Emerging rift between Uganda and Tanzania


..ilikuwa vigumu sana kwa SG kutembelea mataifa mengine.

..ziara nyingi, kama siyo zote, zilikuwa zikifanywa na Andrei Gromicko.

..sasa mimi najiuliza kama hiki kinachoendelea ktk awamu hii ni mfano wa jinsi hali ilivyokuwa wakati wa Brezhnev, Andropov, au Chernenko?

..suala lingine ni hadhi na nafasi ya Tanzania ktk medani ya diplomasia na mahusiano ya kimataifa. We have always punched above our weight.

..Nina wasiwasi tunaweza tukaporomoka kama tutaendelea na utaratibu huu, na ikiwa Raisi wetu atakosa lugha na hoja zenye ushawishi huko nje.

Cc Nguruvi3
 
I
Ni kweli Dayan alikuwa kwenye ndege aina ya Boeing 707 wanazunguka sehemu.hizo hizo za Uganda ikiwa juu sana ndio maana pamoja na injini zake kuwa za kelele sana kama za DC-9 siku hiyo zilikuwa azisisikiki sana kutoka na umbali mkubwa kutoka aridhini - ndege hiyo ilitumika kama command post in the sky kuongozea na kuratibu operation ya makomando ilivyo kuwa inaendelea pale Entebbe.
 
Mbona apo nyuma walipo kaa naona kuna bendera yetu ya Kibongo ila mimi sioni shidaa
 
Nakumbuka Chairman Mao Tse tung alikuwa hatoki China. Gharama zake ikawa ni China iliyojitenga na dunia (reclusive)

Papa John Paul I alikuwa hatoki Vatcan. Ukatoliki ukaanza kupoteza nguvu

Rais wa Marekani ilikuwa Nadra sana kutoka katika dunia. America ikajikuta ikipoteza ushawishi

Xi Jiaping akafungua Milango, na ziara yake ya kwanza nje hakuiacha Afrika ikiwemo Tanzania.
Obama kaja kuongea katika mkutano wa AU, akikutana na viongozi kuanzia Asia/Latin America/ Africa na Europe

Kwa mifano hii, ziara za viongozi hao zinawakumbusha kitu kimoja ''out of sight out of mind'
 
Watanzania tunaakili bwana, hizo propaganda za wakenya haziwezi kutuyumbisha.
 
Mkuu hii si ni fursa ya kuelimisha wenye tatizo kwanini hali imekuwa hivi.
Hayo uliyoandika hayahusiani na mada wala hayajibu mada , kufafanua au vinginevyo. Yanonyesha utupu wa hoja na hivyo mashudu yanaweza kujazia


Historia ya mtu kwanza
Huwezi kujibu hoja ya mtu bila yakuangalia msimamo wake,

Mtu mwenye msimamo wa kila kizuri serikalini kwake ni kibaya,
Na kibaya kimoja kwake ndio hoja kuu Kisiasa huyo utamjibu hoja ipi?

Kutokusafiri kwa Rais Magu hakukufanyi upate hoja ya maana kujitambia jf
Kama hakuna hoja mtulie tu,
Waziri mkuu yupo
Makamu wa Rais yupo
Sio lazima Aende Rais.

Kama katiba inapinga waziri mkuu kushiriki vikao vya kimataifa
Ikiwa rais yupo
Mkazane kukuza hoja yenu kisiasa
Vinginevyo
Mna ongeza Pumba kwenye Dishi la Mashudu
 
labda Magu ako na flight phobia na si hatujui. atachukua safari only when its really necesary
 

..wewe umesema unamtetea kwasababu wote mmetoka kanda ya ziwa.

..unatetea na kusifia tu hata pale pasipostahili.
 
..wewe umesema unamtetea kwasababu wote mmetoka kanda ya ziwa.

..unatetea na kusifia tu hata pale pasipostahili.

Hahaha JokaKuu wapi nimesema hayo!!
Wewe na Nguruvi3 mpo kikanda zaidi
Kamwe hamuoni jema lolote kwa serikali.
Lakini ukisha mfahamu mtu kamwe hawezi sumbua.
 
Kwani alienda Rwanda au Ethiopia?
 
Maguli though is not my favorite person,lakini ana kazi nyingi za kufanya nyumbani.
Yeye kama Ian Khama hashabikii useless talk shops kama huyo wa kwenu kila mkutano hakosi
 
Hapo ndipo unakosea. Ukisoma bandiko kwa kuangalia nani kaandika na si hoja unakosa ile maana ya hoja.
Hate me love me siyo muhimu, muhimu ni je tunazungumzia hoja kwa mantiki

Mazuri yakifanywa tunasema, na mabaya pia.
Tofauti unayoiona ni kutaka kila mtu ashangilie tuu hata madudu kama ya teuzi!

Pili, usizungumzie katiba kabisa katika utawala huu. Kama utazungumzia tutakuuliza ni wakati gani katiba inatumika na wakati gani inawekwa pembeni. Hilo la katiba liache kabisa

Hoja iliyopo hapa ni kuwa kuna tatizo katika diplomasia yetu.
Kuna mahali lazima mkubwa aende kukutana na wenzake kwa masilahi ya umma.

Kama yapo ya binafsi yasiathiri masilahi ya umma.
Hili ni tatizo tusiloweza kulificha ficha kwa hoja nyepesi.
 
Hahaha JokaKuu wapi nimesema hayo!!
Wewe na Nguruvi3 mpo kikanda zaidi
Kamwe hamuoni jema lolote kwa serikali.
Lakini ukisha mfahamu mtu kamwe hawezi sumbua.
Hizi huwa ni hoja za kutaka kuondoa watukatika mijadala.JK alikuwa anasemwa hapa kama kawaida, Nyerere kila siku n.k.

Ukweli utasemwa tu, hatuwezi kuishi na hisia hisia na maneno ya maitaani.

Wapo wanaosema lugha , wengine diplomasia haipandi, wengi debate patupu na kila aina ya maneno ya hisia au uongo.

Tunautaka ukweli, kwanini tumeporomoka kidiplomasia katika kiwango hiki.

Na kwamba huu ndio mwanzo wa mwisho wa Tanzania kutawala diplomasia za dunia?

Sera za mambo ya nje zina mwelekeo gani.

Hizo ndizo hoja, si nani anaitwa nani katoka wapi. Hatuyafikirii hata kwa bahati mbaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…