Enyi wachambuzi wa mpira, mbona hampazi sauti juu ya uhuni uliofanywa na TFF kuwadhurumu watoto haki yao?

Hio jezi ni kumbukumbu kwa mchezaji unapo wapokonyonya wakati mashindano yamefika mwisho unazipeleka wapi? in addition kila tournament hua zinatengenezwa kits mpya
 
MBONA UNATETEA UJINGA MZEE KWA HIYO ZAWADI ANAPEWA NANI??

ACHA KUTETEA UJINGA
Zawadi linapewa Taifa mshindi.......
Kwa maana ya Shirikisho la mpira la nchi husika, na kama zawadi haina limitation za matumizi ni wao ndio wataamua inaenda wapi.
Wachezaji hawachezi Team za Taifa ili walipwe, ukiona mtoto wa miaka 15 analilia hela kuna shida pahala.
 
Washaokulaa bahashaaa haoo
 
Kwani hawana wazazi??
Kwahiyo walipwe wazazi? Tsh ngapi kila mmoja unapendekeza.
Vipi Gharama za kuwatunza wakiwa kule walitoa wazazi?
Vipi gharama za watoto mwakani watatoa wazazi?
Hivi nyie watu huwa mnawaza Namna gani?
 
Hayo
Hayo ni miongoni mwa maajabu yanayopatikana Tanganyika ndio maana wageni hawaishi kuja kushangaa mkuu.
Na mengi mno sema tu wengi huwa wanaambiwa wakiyasema hawataitwa tena na vipaji vyao vitateketea.
 
Hio jezi ni kumbukumbu kwa mchezaji unapo wapokonyonya wakati mashindano yamefika mwisho unazipeleka wapi? in addition kila tournament hua zinatengenezwa kits mpya
Kupokonywa una maanisha nini?
Wachezaji wamerudisha Jezi.
Hawajapokonywa......
Na sioni hoja hapa, ni lini Jezi mtu anaondoka nazo Bongo hii?
Kwani hamfahamu Jezi zinafuliwa......

Ni vizuri kama jezi wangeondoka nazo, ila kuambiwa wazirudishe haipaswi kuwa hoja ya malalamiko.
 
Hio jezi ni kumbukumbu kwa mchezaji unapo wapokonyonya wakati mashindano yamefika mwisho unazipeleka wapi? in addition kila tournament hua zinatengenezwa kits mpya
Uonevu tu. Mbaya zaidi hilo shirikisho lina mkataba na Sandaland kwa ajili ya kudhamini jezi, nk!! Halafu watoto baada ya kutumia jezi, eti wanatakiwa kuzirejesha!!

Wizi mtupu!! 😁
 
Kw
Kwa hiyo walikuwa wanajitolea na hivyo hawapaswi kupewa hamasa?
 
Endelea kuchelewa kusikia.
Kwani TFF wamepewa fedha zitokanazo na hayo mashindano ama hawaiupewa?

Km wamepewa,ni kwa nini?
 
Kw

Kwa hiyo walikuwa wanajitolea na hivyo hawapaswi kupewa hamasa?
Mtoto wa miaka 15?
Analipwa? Ni nchi gani inawalipa watoto wa miaka 15.
Mpira wa team ya Taifa haijawahi kuwa ni kuhusu Fedha, ni Pride ya Kuwa Mtanzania.
Pandikiza mawazo ya malipo kwa watoto wa miaka 15.
Miaka 10 mbele utaona unakuwa na team ya taifa ya namna gani.
 
Kwa hiyo baada ya kuzirejesha hizo jezi, mnazipeleka wapi? Mnaenda kuziuza, kuzigawa kwa wajumbe wenu wa TFF! Au mnaenda kuzihifadhi kwa ajili ya mashindano yajayo?

Mlichokifanya kwa hao watoto siyo poa hata kidogo. Yaani nyinyi ambao hata kupiga danadana tu hamuwezi, mnajilipa posho za kila aina!! Halafu watoto waliohangaika kuwapatia hayo mafanikio, mnaishia kuwapa tu nauli ya kurejea makwao!! Eti kwa sababu ni watoto!!

Mlishindwa hata kuwanunulia zawadi zinazoendana na umri wao kama motisha, kutokana na hicho walichokifanya!! Acheni ubabaishaji nyinyi.
 
Jezi inarudishwa kama mashindano yana endelea yakifika mwisho jezi inarudishwa kufanya nini? Kila shindano lina bajeti yake na kits zake hao watoto wanahitaji hivyo vifaa kuendeleza careers zao tena ingependeza baada ya mashindano wapewe zaidi kumbuka wengi wao wanatoka familia duni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…