Engineer Hersi ataifikisha Yanga mbali ana kitu (mkataba wa Hero)

Engineer Hersi ataifikisha Yanga mbali ana kitu (mkataba wa Hero)

Tusiposhinda hili ni tatizo. Kama tunashinda si tatizo maana ukimwondoa mdhamini tunaobaki tunaweza lisha timu? Ila kama mdhamini yupo na ananufaika ila timu hainufaiki bora kutokuwa nae.
 
Pamoja na kuwa mi ni shabiki lia lia wa Simba lakini huyu jamaa ameibadili Yanga na ana Vission, club ya Simba imezungukwa na genge la wapigaji kuanzia mdhamini mkuu.

Kila mkataba wa Yanga kuna uwazi tofauti na Simba ambayo mikataba na matumizi ya hela wanaojua ni genge la wachache.

Leo Yanga imeingia mkataba wa miezi 18 na kampuni inayotengeneza pikipiki ( Hero).

Mkataba unaruhusu matawi ya Yanga kupata posho na kufaidika.
Simba tuna vyanzo vya kuingiza hela ila matumizi hayajulikani,mkataba wa bidhaa za Mo kwenye jezi ni siri za wachache,Simba App hela inakoingia wanajua wao, matangazo ya kamari shabiki bingwa wanajua wenyewe,hata michango ya wanachama kwa ajili ya uwanja wanasema ni matumizi mengine hatujui ni ya familia za watu au wakati hayakutumika kwenye ujenzi wa uwanja.





Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa anajitahidi sana kila uchao kuongeza vyanzo vya mapato Kwa timu yake. Jamaa ana akili anahitaji pongezi.
 
Uongozi wa Yanga umetengeneza ushindani kwenye idara zake na wafanyakazi Wana mikataba.

Endapo idara Yako haifanyi vizuri katika ubunifu wa kui ingizia klabu mapato ina maana hakuna sababu ya kufanya klabu indelee kuwa na wewe.
Hali iyo inaongeza ubunifu katika kui ingizia kipato idara/klabu.
 
Kwahiyo wenye akili akili toka wameongezeka sasa....

Kule kwingine kuna Mangungu na umbumbumbu unategemea nn?
 
Uongozi wa Yanga umetengeneza ushindani kwenye idara zake na wafanyakazi Wana mikataba.

Endapo idara Yako haifanyi vizuri katika ubunifu wa kui ingizia klabu mapato ina maana hakuna sababu ya kufanya klabu indelee kuwa na wewe.
Hali iyo inaongeza ubunifu katika kui ingizia kipato idara/klabu.
Safi sana..KPI inafanya kazi
 
Jamaa anajitahidi sana kila uchao kuongeza vyanzo vya mapato Kwa timu yake. Jamaa ana akili anahitaji pongezi.
Hersi na GSM walikua wana utaka mpira ..jamaa walianza na Maji Maji ya Songea wakaona kule ni kupoteza muda ..wakajipanga wakaingia Yanga
 
Uongozi wa Yanga umetengeneza ushindani kwenye idara zake na wafanyakazi Wana mikataba.

Endapo idara Yako haifanyi vizuri katika ubunifu wa kui ingizia klabu mapato ina maana hakuna sababu ya kufanya klabu indelee kuwa na wewe.
Hali iyo inaongeza ubunifu katika kui ingizia kipato idara/klabu.
Mkuu uongozi wa Yanga hauna urasimu mkubwa, Boss na mdhamini mkuu ni GSM, anayefuata ni Hersi ambaye ndo rais wa timu ,kwa upande wa wanachama yeye ndo wa mwisho,vingine ni vitengo vidogo, ambavyo viko chini yake.

Ukija Simba, Mdhamini/Rais ni Mo,CEO ni Kajuni,Mwenyekiti wa mashabiki ni Magungu na bado kuna vigogo wengi kwenye bodi yaani cycle ya ulaji na upigaji ni mkubwa wakati huko hata kama wanakula cycle ni ndogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lengo lako ni kuona timu ya Simba inasonga mbele kimaendeleo maana raslimali watu na vyanzo inavyo. Unasema kasoro unayoiona ni matumizi ya hivyo vyanzo (fursa) na uwazi katika mauzo na matumizi. Utashangaa anajaitokeza hapa Simba asili atakupinga bila vigezo na atatoa mifano ya Pan African au Azam.
Unanisema mimi

Nami nakujibu direct sitaki mambo ya ku back bite.

Nitajie mkataba hewa wowote ambao Simba amewahi kuutaja public.

Yanga tayari nimetaja hapo mkataba hewa wa Azam Tv wakati Agakhan ukiwa pending unasubiri muda tu uje ufe natural death kama huo wa Azam.

Au wewe kwenye kisimbuzi chako hiyo chaneli ipo??
 
Sijawahi kuiona mkuu,ila sisi kuna mengi hayaeleweki compare na upande wa pili,labda chain ya wapigaji wetu ni kubwa kuliko wao

Sent using Jamii Forums mobile app
Katika hayo ambayo hayaeleweki, kuna jambo ambalo linahusisha mkataba hewa?

Nitajie hayo ambayo hayaeleweki tupime uzito.

Simba kwenye mikataba ni timu ambayo imeonesha unafuu wa kuwa makini kuliko timu nyingine yeyote.

Nipe references kutoka Simba ambazo zinakufanya uione Yanga ipo bora eneo hilo.
 
active leader Injinia yupo mbele anaongoza mambo wengine wapo ubavuni wanafata magizo mambo yanaende.

huku kwetu muwekezaji kajaza matangazo kwenye jezi,return haijulikani na bado anakwambia anapata hasara.
 
Au unazungumzia mkataba wa punguzo la 5% kumuona daktari wa Aga Khan kwa sh. 70,000/= wakati kuna mahali daktani anaonwa kwa sh. 10,000/= bila punguzo? Akili ni nywele, muhindi ana akili kulko mwarabu na msomali
Hiyo ya Agakhan nainafanisha na vitambulisho vya machinga

Baadhi ya machinga waliamini ile kauli wakaenda benki kuchukua mkopo.
 
Katika hayo ambayo hayaeleweki, kuna jambo ambalo linahusisha mkataba hewa?

Nitajie hayo ambayo hayaeleweki tupime uzito.

Simba kwenye mikataba ni timu ambayo imeonesha unafuu wa kuwa makini kuliko timu nyingine yeyote.

Nipe references kutoka Simba ambazo zinakufanya uione Yanga ipo bora eneo hilo.
Hebu tuanze kwanza na ile 20b ya uwekezaji iko wapi?
 
Kwanini Hersi na sio uongozi wa Timu ya Yanga? Au ni jeshi la mtu mmoja?
 
Back
Top Bottom