Eng.Hersi ulituahidi wanayanga tutaingia makundi huu mwaka. Tusipoingia hiyo 9/11/2022 naomba ujiuzulu nafasi yako

Eng.Hersi ulituahidi wanayanga tutaingia makundi huu mwaka. Tusipoingia hiyo 9/11/2022 naomba ujiuzulu nafasi yako

Poker

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2016
Posts
5,445
Reaction score
14,828
Raisi wetu wa klabu pendwa ya kihistoria hapa nchini na Africa mashariki. Yanga ni klabu kubwa yenye historia nzuri na Pana, hata pepe kalle aliwahi kuimba kuhusu ubora wa yanga.

Kuwa wa Rais wa klabu kama yanga yenye mashabiki lukuki ndani ya nchi na nje ya nchi si kitu kidogo wala cha mzaha mzaha. Ulituahidi wanayanga tutaingia makundi huu mwaka, lakini mpaka sasa hatuoni hiyo dalili na mbaya zaidi tukihoji ni kwanini hatufuzu makundi na huku kwenye ligi tukiwa unbeaten mpaka sasa unatuita wala mihogo.

Kiufupi hutaki mashabiki wa yanga wahoji chochote kuhusu matokeo? Kisa ni unbeaten ya kwenye ligi ambayo haina mashiko kama klabu itakuwa haifanyi vizuri kimataifa ili kuakisi yale maneno ya Young Africans mabingwa wa Tanzania na Africa.

Jwaneng Galaxy ilimtoa simba tena kwa mkapa lupaso na hawakuwa na uzoefu wa aina yoyote na hayo mashindano Yanga ya Eng. Hersi inataka uzoefu gani? Vipers ya Uganda imemtoa TP Mazembe je vipers ilikuwa na uzoefu gani?

Eng. Hersi Yanga tunamafanikio sana kwa Tanzania na malengo yetu ni kuhakikisha tunaitawala Africa ili kuakisi jina letu. Hivyo basi kwakuwa ulituahidi makundi na tulipohoji juu ya uwezo wa timu kimataifa ukatuita wala mihogo, endapo hatutofikia lengo hilo kuwa muungwana kama raisi ukubali lawama na ujiuzulu nafasi yako, ili upishe wengine waje ambao wataweza kutuvusha.

Na endapo tutafuzu makundi pia ujiuzulu nafasi yako maana bado ulitutukana na huenda ukatutukana zaidi huko mbeleni kwasababu huna busara hata kidogo.

#enghersiout
 
Raisi wetu wa klabu pendwa ya kihistoria hapa nchini na Africa mashariki. Yanga ni klabu kubwa yenye historia nzuri na Pana, hata pepe kalle aliwahi kuimba kuhusu ubora wa yanga.
Yanga hii kwenda hatua ya mbele zaidi ya hapa ni sawa na kumtaka ng'ombe dume atoe maziwa.
 
Sisi wala mihogo sisi?[emoji23]
IMG_20221104_081434.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makamu Mwenyekiti, Ndg. Arafat nae aliahidi msimu huu Yanga Princess wasipochukua Ubingwa aulizwe yeye. Nakala tunazo. Ni suala la muda tu.
 
Makamu Mwenyekiti, Ndg. Arafat nae aliahidi msimu huu Yanga Princess wasipochukua Ubingwa aulizwe yeye. Nakala tunazo. Ni suala la muda tu.
Haya ni mapambano ya ukombozi wa yanga kutoka kwa mamluki ambao hawana nia nzuri na timu yetu zidi ya kutukashifu mashabiki wake tunaumia sana.
 
Tatizo sio yanga..hapo tatizo ni simba..ndio kaleta mabalaa yotr haya..kufudhu fudhu mfululizo makundi robo fainali tatu watu wanaona ni rahisi kila mtu anaeza fanya..babu ile sio kazi nyepesi..huyo mazembe mwaka wa tatu mfululizo hajaingia makundi cl, zamalek mwaka jana chali hatua ya mwanzo kabisa.... as vita chaalli mwaka jana hajacheza sio cl wala ccf.. msione simba anacheza mkazani ni kazi rahisi msilaumiane jengeni timu yenu kiushindani sio kushinda kimagumashi..mnasema simba kimataifa anacheza na marefa..lini tulipewa bao la offside pale au pernaty ya mchongo...mkitaka kufdhu makundi shindeni kihalali mechi za ndani
 
Tatizo sio yanga..hapo tatizo ni simba..ndio kaleta mabalaa yotr haya..kufudhu fudhu mfululizo makundi robo fainali tatu watu wanaona ni rahisi kila mtu anaeza fanya..babu ile sio kazi nyepesi..huyo mazembe mwaka wa tatu mfululizo hajaingia makundi cl, zamalek mwaka jana chali hatua ya mwanzo kabisa.... as vita chaalli mwaka jana hajacheza sio cl wala ccf.. msione simba anacheza mkazani ni kazi rahisi msilaumiane jengeni timu yenu kiushindani sio kushinda kimagumashi..mnasema simba kimataifa anacheza na marefa..lini tulipewa bao la offside pale au pernaty ya mchongo...mkitaka kufdhu makundi shindeni kihalali mechi za ndani
Tuelewane.
IMG-20221104-WA0001.jpeg
 
Wanachama wa Simba na Yanga hawana faida kwa hizi timu
 
Back
Top Bottom