Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Fedha hizo zimetumika kuhakikisha kuwa miundombinu yote ya Barabara iliyoathiriwa na wananchi kushindwa kutoka eneo moja Kwenda jingine inapitika kwa haraka kama ambavyo serikali imekusudia.
Akizungumza mara baada ya kukagua miundombinu ya miradi ya Barabara inayoendelea na matengenzo mbalimbali Meneja wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Njombe Mhandisi Ruth Shaluwa amesema kuwa Maeneo ya miundombinu ya barabara na madaraja yaliyoathiriwa na Mvua za El Nino mwezi Januari – Mei, 2024 ni Itoni – Ludewa – Manda Km 211.4; Sehemu ya Lusitu – Mawengi Km 50 (Maporomoko ya Udongo, Gangitoroli Km 62 – Km 64 na Jongojongo Km 82 – Km 85), ambapo kiasi cha shilingi Milioni 350 zimetumika.
Pia Milioni 250 zimetumika kwa ajili ya ukarabati wa tuta la Barabara eneo la Ikowo katika Barabara ya Ndulamo – Nkenja – Kitulo I Km 42.28 ambao ujenzi umefikia asilimia 58 kwa gharama ya shilingi Milioni 150, Matengenezo ya eneo lililofurika kwenye Mto Rumakali na Maporomoko ya Udongo eneo la Utanziwa katika Barabara ya Kikondo – Bulongwa – Makete Km 74.2
Mhandisi Ruth amesema kuwa Milioni 359.76 zimetumika kwa ajili ya matengenezo kwenye Barabara ya Nkenja – Ikuwo – Usalimwani Km 42.70, huku Milioni 257.24 zikitumika kwa ajili ya matengenezo kwenye Barabara ya Kitulo II – Matamba – Mfumbi.