Elimu ya Tanzania na elimu ya Marekani,mbona sisi tunatumia nguvu nyingi?

Elimu ya Tanzania na elimu ya Marekani,mbona sisi tunatumia nguvu nyingi?

Zipo sababu za msingi za utofauti ambazo ziko kwenye mitaala,pia ukae ukijua sisi tunafuata mfumo wa elimu wa UK.

Kwenye hoja yako:Tz na USA ni context mbili tofauti..kwa level tu ya maendeleo huku hata idadi ya taasisi za kutoa elimu ni chache pia mfumo wa utoaji w elimu una issues nyingi ambazo bado haziko vizuri zinahitaji uwekezaji na maboresho, pia mazingira na tamaduni zetu kuna mambo ambayo usipofanya watoto watapotea kabisa..mfano. viboko huku kwetu bado ni sahihi ingawa haki za binadamu zinakataza. Level ya tech wangapi wanaweza kuwa na simu (affordability)

Vipi kuhusu mfumo wa ku train waalimu..mwalimu anakua ni product ya waliofeli ndio awe huko (mostly sec and primary schools),vipi juu ya working conditions (salary..fringe benefits..motivation)

So kuna issues za mifumo, uchumi, context(social cultural issues),
Political will(planning_prioritisation and allocation of appropriate resources for ed provision) haya yote ndio yanafanya tuwe tulivyo..ingawa jutihada zinaonekana na changes ila itatuchukua muda sana as rate ya maboresho haiendani na demand.
Angalau umejitahidi kujibu kisomi. Hizi ndiyo sababu haswaaa (70%).
 
Ni Tanzania pekee duniani ambayo mtoto anapewa elimu ya msingi kwa kiswahili kwa miaka saba hadi nane (ukijumlishia na chekechea) kisha anabadilishiwa gear angani anaanza kupewa elimu ya sekondari kwa lugha ya kiingereza kwa miaka minne na anategemewa afaulu.

Tutasubiri sana.

ni kukremu kwa kwenda mbele lol
 
I think tujenge syllabus tailored to our environment.

pili,tuangalie structures za nje elimu yao ikoje,how can it be improved to suit our needs.

walimu wachaguliwe waliofaulu vizuri,sio waliofeli

mshahara wa walimu upandishwe uwe the same level as majaji etc
 
Inaendelea.......
4.Marekani wanafunzi wanakula chakula kizuri,lakini TZ wanafunzi wanalishwa maharage mabovu yaliyooza na wadudu wakutosha, ugali mbaya wenye harufu mbaya halafu walimu na wazazi wanakuambia eti chakula hicho kibaya kinamfanya mwanafunzi awe na akili na kupata afya bora huu ni ubutu wa fikra.
Mambo hayo manne yanaonesha sisi tunatumia nguvu nyingi ila tunaishia kuzalisha ziro nyingi na elimu yetu inazidi kuwa mbovu, wakati hawa wamarekani wasiotumia nguvu sana elimu yao ipo juu sana.
Unaweza kusingizia uhaba wa walimu na vitabu sawa,ila hii sio sababu ya kusingizia,kwa mfano mimi nimesoma o-level shule ilikuwa na walimu wa kutosha,vitabu vya kutosha na fimbo za kutosha lakini 2014 shule ilipata ziro 42 kwenye mtihani wa kidato cha nne.
Je sisi tunakosea wapi? ,je kuvaa sare,chakula kibaya kuzuia simu na kuchapa wanafunzi fimbo ma adhabu kali inasaidia chochote kwenye elimu yetu? kipi kifanyike kukuza elimu yetu?Karibu wakuu
%by Sir Khan.Born 2 win%
5. Wamarekani Wanatumia nguvu nyingi kuwekeza kwenye elimu, wakati CCM wanatumia nguvu nyingi kuwadanganya watanzania eti Elimu yetu nzuri.
 
Ukitaka kumtawala masikini mnyime elimu,ukitaka kumsaidia masikini mpe mwanae elimu!!ukitazama vizuri hiyo elimu ni ya wananchi wahali ya chini na wahali yakati kwa uchache je niviongozi wangapi na matajiri wangapi watoto wao wanasoma hizi shule,hata raisi wawa nyonge wanae wanasoma hapo??
 
Siyo jibu. Tusaidiane kutafuta hili tatizo kwa mawazo

Tatizo litatatuka endapo mfumo wa elimu utarekebishwa kuendana na hitajio letu na dunia kwa ujumla...

Wenzetu mambo mengi wamepunguza au kuachana nayo kabisa... mifumo yao ya elimu wanairekebisha siyo kwa ajili ya kupata ufaulu mkubwa ili kuonesha shule fulani inafaulisha zaidi...hapana na kuendana na matakwa na mabadiliko ya dunia...

Cc: mahondaw
 
I think tujenge syllabus tailored to our environment.

pili,tuangalie structures za nje elimu yao ikoje,how can it be improved to suit our needs.

walimu wachaguliwe waliofaulu vizuri,sio waliofeli

mshahara wa walimu upandishwe uwe the same level as majaji etc
Bado tunatumia elimu ya mkoloni na mwalimu ya kuwafunza majority kujua kusoma,kuhesabu nakuandika!!lakini si yakufuta ujinga nadhani njia sahihi ya kubadili mfumo wa elimu ni kubadii utawala na watawala waliopo nakuleta viongozi sahihi!!kuanzia kwa mzee Mkapa kilio likuwa hiki walipofanya marekebisho ndo elimu ikazikuwa worse,Kikwete nae akajaribu kurudisha alicho ondoa mwenzie na kuongezea maboresho yake ndio tukaibuka na darasa la saba wasiojua kusoma nakuandika na wamefaulu kwenda sekondari,kinachoendelea awamu hii nadhani kila mmoja anakiona kutoka kwa watoto wasiojua kusoma na kuandika kwa ufasaha mpaka kwa waandaji wavitabu vya kufundushia vye makosa katika upande wa lugha nakadhalika
 
Kwa nchi kama Tanzania elimu inayotufaa kwasasa ni elimu vocational kwanza yaani tuachane kwanza na phd,masters hizi elimu za wakina mafundi mchundo ndio zinachochea ukuaji wa uchumi tujifunze kwa Bangladesh,Korea kusini n.k
 
mie still naona inawezekana kwa serikali hii kuimprove sekta ya elimu kwa kuangalia AWAMU ZOTE ZILIZOPITA walipatia wapi na walikosea wapi,kisha waje na PLAN yao wenyewe…..
 
mie still naona inawezekana kwa serikali hii kuimprove sekta ya elimu kwa kuangalia AWAMU ZOTE ZILIZOPITA walipatia wapi na walikosea wapi,kisha waje na PLAN yao wenyewe…..
Tulitegemea kuyaona mapema pale ndalichoko alipoteuliwa lakini nini kipya mpaka sasa maana yeye nimiongoni waliopinga mwenwndo wa awamu iliopita mpaka sasa kuna innovation ipi katika sekta ya elimu mwaka watatu huu
 
Tulitegemea kuyaona mapema pale ndalichoko alipoteuliwa lakini nini kipya mpaka sasa maana yeye nimiongoni waliopinga mwenwndo wa awamu iliopita mpaka sasa kuna innovation ipi katika sekta ya elimu mwaka watatu huu

naona tuna culture ya kuleana,nchi nyingine ni performance ndiyo inakuweka ofisini,sasa damage inaonekana mapema ila mtu anaachwa ofisini kwa miaka mitano,by then damage imekua inakua kubwa sana….this is sad mkuu
 
Inaendelea.......
4.Marekani wanafunzi wanakula chakula kizuri,lakini TZ wanafunzi wanalishwa maharage mabovu yaliyooza na wadudu wakutosha, ugali mbaya wenye harufu mbaya halafu walimu na wazazi wanakuambia eti chakula hicho kibaya kinamfanya mwanafunzi awe na akili na kupata afya bora huu ni ubutu wa fikra.
Mambo hayo manne yanaonesha sisi tunatumia nguvu nyingi ila tunaishia kuzalisha ziro nyingi na elimu yetu inazidi kuwa mbovu, wakati hawa wamarekani wasiotumia nguvu sana elimu yao ipo juu sana.
Unaweza kusingizia uhaba wa walimu na vitabu sawa,ila hii sio sababu ya kusingizia,kwa mfano mimi nimesoma o-level shule ilikuwa na walimu wa kutosha,vitabu vya kutosha na fimbo za kutosha lakini 2014 shule ilipata ziro 42 kwenye mtihani wa kidato cha nne.
Je sisi tunakosea wapi? ,je kuvaa sare,chakula kibaya kuzuia simu na kuchapa wanafunzi fimbo ma adhabu kali inasaidia chochote kwenye elimu yetu? kipi kifanyike kukuza elimu yetu?Karibu wakuu
%by Sir Khan.Born 2 win%
Elimu irekebishwe kuanzia msingi lugha ya kufundishia iwe ni kiingereza hii itasaidia kuondoa wale wanaoshindwa kwenda na mabadiliko ya kutoka kiswahili (msingi) kwenda kingereza (sekondari). Nadhani hiyo pia ingesaidia kupunguza miaka ya kukaa shule kwa sababu kuna baadhi ya vitu vinavyofundishwa ktk shule za msingi ndio vinakuja kurudiwa sekondari kwa lugha ya kiingereza. Kuna nchi za wenzetu utashangaa kijana mdogo kiumri tayari amemaliza elimu yake hivyo anakua na muda mrefu wa kuitumia taaluma yake.
 
swali la kujiuliza kwanini wa ughaibuni wanatumia na elimu yao ipo juu,au wanafunzi wa bongo hawana akili ya kujitawala hasa katika kutumia simu?
Kuna utafiti wa UNESCO ulisema kuna udumavu wa akili miingoni mwa watoto Sababu zilikuwa nyingi.
 
Je ni Kwa kiasi gani na Kwa dhamira/nia dhabiti kabisa Kwa miaka hii ya karibuni tumewekeza katika kujenga mfumo bora wa elimu?

Tukianza kujitathmini hapo tunaweza sasa fikiria kuanza kujilinganisha na wengine ambao tayari wameendelea.

Hatuwezi kuanza kulinganisha elimu yetu kwa hatua hii na nchi zilizoendelea wakati ambapo vifaa vya kufundishia bado no mtihani kupatikana mashuleni , maslahi ya walimu na wengine walio Kwenye sekta ya elimu ipo Chini, ualimu kuonekana ni fani duni na mengine mengi ya kufanyiwa maboresho.
 
Ni Tanzania pekee duniani ambayo mtoto anapewa elimu ya msingi kwa kiswahili kwa miaka saba hadi nane (ukijumlishia na chekechea) kisha anabadilishiwa gear angani anaanza kupewa elimu ya sekondari kwa lugha ya kiingereza kwa miaka minne na anategemewa afaulu.

Tutasubiri sana.
Moja ya point muhimu sana hii
 
Back
Top Bottom