Elimu ya Ufundi ni muhimu lakini inategemea sana mambo yafuatayo ili ilete tija na matokeo katika kupambana na Tatizo la ajira

Elimu ya Ufundi ni muhimu lakini inategemea sana mambo yafuatayo ili ilete tija na matokeo katika kupambana na Tatizo la ajira

Fohadi

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2020
Posts
772
Reaction score
2,421
Natambua na nathamini sana mawazo ya Mh. Rais ya kubadili mitaala yetu ya elimu ili kuwawezesha vijana kupata elimu ujuzi itakayowasaidia kujiajiri na kuajiri watu wengine.

Licha ya umuhimu wa elimu ya ufundi katika kutatua tatizo hili, bado elimu hii hii ya ufundi inaweza kuturudisha kule kule kwenye tatizo la ukosefu wa ajira na vipato kwa vijana endapo tu baadhi ya mambo ambayo yanapaswa kwenda sambamba na elimu ya ufundi hatutayapa kipaumbele au 'tutayasahau'.

Kwanini nasema hivi:
Naomba tuutazame utekelezaji wa elimu ya ujuzi na matokeo yake kwa miaka ya baadae ( Long run). Ninaamini, tukianza utoaji wa elimu kwa mitaala mipya (elimu ya ujuzi) baada ya miaka mingi (10 au 15) kutakuwa na matokeo haya:-

1. Idadi ya vijana wenye ujuzi katika ufundi wa taaluma mbalimbali kama umeme, ujenzi, magari na ufundi au ujuzi mwingine wa aina hiyo itakuwa imeongezeka sana kama jinsi ambavyo degree zimejaa leo hii. Hii itafanya katika kila kundi la vijana 10, basi 6 au 5 kati yao wana ujuzi au ufundi kutoka vyuoni.

2. Hii itapelekea hata ndani ya familia au jamii kuwe na vijana ambao pengine wamesoma ufundi unaofanana kama ilivyo leo ambapo ndani ya familia moja unakuta kuna watu wenye fani za uhasibu wapo 3. Au ndani ya mtaa mmoja unakuta watu wenye ujuzi wa maswala ya umeme wapo hata 9 au zaidi. Sasa je, ni nani atahitaji huduma kutoka kwa mwingine? ni kwa namna gani ujuzi utawasaidia hawa wasomi kujipatia kipato chao ikiwa kila mtu ana utaalamu wa hicho kitu?

Bila shaka, baada ya miaka mingi kupita (LONG RUN), tunaweza kurudi kulekule ambapo vijana wana elimu au ujuzi ambao hauwasaidii kwa namna ya kujiingizia kipato kwa sababu wasomi au wajuzi wa fani hizo watakuwa wamejaa.

Maoni kuhusu nini kifanyike ili elimu ya ujuzi iwe na tija tunayoitarajia
Binafsi, ningependa kushauri yafuatayo ambayo inabidi yaende sambamba na mitaala hii mipya ya elimu ili kuja kusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira nchini kwa miaka mingi ijayo:-

1. Elimu ya msingi/lazima iwe hadi kidato cha nne.
Elimu ya kidato cha nne iwe ni ya lazima ili kumjenga kifikra mwanafunzi. Baada ya matokeo ya kidato cha nne, mgawanyo wa wanafunzi ufanyike kama ifuatavyo. Wale waliopata ufaulu mkubwa hasa DIVISION ONE tu ndio waendelee na kidato cha tano na sita hadi chuo kikuu kwa hii mitaala ya kawaida katika fani muhimu kama afya, ualimu, uchumi, sheria, biashara, kilimo, uhandisi n.k. Hili kundi litaandaliwa ili kuja kuwa wasimamizi au waajiriwa katika fani hizi. Na ni vema kuchukua Division one pekee ili kuzuia SURPLUS ya wataalamu kwenye fani hizi ukilinganisha na soko la ajira.

DIVISION TWO NA THREE hawa waende moja kwa moja katika vyuo vya ufundi katika fani mbalimbali kama umeme, kilimo, uchongaji, ushonaji,ujenzi n.k ili kutengeneza wataalamu ambao watasaidia kujiajiri na kutengeneza ajira kwa wasimamizi wale juu.

DIVISION 4 NA ZERO kwa utafiti wangu mdogo, asilimia kubwa ya wanafunzi kwenye kundi hili, huwa sio wazuri kwenye masomo na muda wao mwingi wanautumia kwenye fani wazipendazo. Hapa inatakiwa kuwe na shule maalumu za michezo na Sanaa kama mziki, uigizaji, uchongaji n.k ili kuwasaidia hawa kupata ujuzi zaidi katika fani zao. Hapa tutazalisha wasanii wazuri ambao watapata fursa mbali mbali ndani na nje ya nchi na kutengeneza ajira kwa wengine. Nadhani tukipata wasanii 15 kama Diamond, kuna ajira nyingi zitazalishwa na hii inawezekana mbona Nigeria kuna wasanii wengi wakubwa. Na wale wasanii ambao hwatakuwa wakubwa basi angalau watakuwa na kipato cha kuendesha maisha yao kwa uhakika.

NB: Kuwe na shule maalum za vipaji mbalimbali kama soka, netball, tennis, ngumi n.k. Tukiwafundisha watoto wenye fani hizi kuanzia chini basi ni rahisi kuzalisha akina samatta, hasheem thabit, mwakinyo na wengine wengi kimataifa. INAWEZEKANA.

2. Uboreshaji maslahi ya watumishi wa umma.
Hili kundi likiweza kufanyiwa haya, litaweza kuhitaji huduma kama kujengewa nyumba mpya, umeme na huduma zingine za kiufundi ambapo vijana wetu waliosoma VETA kupitia kujiajiri kwao watauza huduma kwa kundi hili. Bila hivyo, vijana wetu wenye ujuzi wataishia kukosa sehemu ya kuuza ujuzi wao.

3. Tax exemption na Grace periods kwa wawekezaji wadogo wadogo.
Vijana wengi wana ideas na wana taka kuwekeza na kukuza biashara zao. Ila tatizo linakuwa kodi ambazo zingine wanatakiwa kuanza kuzilipa hata kabla ya kuanza kusimama vizuri. Kukiwa na tax exemption kwa kipindi Fulani, itasaidia kukuza biashara hizi na kuzalisha ajira nyingi sana kwa wengine na kuajiri hata vijana wetu wa VETA. Hii iende pamoja na uongezaji wa utoaji mikopo isiyo na riba kwa vijana huku serikali ikifatilia kuhakikisha mikopo hiyo/mitaji inatumika na kuleta matokeo yaliyotarajiwa.

4. Mazingira mazuri ya uwekezaji hasa kwa wawekezaji wa nje.
Kundi hili linauwezo wa kuzalisha ajira nyingi kwa wakati mmoja. Hili halihitaji maelezo mengi maana mifano ni mingi na nashukuru Mh. Rais ameliwekea msisitizo mkubwa.

5. Mazingira mazuri kwa asai za kiraia.
Asasi za kiraia (NGOs) zina mchango kubwa sana katika kuzalisha ajira kwa watu wengi. Kuna NGOs nyingi sana ambazo zinatoa ajira kwa wengi na kuisaidia serikali. Na faida nyingine hizi asasi zinasaidia jamii kwa kutatua kero za beneficiaries wao. Ushauri wangu ni kwa serikali kuzisimamia hizi asasi ili ziweze kufanya kazi zao kwa ufanisi kwa kufata sheria, taratibu na kanuni za nchi na pia kufanya shughuli zao kwa UFANISI kama zilivyo kwenye documents zao za usajili.

6. Family Planning
Hapa nashauri mkazo uwekwe ili kuweza kuwa na idadi ya watu ambayo inaendana na rasilimali zilizopo. Kila mwaka idadi ya watoto wanaoanza shule inaongezeka kwa sababu watoto wanaozaliwa ni wengi sana. Hata tukitoa elimu ya ufundi kuanzia darasa la saba, bado tutakuwa na vijana wenye ujuzi huku wakibaki tegemezi kwa kukosa sehemu ya kufanya kazi au kuuza ujuzi wao maana idadi yao ni kubwa sana. Ni vyema tukaweka mkazo mkubwa katika agenda hii pia.

7. Mifumo mizuri ya ukusanyaji kodi.
Naunga mkono kama ambavyo mh. Rais anasisitiza uwepo wa mifumo mizuri ya ukusanyaji wa kodi na matumizi ya pesa za umma. Asilimia kubwa ya mambo niliyoshauri yanahitaji uwezo mzuri wa serikali kiuchumi. Huwezi kutoa tax exemption kwa vijana kama huna pato la kutosha. Huwezi kujenga vyuo vya ufundi kama huna pato la kutosha. Basi mifumo ya ukusanyaji na usimamizi wa kodi iboreshwe.

8. Ubanaji wa matumizi ya serikali.
Mbinu za ubanaji na upunguzaji matumizi ya serikali zipo na ambazo zinaweza kutumika ili pesa hiyo ikatumike katika moja ya mambo niliyoyagusia hapo juu ili kuleta tija katika elimu yetu ya ufundi. Tunaweza punguza idadi ya wabunge na wawakilishi na kupunguza mishahara yao na posho, na pia tukaamua nafasi moja kati ya Mkuu wa wilaya au mkurugenzi wa halmashauri ikavunjwa. Na tukafanya mengi kama alivyofanya Mwendazake kuvunja Halimashauri ya Jiji la DSM ili kubana matumizi na kuleta maendeleo kwa watanzania.

MWISHO
Elimu ya ufundi ni muhimu na ina tija ila nina amini itakuwa na tija Zaidi endapo hayo niliyoyashauri na mengine mazuri yaliyo/yatakayoshauriwa na wengine yatasimamiwa vema na kupewa kipaumbele sambamba na mitaala yetu mipya ambayo ni mizuri ili kupata matokeo chanya in LONG RUN.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA – Kazi Iendelee.​
 
Mleta mada, huoni kuwa hata utaratibu wako wa kuwagawa wanafunzi katika makundi hayo bado upo uwezekano kila baada ya muda mfupi kila kundi likajaa watu wa aina yake na hivyo tukarudi palepale?

Hoja hapa ni kuwa Skills bado ni muhimu, natural selection italazimisha kila kundi liwe na watu wa skill fulani wanayoendana nayo, kwa hiyo mambo yatajibalance
 
Natambua na nathamini sana mawazo ya Mh. Rais ya kubadili mitaala yetu ya elimu ili kuwawezesha vijana kupata elimu ujuzi itakayowasaidia kujiajiri na kuajiri watu wengine.

Licha ya umuhimu wa elimu ya ufundi katika kutatua tatizo hili, bado elimu hii hii ya ufundi inaweza kuturudisha kule kule kwenye tatizo la ukosefu wa ajira na vipato kwa vijana endapo tu baadhi ya mambo ambayo yanapaswa kwenda sambamba na elimu ya ufundi hatutayapa kipaumbele au 'tutayasahau'.

Kwanini nasema hivi:
Naomba tuutazame utekelezaji wa elimu ya ujuzi na matokeo yake kwa miaka ya baadae ( Long run). Ninaamini, tukianza utoaji wa elimu kwa mitaala mipya (elimu ya ujuzi) baada ya miaka mingi (10 au 15) kutakuwa na matokeo haya:-

1. Idadi ya vijana wenye ujuzi katika ufundi wa taaluma mbalimbali kama umeme, ujenzi, magari na ufundi au ujuzi mwingine wa aina hiyo itakuwa imeongezeka sana kama jinsi ambavyo degree zimejaa leo hii. Hii itafanya katika kila kundi la vijana 10, basi 6 au 5 kati yao wana ujuzi au ufundi kutoka vyuoni.

2. Hii itapelekea hata ndani ya familia au jamii kuwe na vijana ambao pengine wamesoma ufundi unaofanana kama ilivyo leo ambapo ndani ya familia moja unakuta kuna watu wenye fani za uhasibu wapo 3. Au ndani ya mtaa mmoja unakuta watu wenye ujuzi wa maswala ya umeme wapo hata 9 au zaidi. Sasa je, ni nani atahitaji huduma kutoka kwa mwingine? ni kwa namna gani ujuzi utawasaidia hawa wasomi kujipatia kipato chao ikiwa kila mtu ana utaalamu wa hicho kitu?

Bila shaka, baada ya miaka mingi kupita (LONG RUN), tunaweza kurudi kulekule ambapo vijana wana elimu au ujuzi ambao hauwasaidii kwa namna ya kujiingizia kipato kwa sababu wasomi au wajuzi wa fani hizo watakuwa wamejaa.

Maoni kuhusu nini kifanyike ili elimu ya ujuzi iwe na tija tunayoitarajia
Binafsi, ningependa kushauri yafuatayo ambayo inabidi yaende sambamba na mitaala hii mipya ya elimu ili kuja kusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira nchini kwa miaka mingi ijayo:-

1. Elimu ya msingi/lazima iwe hadi kidato cha nne.
Elimu ya kidato cha nne iwe ni ya lazima ili kumjenga kifikra mwanafunzi. Baada ya matokeo ya kidato cha nne, mgawanyo wa wanafunzi ufanyike kama ifuatavyo. Wale waliopata ufaulu mkubwa hasa DIVISION ONE tu ndio waendelee na kidato cha tano na sita hadi chuo kikuu kwa hii mitaala ya kawaida katika fani muhimu kama afya, ualimu, uchumi, sheria, biashara, kilimo, uhandisi n.k. Hili kundi litaandaliwa ili kuja kuwa wasimamizi au waajiriwa katika fani hizi. Na ni vema kuchukua Division one pekee ili kuzuia SURPLUS ya wataalamu kwenye fani hizi ukilinganisha na soko la ajira.

DIVISION TWO NA THREE hawa waende moja kwa moja katika vyuo vya ufundi katika fani mbalimbali kama umeme, kilimo, uchongaji, ushonaji,ujenzi n.k ili kutengeneza wataalamu ambao watasaidia kujiajiri na kutengeneza ajira kwa wasimamizi wale juu.

DIVISION 4 NA ZERO kwa utafiti wangu mdogo, asilimia kubwa ya wanafunzi kwenye kundi hili, huwa sio wazuri kwenye masomo na muda wao mwingi wanautumia kwenye fani wazipendazo. Hapa inatakiwa kuwe na shule maalumu za michezo na Sanaa kama mziki, uigizaji, uchongaji n.k ili kuwasaidia hawa kupata ujuzi zaidi katika fani zao. Hapa tutazalisha wasanii wazuri ambao watapata fursa mbali mbali ndani na nje ya nchi na kutengeneza ajira kwa wengine. Nadhani tukipata wasanii 15 kama Diamond, kuna ajira nyingi zitazalishwa na hii inawezekana mbona Nigeria kuna wasanii wengi wakubwa. Na wale wasanii ambao hwatakuwa wakubwa basi angalau watakuwa na kipato cha kuendesha maisha yao kwa uhakika.

NB: Kuwe na shule maalum za vipaji mbalimbali kama soka, netball, tennis, ngumi n.k. Tukiwafundisha watoto wenye fani hizi kuanzia chini basi ni rahisi kuzalisha akina samatta, hasheem thabit, mwakinyo na wengine wengi kimataifa. INAWEZEKANA.

2. Uboreshaji maslahi ya watumishi wa umma.
Hili kundi likiweza kufanyiwa haya, litaweza kuhitaji huduma kama kujengewa nyumba mpya, umeme na huduma zingine za kiufundi ambapo vijana wetu waliosoma VETA kupitia kujiajiri kwao watauza huduma kwa kundi hili. Bila hivyo, vijana wetu wenye ujuzi wataishia kukosa sehemu ya kuuza ujuzi wao.

3. Tax exemption na Grace periods kwa wawekezaji wadogo wadogo.
Vijana wengi wana ideas na wana taka kuwekeza na kukuza biashara zao. Ila tatizo linakuwa kodi ambazo zingine wanatakiwa kuanza kuzilipa hata kabla ya kuanza kusimama vizuri. Kukiwa na tax exemption kwa kipindi Fulani, itasaidia kukuza biashara hizi na kuzalisha ajira nyingi sana kwa wengine na kuajiri hata vijana wetu wa VETA. Hii iende pamoja na uongezaji wa utoaji mikopo isiyo na riba kwa vijana huku serikali ikifatilia kuhakikisha mikopo hiyo/mitaji inatumika na kuleta matokeo yaliyotarajiwa.

4. Mazingira mazuri ya uwekezaji hasa kwa wawekezaji wa nje.
Kundi hili linauwezo wa kuzalisha ajira nyingi kwa wakati mmoja. Hili halihitaji maelezo mengi maana mifano ni mingi na nashukuru Mh. Rais ameliwekea msisitizo mkubwa.

5. Mazingira mazuri kwa asai za kiraia.
Asasi za kiraia (NGOs) zina mchango kubwa sana katika kuzalisha ajira kwa watu wengi. Kuna NGOs nyingi sana ambazo zinatoa ajira kwa wengi na kuisaidia serikali. Na faida nyingine hizi asasi zinasaidia jamii kwa kutatua kero za beneficiaries wao. Ushauri wangu ni kwa serikali kuzisimamia hizi asasi ili ziweze kufanya kazi zao kwa ufanisi kwa kufata sheria, taratibu na kanuni za nchi na pia kufanya shughuli zao kwa UFANISI kama zilivyo kwenye documents zao za usajili.

6. Family Planning
Hapa nashauri mkazo uwekwe ili kuweza kuwa na idadi ya watu ambayo inaendana na rasilimali zilizopo. Kila mwaka idadi ya watoto wanaoanza shule inaongezeka kwa sababu watoto wanaozaliwa ni wengi sana. Hata tukitoa elimu ya ufundi kuanzia darasa la saba, bado tutakuwa na vijana wenye ujuzi huku wakibaki tegemezi kwa kukosa sehemu ya kufanya kazi au kuuza ujuzi wao maana idadi yao ni kubwa sana. Ni vyema tukaweka mkazo mkubwa katika agenda hii pia.

7. Mifumo mizuri ya ukusanyaji kodi.
Naunga mkono kama ambavyo mh. Rais anasisitiza uwepo wa mifumo mizuri ya ukusanyaji wa kodi na matumizi ya pesa za umma. Asilimia kubwa ya mambo niliyoshauri yanahitaji uwezo mzuri wa serikali kiuchumi. Huwezi kutoa tax exemption kwa vijana kama huna pato la kutosha. Huwezi kujenga vyuo vya ufundi kama huna pato la kutosha. Basi mifumo ya ukusanyaji na usimamizi wa kodi iboreshwe.

8. Ubanaji wa matumizi ya serikali.
Mbinu za ubanaji na upunguzaji matumizi ya serikali zipo na ambazo zinaweza kutumika ili pesa hiyo ikatumike katika moja ya mambo niliyoyagusia hapo juu ili kuleta tija katika elimu yetu ya ufundi. Tunaweza punguza idadi ya wabunge na wawakilishi na kupunguza mishahara yao na posho, na pia tukaamua nafasi moja kati ya Mkuu wa wilaya au mkurugenzi wa halmashauri ikavunjwa. Na tukafanya mengi kama alivyofanya Mwendazake kuvunja Halimashauri ya Jiji la DSM ili kubana matumizi na kuleta maendeleo kwa watanzania.

MWISHO
Elimu ya ufundi ni muhimu na ina tija ila nina amini itakuwa na tija Zaidi endapo hayo niliyoyashauri na mengine mazuri yaliyo/yatakayoshauriwa na wengine yatasimamiwa vema na kupewa kipaumbele sambamba na mitaala yetu mipya ambayo ni mizuri ili kupata matokeo chanya in LONG RUN.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA – Kazi Iendelee.​
Uchambuzi mzuri sana! Kuna wakati niliipata bahati ya kushiriki mjadala kuhusu elimu ya Tanzania na wadau muhimu kabisa wa elimu na ambao kimsingi wana dhamana kubwa ya kuangalia ubora wa elimu katika shule zetu hizi

Maoni yangu yalifanana kwa kiasi fulani na ulichokisema kuhusu elimu msingi iwe hadi kidato Cha nne.

Baada ya darasa la saba wote waende kidato Cha kwanza halafu wakifika form two kwenye mtihani wa Taifa wafanye tathimini ya kina na yenye uhalisia ili wanaopata division one na two waendelee na kidato Cha tatu katika michepuo wanayoihitaji

Wale wa division three waandaliwe utaratibu wa kuhamishiwa vyuo vya kati kulingana na fani aipendayo mwanafunzi Kama ni ICT, RECORDS MNG, UMEME, NK

Halafu wale wa division four na zero waandaliwe utaratibu wa kupelekwa VETA nao katika fani wanazohitaji

Nilijenga hoja yangu katika Mambo mawili;

Kwanza ukiangalia wanaofeli darasa la saba siku hizi ni asilimia ndogo sana na ukifuatilia vizuri hawatofautiana kiuwezo na asilimia kubwa ya wanaochaguliwa. Yaani ukichimba zaidi utakuta sababu zilizowafanya wasichaguliwe ni uhaba wa madarasa na madawati wala sio uwezo. Kwasababu siku hizi wapo wanafunzi wengi wanapelekwa Kidato Cha kwanza hawajui kuandika 'my name is...' badala yake anaandika "mai nemu izi...."

Pili, baada ya kumaliza kidato Cha nne kundi kubwa sana linarudi mtaani na hapo ndo waliowengi ndio mwisho wao maana baada ya kidato Cha nne serikali inabaki na wale waliofaulu hawa wengine waliofeli hawana uangalizi au ufuatiliaji rasmi wa serikali tena

Nilichojibiwa kilinishangaza kwani ilionekana naongea kitu ambacho HAKIWEZEKANI KABISAA!

Baadae mjumbe mmoja akaniunga mkono kwa kuboresha kwamba hilo lifanyike baada ya kidato Cha nne kwa kutoa hoja ya umri. Kwamba kidato Cha tatu wanakuwa bado wadogo kuhimili mitaala ya vyuo vya Kati

Hata hivyo hoja hiyo Mimi sikuiona Kama ni ya msingi kwasababu naamini mtoto akikua anajifunza anachokipenda ndo anakuwa mahili zaidi

Itoshe kusema tu Kuna baadhi ya wadau wa elimu hawako tayari kupokea mabadiliko. Wanaogopa sana mabadiliko ila ulichoshauri ni kitu kizuri sana na chenye manufaa
 
Tulikuwa na shule za ufundi kama ifunda, moshi tech, Arusha tech, mbeya tech hizi tuliziua na nyingine ziligeuzwa vyuo lakini wanafunzi walitoka wakiwa na ujuzi kamili.
Binafsi nimesoma shule ya kilimo o level tulifundishwa vitu vingi kuanzia soil science, livestock keeping, agro mechanics, rural economy, bee keeping, fishing ni knowledge ambazo zinamsaidia mwanafunzi akimaliza shule changamoto kuna baadhi ya topic kama soil science hazina walimu wa kutosha
 
Nimekuelewa kidogo na ninaona kuna logic kwenye comment yako. Ila kama hutojali naomba ufafanue zaidi kuhusu Natural balance na kwa jinsi gani itasaidia kuleta balance katika demand na supply ya labour...Karibu.
Mleta mada, huoni kuwa hata utaratibu wako wa kuwagawa wanafunzi katika makundi hayo bado upo uwezekano kila baada ya muda mfupi kila kundi likajaa watu wa aina yake na hivyo tukarudi palepale?

Hoja hapa ni kuwa Skills bado ni muhimu, natural selection italazimisha kila kundi liwe na watu wa skill fulani wanayoendana nayo, kwa hiyo mambo yatajibalance
 
Uchambuzi mzuri sana! Kuna wakati niliipata bahati ya kushiriki mjadala kuhusu elimu ya Tanzania na wadau muhimu kabisa wa elimu na ambao kimsingi wana dhamana kubwa ya kuangalia ubora wa elimu katika shule zetu hizi

Maoni yangu yalifanana kwa kiasi fulani na ulichokisema kuhusu elimu msingi iwe hadi kidato Cha nne.

Baada ya darasa la saba wote waende kidato Cha kwanza halafu wakifika form two kwenye mtihani wa Taifa wafanye tathimini ya kina na yenye uhalisia ili wanaopata division one na two waendelee na kidato Cha tatu katika michepuo wanayoihitaji

Wale wa division three waandaliwe utaratibu wa kuhamishiwa vyuo vya kati kulingana na fani aipendayo mwanafunzi Kama ni ICT, RECORDS MNG, UMEME, NK

Halafu wale wa division four na zero waandaliwe utaratibu wa kupelekwa VETA nao katika fani wanazohitaji

Nilijenga hoja yangu katika Mambo mawili;

Kwanza ukiangalia wanaofeli darasa la saba siku hizi ni asilimia ndogo sana na ukifuatilia vizuri hawatofautiana kiuwezo na asilimia kubwa ya wanaochaguliwa. Yaani ukichimba zaidi utakuta sababu zilizowafanya wasichaguliwe ni uhaba wa madarasa na madawati wala sio uwezo. Kwasababu siku hizi wapo wanafunzi wengi wanapelekwa Kidato Cha kwanza hawajui kuandika 'my name is...' badala yake anaandika "mai nemu izi...."

Pili, baada ya kumaliza kidato Cha nne kundi kubwa sana linarudi mtaani na hapo ndo waliowengi ndio mwisho wao maana baada ya kidato Cha nne serikali inabaki na wale waliofaulu hawa wengine waliofeli hawana uangalizi au ufuatiliaji rasmi wa serikali tena

Nilichojibiwa kilinishangaza kwani ilionekana naongea kitu ambacho HAKIWEZEKANI KABISAA!

Baadae mjumbe mmoja akaniunga mkono kwa kuboresha kwamba hilo lifanyike baada ya kidato Cha nne kwa kutoa hoja ya umri. Kwamba kidato Cha tatu wanakuwa bado wadogo kuhimili mitaala ya vyuo vya Kati

Hata hivyo hoja hiyo Mimi sikuiona Kama ni ya msingi kwasababu naamini mtoto akikua anajifunza anachokipenda ndo anakuwa mahili zaidi

Itoshe kusema tu Kuna baadhi ya wadau wa elimu hawako tayari kupokea mabadiliko. Wanaogopa sana mabadiliko ila ulichoshauri ni kitu kizuri sana na chenye manufaa
umenena vyema sana mkuu..Tunahitaji mawazo kama haya ili angalau kupunguza tatizo la ajira ambalo kiuhalisia haliwezi kumalizika
 
Tulikuwa na shule za ufundi kama ifunda, moshi tech, Arusha tech, mbeya tech hizi tuliziua na nyingine ziligeuzwa vyuo lakini wanafunzi walitoka wakiwa na ujuzi kamili.
Binafsi nimesoma shule ya kilimo o level tulifundishwa vitu vingi kuanzia soil science, livestock keeping, agro mechanics, rural economy, bee keeping, fishing ni knowledge ambazo zinamsaidia mwanafunzi akimaliza shule changamoto kuna baadhi ya topic kama soil science hazina walimu wa kutosha
Nakumbuka hata dada yangu kipindi anasoma secondary miaka ya 2003 alikuwa anasoma na somo la agriculture....sijui imeishia wapi hii...asante kwa mchango wako.
 
Nakumbuka hata dada yangu kipindi anasoma secondary miaka ya 2003 alikuwa anasoma na somo la agriculture....sijui imeishia wapi hii...asante kwa mchango wako.
Haya mambo yanayoletwa jukwaa la kilimo sijui namna ya kulima vitunguu, nyanya, mapapai au ufugaji kuku, mbuzi , ng'ombe, ufugaji nyuki, samaki mpaka utengenezaji mabwawa ya samaki yote tulikuwa tunafundishwa darasani
 
Natambua na nathamini sana mawazo ya Mh. Rais ya kubadili mitaala yetu ya elimu ili kuwawezesha vijana kupata elimu ujuzi itakayowasaidia kujiajiri na kuajiri watu wengine.

Licha ya umuhimu wa elimu ya ufundi katika kutatua tatizo hili, bado elimu hii hii ya ufundi inaweza kuturudisha kule kule kwenye tatizo la ukosefu wa ajira na vipato kwa vijana endapo tu baadhi ya mambo ambayo yanapaswa kwenda sambamba na elimu ya ufundi hatutayapa kipaumbele au 'tutayasahau'.

Kwanini nasema hivi:
Naomba tuutazame utekelezaji wa elimu ya ujuzi na matokeo yake kwa miaka ya baadae ( Long run). Ninaamini, tukianza utoaji wa elimu kwa mitaala mipya (elimu ya ujuzi) baada ya miaka mingi (10 au 15) kutakuwa na matokeo haya:-

1. Idadi ya vijana wenye ujuzi katika ufundi wa taaluma mbalimbali kama umeme, ujenzi, magari na ufundi au ujuzi mwingine wa aina hiyo itakuwa imeongezeka sana kama jinsi ambavyo degree zimejaa leo hii. Hii itafanya katika kila kundi la vijana 10, basi 6 au 5 kati yao wana ujuzi au ufundi kutoka vyuoni.

2. Hii itapelekea hata ndani ya familia au jamii kuwe na vijana ambao pengine wamesoma ufundi unaofanana kama ilivyo leo ambapo ndani ya familia moja unakuta kuna watu wenye fani za uhasibu wapo 3. Au ndani ya mtaa mmoja unakuta watu wenye ujuzi wa maswala ya umeme wapo hata 9 au zaidi. Sasa je, ni nani atahitaji huduma kutoka kwa mwingine? ni kwa namna gani ujuzi utawasaidia hawa wasomi kujipatia kipato chao ikiwa kila mtu ana utaalamu wa hicho kitu?

Bila shaka, baada ya miaka mingi kupita (LONG RUN), tunaweza kurudi kulekule ambapo vijana wana elimu au ujuzi ambao hauwasaidii kwa namna ya kujiingizia kipato kwa sababu wasomi au wajuzi wa fani hizo watakuwa wamejaa.

Maoni kuhusu nini kifanyike ili elimu ya ujuzi iwe na tija tunayoitarajia
Binafsi, ningependa kushauri yafuatayo ambayo inabidi yaende sambamba na mitaala hii mipya ya elimu ili kuja kusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira nchini kwa miaka mingi ijayo:-

1. Elimu ya msingi/lazima iwe hadi kidato cha nne.
Elimu ya kidato cha nne iwe ni ya lazima ili kumjenga kifikra mwanafunzi. Baada ya matokeo ya kidato cha nne, mgawanyo wa wanafunzi ufanyike kama ifuatavyo. Wale waliopata ufaulu mkubwa hasa DIVISION ONE tu ndio waendelee na kidato cha tano na sita hadi chuo kikuu kwa hii mitaala ya kawaida katika fani muhimu kama afya, ualimu, uchumi, sheria, biashara, kilimo, uhandisi n.k. Hili kundi litaandaliwa ili kuja kuwa wasimamizi au waajiriwa katika fani hizi. Na ni vema kuchukua Division one pekee ili kuzuia SURPLUS ya wataalamu kwenye fani hizi ukilinganisha na soko la ajira.

DIVISION TWO NA THREE hawa waende moja kwa moja katika vyuo vya ufundi katika fani mbalimbali kama umeme, kilimo, uchongaji, ushonaji,ujenzi n.k ili kutengeneza wataalamu ambao watasaidia kujiajiri na kutengeneza ajira kwa wasimamizi wale juu.

DIVISION 4 NA ZERO kwa utafiti wangu mdogo, asilimia kubwa ya wanafunzi kwenye kundi hili, huwa sio wazuri kwenye masomo na muda wao mwingi wanautumia kwenye fani wazipendazo. Hapa inatakiwa kuwe na shule maalumu za michezo na Sanaa kama mziki, uigizaji, uchongaji n.k ili kuwasaidia hawa kupata ujuzi zaidi katika fani zao. Hapa tutazalisha wasanii wazuri ambao watapata fursa mbali mbali ndani na nje ya nchi na kutengeneza ajira kwa wengine. Nadhani tukipata wasanii 15 kama Diamond, kuna ajira nyingi zitazalishwa na hii inawezekana mbona Nigeria kuna wasanii wengi wakubwa. Na wale wasanii ambao hwatakuwa wakubwa basi angalau watakuwa na kipato cha kuendesha maisha yao kwa uhakika.

NB: Kuwe na shule maalum za vipaji mbalimbali kama soka, netball, tennis, ngumi n.k. Tukiwafundisha watoto wenye fani hizi kuanzia chini basi ni rahisi kuzalisha akina samatta, hasheem thabit, mwakinyo na wengine wengi kimataifa. INAWEZEKANA.

2. Uboreshaji maslahi ya watumishi wa umma.
Hili kundi likiweza kufanyiwa haya, litaweza kuhitaji huduma kama kujengewa nyumba mpya, umeme na huduma zingine za kiufundi ambapo vijana wetu waliosoma VETA kupitia kujiajiri kwao watauza huduma kwa kundi hili. Bila hivyo, vijana wetu wenye ujuzi wataishia kukosa sehemu ya kuuza ujuzi wao.

3. Tax exemption na Grace periods kwa wawekezaji wadogo wadogo.
Vijana wengi wana ideas na wana taka kuwekeza na kukuza biashara zao. Ila tatizo linakuwa kodi ambazo zingine wanatakiwa kuanza kuzilipa hata kabla ya kuanza kusimama vizuri. Kukiwa na tax exemption kwa kipindi Fulani, itasaidia kukuza biashara hizi na kuzalisha ajira nyingi sana kwa wengine na kuajiri hata vijana wetu wa VETA. Hii iende pamoja na uongezaji wa utoaji mikopo isiyo na riba kwa vijana huku serikali ikifatilia kuhakikisha mikopo hiyo/mitaji inatumika na kuleta matokeo yaliyotarajiwa.

4. Mazingira mazuri ya uwekezaji hasa kwa wawekezaji wa nje.
Kundi hili linauwezo wa kuzalisha ajira nyingi kwa wakati mmoja. Hili halihitaji maelezo mengi maana mifano ni mingi na nashukuru Mh. Rais ameliwekea msisitizo mkubwa.

5. Mazingira mazuri kwa asai za kiraia.
Asasi za kiraia (NGOs) zina mchango kubwa sana katika kuzalisha ajira kwa watu wengi. Kuna NGOs nyingi sana ambazo zinatoa ajira kwa wengi na kuisaidia serikali. Na faida nyingine hizi asasi zinasaidia jamii kwa kutatua kero za beneficiaries wao. Ushauri wangu ni kwa serikali kuzisimamia hizi asasi ili ziweze kufanya kazi zao kwa ufanisi kwa kufata sheria, taratibu na kanuni za nchi na pia kufanya shughuli zao kwa UFANISI kama zilivyo kwenye documents zao za usajili.

6. Family Planning
Hapa nashauri mkazo uwekwe ili kuweza kuwa na idadi ya watu ambayo inaendana na rasilimali zilizopo. Kila mwaka idadi ya watoto wanaoanza shule inaongezeka kwa sababu watoto wanaozaliwa ni wengi sana. Hata tukitoa elimu ya ufundi kuanzia darasa la saba, bado tutakuwa na vijana wenye ujuzi huku wakibaki tegemezi kwa kukosa sehemu ya kufanya kazi au kuuza ujuzi wao maana idadi yao ni kubwa sana. Ni vyema tukaweka mkazo mkubwa katika agenda hii pia.

7. Mifumo mizuri ya ukusanyaji kodi.
Naunga mkono kama ambavyo mh. Rais anasisitiza uwepo wa mifumo mizuri ya ukusanyaji wa kodi na matumizi ya pesa za umma. Asilimia kubwa ya mambo niliyoshauri yanahitaji uwezo mzuri wa serikali kiuchumi. Huwezi kutoa tax exemption kwa vijana kama huna pato la kutosha. Huwezi kujenga vyuo vya ufundi kama huna pato la kutosha. Basi mifumo ya ukusanyaji na usimamizi wa kodi iboreshwe.

8. Ubanaji wa matumizi ya serikali.
Mbinu za ubanaji na upunguzaji matumizi ya serikali zipo na ambazo zinaweza kutumika ili pesa hiyo ikatumike katika moja ya mambo niliyoyagusia hapo juu ili kuleta tija katika elimu yetu ya ufundi. Tunaweza punguza idadi ya wabunge na wawakilishi na kupunguza mishahara yao na posho, na pia tukaamua nafasi moja kati ya Mkuu wa wilaya au mkurugenzi wa halmashauri ikavunjwa. Na tukafanya mengi kama alivyofanya Mwendazake kuvunja Halimashauri ya Jiji la DSM ili kubana matumizi na kuleta maendeleo kwa watanzania.

MWISHO
Elimu ya ufundi ni muhimu na ina tija ila nina amini itakuwa na tija Zaidi endapo hayo niliyoyashauri na mengine mazuri yaliyo/yatakayoshauriwa na wengine yatasimamiwa vema na kupewa kipaumbele sambamba na mitaala yetu mipya ambayo ni mizuri ili kupata matokeo chanya in LONG RUN.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA – Kazi Iendelee.​
Mleta mada,
Ulichoobgea sio kipya hivyo ndio ilikua zamani. Hiyo ndio ilya system ya Mwalimu Nyerere, imekuja kubadilika kipindi cha JK.
 
Tulikuwa na shule za ufundi kama ifunda, moshi tech, Arusha tech, mbeya tech hizi tuliziua na nyingine ziligeuzwa vyuo lakini wanafunzi walitoka wakiwa na ujuzi kamili.
Binafsi nimesoma shule ya kilimo o level tulifundishwa vitu vingi kuanzia soil science, livestock keeping, agro mechanics, rural economy, bee keeping, fishing ni knowledge ambazo zinamsaidia mwanafunzi akimaliza shule changamoto kuna baadhi ya topic kama soil science hazina walimu wa kutosha
Well said my friend!!!

Naona Serikali inachukulia kama fashion tu kuanzisha vyuo vikuu, huu ni ushamba eti!!. Kulikuwa na vyuo vingi sana vya ufundi vilivyokuwa na manufaa sana kwa jamii lakini most if them vimegeuzwa kuwa vyuo vikuu huu ni ulimbukeni eti.

Angalia, ni kweli kabisa kulikuwa na vyuo kama Mbeya tech, Moshi tech, Mtwara tech, Arusha tech n.k lakini kati ya hivi vyuo vimegeuzwa vyuo vikuu. Kuvi-equip hivi vyuo ingesaidia sana.

Zamani hata kwenye shule za msingi kulikuwa na somo la ufundi walikuwa wanafanya mpaka practical lakini siku hizi hakuna kitu kama hicho hii ilikuwa inawasaidia sana vijana kuanza kupata utaalamu tangia wakiwa chini.

Prof. Ndalichako hili nijukumu lako la kuishauli Serikali ktk nyanja mbalimbli za elimu hapa nchini ili kuendana na uhalisia na kupunguza suala la tatizo la ajira kwa vijana.

Andaa kikao na wadau wa elimu ili wakupe mawazo mbadala. Kusema tumejenga madarasa mengi haitusaidii kama hauna mkakati wa kuboresha elimu inayotolewa kuendana na mazingira yaliyopo.

Vyuo kama; Mulutungulu, Tandala, Bugando TTC, Bustani, Mpuguso, n.k viko wapi siku hizi? Je Serikali imefanya juhudi zozote kuviboresha hivi vyuo ili visaidie kutoa wataalamu?

Asante!
 
Natambua na nathamini sana mawazo ya Mh. Rais ya kubadili mitaala yetu ya elimu ili kuwawezesha vijana kupata elimu ujuzi itakayowasaidia kujiajiri na kuajiri watu wengine.

Licha ya umuhimu wa elimu ya ufundi katika kutatua tatizo hili, bado elimu hii hii ya ufundi inaweza kuturudisha kule kule kwenye tatizo la ukosefu wa ajira na vipato kwa vijana endapo tu baadhi ya mambo ambayo yanapaswa kwenda sambamba na elimu ya ufundi hatutayapa kipaumbele au 'tutayasahau'.

Kwanini nasema hivi:
Naomba tuutazame utekelezaji wa elimu ya ujuzi na matokeo yake kwa miaka ya baadae ( Long run). Ninaamini, tukianza utoaji wa elimu kwa mitaala mipya (elimu ya ujuzi) baada ya miaka mingi (10 au 15) kutakuwa na matokeo haya:-

1. Idadi ya vijana wenye ujuzi katika ufundi wa taaluma mbalimbali kama umeme, ujenzi, magari na ufundi au ujuzi mwingine wa aina hiyo itakuwa imeongezeka sana kama jinsi ambavyo degree zimejaa leo hii. Hii itafanya katika kila kundi la vijana 10, basi 6 au 5 kati yao wana ujuzi au ufundi kutoka vyuoni.

2. Hii itapelekea hata ndani ya familia au jamii kuwe na vijana ambao pengine wamesoma ufundi unaofanana kama ilivyo leo ambapo ndani ya familia moja unakuta kuna watu wenye fani za uhasibu wapo 3. Au ndani ya mtaa mmoja unakuta watu wenye ujuzi wa maswala ya umeme wapo hata 9 au zaidi. Sasa je, ni nani atahitaji huduma kutoka kwa mwingine? ni kwa namna gani ujuzi utawasaidia hawa wasomi kujipatia kipato chao ikiwa kila mtu ana utaalamu wa hicho kitu?

Bila shaka, baada ya miaka mingi kupita (LONG RUN), tunaweza kurudi kulekule ambapo vijana wana elimu au ujuzi ambao hauwasaidii kwa namna ya kujiingizia kipato kwa sababu wasomi au wajuzi wa fani hizo watakuwa wamejaa.

Maoni kuhusu nini kifanyike ili elimu ya ujuzi iwe na tija tunayoitarajia
Binafsi, ningependa kushauri yafuatayo ambayo inabidi yaende sambamba na mitaala hii mipya ya elimu ili kuja kusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira nchini kwa miaka mingi ijayo:-

1. Elimu ya msingi/lazima iwe hadi kidato cha nne.
Elimu ya kidato cha nne iwe ni ya lazima ili kumjenga kifikra mwanafunzi. Baada ya matokeo ya kidato cha nne, mgawanyo wa wanafunzi ufanyike kama ifuatavyo. Wale waliopata ufaulu mkubwa hasa DIVISION ONE tu ndio waendelee na kidato cha tano na sita hadi chuo kikuu kwa hii mitaala ya kawaida katika fani muhimu kama afya, ualimu, uchumi, sheria, biashara, kilimo, uhandisi n.k. Hili kundi litaandaliwa ili kuja kuwa wasimamizi au waajiriwa katika fani hizi. Na ni vema kuchukua Division one pekee ili kuzuia SURPLUS ya wataalamu kwenye fani hizi ukilinganisha na soko la ajira.

DIVISION TWO NA THREE hawa waende moja kwa moja katika vyuo vya ufundi katika fani mbalimbali kama umeme, kilimo, uchongaji, ushonaji,ujenzi n.k ili kutengeneza wataalamu ambao watasaidia kujiajiri na kutengeneza ajira kwa wasimamizi wale juu.

DIVISION 4 NA ZERO kwa utafiti wangu mdogo, asilimia kubwa ya wanafunzi kwenye kundi hili, huwa sio wazuri kwenye masomo na muda wao mwingi wanautumia kwenye fani wazipendazo. Hapa inatakiwa kuwe na shule maalumu za michezo na Sanaa kama mziki, uigizaji, uchongaji n.k ili kuwasaidia hawa kupata ujuzi zaidi katika fani zao. Hapa tutazalisha wasanii wazuri ambao watapata fursa mbali mbali ndani na nje ya nchi na kutengeneza ajira kwa wengine. Nadhani tukipata wasanii 15 kama Diamond, kuna ajira nyingi zitazalishwa na hii inawezekana mbona Nigeria kuna wasanii wengi wakubwa. Na wale wasanii ambao hwatakuwa wakubwa basi angalau watakuwa na kipato cha kuendesha maisha yao kwa uhakika.

NB: Kuwe na shule maalum za vipaji mbalimbali kama soka, netball, tennis, ngumi n.k. Tukiwafundisha watoto wenye fani hizi kuanzia chini basi ni rahisi kuzalisha akina samatta, hasheem thabit, mwakinyo na wengine wengi kimataifa. INAWEZEKANA.

2. Uboreshaji maslahi ya watumishi wa umma.
Hili kundi likiweza kufanyiwa haya, litaweza kuhitaji huduma kama kujengewa nyumba mpya, umeme na huduma zingine za kiufundi ambapo vijana wetu waliosoma VETA kupitia kujiajiri kwao watauza huduma kwa kundi hili. Bila hivyo, vijana wetu wenye ujuzi wataishia kukosa sehemu ya kuuza ujuzi wao.

3. Tax exemption na Grace periods kwa wawekezaji wadogo wadogo.
Vijana wengi wana ideas na wana taka kuwekeza na kukuza biashara zao. Ila tatizo linakuwa kodi ambazo zingine wanatakiwa kuanza kuzilipa hata kabla ya kuanza kusimama vizuri. Kukiwa na tax exemption kwa kipindi Fulani, itasaidia kukuza biashara hizi na kuzalisha ajira nyingi sana kwa wengine na kuajiri hata vijana wetu wa VETA. Hii iende pamoja na uongezaji wa utoaji mikopo isiyo na riba kwa vijana huku serikali ikifatilia kuhakikisha mikopo hiyo/mitaji inatumika na kuleta matokeo yaliyotarajiwa.

4. Mazingira mazuri ya uwekezaji hasa kwa wawekezaji wa nje.
Kundi hili linauwezo wa kuzalisha ajira nyingi kwa wakati mmoja. Hili halihitaji maelezo mengi maana mifano ni mingi na nashukuru Mh. Rais ameliwekea msisitizo mkubwa.

5. Mazingira mazuri kwa asai za kiraia.
Asasi za kiraia (NGOs) zina mchango kubwa sana katika kuzalisha ajira kwa watu wengi. Kuna NGOs nyingi sana ambazo zinatoa ajira kwa wengi na kuisaidia serikali. Na faida nyingine hizi asasi zinasaidia jamii kwa kutatua kero za beneficiaries wao. Ushauri wangu ni kwa serikali kuzisimamia hizi asasi ili ziweze kufanya kazi zao kwa ufanisi kwa kufata sheria, taratibu na kanuni za nchi na pia kufanya shughuli zao kwa UFANISI kama zilivyo kwenye documents zao za usajili.

6. Family Planning
Hapa nashauri mkazo uwekwe ili kuweza kuwa na idadi ya watu ambayo inaendana na rasilimali zilizopo. Kila mwaka idadi ya watoto wanaoanza shule inaongezeka kwa sababu watoto wanaozaliwa ni wengi sana. Hata tukitoa elimu ya ufundi kuanzia darasa la saba, bado tutakuwa na vijana wenye ujuzi huku wakibaki tegemezi kwa kukosa sehemu ya kufanya kazi au kuuza ujuzi wao maana idadi yao ni kubwa sana. Ni vyema tukaweka mkazo mkubwa katika agenda hii pia.

7. Mifumo mizuri ya ukusanyaji kodi.
Naunga mkono kama ambavyo mh. Rais anasisitiza uwepo wa mifumo mizuri ya ukusanyaji wa kodi na matumizi ya pesa za umma. Asilimia kubwa ya mambo niliyoshauri yanahitaji uwezo mzuri wa serikali kiuchumi. Huwezi kutoa tax exemption kwa vijana kama huna pato la kutosha. Huwezi kujenga vyuo vya ufundi kama huna pato la kutosha. Basi mifumo ya ukusanyaji na usimamizi wa kodi iboreshwe.

8. Ubanaji wa matumizi ya serikali.
Mbinu za ubanaji na upunguzaji matumizi ya serikali zipo na ambazo zinaweza kutumika ili pesa hiyo ikatumike katika moja ya mambo niliyoyagusia hapo juu ili kuleta tija katika elimu yetu ya ufundi. Tunaweza punguza idadi ya wabunge na wawakilishi na kupunguza mishahara yao na posho, na pia tukaamua nafasi moja kati ya Mkuu wa wilaya au mkurugenzi wa halmashauri ikavunjwa. Na tukafanya mengi kama alivyofanya Mwendazake kuvunja Halimashauri ya Jiji la DSM ili kubana matumizi na kuleta maendeleo kwa watanzania.

MWISHO
Elimu ya ufundi ni muhimu na ina tija ila nina amini itakuwa na tija Zaidi endapo hayo niliyoyashauri na mengine mazuri yaliyo/yatakayoshauriwa na wengine yatasimamiwa vema na kupewa kipaumbele sambamba na mitaala yetu mipya ambayo ni mizuri ili kupata matokeo chanya in LONG RUN.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA – Kazi Iendelee.​
Bahati mbaya naona hujui msingi mkuu wa taaluma ya ufundi, ni hesabu. Ukiwachukua waliopata div 2 na kushuka na kuwapeleka kusomea taaluma ya ufundi bila kigezo cha hesabu utaleta shida kwa wafundishaji na kupata wahitimu wa kubumba. Ni kweli mitaala imevurugwa na nchi haina dira kwa upande wa elimu. Ni wajibu wa serikali kuwatumia wataalamu wake wa elimu na kuona ni lipi la kufanya kuuokoa mfumo wa elimu uliovurugwa.
 
Bahati mbaya naona hujui msingi mkuu wa taaluma ya ufundi, ni hesabu. Ukiwachukua waliopata div 2 na kushuka na kuwapeleka kusomea taaluma ya ufundi bila kigezo cha hesabu utaleta shida kwa wafundishaji na kupata wahitimu wa kubumba. Ni kweli mitaala imevurugwa na nchi haina dira kwa upande wa elimu. Ni wajibu wa serikali kuwatumia wataalamu wake wa elimu na kuona ni lipi la kufanya kuuokoa mfumo wa elimu uliovurugwa.
asante
 
Tulikuwa na shule za ufundi kama ifunda, moshi tech, Arusha tech, mbeya tech hizi tuliziua na nyingine ziligeuzwa vyuo lakini wanafunzi walitoka wakiwa na ujuzi kamili.
Binafsi nimesoma shule ya kilimo o level tulifundishwa vitu vingi kuanzia soil science, livestock keeping, agro mechanics, rural economy, bee keeping, fishing ni knowledge ambazo zinamsaidia mwanafunzi akimaliza shule changamoto kuna baadhi ya topic kama soil science hazina walimu wa kutosha
Sema wewe kiazi, mimi mhogo nitaambiwa nina mizizi. Asante sana. Mengi ya mambo yanapigiwa kelele na kusifiwa sasa hivi yalifanyika miaka ya nyuma kipindi cha mwalimu. Waafrika tu watu wa nadharia zaidi. Maneno na mipango mingi lakini utelezaji hamna. Hata nchi nzima wananchi wangejua ufundi bila mipango ya vitendo tuwatumieje hao mafundi ni kelele tu.
 
Bahati mbaya naona hujui msingi mkuu wa taaluma ya ufundi, ni hesabu. Ukiwachukua waliopata div 2 na kushuka na kuwapeleka kusomea taaluma ya ufundi bila kigezo cha hesabu utaleta shida kwa wafundishaji na kupata wahitimu wa kubumba. Ni kweli mitaala imevurugwa na nchi haina dira kwa upande wa elimu. Ni wajibu wa serikali kuwatumia wataalamu wake wa elimu na kuona ni lipi la kufanya kuuokoa mfumo wa elimu uliovurugwa.
Lakini mkuu..bado waliopata div two na three wengi miongoni wengi wana idea ya hesabu..so sidhani kama ni tatizo..ndio maana hata vijana waliomaliza darasa la 7 wakienda veta wanapata ujuzi so mtu wa divisio 2 na 3 inakuwa ni rahisi zaidi...pengine una maelezo mazuri nikakuelewa zaidi.
 
Ushauri wako utakua umekosa mana endapo hujazungumzia 'Uboreshaji wa sekta ya AFYA'...AFYA nimuhimu sana kuliko yote hayo...ongeza kitu hiyo
 
Back
Top Bottom