Endapo Kivuko kingekarabatiwa Tanzania kwa zaidi ya bilioni 7.5, haya yangetokea...

Endapo Kivuko kingekarabatiwa Tanzania kwa zaidi ya bilioni 7.5, haya yangetokea...

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Kwenye manunuzi huwa hatuangalii bei peke yake labda uwe mwehu wa kutupwa! Kuna factors nyingi zinakua considered na mara nyingi price inakua ndio ya mwisho, mnaweza mka-negotiage price.

Sasa, tunaambiwa kuwa Kivuko kipelekwa Kenya kwenye ukarabati kwa Bei ya 7.5B kwakua wale competitors wa ndani wao walikua na bei ya juu, japo binafsi sijasikia hio bei ya juu ilikua ngapi.

Kwa mtazamo wangu, ni wa kwangu siyo wako; Endapo kivuko kingekarabatiwa hapa hapa Bongo. Machache yafuatayo yangesaidia sana sana kuziba hio "Excess";

1. Hizi 7.5B au zaidi pengine 75% ingebaki ndani ya nchi na hivyo kuongeza mzunguko wa fedha.

2. Baadhi ya materials zingenunuliwa humu humu nchini na hivyo kuboresha mzunguko wa biashara na viwanda.

3. Vijana wetu na Mainjinia wetu wangepata fursa ya ku-practice kile walichosoma.

4. Ustawi wa jamii, hapa nazungumzia category mbili, ya kwanza niwaajiriwa ambao mishahara yao inapita kwenye mabenki na wangekatwa Kodi ambayo ingeinufaisha serikali na pili, ni wale Mama Ntilie wa eneo husika at least wangekua na uwezo wa kuendelea kuuza vyakula vyao.

5. Kampuni ambayo ingepewa tender hio ingelipa Kodi, Kodi ambayo ingeingia serikalini na kusaidia kwenye sector nyingine.

7. Usimamizi wake wakati wa Ukarabati ungekua rahisi na madhubuti kuliko itakavyokua huko Kenya ambako itabidi Kila wakati wasimamizi kutoka Tanzania wataenda, mnakumbuka kwenye Ndege? Kuna Watanzania wanaendaga huko majuu kukagua! Hili halikua na ulazima.

8. Kwa hali hii au Kwa kiswahili cha Kawaida ni kwamba, Tanzania imeipa Kenya 7.5b ambazo ingeweza kuzitumia yenyewe.

Ruksa kuongeza na wale wakosoaji karibuni.
 
Huu ukarabati ungefanyika hapa bongo akina @zumnemkuu Chakaza na wengine tungepata ajira
 
Huwa najiuliza ndani ya hizi sekta za kiserikali huwa hakuna watu wanaoweza kufikiria kwa mapana kwa faida ya Tanzania Kama mtoa mada?
 
Huwa najiuliza ndani ya hizi sekta za kiserikali huwa hakuna watu wanaoweza kufikiria kwa mapana kwa faida ya Tanzania Kama mtoa mada?
Upana wao ni namna gani watapiga deal bila kukamatwa!
 
Kwani kivuko kipya bei gani?

Kwangu hiyo pesa 7.5 bilioni ni nyingi sana, au kama haitoshi wangeongezea kidogo hapo watengeneze kipya.
Wangeongeza wakanunua cha kisasa zaidi
 
Kipya kama hicho cha MV Magogoni kwa sasa bei ni zaidi ya 25 Billion-Eng Lukombe King'ombe (Meneja wa vivuko kanda ya Mashariki na Kusini)
Wangekiuza then wakaongeza pesa wakanunua cha kisasa zaiidi
 
Songoro Marines walihitaji zaidi ya 10B kukarabati hicho kivuko- Eng King'ombe.

Kuna ufafanuzi ushatolewa kuhusu mambo kadhaa upo mtandaoni na aliyetajwa kuwa Meneja wa vivuko.
 
Songoro Marines walihitaji zaidi ya 10B kukarabati hicho kivuko- Eng King'ombe.

Kuna ufafanuzi ushatolewa kuhusu mambo kadhaa upo mtandaoni na aliyetajwa kuwa Meneja wa vivuko.
Bado kwangu ingekua ni sahihi zaidi kukikarabati ndani ya nchi kuliko nje ya nchi. Risk ni kubwa sana kwa difference ya 2.5B
 
Hivi inakuwaje sisi Raia tukitizama hayo makampuni ya nje yanayouza hizi bidhaa tunakuta bei nzuri sana halafu watu wa serikali wakiwa wanataka kufanya manunuzi bei inapanda mara tisa kupitiliza ile halali ya soko?!

Sasa hivi vivuko mimi nimetazama vilivyotumika na hata vipya kabisa nakuta bei zake ni muafaka kabisa na zinacheza kwenye 10% hadi 30% ya hiyo pesa.

Nasema hivi kwasababu kwa hapo kigamboni hatuhitaji Ferry boat kubwa sana sababu ya umbali mfupi sana na hivyo basi vikiwapo vivuko hata vinne vinatosha kabisa kupiga mzigo kwa shift usiku na mchana.

Sasa ukitazama naona bei ndogo sana ambazo zipo ndani ya uwezo na ni za kufanya haraka sana manunuzi yakakamilika na vikaanza tumika.

Hizi chenga chenga za mwili maneno maneno mengi na story za paukwa pakawa huwa zinatokea wapi unajua huwa sielewi hata kidogo?!
 
Back
Top Bottom