Ester Matiko: Kama Chama kikiona kuna mwingine anafaa zaidi ya Ester Matiko, niko tayari

Ester Matiko: Kama Chama kikiona kuna mwingine anafaa zaidi ya Ester Matiko, niko tayari

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Baada ya jana wabunge wa viti maalum kuapishwa, waandishi wa habari walifanikiwa kufanya mahojiano madogo na mbunge mmojawapo, Ester Matiko huku wengine wakigoma. Yafuatayo ni maswali kutoka kwa waandishi na majibu kutoka kwa Ester Matiko.

MWANDISHI: Mmepata baraka za Chama?

MATIKO: Nadhani wote tunajua taratibu za viti maalum mpaka kuweza kufika wabunge kuteuliwa, kuna utaratibu ambao unaendelea ndani ya chama kupitia wings mbalimbali na baadae chama kinabariki na majina yanaenda kwenye tume ya Taifa ya uchaguzi, binafsi nilitaarifiwa nimeteuliwa ndio maana nimefika hapa kuja kuapa.

MWANDISHI: Ulitaarifiwa na katibu?

MATIKO: Na mamlaka husika

MWANDISHI: Lakini katibu wa chama anasema hana taarifa na hilo na watachukua hatua kali dhidi yenu, hili unalizungumziaje?

MATIKO: Sijui zaidi ya hapo, kwa uchache wetu ambao tumekuja hapa, nipende tu kuwaambia watanzania, wategemee makubwa kwetu pamoja na kwamba tuko 19. Tunajua yote yaliyojiri kwenye uchaguzi mkuu ulioisha hadi tukapata hiki kidogo katika ushindi wetu mkubwa tuliokuwa nao.

MWANDISHI: Endapo chama kikiwafuta uanachama, mmejiandaa kuchukua hatua?

MATIKO: Tupo hapa kwa sababu ya chama kwa hiyo kikiona kuna mwingine anafaa zaidi ya Ester Matiko, niko tayari.

MWANDISHI: Awali msimamo wa chama chenu ilionekana haukubaliani kuweza nyie kushiriki hapa

MATIKO: Nadhani leo jukumu kubwa ni kuapa na tumetimiza hilo, yanayojiri mengine yote yanawezwa kuzungumzwa kwa wakati muafaka. Katika neno letu la shukrani tumesema dhahiri kabisa tunakishkuru chama cha demokrasia na maendeleo kututeua sisi watu 19 kukiwakilisha katika bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuweza kuwasemea watanzania na chama chetu sasa mengine kama yalijiri yakaenda yakarudi, yatazungumzwa kwa wakati muafaka. Asante.

MWANDISHI: Ndio kusema mmesalimu amri

MATIKO: Sio msemaji wa chama, mimi ni mbunge mteule, ASANTENI SANA.


 
Kwa maoni yangu, wananchi tunahitaji watu wa kutusemea Bungeni hata kama ni wachache. Wale wengi wapo upande wa serikali hivyo hawatakuwa upande wetu sana; hawa 20 ni bora waachwe tuu kwani wachache hupewa nafasi kubwa ya kusikilizwa naamini tutawakilishwa vyema.

Hayo mengine yaliyotokea kwa kuwa wanasiasa wengi huubiri suala la KUJIAJIRI ni vizuri NAO wakajiajiri hii miaka mitano.
 
Njaa huwa inaanzia tumboni ila ujinga ni mara chache sana kuanzia kichwani.

Kazi iendelee.
 
Sasa katika hiyo habari ni wapi Matiko kasema kama watafukuzwa na chama yeye yupo tayari? Mimi sijaona.
 
Anahalalisha kidogo kwa kikubwa walichoporwa wananchi! Shauri yao wanaoendelea kukipigania chama!
 
MATIKO: Sijui zaidi ya hapo, kwa uchache wetu ambao tumekuja hapa, nipende tu kuwaambia watanzania, wategemee makubwa kwetu pamoja na kwamba tuko 19. Tunajua yote yaliyojiri kwenye uchaguzi mkuu ulioisha hadi tukapata hiki kidogo katika ushindi wetu mkubwa tuliokuwa nao.

Hahahaha
emoji23.png
emoji1787.png


Eti wanajua kilichotokea kwa ushindi wao mdogo.

Sasa kwa nini walikuwa wanakaza fuvu?
 
We dada ule udhalilishaji uliofanyiwa na wale Mapolice umeukubali kwa kukisaliti chama kwa kulipwa ujira huu? kweli dunia ina mambo!!
Hela ya ubunge hadi anamaliza muda wake unaijua wewe?? Pia police hawadhalilishi bali wanafanya kazi yao...acha wivu kwakua mwanamke mwenzio kachaguliwa
 
Ameulizwa alitaarifiwa na Katibu? anatoa jibu la jumla akisema na mamlaka husika, hapa kuna kitu anaficha, probably anamaanisha hizo mamlaka ni Spika wa bunge.

Anazidi kuthibitisha jinsi walivyosukumwa na maamuzi yao binafsi bila kupata baraka za chama anavyoshindwa kujibu swali la "Katibu anasema watachukua hatua kali dhidi yao", anakimbilia kusema "watanzania wategemee makubwa toka kwetu"

Huyu ndio kathibitisha kabisa hawa wanawake wanastahili kuitwa wasaliti, na yeye binafsi anaonekana alikuwa hajui lolote, kapigiwa simu tu njoo bungeni uje kuapishwa akaenda straight badala ya kwanza kuwauliza viongozi wake wa chama.
 
Swali: Ulitaarifa na Katibu?! Jibu: na Mamlaka husika😊😊

Mwenyekiti kaamua kuingia front mwenyewe.
 
Haaa haaa ulipewa taarifa na katibu? Eti na mamlaka husika. Hizi sanaa za kisenge mnatuletea
 
Mimi hao wengine wote sina muda nao, nalia na Halima tu mimi.
Halima amekivunja chama kabisa, Halima tulimuamini na kumpa jeshi letu la wanawake na nilitegemea pasi na shaka Mbowe akistaafu uwenyekiti basi kama sio Lissu, Heche basi ni yeye!
I’m disappointed
 
Anaongea kwa kiburi kwa sababu jana usiku walikutana na meko na spika, meko kawahakikishia kuwa hakuna wa kuwagusa iwe mahakamani ama wapi.. ester atakuwa naibu spika na mdee pia atakuwa naibu spika.imeisha hiooo. dont trust politicians
 
We dada ule udhalilishaji uliofanyiwa na wale Mapolice umeukubali kwa kukisaliti chama kwa kulipwa ujira huu? Kweli dunia ina mambo!!
Ulitaka aendelee kukaa tu nyumbani anaosha vyombo?
 
Back
Top Bottom