bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,679
Anachukua mikoba ya Luis Enrique alikua kocha wa Atl Bilbao.
Karibu Catalunya Ernesto Valverde.
=====
Kocha Ernesto Valverde ametangazwa rasmi na uongozi wa Barcelona kuwa ndiye mrithi wa Luis Enrique.
Kocha huyo mpya kutoka klabu ya Athletic Bilbao, alisema kwamba kukabidhiwa mikoba kuinoa Barcelona ni jambo kubwa na gumu hata hivyo amejipanga vyema kwa ajili ya kukisuka kikosi hicho ili kuongeza makali msimu ujao.
Alisema kwa kuanza atahakikisha wanafanya usajili ambao utasaidia timu hiyo kufanya vyema kwenye La Liga msimu ujao na mashindano ya Ulaya.
Rais wa Barcelona Josep Bartomeu alisema, “Nimeongea na Varverde na kumweleza uamuzi wetu, naye ameupokea kwa moyo mkunjufu.”
“Alisema amefurahia uamuzi huo na yupo tayari kukabiliana na changamoto zote zinazohusiana na kuwa kocha mkuu wa klabu kubwa kama Barcelona.
‘Tuna muda mwingi wa kuzungumza naye, tumejirdhisha kutoka na uwezo wake mkubwa pamoja na elimu yake pia ana uzoefu wa kutosha.”
Kocha huyo amekuwa akipenda zaidi soka la vijana ikiwa ni pamoja na kuwa na mtindo wake wa kipekee ambao hata hivyo unaelekeana na mambo mengi yanayofanyika Barcelona.
Ververde alihamia Athletic Bilbao na kuwa kocha timu ya vijana mwaka 2002, kabla ya kupandishwa kuwa kocha mkuu msimu uliofuata.
Pia amewahi kuzifundisha Espanyol, Olympiacos, Villarreal na Valencia kabla ya kurudi tena Athletic mwaka 2013.
Kocha huyo mwenye miaka 53 alitangaza uamuzi wake wa kujiunga na Barcelona baada ya kuitumikia timu yake ya zamani kwa miaka minne.
Luis Enrique akinyanyua kombe la Copa Del Rey enzi zake akiwa Barcelona ambayo anaachana nayo rasmi.
Karibu Catalunya Ernesto Valverde.
=====
Kocha Ernesto Valverde ametangazwa rasmi na uongozi wa Barcelona kuwa ndiye mrithi wa Luis Enrique.
Kocha huyo mpya kutoka klabu ya Athletic Bilbao, alisema kwamba kukabidhiwa mikoba kuinoa Barcelona ni jambo kubwa na gumu hata hivyo amejipanga vyema kwa ajili ya kukisuka kikosi hicho ili kuongeza makali msimu ujao.
Alisema kwa kuanza atahakikisha wanafanya usajili ambao utasaidia timu hiyo kufanya vyema kwenye La Liga msimu ujao na mashindano ya Ulaya.
Rais wa Barcelona Josep Bartomeu alisema, “Nimeongea na Varverde na kumweleza uamuzi wetu, naye ameupokea kwa moyo mkunjufu.”
“Alisema amefurahia uamuzi huo na yupo tayari kukabiliana na changamoto zote zinazohusiana na kuwa kocha mkuu wa klabu kubwa kama Barcelona.
‘Tuna muda mwingi wa kuzungumza naye, tumejirdhisha kutoka na uwezo wake mkubwa pamoja na elimu yake pia ana uzoefu wa kutosha.”
Kocha huyo amekuwa akipenda zaidi soka la vijana ikiwa ni pamoja na kuwa na mtindo wake wa kipekee ambao hata hivyo unaelekeana na mambo mengi yanayofanyika Barcelona.
Ververde alihamia Athletic Bilbao na kuwa kocha timu ya vijana mwaka 2002, kabla ya kupandishwa kuwa kocha mkuu msimu uliofuata.
Pia amewahi kuzifundisha Espanyol, Olympiacos, Villarreal na Valencia kabla ya kurudi tena Athletic mwaka 2013.
Kocha huyo mwenye miaka 53 alitangaza uamuzi wake wa kujiunga na Barcelona baada ya kuitumikia timu yake ya zamani kwa miaka minne.
Luis Enrique akinyanyua kombe la Copa Del Rey enzi zake akiwa Barcelona ambayo anaachana nayo rasmi.