Enzi za utotoni,chakula gani kikipikwa usiku home kwenu ulikuwa unachukia?

Aisee kande...... Utasema nilikua na allegi nalo
 
Kuna siku nilikua na njaa sana halafu mfukoni nina 500. Ilikua ni usiku saa nne naishi mbali na nyumbani sina wa kumuomba kwa nyumbani na hua sipendi kuomba vya watu.

Nikanunua maembe matano ya shilingi mia nikarudi nayo nyumbani ili nile. Kufika nagundua maembe yote mabovu.

What do I do?

Nikamenya maembe yote nikazima taa nikajifunika na shuka nikala nikalala.
 
kipikwe chochote kile lakini mboga isiwe kunde....! dah halafu bi mkubwa aligunduaga yaan kama ni ugali atakukodolea macho mpaka aone tonge lina kunde za kutosha, vivyo hivyo kwenye wali.
 
Duh!!
 
Ukirudi nyumbani jioni saa kumi na mbili ukiwa umetoka kucheza usiposikia wakipeta nyungo au kuona maji meupe yamemwagwa ujue kishanuka tayari

I miss those days
 
Ukirudi nyumbani jioni saa kumi na mbili ukiwa umetoka kucheza usiposikia wakipeta nyungo au kuona maji meupe yamemwagwa ujue kishanuka tayari

I miss those days
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Duuh ulikuwa na roho ngumu!! Unakula mafinyofinyo.
 
Nilikuwa nachukia sana Tambi na mboga ya cabbage
 
Binafsi ilikuwa ukipikwa ugali usiku nilikuwa nachukia sana,nakula matonge mawili tu nimeshiba naenda zangu kulala
Kibulu..... Siku kikipikwa kibulu..... unatamani kulia.... ila hakuna namna..... ni lazima kula.....!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…