Eng Hersi mwache Mzize akamalize soka lake Wydad, unamuharibia maisha

Eng Hersi mwache Mzize akamalize soka lake Wydad, unamuharibia maisha

Acheni kujipa jukumu la kuwa mshauri wa mchezaji kwa maslahi yenu binafsi. Wachezaji wana meneja na wakala, suala la kumzuia mchezaji fulani kisa mnahisi timu inayomtaka ni ndogo halikuhusu wewe kama mshabiki au hata kiongozi wa timu ni kazi ya wale wanaomsimamia mchezaji mwenyewe.

Eti Wydad ni timu ndogo? Unajua exposure ya Club World Cup wewe? Umeona uwekezaji wanaoufanya sasa kwa kuanzia kwa benchi la ufundi? Kaizer Chiefs ingekuwa timu ndogo mngeshangilia kama wehu baada ya kuwafunga katika mechi ya kirafiki?

Huu mnaofanya ndiyo tunaita ushabiki maandazi, kutetea uovu kisa timu yako imeweka msimamo fulani.


Nani kaongelea pesa ndogo? Kwani dola 100K ni pesa ndogo? Yaani unataka kusema Mzize ana thamani kubwa kuliko kikosi kizima cha Yanga? Mnachekesha sana nyie watu.
Pesa ndogo sana hiyo.
Uzeni wachezaji wenu sisi Young African hatuuzi hiyo bei.
 
Mzize hana umri unaotaka kuwaaminisha watu, sio young player, wengi tunamfahamu Mzize, muache akacheze soka huko anakoliliwa, Mzize maisha yake bado hayajakaa sawa na njia pekee kwake kutoboa ni kwenda Wydad akacheze, hapa Yanga wewe shs ngapi Injinia.

Halafu nikuambie tu washabiki wengi wa Yanga tunaokaa nao mitaani hawamkubali Mzize kivile, wanaomuona ana papara sana, mchoyo, sio striker tishio, anakosa sana mabao, Mzize hawezi kucheza mechi bila mashabiki kumsonya kwa mambo anayofanya uwanjani, halafu mpira wa kibongo una muda, akichuja huyo msimu ujao unampeleka kwa mkopo Singida au KMC, mwache akale maisha WYDAD msimu mmoja tu anatoboa hata akiachwa ameshajitafuta.

Kuendelea kukataa ofa za Mzize unamchanganya na unamharibia sana, sawa kwa vile Mzize ana mkataba na Yanga lakini hebu fikiria ndugu yetu kwa umakini suala hili, Yanga ina washambuliaji wakali kama nyoka sasa hivi, Yanga kwa viungo waliokuwa nao wanaweza kumpelekea moto mtu bila hata kuwepo mshambuliaji, Mzize mwache aende bro, mmekaa na Nkane hadi ameota sugu, dogo kucheza hachezi anaona raha tu kuozea benchi.

Huyo Mzize hawezi kubadilika tena, uchezaji wake ndio ule ule, kama unadhani kuna dili kubwa zaidi kwa mchezaji huyo andika umeumia.Washabiki wa Yanga hawana shida na Mzize, kwanza akipangwa wanaona kama anawachelewesha vile.
Huyu ni mchezaji wa 2 anamlalamikia huyo Hersi wenu.

Wa kwanza alikuwa Feitoto,seems huyu bwana wa Yanga ni mshenzi wa wivu Kwa wengine
 
Kwa Morocco inaruhusiwa wachezaji wangapi wa kigeni?

Na hivi sasa Waydad imeshasajili wangapi?

Waydad kwasasa hata Yanga Ina afadhali. Mashindano makubwa pekee wanayocheza Waydad ni Club World Cup, kwa Africa hakuna.

Kaizer Chiefs ndio kabisa iko nafasi ya 10, hata mashindano yao Super8 hachezi.

Simba na Yanga zimeshakuwa timu kubwa Africa tuziheshimu. Siyo timu za kitoto wala academy zile ambazo unaenda tu kuzoa wachezaji wazuri Kama Coaster Union.

Mbona timu hazipeleki ofa, Al ahly, Mamelodi au Raja Casablanca??

Mnataka wachezaji wetu wakacheze nje ilimradi tu, ndio kuzurura nje Kama kina Msuva, Himid Mao na Novastus.

Jambo la msingi apambanie maslahi yake ndani ya Yanga.

Akilipwa hata milioni 8 au 10 ndani ya Yanga na signing on fee ya hata 300M maisha ya bongo Mungu akupe nini, maana ni Bora kuliko huko anakotaka kwenda.

Ingekuwa Mamelodi, Al ahly Egypt, Esperance au timu B za England premiee,Serie A, Laliga, ligi kuu Belgium Kama Genk hata Mimi ningeshauri aachiwe aende
Nimesikitika sana baada ya kusoma hii comment
 
ubinafsi unatuua wabongo , mtu analipwa laki 6 ww unashabikia abakie na kuacha ofa ya mamilioni , ebu tupendane asee wabongo , azizi angelipwa hata 1 M ungesema ananyonywa ila mtz mwenzio ni sw abakie asote kwa laki 6

WABONGO HATUPENDANI NDIO MAANA FISIEN WANAENDELEA KUTUNYOOSHA BILA WATZ KUKEMEA UTEKAJ WA WATZ WENZETU
Nimesikitika sana eti mtu anakwambia kuliko kwenda Wydad ni bora abakie Yanga akiwa kama substitute anayeingia dk ya 80.

Aisee kweli wabongo ni watu wenye upeo duni sana na dhaifu wa kifikra
 
Nimesikitika sana eti mtu anakwambia kuliko kwenda Wydad ni bora abakie Yanga akiwa kama substitute anayeingia dk ya 80.

Aisee kweli wabongo ni watu wenye upeo duni sana na dhaifu wa kifikra

Nyie kama nani mpaka mtulazimishe kumuachia mzize yanga wenyewe wana malengo yao yaaani umuuzie silaha adui yako embu msitake kulazimisha mambo tengenezeni timu yenu ajiri wachezaji halafu muwauze kiholela
 
Nyie kama nani mpaka mtulazimishe kumuachia mzize yanga wenyewe wana malengo yao yaaani umuuzie silaha adui yako embu msitake kulazimisha mambo tengenezeni timu yenu ajiri wachezaji halafu muwauze kiholela
Sawa tumekuskia....
 
Back
Top Bottom