Eng. Hersi 2021: Yanga inajiendesha kwa Hasara

Eng. Hersi 2021: Yanga inajiendesha kwa Hasara


Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Kampuni ya GSM Eng. Hersi Said amewashukia baadhi ya wadau wa soka nchini Tanzania walioibua hoja inayogusa udhamini wa kampuni hiyo kwenye klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara.

Hoja hiyo imeibuka kufuatia Kampuni ya GSM kuwa mdhamini ya Young Africans, Namungo FC na Coastal Union, huku ikijaribu kuisafirisha Biashara Utd kwenda Libya (safari ambayo ilishindikana).

Wasiwasi uliopo ni kwamba kama kampuni ya GSM imewekeza kwenye klabu zaidi ya moja itakua na sababu ya kushawishi upangaji wa matokeo hasa kwa timu wanazozidhamini zitakapokutana.

Hersi ameandika kuwa: ”Timu hizi zinajiendesha kwa hasara kwa miaka mingi ndio maana zimekwama. Ukisema hivi mtu anaweza asikuelewe lakini ukitazama mapato ya klabu na matumizi ndio utajua kwanini zinajiendesha kwa hasara”

”Yanga inalipa mishahara yenyewe, ina mifumo yake ya kuajiri watu sisi tuna-support tu. Yanga ni timu kubwa huwezi kufananisha na hawa makolo. Huwezi kumleta mchezaji kama Bangala halafu hajui mshahara analipwa na nani”

”Hii ni klabu kubwa, tunafanya kazi ya kurejesha heshima yake, watu waipende tena. Mechi ya juzi Yanga inafungwa goli mashabiki wanapiga makofi, tunarudisha tunafunga la pili na la tatu na bado kuna dakika kama 900 za kucheza”

”Watu wanaleta siasa chafu na mimi nasema hizi ni takataka. Mbona kampuni kama Emirates inadhamini vilabu vingi tu vinacheza Champions League. Ina maana Arsenal wakicheza na AC Milan utasema mmoja amwachie mwenzake?”

My Take
Sina My Take yeyote

Kuna tofauti kubwa kati ya Club kujiendesha kwa hasara na Club kumtia mtu hasara

Au tuiweke hivi;
1. "Hii Club inajiendesha kwa hasara, hii ni Club kubwa, yunafanya kazi ya kurudisha heshima yake"

2. "Hii Club inania hasara, natoa hela zangu kwa mapenzi tu wala hakuna numachokipata zaidi ya hasara. Gharama ninazotumia kwenye hii club kwenye hii club nimgeweza hata kununua ndege:

Tafakari
 
Uendeshaji wa klabu ni hasara katika taifa hili la TANZANIA na hata nchi nyingi za kiafrica.

Watu hawajiulizi tu Simba inatumia kiasi gani kulipa mishahara ya wachezaji, makocha na waajiriwa wengine kwa mwaka mzima,

Gharama za kuisafirisha timu, benchi la ufundi na viongozi kuzunguka Tanzania katika mechi 15 za msimu ni kiasi gani ? (NOTE: Usafiri wa ndege)

Gharama za kusafirisha timu na viongozi kwenda nje ya nchi kwa ajili ya mechi za kimataifa?

Gharama za hoteli!?

Gharama za posho, makazi ya wachezaji n.k

Gharama za usajili n.k

Ukishapiga hesabu haya njoo uangalie vyanzo vya mapato ya timu na kiasi cha pesa inayokusanywa! Mechi za taifa ukitoa big matches mahudhurio huwa ni hafifu licha ya kuwa viingilio huwekwa hadi 3000 na bado watu hawazidi hata 20000.
 
Back
Top Bottom