Ellon Musk amdhihaki vibaya Zelensky

Ellon Musk amdhihaki vibaya Zelensky

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Katika hali inayoonesha mambo kuzidi kumgeukia Rais Zelensky wa Ukraine, tajiri mkubwa wa mawasiliano na aliyekuwa mfadhili mkubwa wa Ukraine Ellon Musk amemdhihaki kiongozi huyo kwa kumuonesha kama mtu ombaomba aliyepitiliza viwango.

Katika picha aliyoitengeneza na kuiweka kwenye akaunti yake, Ellon Musk amemchora Zelensky akiwa darasani na mwenye wasiwasi wa kama mwanafunzi anayetaka kuuliza swali.

Pembeni mwa picha hiyo Musk akamuuliza Zelensky imekuwaje zimepita dakika 5 na hajaomba dola bilioni.

Picha hiyo inayoitwa meme imewakasirisha sana wabunge wa Ukraine ambao wameanza kumjibu Ellon Musk na wao kujaribu kuchora vikatuni vyake.

Ukraine Hits Back at Elon Musk Over Meme Taunting Zelensky

1696398782144.png


Mkasa huu unamkuta Zelensky ikiwa ni siku chache tu bunge la Marekani kusitisha misaada zaidi kwa Ukraine maamuzi ambayo yamesababisha mvurugano kwenye bunge hilo mpaka kuondolewa kwa Spika wake Kevin McCarthy kwa kura maamuzi ambayo hayajawahi kufanyika katika historia ya Marekani.

Hilo pia linakuja wakati Uiengereza imetangaza haina tena silaha za kuipatia Ukraine na kama yuko mwengine anayeweza kuisaidia achukue nafasi yake.

Sambamba na hayo kuna vuguvugu kubwa Poland aliyekuwa rafiki mkubwa na muungaji mkono wa vita ambapo ajenda za uhusiano na Ukraine zikishika nguvu kuelekea uchaguzi wa Oktoba 15 ijayo.

Vyama vinavyopinga vita na kuisaidia Ukraine vimeonekana kupata uungwaji mkono mkubwa miongoni mwa wapiga kura,
 
Katika hali inayoonesha mambo kuzidi kumgeukia raisi Zelensky wa Ukraine,tajiri mkubwa wa mawasiliano na aliyekuwa mfadhili mkubwa wa Ukraine Ellon Musk amemdhihaki kiongozi huyo kwa kumuonesha kama mtu omba omba aliyepitiliza viwango.
Katika picha aliyoitengeneza na kuiweka kwenye akaunti yake,Ellon Musk amemchora Zelensky akiwa darasani na mwenye wasi wasi wa kama mwanafunzi anayetaka kuuliza swali.Pembeni mwa picha hiyo Musk akamuuliza Zelensky imekuwaje zimepita dakika 5 na hajaomba dola bilioni.Picha hiyo inayoitwa meme imewakasirisha sana wabunge wa Ukraine ambao wameanza kumjibu Ellon Musk na wao kujaribu kuchora vikatuni vyake.

Ukraine Hits Back at Elon Musk Over Meme Taunting Zelensky

View attachment 2771251
Mkasa huu unamkuta Zelensky ikiwa ni siku chache tu bunge la Marekani kusitisha misaada zaidi kwa Ukraine maamuzi ambayo yamesababisha mvurugano kwenye bunge hilo mpaka kuondolewa kwa spika wake Kevin McCarthy kwa kura maamuzi ambayo hayajawahi kufanyika katika historia ya Marekani.
Hilo pia linakuja wakati Uiengereza imetangaza haina tena silaha za kuipatia Ukraine na kama yuko mwengine anayeweza kuisaidia achukue nafasi yake.
Sambamba na hayo kuna vuguvugu kubwa Poland aliyekuwa rafiki mkubwa na muungaji mkono wa vita ambapo ajenda za uhusiano na Ukraine zikishika nguvu kuelekea uchaguzi wa Oktoba 15 ijayo.Vyama vinavyopinga vita na kuisaidia Ukraine vimeonekana kupata uungwaji mkono mkubwa miongoni mwa wapiga kura,
Zelensky dau linazama haraka. Ni malipo ya usaliti. Waukraine wote watalipa kuwasaliti warusi ndugu zao wa jadi.
 
Mgao wa umeme umeanza baada ya sa100 kuingia madarakani.
hapana hizi zote ni bom zilio tegenezwa kipindi kuanzia cha Mkapa, JK magufuli zinakuja kulipuka kwasasa, kwasbb mipango ya kua na umeme costant haifanywi dani ya miaka 3 au 2 kama ya Raisi samia, yeye amekua muazi na kuweka hali yote hadharani sio jpm aliofisha uozo wa tanesco
 
hapana hizi zote ni bom zilio tegenezwa kipindi kuanzia cha Mkapa, JK magufuli zinakuja kulipuka kwasasa, kwasbb mipango ya kua na umeme costant haifanywi dani ya miaka 3 au 2 kama ya Raisi samia, yeye amekua muazi na kuweka hali yote hadharani sio jpm aliofisha uozo wa tanesco
Kama unampenda sana huyu ajuz amia kwakwe ukawe shamba boy .serikali iliyofitinika ndo husingizia kila kitu badala ya kutatua changamoto, bwa la nyerere limefika waapi
 
Weka na majibu waliyompa Ukraine. Kupigwa za udo nyingi sana huyo Musk wenu
 
Ok, Sasa tumeelewena misaada imesitishwa kwa Zelensky, kwa hiyo Zelensky anavyoendelea kumtoa kamasi mvamizi Putin kwa muda wote unaofuta ni kwa nguvu zake mwenyewe, kwa hiyo hatutarajii kusikia warusi wa ikwiriri wakilialia hapa kwamba mvamizi anapambana na nchi nyingi, hivi Sasa ni Zele vs Mvamivazi kavukavu yaani.
 
Ok, Sasa tumeelewena misaada imesitishwa kwa Zelensky, kwa hiyo Zelensky anavyoendelea kumtoa kamasi mvamizi Putin kwa muda wote unaofuta ni kwa nguvu zake mwenyewe, kwa hiyo hatutarajii kusikia warusi wa ikwiriri wakilialia hapa kwamba mvamizi anapambana na nchi nyingi, hivi Sasa ni Zele vs Mvamivazi kavukavu yaani.
Alipokuwa akisaidiwa alishindwa.Vipi atashinda sasa.Ni muda wa kuinua mikono kusalimu amri.Hawezi kutoboa Roboynite wala Bakhmut.
 
Alipokuwa akisaidiwa alishindwa.Vipi atashinda sasa.Ni muda wa kuinua mikono kusalimu amri.Hawezi kutoboa Roboynite wala Bakhmut.
Ndo hainui Mikono Sasa, anaendelea kumchapa mvamizi kavukavu yeye peke yake.
 
Ok, Sasa tumeelewena misaada imesitishwa kwa Zelensky, kwa hiyo Zelensky anavyoendelea kumtoa kamasi mvamizi Putin kwa muda wote unaofuta ni kwa nguvu zake mwenyewe, kwa hiyo hatutarajii kusikia warusi wa ikwiriri wakilialia hapa kwamba mvamizi anapambana na nchi nyingi, hivi Sasa ni Zele vs Mvamivazi kavukavu yaani.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]wavaa kobazi, msuli,baraghashia,kilemba,wala tende yaani hawa ni wayemen kabisa!
 
Back
Top Bottom