Elon Musk angekuwa China asingeendeleza hivi vituko vyake yeye na Trump

Elon Musk angekuwa China asingeendeleza hivi vituko vyake yeye na Trump

Huyu tajiri Elon na tajiri mwenzake Trump waliovamia siasa na kuziendesha vile watakavyo wao sioni kama watakuwa na mwisho bora.

Kwa siasa za China Trump asingefika hata hapa alipofika tena huyu chawa wake Elon muda huu nina uhahika angekuwa Jack Ma wakimarekani.

Nakumbuka Jack Ma naye alianza tabia fulani za matajiri wanaovamia siasa za nchi sijui wakomunisti wale wa Beijing walimfanya nini mpaka leo amekuwa pole kweli.

Nachokumbuka kwa udogo Jack Ma aliwaponda viongozi wa serikali ya Beijing kwenye summit moja iliyofanyika China alipopewa nafasi ya kuzungumza aliwaponda Havana wa Bank ya China,naibu waziri wa fedha alikuwa mule na viongozi wengi wa serikali walikuwa mule hili lilikuwa kosa kubwa sana Jack Ma alifanya maybe fedha na umaarufu ulimchanganya na kuhisi China ni Amerika kilichofuatia sasa ilikuwa ni habari isiyovutia kwa Jack Ma na kwa baadhi ya makampuni yake hasa Ant group.

Sasa hii room anayopata Trump na mwenzake Musk kuvamia siasa na kuleta mambo yao jinsi wanavyo jisikia wao kwa China Elon angekutana na hatua ya hatari sana kutoka katika serikali.

Elon Musk ni rahisi sana yeye kuwaponda Venezuela mara Brazil mara Afrika kusini mara Ulaya na kuhamasisha juki,mapinduzi na ubaguzi lakini kwa China hajawahi kuthubutu kufanya maybe anajua reaction ya wakomunisti wa pale Beijing hawana muda wa kucheka na mjinga tofauti na hao wengine anao wachezea kama marekani.
Musk Ana biashara kubwa sana China. Hana jeuri kule.

Ni changamoto kubwa kwa utawala wa Trump unaoiona China kama ndiye adui mkubwa wa US.
 
Back
Top Bottom