eSIM ni kitu gani? nini tofauti yake na SIM(Line za kawaida)?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Wakuu nimeona baadhi ya simu zinakuwa na sehemu ya SIM na eSIM. ni sawa na hizi zenye dual SIM? Line za eSIM ni kitu gani. Tofauti yake na line za kawaida nini? Unaweza kuzitumia Bongo? Natanguliza shukrani.
 
Wakuu nimeona baadhi ya simu zinakuwa na sehemu ya SIM na eSIM. ni sawa na hizi zenye dual SIM? Line za eSIM ni kitu gani. Tofauti yake na line za kawaida nini? Unaweza kuzitumia Bongo? Natanguliza shukrani.

Kifupi tu, eSIM ni SIM card iliyojengewa moja kwa moja kwenye simu toka kwa mtengenezaji wa simu, si kama hizi SIM card za kuweka na kupachua...

Pia eSIM inakuwa haihusiani na provider yeyote wa mawasiliano ya simu, yaani mtumiaji wa simu anakuwa huru kuamua wakati gani atumie mtandao upi...
 
Arigato mkuu.
 
Kwakweli na mimi leo ndio nimeifahamu eSIM.
 
Umeeleweka Lakini Fafanua Kidogo Unaposema Haihusiani Na Providers Yoyote
Je Itatumikaje Sasa,
 
Umeeleweka Lakini Fafanua Kidogo Unaposema Haihusiani Na Providers Yoyote
Je Itatumikaje Sasa,

Ukiwa na simu ambayo ipo compatible na eSIM, unafanya kuinstall eSIM profile ambayo hutolewa na waendeshaji/watoa huduma mathalani tiGO, Airtel, Voda n.k, baada ya kuweka hiyo profile itakuwezesha kununua e-SIM bundles (kama ilivyo kwa bundles za SIM ya kawaida) unapozihitaji, popote ulipo...

Pia unaweza kutumia profiles toka kwa mobile operators tofauti na ukajiandikisha kwa wakati mmoja kwa bundles/plans kadha wa kadha kulingana na mahitaji yako...
 
Mimi nimeona hii kwenye simu ni provider gani kwasasa hap TZ
 
Hapo Sawa
Acha Makafr Watuletee Technology Siye Tutumie
Mbna hii ipo kabla hata ANDROID haijazaliwa
IPhone haijulikani itakuja lini
Yaan hii ipo tangu 2000s simu hata hapa TANZANIA baadhi zilikuwa zinatumika hiyo
Zilizokuwa zinatoka nje hasa ULAYA na MAREKANI
Ilikuwa zinakija hazina sehemu ya LINE mpk uende makao makuu edhi hizo
 
Mkuu
Bila Shaka Zilikuwa Zinakuja Kwa Uchache Ndiyo Maana Limekuwa Kama Jambo Jipya Kumbe Ni La Zamani Kidogo
 

Kwahiyi kwa sasa kama simu yako ina Esim unatakiwa ufanyaje ili kuwezesha huduma hii ya pili ukiacha line physical??
 
Usikariri kaagize iphone 14 itokee marekani isiwe global iwe ya amerika uone kama utapata tundu la kuweka laini
 
Kwahiyi kwa sasa kama simu yako ina Esim unatakiwa ufanyaje ili kuwezesha huduma hii ya pili ukiacha line physical??
Mkuu kipindi hicho nilikuwa naona tu wanaelekezana uende MAKAO MAKUU sasa sijui walifanikiwa au ilikuaje ila nakumbuka miaka hiyo HataTTCL walitoaga simu za AINA hiyo hazikuwa na sehemu ya kuweka laini
Ilitokeag kuna mtu alikiokotaga kimeunganishwa na TTCL kila tukiatafuta tutie laini wapi JAMAA akiwasha tu kinapigwa na mwenyewe mpk akairudisha

Mimi nimeongelea kuwajuza kwamba hiyo mifumo sio mipya ni tangu zamani
Hiyo story nilokupigia ni mwaka 2004 au 2006 km sikosei sema sikuwa najua kama ndo inaitwa Esim ila kuanza kuiona nilianza kuiona kitambo sana

Kuna mdau uko juu katoa ufafanuzi kuwa unaenda TIGO au VODA wanakufanyia configuration nadhani itakuwa hivyo
Mm sikuwahi kumiliki simu ya aina hiyo na ni miaka mingi sana hata 15 inapita tangu mara ya mwisho nione simu ya hvyo
nilivyoona hii thread ndio nikakumbuka
 
Nimekuelewa sikusoma vizur hoja yako .Kumbe ulimaanisha nani aliewahi kuanza kuja na esim system mie nikanukuu vibaya kuhusu Iphone .Sasa nikuweke wazi nowdayz hata TTCl hawana hio huduma tena plus voda na Tigo kuhusu wengine hawa sikuwahi kuulizia ila huko nimejibiwa mara kadhaa hivo
 
Pamoja man wangu
 
Usajili wake kwa biometrics inakuwaje?
 
Hakuna huduma ya eSIM Tanzania,wala haijawahi kuwepo. Nimeenda tigo, Vodacom na Airtel na Samsung yenye line moja na esim nimeambiwa hivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…