Enzi zetu waliosoma shule binafsi yani private ni waliofeli

Enzi zetu waliosoma shule binafsi yani private ni waliofeli

Enzi zile shule za serikali ziliheshimika sana,
Ningekuwa waziri wa Elimu kwa sasa, ningefanya mapinduzi kama yale ya Viwanda kwenye historia yaliyofanyika 1760 - 1840 kwa kuajiri waalimu wa Hesabu na Sayansi tu kwa shule za msingi na Sekondary.
Kwa kufanya hivyo naamini Ndani ya miaka mitano ungeshangazwa na matokeo.........heshima ingerudi......
 
Tunakumbushana tu, ndivo ilivokuwa.

Shule private maarufu enzi zetu kulikuwa Jitegemee, Vituka na sait Antony Mbagala
huku tarime kulikuwa na Shirati sec school.

Je wewe unakumbuka lipi? Gen Z mtupishe.
Mkuu imekosea kusema ni waliofeli! Ukweli ni kwamba ni wale waliokosa nafasi ya kwenda shule za serikali. Hii ilitokana na shule za serikali kuwa chache. Private kulikuwa na vichwa hasa, nakumbuka enzi zetu tuliokuwa private kama GESECO kwenye mitihani ya ujirani mwema (Mock) tulikuwa tunawakimbiza akina Sengerema, Nsumba na wengine kama machizi!
 
Tunakumbushana tu, ndivo ilivokuwa.

Shule private maarufu enzi zetu kulikuwa Jitegemee, Vituka na sait Antony Mbagala
huku tarime kulikuwa na Shirati sec school.

Je wewe unakumbuka lipi? Gen Z mtupishe.
Hatukuwa tunafeli,tulikuwa hatukuchaguliwa!Sasa mtu anarudia ya msingi hadi mara3 ndio kwa bahati anachaguliwa!
 
Tunakumbushana tu, ndivo ilivokuwa.

Shule private maarufu enzi zetu kulikuwa Jitegemee, Vituka na sait Antony Mbagala
huku tarime kulikuwa na Shirati sec school.

Je wewe unakumbuka lipi? Gen Z mtupishe.
Waliokuwa wanasoma shule private ni wale waliofeli mitihani ya kuingia kidato cha kwanza na kidato cha tano, enzi hizo walikuwa takataka, wengi wao walikimbilia shule za seminari, pale Mbeya tulikuwa na Sangu Secondary School, na Darisalama palikuwa na Kinondoni Muslim, kule Kilimanjaro boys' enzi zile private school walichokuwa wanakiweza ni michezo tu,mashindano ya UMISETA, pia wengi walikuwa wanyonge wanyonge watemi walikuwa shule za serikali, ukienda kule Ruvuma utakuta Kaigo,Box 2 pale Mbeya utakuta Rungwe na Iyunga, Pwani utakuta Kibaha Sec, Kagera Ihungo, Kigoma Sec, Ndanda, Masasi girls,Mazengo,Ilboru,Mzumbe,Mazengo n,k ilikuwa raha sana, kila kitu bure,tunakatiwa tiketi kwenda na kurudi nyumbani kwa treni au mabasi ya Relwe unachagua tu wapi uende wakati wa likizo. Ukiwa kiranja mkuu unakuwa kama raisi, unakuwa na menu yako na chumba chako binafsi cha kulala. Ukikosea unalambwa bakora au unapewa adhabu ya kuchimba visiki, tuliosma wengi tulikuwa watoto wa masikini, utakuta una kaptula moja na shati moja, suruali unaazima. Wengine walikuwa wanaamua kubaki mashuleni wakati wa likizo na kufanya vibarua vya kulima ili waweze kujikimu,makwao hali ilikuwa ni tete kimaisha, wengi wao hivi sasa ndio wanatupangia maisha na kutoa maamuzi ya hovyo hovyo wamesahau walikotoka.
 
Tunakumbushana tu, ndivo ilivokuwa.

Shule private maarufu enzi zetu kulikuwa Jitegemee, Vituka na sait Antony Mbagala
huku tarime kulikuwa na Shirati sec school.

Je wewe unakumbuka lipi? Gen Z mtupishe.
Si kweli kwani magazeti yalikuwa yanatoa malalamiko ya wanafunzi wa masikini waliofaulu lakini nafasi zao zikachukuliwa na akina Nape. Nikukumbushe kilichoua shule za vipaji maalumu, watoto wa masikini ndio waliokuwa wakifaulu vizuri sana na kuanzishiwa hizo shule za vipaji maalum, lakini viongozi wakaingilia kwa kuwapeleka watoto wao ambao hawakufaulu kwenye hizo shule kiasi kwamba walimu walianza kulalamika kupewa wasiojua kusoma na kuandika.
 
Tunakumbushana tu, ndivo ilivokuwa.

Shule private maarufu enzi zetu kulikuwa Jitegemee, Vituka na sait Antony Mbagala
huku tarime kulikuwa na Shirati sec school.

Je wewe unakumbuka lipi? Gen Z mtupishe.
1. Al Haramain Sec - Shauri Moyo
2. Mzizima - Upanga
3. Loyola - Mabibo
4. Navy - Kigamboni
5. Air wing - Ukonga
6. Shaban Robert - Upanga
7. Nuruyakin - Mwembe yanga
8. Lombeta - Kilema
9. Agape Lutheran - Moro
10. Forest - Moro
 
Back
Top Bottom