Erick Kabendera kupitia Kitabu chake: Ben Saanane aliuawa na Rais Magufuli na maiti yake ikatupwa Mto Rufiji

Mwangosi bomu la machozi la ffu lilimpata tumboni,mi lilinipiga mgongoni 2002 maandamano ya waislam,lengo la bom la machozi siyo kuua
Picha ya mwangosi akipigwa bomu ziliwekwa mitandaoni na magazetini uliziona? Hivyo ndio mabomu ya machozi yanavofyatuliwa kwa kupigwa close range tena tumboni kwa mtu? Unataka kusemaje? Umeamua kutetea kilicho chako kiimani kipuuzi kabisa
 
Kwani umeambiwa hiyo ndio siku aliyomuua Ben Saa Nane?
 
Tumshukuru Mungu kwa kuwa awamu hii watu hawatekwi na kuuawa sababu za kisiasa,
Awamu hii watu wanatekana na kuuana. Awamu ya Magufuli ni yeye mwenyewe alikuwa anamiliki kikundi cha "wasiojulikana" na kilikuwa chini ya Makonda.

Haya yanayotokea sasa hivi ni athari alizoanzisha Magu ambazo watu wameiga, both CCM na Upinzani. Wanatekana
 
JPM kama alifanya hivyo kweli! Mungu alijibu mapema
 
Ni vigumu kuaminika, ni vigumu kuthibitishika.

Lakini wanasema Magufuli alikuwa na faili Mirembe.

Kuna mambo mengi kafanya yalikuwa magumu kuaminika.

Alivyotekwa Mo Dewji nilipata tatizo sana kuamini kuwa utekaji ule unaweza kuwa na mkono wa serikali. Niliona si rahisi serikali kifanya utekaji hivyo. Sikuziea utamaduni wa serikali kuteka watu kwa wazi hivyo.

Lakini, baadaye imejulikana kwa ushahidi wa kuridhisha kwa kiasi kwamba serikali imehusika sana kwenye utekaji.

Mara nyingine hatutaki kukubali kuwa vitu fulani ambavyo sisi tunaviona vibaya sana vinaweza kutokea.

Ukweli ni kwamba, ni vigumu kuhakikisha Magufuli aliua au hakuua. Kama kaua kweli, wanaojua na kuweza kuaminika (mfano walinzi wa ndani wa Ikulu) hawawezi kukubali kwa sasa. Labda baadaye.

Mawazo ya watu hayataki kukubali ukweli wa kwamba "hapa hatuna jibu la uhakika, tusubiri tuchunguze tupate jibu la uhakika".

Karibu mara zote yanataka kuchukua upande na kuuamini bila ushahidi wa kutisha.
 
Umeandika maelezo marefu.

Na mimi nakuuliza hoja yako ni nini kwenye maelezo yote haya?
 
Hadithi za kipumbafu kabisa...

Namshukuru Mungu, mauwaji na utekaji haujaisha...

Hivyo watu wanaotumia akili zao wanajua tatizo liko wapi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…