Engine gani ya Toyota inaweza kufit katika VW golf mk3?

Chukua engine yake urudishie mkuu, au hio iliopo ina shida gani?

Kaka hii ina sumbua vitu vingi. Kwanza kuna sensor imekufa linajia accelerate mpaka inaweza fika 100km/hr bila kukanyaga mafuta. Inabidi ung’ang’anie break na steering kama unaendesha farasi.

Pili ina chemsha balaa. Tatu gear box, niliwahi pamia tuta nikiwa 140, lile oil pan katika gearbox ikapinda basi inavujisha oil ya gearbox. Kwa ujumla gharama za kutengeneza kubwa sana
 
Kaka hii ina sumbua vitu vingi. Kwanza kuna sensor imekufa linajia accelerate mpaka inaweza fika 100km/hr bila kukanyaga mafuta. Inabidi ung’ang’anie break na steering kama unaendesha farasi...
Kauze screpa jipange ununue gari nyingine. Tafuta hata kipasso kikusogeze ukijipanga ununue golf ingine.

Hiyo gari huiwezi tena.

Hata ukiweka engine ya toyota ndo itakupasua kichwa na moyo.
 
Mkuuu pole sana.
Yaani gari inajipa mafuta yenyewe??? Hiii kali sana ayseee sijawahi skia hiii gari kujipelekea moto yenyewe.
 
Chuma gani hiyo mbona naona mercedes kwa bonnet
 
Hiyo VW yako inabidi uweke injini ya 3s-gte ndio itafanya vizuri. Ambayo imetumika kwenye Toyota Caldina,Alteza na Celica.

Kama ni mtunzaji mzuri wa gari tafuta engine ya Nissan Skyline RB26DETT ukifunga hii performance ni kubwa zaidi hata ya injini hiyo ya awali ya Golf.
 

Lile li injuni la alteza linakaa kweli kwenye golf
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…