotiation, Promotion, marketing planing, financial planing, Business planing, customer care, na kazalika, Hizi ndo kozi zinazo tolewa n hakuna zaidi ya hapa

SO HAKUNA MAHALI UNAPO WEZA PATA ELIMU YA WEWE KUWA MJASIRIMALI, HAKUNA, ILA KUNA SEHEMU YA WEWE MJASIRIMALI KUONGEZA ELIMU HASA ELIMU YA BIASHARA.

Ni kwa sababu hakuna Chuo chini ya Jua kinacho weza kufundisha haya, na aliye wahi kuhudhuria seina za Ujasirimal kama aisha wahi kufundishwa haya ajitokeza hapa

- Commitment,
- Confidance
- mambo ya risk taking
- Spirit nzima ya ujasiriamali

SO AMBAYE TIYALI NI MJASIRIAMALI ANAHITAJI ELIMU YA BIASHARA ILI AWEZE KUSONGA MBELE,

watu waache kuchangaya Madesa kwanza tukumbuke hakuna Mjasirimali mfanya kazi, make kuna watu ni full wafanya kazi then wanajiita wajasirimali, hakuna na hii iko Tanzania pekee ambapo wafanyakazi nao hujiita wajasirimali

Passion is something that people develop, not something that can be instilled through a series of lectures. It is possible to inspire through lecturing, but if someone isn’t passionate about issue,
no amount of convincing or hard facts is going to change that.
Passion is what drives an entrepreneur-

Hapo kwenye Green ndo shida ilipo

Mkuu i agree with you!
 
Tatizo watu ni wabishi sana hawataki kuelewa


Kutokuelewa kwamba jambo fulani linaweza kufanyika au kutekelezeka hukuondoi uwepo wa jambo hilo. Hayo ambayo yanadhaniwa hayafundishiki ni upeo wa uelewa wa mtu binafsi ulipoishia, ni kama enzi hizo ikidhaniwa dunia ina shepu ya meza, iko flat, akatokea mtaalamu akasema dunia ni duara akanyongwa! Galileo Galilei. Mkuu umethibitisha hapa kwamba ulifundisha ujasiliamali yakakushinda, then uka-prove kwamba ujasilia mali haufundishiki, why did you go to teach in the first place if you knew that it cannt be taught, ones failure should not rule out for the whole world that it is imposible to do what he/she failed! Unaelewa kitu kinaitwa TRAINING? Do you know what training is all about? Are you a proffesional trainer? Ni sheria zipi za kitaaluma unazotumia kuthibitisha kuwa kumfundisha mtu hayo unayodhania hayafundishiki. Kufundishika au kutokufundishika kwa mtu ni suala la quality ya trainer and not trainee!! Kila jambo linafundishika!!!!!!!! I am prepared to start a thread which will change some peoples thinking! Never and never again dare to say that "THIS CAN NEVER BE DONE" in this world !! Watu wenye busara daima huuliza "NI KWA NAMNA GANI HILI LINAWEZA KUFANYIKA? "!

Elements za ujasilia mali zipo kwenye ishu nyingi za kimaisha! Hiyo uniquness inayopelekewa kwenye ujasiria mali hii kitu ni kukuza mambo tu. Kama courage, confidence, risk taking, uvumilivu, subira, kujituma etc kama vitu hivi havifundishiki hawa makocha (couches), spirital healers, priests, sheiks, monks, makamanda wa majeshi, wahamasishaji mbalimbali wana role gani kwenye jamii! Same principles and methods wanazotumia hawa watu niliowaorodhesha hapo juu hivi sasa zinatumika kufundisha ujasiliamali na zinabadili watu. Mtu anaamka asubuhi hajiamini, mwoga, aliekata tamaa na mnyonge, anakutana na mtaalamu anamkalisha chini na kumpiga A, B, C at the end of a day huyo mtu anabadilika! Kunamchakato hufanyika wa kumbadilisha mtu Beliefs then behaviours then anatengenezewa routine ambayo at the end of a day ana-acquire new habits and behaviour! Kinacholeta tofauti ya kufanikiwa kwenye ujasilia mali kimejichimbia sana kwenye Habits and behaviours za watu. Na hii ni uwanja wa watu wanaojua kushughulika na psychology, jinsi ya kumbadili mtu habits and behaviour! It takes time, it takes several practices! Ndiyo maana nimekuwa nikiwashauri watu mara nyingi wanapoanza mambo ya ujasiliamali waanze kidogo au waanze kujishikiza kwa waliofanikiwa, maana it takes time to change ones habits, behaviour etc.

Hii ni taaluma Mkuu, watakuja wengine watajazia nilipoishia. Maisha yenyewe ni ujasilia mali mtupu, kama sivyo kila mtu angeachwa aishi apendavyo na aende apendavyo maana tungeamini kuwa you can not change anybody! Kumfundisha mtu ni kumbadili maana matokeo yake mtu hubadilika mienendo yake! What you are telling here is people can not be changed, people can not be taught! Ngoja nijirudie kwenye darasa letu la wafuga kuku wa kienyeji kule tunasikilizana maana huku mnasema kama mtu ulizaliwa huwezi kujituma basi hakuna anaeweza kukufundisha ukawa mtu wa kujituma.
 
Mkuu naomba unijibu kwenye ujasirimali watu hufundishwa nini hasa, make unaendelea kuchanganya mwanzo mwisho masomo ya biashara na ujasirimali, kama huwezi tofautisha hapa hatutaelewana mwanzo mwisho.

OK hadi leo nafundisha ingawa kidogo ratiba huwa ni ngumu, Sijaacha kufundisha. Ila nina cho fundisha si ujasiriamali bali Business skills, NA BUSINESS SKILLS SIO UJASIRIAMALI HATA SIKU MOJA NA NIMEKUULIZA NI WAPI HAPA TANZANIA WANAFUNDISHA MTU KUWA MJASIRIAMALI.

Huwezi fundishwa kuwa mjasiriamali bali utafundishwa kufanya biashara.
 
Mkuu naomba unijibu kwenye ujasirimali watu hufundishwa nini hasa, make unaendelea kuchanganya mwanzo mwisho masomo ya biashara na ujasirimali, kama huwezi tofautisha hapa hatutaelewana mwanzo mwisho.

OK hadi leo nafundisha ingawa kidogo ratiba huwa ni ngumu, Sijaacha kufundisha. Ila nina cho fundisha si ujasiriamali bali Business skills, NA BUSINESS SKILLS SIO UJASIRIAMALI HATA SIKU MOJA NA NIMEKUULIZA NI WAPI HAPA TANZANIA WANAFUNDISHA MTU KUWA MJASIRIAMALI.

Huwezi fundishwa kuwa mjasiriamali bali utafundishwa kufanya biashara.

Mkuu Chasha huko nyuma ulisema kuwa ujasilia mali haufundishiki kwa vile ulisema huwezi kufundisha mtu commitment, courage, confidence n.k hapa nimekupa mifano categorically, sasa tena unaruka kuwa nachanganya ishu, haina neno Mkuu najua hapa imekuwa Tommy and Jerry game! Sasa hebu tena tuelezee tena ni mambo yapi kwenye ujasilia mali ambayo si rahisi kufundisha, au kumtrain mtu?

Ninachokuomba Mkuu Chasha huu ni wakati wako muafaka sasa uweke wazi definition au description ya Ujasilia mali ili tuweze kuona jinsi ujasiliamali unavyojitofautisha na usivyofundishika kama ilivyo kwa Biasahara! Halafu pia inawezekana kwa mwelekeo wako hata hili jukwaa la ujasilia mali liko kimakosa, maana tunajadiliana kitu ambacho ni hewa! Labda lingepaswa liitwe jukwaa la Biashara! Maana maarifa mengi wanayobadilishana watu hapa inavyoonekana kwa mtazamo wako ni ya biashara tu na si ujasilia mali! Ujasilia mali ni nini hasa? Na ni vitu gani visivyofundisha? Kwa moyo mkunjufu anzia hapo.
 
Kila mjasiriamali ni mfanyabiashara, ila sio kila mfanyabiashara ni mjasiriamali!
 
Mkuu nitaelezea baadae, make ni maelezo marefu sana.

Ila ishu ni kwanba sifa za mjasiriamali hazifundishwi.
Huwezi jifunza uvumilivu, huwezi jifunza ku take risk, na ishu kama uvumilivu huwezi sema utajifunza kwa wenzako.

Kuna vitu ambavyo unaweza jifunza kama vile kuuza, kupanga bei, na kazalika, ila hata kama ukajifunza jinsi ya kuanza biashara, jama huna internal force ni kazi bure, kuna Driving force ambazo ni kutoka moyoni mwako

Kama Ingekuwa hi yo basi wasomi wengi sana wangekuwa wahasiriamali.

Na je usha wahi kujiuliza kwa nini kuna watu wana Degree za Business. Lakini hawawezi hatz kuuza pipi? Nisha kuambia nenda kwenye vyuo vyetu vinavyo toa degree za Ujasiriamali jaribu kufanya kautafiti hapo utagundua kitu fulani,
So humu Hanvini tunafundishana mbinu za biashara ila kama huna Spirt ya Ujasiriamali ni kazi bure, ni lazima uwe na driving force na wala huwezi ipata kwa jirani bali ni wewe mwemyewe


Mkuu Chasha huko nyuma ulisema kuwa ujasilia mali haufundishiki kwa vile ulisema huwezi kufundisha mtu commitment, courage, confidence n.k hapa nimekupa mifano categorically, sasa tena unaruka kuwa nachanganya ishu, haina neno Mkuu najua hapa imekuwa Tommy and Jerry game! Sasa hebu tena tuelezee tena ni mambo yapi kwenye ujasilia mali ambayo si rahisi kufundisha, au kumtrain mtu?

Ninachokuomba Mkuu Chasha huu ni wakati wako muafaka sasa uweke wazi definition au description ya Ujasilia mali ili tuweze kuona jinsi ujasiliamali unavyojitofautisha na usivyofundishika kama ilivyo kwa Biasahara! Halafu pia inawezekana kwa mwelekeo wako hata hili jukwaa la ujasilia mali liko kimakosa, maana tunajadiliana kitu ambacho ni hewa! Labda lingepaswa liitwe jukwaa la Biashara! Maana maarifa mengi wanayobadilishana watu hapa inavyoonekana kwa mtazamo wako ni ya biashara tu na si ujasilia mali! Ujasilia mali ni nini hasa? Na ni vitu gani visivyofundisha? Kwa moyo mkunjufu anzia hapo.
 
Mkuu nitaelezea baadae, make ni maelezo marefu sana.

Ila ishu ni kwanba sifa za mjasiriamali hazifundishwi.
Huwezi jifunza uvumilivu, huwezi jifunza ku take risk, na ishu kama uvumilivu huwezi sema utajifunza kwa wenzako.

Kuna vitu ambavyo unaweza jifunza kama vile kuuza, kupanga bei, na kazalika, ila hata kama ukajifunza jinsi ya kuanza biashara, jama huna internal force ni kazi bure, kuna Driving force ambazo ni kutoka moyoni mwako

Kama Ingekuwa hi yo basi wasomi wengi sana wangekuwa wahasiriamali.

Na je usha wahi kujiuliza kwa nini kuna watu wana Degree za Business. Lakini hawawezi hatz kuuza pipi? Nisha kuambia nenda kwenye vyuo vyetu vinavyo toa degree za Ujasiriamali jaribu kufanya kautafiti hapo utagundua kitu fulani,
So humu Hanvini tunafundishana mbinu za biashara ila kama huna Spirt ya Ujasiriamali ni kazi bure, ni lazima uwe na driving force na wala huwezi ipata kwa jirani bali ni wewe mwemyewe

Tuko pamoja Mkuu!
 
kila kitu kinafundishika ila kiwango cha kuelewa kwa wafundishwa hutofautiana, ndo maana kuna wanafunzi wanapata A, B,... hadi F. kufundishwa darasani(elimu ya nadharia) ni swala moja na elimu kwa vitendo ni swala jingine. kila kitu duniani huwa kama si kufundiswa, tumeiga,au tumesikia hatimaye likakuvutia na hatimaye ikawa ndo tabia/hoby. cha msingi kuwa interest na hicho kitu hatimaye utakipenda na utapenda jinsi ya behave ili ufanikiwe
 
T
Kutokuelewa kwamba jambo fulani linaweza kufanyika au kutekelezeka hukuondoi uwepo wa jambo hilo. Hayo ambayo yanadhaniwa hayafundishiki ni upeo wa uelewa wa mtu binafsi ulipoishia, ni kama enzi hizo ikidhaniwa dunia ina shepu ya meza, iko flat, akatokea mtaalamu akasema dunia ni duara akanyongwa! Galileo Galilei. Mkuu umethibitisha hapa kwamba ulifundisha ujasiliamali yakakushinda, then uka-prove kwamba ujasilia mali haufundishiki, why did you go to teach in the first place if you knew that it cannt be taught, ones failure should not rule out for the whole world that it is imposible to do what he/she failed! Unaelewa kitu kinaitwa TRAINING? Do you know what training is all about? Are you a proffesional trainer? Ni sheria zipi za kitaaluma unazotumia kuthibitisha kuwa kumfundisha mtu hayo unayodhania hayafundishiki. Kufundishika au kutokufundishika kwa mtu ni suala la quality ya trainer and not trainee!! Kila jambo linafundishika!!!!!!!! I am prepared to start a thread which will change some peoples thinking! Never and never again dare to say that "THIS CAN NEVER BE DONE" in this world !! Watu wenye busara daima huuliza "NI KWA NAMNA GANI HILI LINAWEZA KUFANYIKA? "!

Elements za ujasilia mali zipo kwenye ishu nyingi za kimaisha! Hiyo uniquness inayopelekewa kwenye ujasiria mali hii kitu ni kukuza mambo tu. Kama courage, confidence, risk taking, uvumilivu, subira, kujituma etc kama vitu hivi havifundishiki hawa makocha (couches), spirital healers, priests, sheiks, monks, makamanda wa majeshi, wahamasishaji mbalimbali wana role gani kwenye jamii! Same principles and methods wanazotumia hawa watu niliowaorodhesha hapo juu hivi sasa zinatumika kufundisha ujasiliamali na zinabadili watu. Mtu anaamka asubuhi hajiamini, mwoga, aliekata tamaa na mnyonge, anakutana na mtaalamu anamkalisha chini na kumpiga A, B, C at the end of a day huyo mtu anabadilika! Kunamchakato hufanyika wa kumbadilisha mtu Beliefs then behaviours then anatengenezewa routine ambayo at the end of a day ana-acquire new habits and behaviour! Kinacholeta tofauti ya kufanikiwa kwenye ujasilia mali kimejichimbia sana kwenye Habits and behaviours za watu. Na hii ni uwanja wa watu wanaojua kushughulika na psychology, jinsi ya kumbadili mtu habits and behaviour! It takes time, it takes several practices! Ndiyo maana nimekuwa nikiwashauri watu mara nyingi wanapoanza mambo ya ujasiliamali waanze kidogo au waanze kujishikiza kwa waliofanikiwa, maana it takes time to change ones habits, behaviour etc.

Hii ni taaluma Mkuu, watakuja wengine watajazia nilipoishia. Maisha yenyewe ni ujasilia mali mtupu, kama sivyo kila mtu angeachwa aishi apendavyo na aende apendavyo maana tungeamini kuwa you can not change anybody! Kumfundisha mtu ni kumbadili maana matokeo yake mtu hubadilika mienendo yake! What you are telling here is people can not be changed, people can not be taught! Ngoja nijirudie kwenye darasa letu la wafuga kuku wa kienyeji kule tunasikilizana maana huku mnasema kama mtu ulizaliwa huwezi kujituma basi hakuna anaeweza kukufundisha ukawa mtu wa kujituma.

binafsi nimekupata vizuri sana mkuu na kunatokana na maelezo yako kuhusu ku aquire new habats hapo ndo nakuja kukubaliana na msemo usemao "Your thoughts makes ur own reality" so kadri mtu utakavynkuwa unafikiria kuwa something is imposible ts can be realy imposible kitu kikubwa ninachokiamin kwamba ni kweli nakubaliana na wewe kuwa unaweza kuwa mjasiriamali through training kwa mfano ukisoma historia kuhusu mtu kama Robert Kiyosaki ambaye ni mmoja wa wajasiriamali wakubwa yeye kwa kiasi kikubwa alipata "training" kwa mtu ambaye yeye anamuita Rich Dad.
 
Back
Top Bottom