''Enchweke'': Sauti za waliokufa, inatokeaje mtu anaongea kwa niaba ya mfu?

''Enchweke'': Sauti za waliokufa, inatokeaje mtu anaongea kwa niaba ya mfu?

"Enchweke" ni kitu ambacho kipo katika jamii hasa ya Wanyambo na Wahaya na labda katika jamii nyingine. Kwa ufupi, "enchweke" ni uingiliaji kati (intervention) wa mtu aliyekwishafariki katika jambo la uonevu au uvunjaji wa haki anaofanyiwa mtu mnyonge ambaye kwa unyonge wake hawezi kujitetea. Huenda ni yatima anadhulumiwa au ni mjane ananyanyaswa au ni fukara anaonewa na ndugu zake matajiri nk. Marehemu ambaye alikuwa labda ni mzazi au mume huingilia kati machozi ya mtu anayenyanyaswa kupitia "enchweke". Ni hali kama ya kumtokea au mdhulumiwa ama mdhulumaji, mtu huyu hupoteza fahamu na kisha sauti ya marehemu hukemea hali ya uvunjaji haki iliyopo mara nyingine hata kwa kutangaza adhabu kwa wadhulumu ama laana. Kisha mtu huzinduka na kwa vyovyote vile yeye husimuliwa kilichotokea na mashuhuda. Wakati mwingine huchukua muda mrefu kwa "nchweke" kumwachia mtokewa mpaka wadhulumu au ndugu wafanye malipizi ya dhuluma inayokuwa imefanyika. Inawezekana ni aina ya Illicination!
 
"Enchweke" ni kitu ambacho kipo katika jamii hasa ya Wanyambo na Wahaya na labda katika jamii nyingine. Kwa ufupi, "enchweke" ni uingiliaji kati (intervention) wa mtu aliyekwishafariki katika jambo la uonevu au uvunjaji wa haki anaofanyiwa mtu mnyonge ambaye kwa unyonge wake hawezi kujitetea. Huenda ni yatima anadhulumiwa au ni mjane ananyanyaswa au ni fukara anaonewa na ndugu zake matajiri nk. Marehemu ambaye alikuwa labda ni mzazi au mume huingilia kati machozi ya mtu anayenyanyaswa kupitia "enchweke". Ni hali kama ya kumtokea au mdhulumiwa ama mdhulumaji, mtu huyu hupoteza fahamu na kisha sauti ya marehemu hukemea hali ya uvunjaji haki iliyopo mara nyingine hata kwa kutangaza adhabu kwa wadhulumu ama laana. Kisha mtu huzinduka na kwa vyovyote vile yeye husimuliwa kilichotokea na mashuhuda. Wakati mwingine huchukua muda mrefu kwa "nchweke" kumwachia mtokewa mpaka wadhulumu au ndugu wafanye malipizi ya dhuluma inayokuwa imefanyika. Inawezekana ni aina ya Illicination!

Asante Mkuu.
 
Kuna shangazi yangu alisema maneno kama hayo lakini kilcho mtokea haddi sasa kichwa chake hakijatulia dk 2 mbele.ukisema nimapepo usiwe mzumaji.
 
"Enchweke" ni kitu ambacho kipo katika jamii hasa ya Wanyambo na Wahaya na labda katika jamii nyingine. Kwa ufupi, "enchweke" ni uingiliaji kati (intervention) wa mtu aliyekwishafariki katika jambo la uonevu au uvunjaji wa haki anaofanyiwa mtu mnyonge ambaye kwa unyonge wake hawezi kujitetea. Huenda ni yatima anadhulumiwa au ni mjane ananyanyaswa au ni fukara anaonewa na ndugu zake matajiri nk. Marehemu ambaye alikuwa labda ni mzazi au mume huingilia kati machozi ya mtu anayenyanyaswa kupitia "enchweke". Ni hali kama ya kumtokea au mdhulumiwa ama mdhulumaji, mtu huyu hupoteza fahamu na kisha sauti ya marehemu hukemea hali ya uvunjaji haki iliyopo mara nyingine hata kwa kutangaza adhabu kwa wadhulumu ama laana. Kisha mtu huzinduka na kwa vyovyote vile yeye husimuliwa kilichotokea na mashuhuda. Wakati mwingine huchukua muda mrefu kwa "nchweke" kumwachia mtokewa mpaka wadhulumu au ndugu wafanye malipizi ya dhuluma inayokuwa imefanyika. Inawezekana ni aina ya Illicination!

Haswaa
 
Enchweke zipo nimezushuhudia uko Muleba ila sina ufaham kwamba zinatikana na nn aswaah ila nadhan kuna usanii kwa baadhi ya wahanga wa Nchweke,,,,
 
tungepata anayesumbuliwa na hili jambo nadhan tungepata sehem nzuri ya kuanzia! siamin kama kuna kitu kama hiki but i am willing to learn and accept kama kuna ushahidi!!


Mifano mingi imetolewa na watu hapo juu Mkuu
 
Kwa uelewa wangu wa harakaharaka hayo ni mapepo,ambayo kama unataka unaweza ukayaepuka kama utaamua kumgeukia Mungu wa kweli,kwani ninauhakika roho mtakatifu akishaingia hapo hakuna kitakochobakia CC: mshana jr Pasco Rakims wekeni ufafanuzi pale.

Ngoja waje
 
Last edited by a moderator:
Wafu hawana fungu lao duniani.neno la Mungu linasema baada ya kufa ni hukumu.in short hayo ni maroho na mizimu ambayo kuyafuata ni against the word of God
Mleta mada inawezekana ni muumini wa Word of God zaidi yako na ndio maana kaileta hii mada kwenye 'jamii intelligence' kwa maana haya mambo yote yapo na kila mtu anaweza kuyajua au kutoyajua sababu ya mtazamo kama wako wa 'kufunga daima mlango wa ufahamu'.
Kumbuka 'Word of God' limekuja takribani miaka 2000 iliyopita lakini hawa watu walikuwepo maelfu ya miaka na waliweza kupambana na dunia! Sio vizuri kuleta hoja za mkato kama za magamba.

 
Hamna lolote hapo. Hayo ni mapepo maovu yanawadangany'a watu. Mtu akiisha kufa ni hukumu ya haki na aidha ataenda mbinguni au tohorani au motoni. Na harudi kusuluhisha jambo lolote.
 
Haya mambo ya ajabu sana...mama yangu aliteswa na baba sana na baadae akafa kwa ugonjwa wa moyo na depression...baba akaoa mke mwingine maisha yakaenda.....tulipokuwa tukionewa na mama wa kambo au baba..."enchweke iliingilia kati" mpaka nikajiuliza huu mzimu wa mama ina maana unatuona tunavyoteseka??? Na unaona vipi??? Mwanzoni alikuwa anashikwa bibi..nkafikiri ni usanii bibi anacheza kwa sababu alikuwa anatuona live tunavyoteseka...baadae ikaamia kwa shangazi ambaye kimsingi hakuwepo maeneo ya home...ndo nikajua sio usanii....

Nilipokua nataka kumjengea baba nyumba..timbwili likazuka tena na akasema nisifanye hivo kwa sababu alimtesa sana wakati wa uhai wake.. cha kushangaza mawazo na mipango ya kujenga nyumba ilikuwa kati yangu na baba tu na hakuna mtu mwingine alijua.....

Baadae nikaona huu uteja na wote waliokuwa wanashikwa na huu mzimu wakaamua kuokoka na kumfuata Yesu...mpaka leo haijawahi tokea tena....


Haya mambo yanashangaza sana ila ukiwa na Mungu wala hayawezi kujitokeza.....kimsingi baada ya kuyashudia yalinifanya imani yangu kwa Mungu iwe dhabiti maana niliamini Ulimwengu wa roho UPO iwe ni giza au nuru ila UPO..
 
Haya mambo ya ajabu sana...mama yangu aliteswa na baba sana na baadae akafa kwa ugonjwa wa moyo na depression...baba akaoa mke mwingine maisha yakaenda.....tulipokuwa tukionewa na mama wa kambo au baba..."enchweke iliingilia kati" mpaka nikajiuliza huu mzimu wa mama ina maana unatuona tunavyoteseka??? Na unaona vipi??? Mwanzoni alikuwa anashikwa bibi..nkafikiri ni usanii bibi anacheza kwa sababu alikuwa anatuona live tunavyoteseka...baadae ikaamia kwa shangazi ambaye kimsingi hakuwepo maeneo ya home...ndo nikajua sio usanii....

Nilipokua nataka kumjengea baba nyumba..timbwili likazuka tena na akasema nisifanye hivo kwa sababu alimtesa sana wakati wa uhai wake.. cha kushangaza mawazo na mipango ya kujenga nyumba ilikuwa kati yangu na baba tu na hakuna mtu mwingine alijua.....

Baadae nikaona huu uteja na wote waliokuwa wanashikwa na huu mzimu wakaamua kuokoka na kumfuata Yesu...mpaka leo haijawahi tokea tena....


Haya mambo yanashangaza sana ila ukiwa na Mungu wala hayawezi kujitokeza.....kimsingi baada ya kuyashudia yalinifanya imani yangu kwa Mungu iwe dhabiti maana niliamini Ulimwengu wa roho UPO iwe ni giza au nuru ila UPO..


Mkuu one point for clarification.Sawa ulijikabidhi kwa Yesu na mambo yakaisha,lakini je kulikuwa na ubaya wowote katika hili?-Je,ungeendelea kuteswa na mama wa kambo ukakosa mtetezi ungejisikiaje?-Je,hukuwa na faraja kwa kitendo cha mama marehemu kuingilia matesi yenu?
 
Kwetu akifa mtu ambaye hajaoa au kuolewa wanamzika na shina la mgomba. Bila ya kufanya hivyo 'enchweke' itamwandama mmoja WA ndugu za hiyo marehemu. 'Enchweke' itakuwa inadai kupewa mke au mme. Ni kitu nimeona live na kinapotea baada ya matambiko ambayo 'enchweke' atahitaji;
 
Kwetu akifa mtu ambaye hajaoa au kuolewa wanamzika na shina la mgomba. Bila ya kufanya hivyo 'enchweke' itamwandama mmoja WA ndugu za hiyo marehemu. 'Enchweke' itakuwa inadai kupewa mke au mme. Ni kitu nimeona live na kinapotea baada ya matambiko ambayo 'enchweke' atahitaji;

Good testimony
 
Mleta mada inawezekana ni muumini wa Word of God zaidi yako na ndio maana kaileta hii mada kwenye 'jamii intelligence' kwa maana haya mambo yote yapo na kila mtu anaweza kuyajua au kutoyajua sababu ya mtazamo kama wako wa 'kufunga daima mlango wa ufahamu'.
Kumbuka 'Word of God' limekuja takribani miaka 2000 iliyopita lakini hawa watu walikuwepo maelfu ya miaka na waliweza kupambana na dunia! Sio vizuri kuleta hoja za mkato kama za magamba.


Umenena vema Mkuu.
 
Yalimtokea Dada yangu ambaye ni mtoto wa mama mkubwa, alimtesa sana mtoto wa marehemu mjomba lakini siku ilipokuja hiyo sauti tena ilimshika Dada mwenyewe na alipewa siku mbili za kumrudisha binti kwao ..ili kumeet deadline ilibidi mtoto awaishwe kwa ndege kutoka mwanza kwenda home ..ni hatari sana hii kitu.
 
Yalimtokea Dada yangu ambaye ni mtoto wa mama mkubwa, alimtesa sana mtoto wa marehemu mjomba lakini siku ilipokuja hiyo sauti tena ilimshika Dada mwenyewe na alipewa siku mbili za kumrudisha binti kwao ..ili kumeet deadline ilibidi mtoto awaishwe kwa ndege kutoka mwanza kwenda home ..ni hatari sana huo kitu.

Dah❕➖hii ilikuwa balaa Mkuu.
 
Back
Top Bottom