Eric shigongo hakusoma shule ya sekondari kabisa

misasa

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2014
Posts
14,244
Reaction score
10,073
Jamaa amekuwa inspirational kwa rika tofauti,mjasiriamali mwenye mafanikio ila historia ya elimu yake ya kushangaza sana alifeli darasa la saba mara mbili na hajasoma secondari kabisa ila ni mwandishi wa hadithi na vitabu mzuri.

Chanzo: Jana alivyohojiwa na Profesa Shaka Ssali wa VOA katika kipindi straight talk of Africa.
 
Kajitahidi ukifananisha na kundi kubwa likiokosa elimu. Lakini apunguze habari za umbeya na uongo kwenye media zake. Credibility ya business inajengwa na clean reputation.
 

Kwa kweli ES pamoja na mapungufu yake anahitaji sifa aisee...nadhani alisoma kozi moja ya afya ya zamani sana inaitwa 'Rural Medical Aid' (RMA) wakitakiwa kufanya kazi vijijini kutoa huduma za afya. Ila kaishia mjini. Nakumbuka wakati bado nasoma udaktari Muhimbili, alikuwa anakuja na kujichanganya na wanafunzi kuingia wodini. Alikuwa anachagua wale wagonjwa wako hoooi na matatizo ya kutisha tisha..anawahoji kwa kificho na kupiga picha, anapublish kwnye gazeti lake la Uwazi. Hata gazeti lenyewe alikuwa anaandikia pale internet café MTC Muhimbili. Umaarufu ukaanzia hapo and now he is on 'Straight Talk Africa, VOA' interviewed by Prof Shaka Ssali! Hongera zake..penye nia pana njia.
 

watanzania atupendi kuwa appreciate wenzetu kama wanafanya vizuri eti kuna watu wanasema anakopi na kupesti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…