Elimu ya uumbaji binadamu bila kujamiiana

Elimu ya uumbaji binadamu bila kujamiiana

Mshana Jr Hii ya Mandela ukisikiliza historia vizuri na baadhi ya ithibati kutoka kwao ikiwemo Ithibati kutoka kwa Winnie mwenyewe alieleza vizuri kuhusu utjfauti wa mandela wa zamani na mpya
Na kupewa nchi ni kwa sababu Mandela yule hakukubali kuwa chini ya wazungu hivyo waliclone ili wapate mandela ataenda sawa na matakwa yao na walifanikiwa na wakampachika urais
 
Mwanzo nilikuelewa ila ulipofika kwa madiba nimegundua unatumia kitu Cha Arusha
Hahahaha mkuu yaani kama tulikuwa tunasoma wote vile mi mwenyewe mwanzo wakati nasoma alipo anza mambo ya mbegu za mahindi nilikuwa namuelewa alipo fika kwa Mandela nikajua ndiyo wale wazee wa stor za kwenye Gahawa na kucheza bao.
 
Mshana Jr Hii ya Mandela ukisikiliza historia vizuri na baadhi ya ithibati kutoka kwao ikiwemo Ithibati kutoka kwa Winnie mwenyewe alieleza vizuri kuhusu utjfauti wa mandela wa zamani na mpya
Na kupewa nchi ni kwa sababu Mandela yule hakukubali kuwa chini ya wazungu hivyo waliclone ili wapate mandela ataenda sawa na matakwa yao na walifanikiwa na wakampachika urais
Sawa lakini baada ya kifo chake na muda kupita kila kitu kingewekwa wazi.. Labda tuupe muda wakati lakini jamani jela kusikieni hivi hivi hasa ukifungwa muda mrefu lazima ubadilike

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa lakini baada ya kifo chake na muda kupita kila kitu kingewekwa wazi.. Labda tuupe muda wakati lakini jamani jela kusikieni hivi hivi hasa ukifungwa muda mrefu lazima ubadilike

Sent using Jamii Forums mobile app
Unajua hata Dot la usoni likuwa kulia baada ya kutoka jela likawa kushoto
FuACia2WwAAktCY.jpg
 
Kwahiyo mwamba sisi hutuamini??😂😂
Get serious man.... kama kichwa yako haifanyi kazi sawasawa!.....

Waza hata Kwa kutumia kalio lako Moja tu!... Hata la kushoto tu....

Hivi.... how can you implant a soul... to a clone...!? Na hiyo clone isurvive!?.....

Ina maana kuna binadamu siku hizi wanatoa pumzi ya uhai kwa binadamu wengine!?...to live as a clone!?

Kusingekuwa na kifo basi...!

Ungeniambia mamidoli ya Elon musk kama clone... hapo tungeelewana.
 
Kuamini upuuzi kama huu kwa karne hii ni UJINGA kama ujinga mwingine

Huu ujinga tulikuaga tunaaminishwa tukiangalia movies enzi hizooooo
 
ELIMU YA UUAMBAJI BINADAMU BILA KUJAMIIANA (CLONING)

Mchakato wa uumbaji wa binadamu bila kujaamiana (Cloning) ulianza mwaka 1938 na wanajeshi wa Nazi chini ya kamanda Hitler. Ian Wilmut muasisi wa uuambaji wa kondoo aitwaye Dolly, raia wa London nchini Uingereza alipata upinzani mkali baada ya kumuumba kondoo huyo akiwa na timu yake ya wanasayansi.

Alifariki akiwa na miaka 79 kwa ugonjwa wa kukakamaa yaani "Parkinson's" aliougua kwa muda mrefu, kilieleza chanzo toka Chuo Kikuu cha Edinburg nchini Scotland. Wilmut aliibua mjadala mkali juu ya maadili ya kuwaumba viumbe bila kujaamiana mara alipotangaza kwamba yeye na timu yake ya taasisi ya Baiolojia kwa wanyama ya Roslin wamemuumba mwanakondoo kwa kutumia seli za kiini kutoka kwa kondoo mkubwa, na mwanakondoo huyo akapewa jina la Dolly, kutokana na jina la mwanamuziki Dolly Parton.

Uuambaji wa mwanakondoo ulikuwa ni wa awali kwa wanasayansi, kupevusha seli za kiumbe mkubwa na kufanya kazi kama seli za kiumbe mkubwa na kuzaa kiinitete walio sawa. Uumbaji wa Dolly ulianzisha mapinduzi ya kisayansi kwa wanasayansi wengi, wakiwemo wakosoaji kuwa jambo hilo sio maadili ya kibinadamu.

Mwaka huohuo Rais wa marekani Billy Clinton akapiga marufuku matumizi ya Fuko la fedha la Shirikisho kwaajili ya uumbaji wa binadamu bila kujaamiana (Cloning), kazi zote za utafiti wa 'cloning' zikasimamishwa, kazi ya Wilmut iliwasukuma wanasayansi wengi kuumba wanyama wengineo.

Mwaka 1996 Niki Minaji ali"tweet" maombi yake kuwa "Acheni uumbaji wa binadamu" aliifuta meseji hiyo lakini wengi tayari walishai "screenshot".

Madaktari wa Illuminati wanashindwa kumpandikiza mtu akili kwa 100% inayowafuata wao kwa kila kitu, kwa sababu teknolojia hiyo ilianza mwaka 2015, hivyo kwa 95% tu ndio wanaweza kuwadhibiti lakini huko nyuma ilikuwa ni 85% tu kuwadhibiti kwa sababu ni binadamu na sio roboti, kwakuwa anatokana na viasili na vinasaba vya mtu, hivyo huwezi kumdhibiti binadamu kwa 100% bali kwa 95% kwa teknolojia ya tangu mwaka 2015.

Hata kuku(Broilers) tunaowala wametoka kwenye mashine ya incubator (kutotoleshea vifaranga). Mbwa wale wa ndani wafupi wanaopendwa na dada zetu,nk Tuna mazao yanayotokana na GMO (Genetic Organism Modified) mbegu za kisasa, Mahindi (Stuka) kwa miezi mitatu, maharage,nk. Hivyo sayansi inakua na binadamu tunaendelea kuwaabudu watu waliotengenezwa bila kujua ni sawa na kuabudu miungu ya uongo. Hivyo hili la kuumba wanyama na watu sio kitu kigeni sana. Binadamu wanaumbwa na Illuminati ili kuwasaidia katika kurahisisha kazi zao na mipango yao.

"Cloning" ni kitendo cha kutengeneza kiumbe kipya labda binadamu au mnyama yoyote, anakuwa na mfanano na mtu au mnyama wa mwanzo ambaye ni halisi na kitendo hiki kinafanyika kwa kutumia vinasaba vya mtu halisi, kisha anatengenezwa mtu mwingine ambaye watafanana kwa asilimia 99.9 na anawekewa kumbukumbu zote kama za yule wa awali. Kitendo hiki hufanyika kwa kumuua binadamu halisi na kuutumia mwili wake uleule akiwa maabara au kuutengeneza mwili mwingine, lakini kumbukumbu zinarudi zilezile.
Vifo vya viumbe walioumbwa kwa 99% huwa mara nyingi ni kupooza na kupata kansa ya Ubongo.

Illuminati waliwahi kumuumba Mzee Madiba kuwa Gibson Makhanda, Dr Dre, Eminem, Niki Minaji, Will Smith, Arnold Vosloo kuwa Billy Zane, Nero wa Empaya ya Roma,nk.
Vyanzo vinaeleza Madiba alifariki Mei 8 mwaka 1985, akiwa na miaka 67, ndio maana wana sherehe inaitwa dakika 67 za Mandela, alipoingia jela alikuwa na kidoti upande wa kulia wa pua lakini alipotoka alikuwa na kidoti upande wa kushoto.

Mandela halisi alifungwa Jela baada ya kutaka kuingiza askari msituni ili kupambana na kuwaondoa Makaburu, hapo ndipo Makaburu wakamshika na kumfunga jela, lengo lilikuwa kuwaondoa kwa mtutu makaburu ili warudi kwao, alipotoka Jela akaja na sera za Amani kupinga ubaguzi, kuwa, watu weusi wasiwabugue makaburu na makaburu wasiwabague weusi, akakabidhiwa tuzo ya Amani na kupewa uraisi. Wazungu wakampa sifa duniani kuwa ni kiongozi bora Afrika na mpaka leo Duniani kote anatambulika kama shujaa wa Afrika.

Mandela aliumbwa"Cloned" na madaktari wa Illuminati na kujifanya Mandela halisi, walimuua akiwa gerezani, hivyo alikaa miaka 18 tu na kuuawa, ghafla wakagundua wamefanya kosa, kwani watu walikuwa wanamtaka Mandela wao atoke jela, hawakuwa na jinsi bali kumuumba Mandela mwingine ajifanye Mandela halisi.

Winnie Mandela aliwahi kulalamika kuwa "Mandela aliyekwenda gerezani alikuwa Mandela wamoto" "huyu aliyerudi toka visiwa vya Roben sio ninayemjua mimi" Baada ya Mandela kutoka Jela Winnie Mandela hakutaka kuendelea kuwa Kimapenzi na Mandela Feki maana siri nzima aliijua kwa hiyo ikatengenezwa namna kwa kukubaliana kwamba amechepuka halafu Mandela akapata hasira hivyo akampa Taraka.

Zuma ni mmoja wa wana ANC, wachache wanaoijua siri hii, ndio maana hakufungwa katika kesi zake, na hana hata cheti angalau cha Matriki, lakini alipewa Uraisi kwaajili ya kumfunga mdomo asiropoke juu ya uumbaji wa Mandela mpya.

Walinzi wake waliwahi kutoa siri nzito sana, kwamba; kuna siku walipokuwa wanamsindikiza Mandela jukwaani ili akatoe hotuba mara ghafla akapotea, kisha wakamuona yupo jukwaani akiongea, na hili limewatokea mara kadhaa. Walisema; wanashuku watawala waliwapa Mandela feki aliyeweza kuwa Gibson Makhanda mwenye makazi yake msumbiji, aliyekuwa na mahusiano na Gracia Marchell, lakini tuhuma hizo zilipewa jina la "Nadharia yenye njama" ili kuficha ukweli.

Jarida la mambo ya fasheni la kifaransa liliwahi kutoa picha za mtu anayeonekana kama Mandela, baadhi wakasema Mandela kaumbwa,"cloned". Mandela alikuwa na digrii ya juu kabisa ya 33 ya Illuminati, akiwa anasali Loji ya "Bloodthirsty order of the Knights " nchini Malta, wakina Rockefeller waliwahi kulifadhili jeshi la ANC, Umkontho "Spear of the Nation".

Mandela ana masanamu huko London, New York, kuliko kiongozi yeyote Afrika.

View attachment 2778478
Mtoa mada tueleweahe vizuri.

Clone ya eminem ilichukua muda gani toka kupandikizwa seli mpaka zikajimultiply na kuwa eminem mkubwa ?

Umetolea mfano wa mandela hapo kwamba alikuwa cloned,lakini ukamtaja mtu ambaye anadhaniwa kuwa gibson.

Sasa maana yake wakati mandela yupo nje hajafa means kwamba huyu bibson makhanda bado alikuwepo anaishi kama binadamu mwingine,hii ni clone gani ?

Kikawaida tumezoea kutoka mbegu kike na kiume ili ziweze kutoa mtu mwenye mwili(kitoto kichanga)basi ipite miezi tisa ndio kitatoka kitoto tena kidogo.

Sasa eminem kama alifanyiwa clone ama hii clone kutokea kupandikizwa mpaka kuwa jitu kubwa lenye mwili kama mtu wa miaka 30 inachukua muda gani ?
 
Mandela aliumbwa"Cloned" na madaktari wa Illuminati na kujifanya Mandela halisi, walimuua akiwa gerezani, hivyo alikaa miaka 18 tu na kuuawa, ghafla wakagundua wamefanya kosa, kwani watu walikuwa wanamtaka Mandela wao atoke jela, hawakuwa na jinsi bali kumuumba Mandela mwingine ajifanye Mandela halisi.
Hekaya za abunuwasi, zitasomwa kama masillmulizi ya kale.
 
Ofcz Mandelela ni clone, mwenyewe halis alijifia soon gerezani kwa mateso makali.

Ila hapo kwa Nik Minaji ku tweet 1996? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
96 Nick was 16' and tweeter founded 2004 launched to public ,2006! Mmmh hio tweet mwenyew hapana asee lakin kuhusu Eminem something is wrong somewhere..may be anatafutwa mtu mfanano inafanyika surgery hapo sawa
 
This is too low, unaweza geuza picha upande wowote. Angalia hapa chini;
View attachment 2861419
SIzungumzii Fliping mkuu ungekuwa Attentive to details ungenielewa zaidi anatomical Structure ya Eneo lililokuwa na Dot ni tofauti na eneo alilokuwa nalo kabla nazubgumzia upande wa eneo na sio flip photo...
Utetezi kama huu ni wa kitoto sana
 
SIzungumzii Fliping mkuu ungekuwa Attentive to details ungenielewa zaidi anatomical Structure ya Eneo lililokuwa na Dot ni tofauti na eneo alilokuwa nalo kabla nazubgumzia upande wa eneo na sio flip photo...
Utetezi kama huu ni wa kitoto sana
Ila hapa una unazungumzia conspiracy theory tu ambayo umesoma kwenye intenet na ukaamua kushare hapa, labda kama evidence unaweza share hapa.

Zaidi hapo ni story tu kama binadamu alikuwa nyani hapo kale.
 
Ila hapa una unazungumzia conspiracy theory tu ambayo umesoma kwenye intenet na ukaamua kushare hapa, labda kama evidence unaweza share hapa.

Zaidi hapo ni story tu kama binadamu alikuwa nyani hapo kale.
Unataka Evidence gani Mkuu...Forensic au?
 
Back
Top Bottom