EPA na mambo yake

wakati mnazitumia na kuchekelea mlikuwa hamjui zitatumika kwenye mdhamana!!!
nexty tym muwe makini
 
Hivi hii thread imewekwa ili tuwaonee huruma kwa kushindwa kutimiza mashariti ya dhamana au imewekwa kwa sababu zipi?

JF si sehemu ya kutetea uovu, waache waozee huko huko, maana hata mtaani hatuwataki. Au na wewe unaye ndugu yako huko?
 
Hivi hii thread imewekwa ili tuwaonee huruma kwa kushindwa kutimiza mashariti ya dhamana au imewekwa kwa sababu zipi?

JF si sehemu ya kutetea uovu, waache waozee huko huko, maana hata mtaani hatuwataki. Au na wewe unaye ndugu yako huko?

DHAMANA NI HAKI YAO. Punguzeni chuki, kama hela ya EPA inakuuma mbona hupi kelele hela walizochukuw CCM kwa mgongo wa kagoda uchaguzi wa 2000 na 2005 EPA ilitumika kuua demokrasia nchini, hao waliokamatwa ni vichuguu vilivyofuata nyayo za mlima kilimanjaro (CCM & RAs)
 
Hivi hii thread imewekwa ili tuwaonee huruma kwa kushindwa kutimiza mashariti ya dhamana au imewekwa kwa sababu zipi?

JF si sehemu ya kutetea uovu, waache waozee huko huko, maana hata mtaani hatuwataki. Au na wewe unaye ndugu yako huko?
..Safi sana kashaija, mi pia sina huruma nao hata kidogo ulafi wao umetusababishia madhira mengi tu wangeendelea tu kunyea debe kwanza watie akili....
 
Hatustahili kuwa wapungufu wa fikira eti tu kwa sababu tunapiga vita ufisadi!!! Nasema ni vema hao jamaa nao wakaangaliwa kwa jicho hilohilo la kifisadi, maana si vema kwao kuanza kuleta monopoly ktk kuhakiki nyaraka za hao watuhumiwa, ni vema jf irejee kwa kutambua kuwa ktk maeneo ambayo yamekuwa kero ni aina hii ya huduma nyoronyoro ambayo mwishowe watu wanahongwa ili watoe hizo data kwa mahakama ili haki ya dhamana itendeke.

Suala si huruma bali mabadiliko kiutendaji ktk kumhudumia mwananchi yeyote yule bila kujali hali yake.
Change waungwana
 
Kwani hela zote wamezichezea ni wapuimbavu kiasi hicho Alafu kwa nini hawakukimbia nchi hivi hawa wezi ni wa aina gani jamani mimi sijasikia wezi wajinga hivi ha ha ha ha au waliambiwa nothing will happen to them they own the country. Thats why we here the economi will go down Please what economy. Tanzanians have the right to very angry they are being played like toys.
 
Nyie si mna hela wapeni hongo kama mlivyohonga kupata hizo Hela za EPA. Au mghushi hizo documents.

Ila poleni sana
 
Jamani hii ni habari ya kuskitisha sana kama si kusosononesha watanzania kumbe ukiiba pesa nyingi unheshimika mpaka jela!!!
Wale wahalifu wa epa wanishi maisha ya peponi,inasemekana wako katika vyumba bora kabisa na vitanda murua wanachomiss haswa ni wake zao na hivyo kuwaongezea hamu !!!gazeti la nipashe linasema hata yule rijali wetu """zombe ""nae anishi room hizo hizo

babu,kubwa!!!
 
Haya Rostam tena huyooooo!!!! Na tuone kama watamgusa

Raia Mwema - Siri mpya ya EPA yaiumbua Kagoda

http://www.raiamwema.co.tz/images/P/8/1112/nyaraka.jpg

 
Watuhumiwa wa EPA waponda raha Keko

2008-11-13 10:21:29
Na Joseph Mwendapole

Washitakiwa 18 wanaokabiliwa na mashitaka tofauti ikiwemo kughushi na kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wanaishi katika vyumba maalum (VIP) katika gereza la Keko tofauti na mahabusu wengine.

Uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa, baadhi ya washitakiwa hao wamewekwa katika vyumba maalum (VIP) katika gereza la Keko ambapo wametengwa kabisa na maabusu wa kawaida maarufu kama walalahoi.

Chanzo cha gazeti hili kilielezwa kuwa, Jayantkumar Patel maarufu kama Jeetu Patel na Jonson Lukaza, wanaishi katika vyumba vya VIP, ambapo Jeetu Patel inadaiwa kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu huku Lukaza akidaiwa kuwa na maradhi kama hayo pia.

Hata hivyo, Ofisa Uhusiano wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Omari Mtega aliliambia gazeti hili kwa njia ya simu jna kuwa, katika magereza yote hapa nchini, hakuna vyumba vya VIP.

Kamishna Mtega alisema ni jukumu la Magereza kuhakikisha ulinzi na usalama wa wahalifu hivyo ni muhimu walindwe kwa utaratibu waliojiwekea.

Aliongeza kuwa, jamii nzima inawachukia watuhumiwa wa EPA hivyo jeshi hilo haliwezi kufanya uzembe kwa kuwachanganya na watuhumiwa wa makosa mengine.

``Unasikia mwandishi, `EPA is EPA`kwa hiyo sio jukumu la vyombo vya habari kujua usalama wa watuhumiwa na wanalindwaje na hatuwezi kuwachanganya na watuhumiwa wengine kwa kuwa wanaweza wakauawa na lawama zikaenda kwa jeshi,`` alisema.

Aliongeza kuwa, mahabusu ambao ni watuhumiwa sugu kwa makosa tofauti, hawachanganywi na wale wanaofikishwa gerezani kwa mara ya kwanza.

``Kwa mfano, ili kuimarisha ulinzi na usalama wa watuhumiwa gerezani, jeshi haliwezi kufanya makosa kwa kuwachanganya na Abdallah Zombe kwa sababu wanaweza kumdhuru au hata kumuua hasa wale waliokamatwa kwa tuhuma mbalimbali kabla Zombe hajakamatwa kwa tuhuma za mauaji,`` alifafanua Kamishna Mtega.

Baadhi ya masharti ya dhamana ambayo wamekuwa wakipewa ni pamoja na kulipa nusu ya fedha wanazodaiwa kuiba BoT au hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.

Sharti lingine ni kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa serikali, kuwasilisha hati za kusafiria na kuripoti polisi kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi na kutosafiri nje ya Dar es Salaam bila kibali cha Mahakama.

Hivi karibuni, gazeti moja liliripoti kuwa, serikali ilikuwa ikifanyia ukarabati vyumba vya VIP kwa ajili ya vigogo waliotarajiwa kufunguliwa mashitaka kutokana na wizi uliotokea BoT.

Hata hivyo, baada ya taarifa hizo, serikali ilikuja juu na kukanusha kuwa ukarabati huo haufanywi kwa ajili ya vigogo bali ni taratibu za kawaida wamewekwa katika vyumba maalum (VIP) katika gereza la Keko ambapo wametengwa kabisa na mahabusu wa kawaida maarufu kama walalahoi.

Chanzo cha gazeti hili kilielezwa kuwa, Jayantkumar Patel maarufu kama Jeetu Patel na Jonson Lukaza, wanaishi katika vyumba vya VIP, ambapo Jeetu Patel inadaiwa kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu huku Lukaza akidaiwa kuwa na maradhi kama hayo pia.

Hata hivyo, Ofisa Uhusiano wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Omari Mtega aliliambia gazeti hili kwa njia ya simu jna kuwa, katika magereza yote hapa nchini, hakuna vyumba vya VIP.

Kamishna Mtega alisema ni jukumu la Magereza kuhakikisha ulinzi na usalama wa wahalifu hivyo ni muhimu walindwe kwa utaratibu waliojiwekea.

Aliongeza kuwa, jamii nzima inawachukia watuhumiwa wa EPA hivyo jeshi hilo haliwezi kufanya uzembe kwa kuwachanganya na watuhumiwa wa makosa mengine.

SOURCE: Nipashe
 
usishangae hilo peke yake. watuhumiwa wengine wakikosa wadhamini, hupelekwa gerezani na kungojea siku zisizopungua 14 kesi itakapotajwa tena ndio suala la dhamana lizungumzwe. hawa, kila siku wanarudishwa mahakamani kuangalia kama masharti ya dhamana yametimia. leo nasikia wawili wengine wametimiza masharti ya dhamana na sasa wako nje. ndio haki hiyo!!!

macikus
 


Kwa nini wachechetuke kukimbia wakati wadanganyika wakiongozwa na KJ ndio wajinga wao?
 
Haya Rostam tena huyooooo!!!! Na tuone kama watamgusa

Halisi
Rostam Aziz ingekuwa dawa...ingetibu magonjwa mengi zaidi ya mwarobaini ila kwa sababu RA ni sumu, ubaya wake unazidi wa arsenic!
 


Dr. na Mheshimiwa Dr. Slaa. Pamoja na kwamba sikumbuki tarehe rasmi ya uteuzi wa Prof.Ndulu kuwa governor ni kwamba Prof. Nduli hausiki kabisa na sakata la EPA.

Kwa taarifa za uhakika ni kwamba, Prof. Ndulu lilikuwa ni pendekezo la World Bank kwa kuwa Beno alikuwa yuko hapa WB Office Dar na baadaye HQ W. DC ndipo alipotakiwa aje hapa TZ. Alichofanya Rais ni kumfanya Naibu huku akisubiri namna ya kumaliza term ya Balali. Ndulu alitoka D,C akiwa na taarifa zote kuwa anakuja kuwa Governor wa Benki. Kilichokuwa kinasubiriwa ni muda tu.

Wakati anakuwa governor soo la EPA tayari siku nyingi. Hata Annual Report ya BOT 2006 ilichelewa sana kuchapwa kwa sababu hiyo na sielewi kama mpaka sasa imeshachapwa. Nakumbuka kuna habari zilitakiwa kutoka ndani ya ripoti hiyo ili kuandika dicument fulani lakini kila ofisa au mkurugenzi aliyeulizwa kuhusu report alijibu "iko mezani kwa gavana!!!!? Tuwe just katika kuhukumu wengine. Habari ndo hiyo.
 
 
 

Lazima tufike mahali tupiginie hata hili kwani wao ni nani mpaka wakae V.I.P? mbona wengine wanachanganywa. Na hapa ndipo inapoonyesha dhamira ya wazi kwa serikali hii ya KIFISADI kuwatetea wahalifu wanaoigusa. Tuanzishe mapambano mengine nao wakaonje selo la kawaida ili watoto wa Keko na wapi sijui nao wawafaidi ili wajue utamu wa selo na wakitoka wakawaonyeshe wake zao na watoto maana wanaweza kuishia kushitakiwa na baada ya uchaguzi wakaachiwa hawa.
 
Hivi kuna ukweli kwenye hii habari kwamba wanalala vyumba vya VIP? Ama watu tu wanadhani hivyo. Kuna wengine wanadai kwamba hawa jamaa wanapelekwa makwao usiku na kurejeshwa asubuhi. Ukweli ni upi? Na kuna evidence gani?
 
hILO LA LURUDISHWA USIKU HALIPO KABISA.....TENA FUTA USEMI WAKO....SUALA NI KULETWA KILA SIKU AJILI YA DHAMANA INGAWA NAJUA NI HAKI YAO MAANA DHAMANA IKO WAZI...KAMA INGEFUNGWA WASINGELETWA....HATA WEWE KABWELA KAMA MIMI TUTAFANYIWA HIVYO,KULETWA KILA SIKU...KAMA WADHAMINI WETU WATAKUWA WANAKAMILISHA MASHARTI BASI REMOVAL ORDER INATUMWA GEREZANI....NA UNALETWA
 

Kinachozungumziwa hapa ni usawa mbele ya sheria. .Hapa kuna double standards na ndicho kinacholalamikiwa na siyo ati kwanini wanapewa dhamana.
Kiutaratibu, kesi hutajwa kila baada ya siku kumi na nne.Na hapo ndipo uamuzi wa masuala yote yanayomhusu mshtakiwa ikiwa ni pamoja na kuangalia kama masharti ya dhamana yametekelezwa hufanyika.Kinachoshangaza kama ni kweli ni hili la washtakiwa wa EPA kurudishwarudishwa mahakamani kabla ya huo muda ati kwa kile kinachosemekana kuwa masharti ya dhamana yametekelezwa. Hii inaleta dhana kuwa hawa jamaa wanatendewa tofauti na washtakiwa wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…