Uchaguzi 2020 Embu tuambizane ukweli, CHADEMA inatumia kigezo gani kusema itashinda?

Uchaguzi 2020 Embu tuambizane ukweli, CHADEMA inatumia kigezo gani kusema itashinda?

Sababu kubwa ya Chadema kushinda ni kwa vile mgombea wa CCM hakubaliki kwa makundi mengi ya kijamii kama vile wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, wahitimu vyuo vikuu, bodaboda, mgombea wa CCM ni katili, mjivuni, mtu wa visasi na asiyewajali wananchi.
Hebu linganisha Magufuli wa 2015 na sasa, Magufuli wa 2015 alijipambanua kama mchapakazi lakini wa sasa anajipambanua kama katili, mjivuni na mwenye visasi.

Wingi wa watu kwenye mikutano ya wagombea hawa isikupe shida sana, wanaoenda kwenye mikutano ya CCM wanafuata mengi tukiachana na malori wengi hufuata wasanii, hukumbuki Clouds ilikuwa inajaza watu kwa kiingilio sasa ni bure kwanini watu wasijae. Tofauti yao ni kwamba wa Lissu ni wachangamfu na Magufuli wamesinyaaa na ukumbuke hao hao wanaoenda kwa Magufuli ndio wanaoenda kwa Lissu.

Kama alipata 57% kipindi kile tegemea kura zake kupungua kwa sababu kipindi kile aligombea akijipambanua kwa uchapakazi, hakuwa amewakera wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi wala wahitimu vyuo vikuu, kipindi kile hali ya Uchumi haikuwa mbaya, kipindi kile aligombea na mgombea mwenye tuhuma za ufisadi ambazo zilikuwa zinawakera Watanzania wengi, mgombea wa upinzani alikuwa dhaifu na ambae hakuwa na uwezo wa kujenga hoja na alikuwa ambae alitokana na chama cha mapinduzi sasa hivi upinzani wana mtu mwenye uwezo wa kujenga hoja na mpinzani halisi.
 
Ndio wapiga kura wenu?

IMG-20200928-WA0066.jpg
 
Wanakwambia"watu wamelala barabarani ili Lissu asimame aongee wamsikie,kweli Lissu ni Rais"

yani kwa watu kulala barabarani basi ndo kigezo cha Lissu kushinda urais. Chadema ndo matahira kweRi kweRi.
Tahira ni jamaa yenu maana sahivi aisindikiza tume wamfungi lisu asifanye kampeni.

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Ukweli lazima usemwe, CHADEMA wana asilimia chache sana za kuibuka na ushindi kwenye kinyang'anyiro hiki.

Wakati wa uboreshaji wa daftari la wapiga kura CCM ilikuwa ipo kwenye mkakati mkali was kuhakikisha wanachama wake wanajiandikisha au wanarekebisha taarifa zao kwenye daftari hilo

CDM wao walikuwa wanafurahia kususia zoezi hilo wakidhani kwamba wanaikomoa serikali, kitu cha kusikitisha ni kwamba, hata viongozi wao walikuwa wanawaunga mkono wasiende kujiandikisha, na wakati mwingine walikuwa wanatupia picha mitandaoni kwa furaha kabisa kuonesha uchache wa watu kwenye vituo.

Baya zaidi wengi wa wafuasi wa CHADEMA sio wapiga kura, we angalia tu kwenye mikutano yao wapiga kura utawajua na wahuni utawajua, wengi hawana hata vitambulisho vya mpiga kura, sasa huo ushindi unatokea wapi.

Hebu acheni kujifariji jamani, mambo sio mazuri kwa upande wenu, ndio maana TL ameanzisha mtindo wa kuhutubia huku anatoa vitisho kwa tume, mara uchaguzi huu unaangaliwa na mataifa mbalimbali, cha kumwambia ni kwamba hakuna wa kumuibia kura ila ajiandae kiakili tu kwamba keshashindwa, CCM inaweza kuwa kwenye migogoro weeeee, lakini wanapofika wakati wa uchaguzi ndio wanaondoa tofauti zao wanaungana kuwa kitu kimoja chenye nguvu kubwa.
 
Wanakwambia"watu wamelala barabarani ili Lissu asimame aongee wamsikie,kweli Lissu ni Rais"
yani kwa watu kulala barabarani basi ndo kigezo cha Lissu kushinda urais.Chadema ndo matahira kweRi kweRi.
😂😂 Kuna mwaka mmoja pia walideki Barabara, Chadema utawaweza mkuu!
 
Unajua mkuu, najitahidi Sana kufuatilia Kampeni hizi, mwitikio wa watu, ukipima vizuri ukaondoa mihemko ya ushabiki wa vyama, utagundua kabisa, hata mwitikio wa watu Kwa mgombea Uraisi Chadema, unafanana Tu na mwitikio wa watu kwenye mikutano anayoendesha waziri mkuu
Media vipi? Kuna usawa? Kuita watu kwenye mkutano kwa wassap na tigo sms ni shughuli, hilo nyomi linaloitikia likienda kitaa litazarisha kura Mara dufu
 
Kwanza wana CCM wengi watampa kura lissu. Sisi wote watanzania bila kujali vyama vyetu wala jinsia zetu tumeathirika mno na vyuma vilivyokaza pamoja kuwa na uchumi mgumu, bila kusahau upandaji wa bei za bidhaa ambazo zinatuumiza sisi wananchi mfano sukari. Ukosefu wa ajira, maji kama matope, barabara mbovu na kodi kubwa za TRA na ushuru.

Sasa sisi watanzania kwa umoja wetu tuna jambo letu oktoba 28. Nalo ni kumpa kura zote Tundu Lissu.
Share ujumbe huu kila sehemu, kila group na kila status.
 
Media vipi? Kuna usawa? Kuita watu kwenye mkutano kwa wassap na tigo sms ni shughuli, hilo nyomi linaloitikia likienda kitaa litazarisha kura Mara dufu
Wewe acha porojo, vipi kuhusu magari yanayopita mitaani kutangaza mikutano ya CHADEMA siku tatu kabla ya tukio?

Hakuna sehemu ambayo mkutano ulifanyika kwa kushitukiza Kama unavyojinasibu hapa,wadanganye watoto 😂😂😂😂
 
Kwanza wana CCM wengi watampa kura lissu. Sisi wote watanzania bila kujali vyama vyetu wala jinsia zetu tumeathirika mno na vyuma vilivyokaza pamoja kuwa na uchumi mgumu, bila kusahau upandaji wa bei za bidhaa ambazo zinatuumiza sisi wananchi mfano sukari. Ukosefu wa ajira, maji kama matope, barabara mbovu na kodi kubwa za TRA na ushuru.

Sasa sisi watanzania kwa umoja wetu tuna jambo letu oktoba 28. Nalo ni kumpa kura zote Tundu lissu.
Share ujumbe huu kila sehemu, kila group na kila status.
Usawa umekaza kwa wavivu,hakuna Cha bure kwenye serikali ya JPM
 
Back
Top Bottom