Ethiopia: Waziri Mkuu Abiy Ahmed atangaza hali ya dharura nchini kote

Ethiopia: Waziri Mkuu Abiy Ahmed atangaza hali ya dharura nchini kote

Nina rafiki yangu KE toka huko alitaka kwenda kumuona mama yake mgonjwa na utu uzima tena lakini anaogopa kutia mguu. Tukiongelea hili mimi humwambia Abiy alianza vizuri kisha akaharibu sasa ITAKULA kwake yeye bado anamfagilia sana Abiy na kuwasagia "Waasi" wa Tigray. Nchi ndiyo imeshaharibika hiyo. Afrika bado tuna safari ndefu sana.

Watu walionya sana PM kuanzisha vita Tigray sasa mambo yamekua mahumu hadi Adis Ababa...sasa ni rasmi ni suala la muda tuu Ethiopoa itakua haitawaliki tena
 
Abdulrahman Babu mwana Umma Party aliyeunga Eritrea


Abdulrahman Mohammed Babu of Tanzania was friend of Eritrean struggle against Ethiopia.
Source : Aida Kidane
 
Very true. Sijaelewa mpaka leo kwanini waliondoka Makelle na kuruhusu waasi kujikusanya upya.
Na kwanini jeshi lote la Ethiopia hasa la anga linashindwa wadhibiti waasi wanaacha wa-davance watakavyo!
Sifa tu aonekane anaweza kutatua migogoro mikubwa bila umwagaji damu.
 
Genesis of Conflict in the North


Mengistu Haile Mariam interview with American Journalist April 1990
Source : Biniam Hirut's History tube
 
Namuonea huruma abbiy Ahmed alianza vizuri ...uongozi Africa ni kitu kigumu Sana...na pia alikuwa ni mtu wa haki ukiwa mtu wa haki hauwezi kudumu mfano magufuli.ghadafi...wenye nguvu duniani hawataki kuona viongozi wapenda haki na wenye maono mazuri wanataka viongozi wababaishaji ukiwa mkweli na mpenda haki ..Kuna raisi alikuwa wa Zambia alikuwa anaitwa Michael sata naye hakudumu ..Kuna mawili la ufe kabla ya wakati au utapata misukosuko ya Vita ...pole Sana abbiy Ahmed nakushauri kimbia mapema maana yake kifo chako hakipo mbali ..kimbia usife kijana...ghadafi aliambiwa akapuuzia matokeo yake Yuko kwenye udongo Sasa hivi ....kimbia ikiwezekana hata kesho...
If he really wants to be a Hero he is not supposed to run away. He has to fight.
 
Hakutoka kwa hizo unazosema haki za binadam .Jeshi lake lilipigwa vibaya na wanajeshi wengi walipoteza maisha akaamua kuondoka.Mhimu tambua vita ni uchumi na mwenye uchumi mzuri lazima ashinde vita.Watigirey Wana uchumi mkubwa Sana pia wabasapoti kutoka mataifa ya magharibi hivo basi wanaludi Tena kuiongoza Ethiopia.
Waliosema wanajeshi wa jeshi la serikali kuu wamepigwa ni waasi wenyewe wa Tigray, Walichofanya waasi hapo ni propaganda tu na wewe umezimeza kama zilivyo. Kwenye vita yoyote lazima wanajeshi wafe lakini hiyo haina maana walizidiwa nguvu na waasi. Tigray hawana uchumi wala silaha nzuri kushinda serikali kilichotokea ni hesabu mbovu za Waziri mkuu kushindwa kutatua tatizo kabla halijawa kubwa.
 
Addis Ababa
Ethiopia

African heads of States arriving in Addis Ababa for OAU meeting July 1990
Dr. Salim Ahmed Salim secretary general OAU / AU with Colonel Mengistu Haile Mariam receiving president Sam Nujoma, President Hosni Mubarak and other african leaders at Bole International Airport Addis Ababa



Source : Biniam Hirut's History Tube
 
The NewsHour with Jim Lehrer - Ethio Eritrean Conflict 1998



Susan Rice, Isaias Afwerki, Meles Zenewi

Source : Biniam Hirut's History Tube
 
Ni kazi sana kujenga taifa kama kuna makabila, utamaduni au dini tofauti. Ni kazi ngumu sana. Africa inaanza kugawanyika kwa misingi hiyo. Ethiopia, Nigeria, Cameroon etc.

Nchi isipokuwa homogeneous lazima Baadhi watajiona kama ni second class citizen na wananyonywa. Wengine watajiona wa juu na kutaka kutawala siku zote.
 
Waliosema wanajeshi wa jeshi la serikali kuu wamepigwa ni waasi wenyewe wa Tigray, Walichofanya waasi hapo ni propaganda tu na wewe umezimeza kama zilivyo. Kwenye vita yoyote lazima wanajeshi wafe lakini hiyo haina maana walizidiwa nguvu na waasi. Tigray hawana uchumi wala silaha nzuri kushinda serikali kilichotokea ni hesabu mbovu za Waziri mkuu kushindwa kutatua tatizo kabla halijawa kubwa.
Vipi hukuziona videos za wanajeshi wa serikali waliotekwa na TPLF?
 
Unatumia tu akili bila ushabiki kwaba ni kweli JPM alikua mtu wa haki,hakupenda mali za waTanzania ziende hovyo na alidili na wananchi wanaounga mkono udhalimu wa mabeberu, hao ndiyo wanaoaminisha kwamba JPM hakua mtu wa haki kwa sababu walibanwa,walikua wanaiuza nchi na waliokua wanafaya biashara walikua wakipora kodi ya serikali

Watu msiwe mnaishia ushabiki tu bila kufikiri kwa makini

Rais anakufa kama mwananchi masikini wa kawaida ulisha ona wapi
Rais aliyekufa masikini tanzania ni Nyerere tu.
 
Hakuna cha hujuma za Misri wala wazungu. Ni upumbavu wa karne wa waafrika wa kubaguana kwa ukabila ndio unalitafuna taifa la Ethiopia
Pumbavu kabisa!
Si kweli jamaa aliyeongelea bwawa yupo sahihi. Wazungu hawataki kabisa huku Africa uwe na kitu cha kukuendeleza labda kama wanafanya wao kama ilivyokuwa Zimbabwe na South Africa kwenye mashamba.
Ethiopia walipogoma kusitisha kujenga bwawa, nakumbuka Trump alisema kuwa Egypt wakalisambaratishe hilo bwawa. Nakumbuka pia Egypt na Sudan walifanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi. Naona Analysis ikaonyesha itakuwa vita kubwa ndipo wakaamua kutumia njia hii ya kuwatumia wasaliti / mapandikizi. Vifaa na wengi wa majeshi ya waasi wanatoka somewhere...

Hakuna sababu ya kuwazuia Ethiopia kujenga bwawa katika nchi yao kutumia maji kutoka nchini kwao.

Angalia hii!
 
Nchi za Kiafrika nafikiri wakati wa kupigania uhuru kuna watu walifanya mazindiko halafu baadae wakasau kuyazindua, maana kila siku kuna kucha na mambo mabaya tu, inawezekana hata kiama kitaanzia Afrika.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 dah aisee hii comment bora ya uzi na ukaigongee hatimiliki
 
Waziri Mkuu huyo amewataka Raia wote wa Nchi hiyo ambao wanamiliki Siraha Kinyume Cha sheria wazisajiri Siraha zao ndani ya mda wa siku mbili ili kujiandaa kuulinda mji mkuu wa Addis Ababa.
Hii kauli inaonyesha serikali ya Abiy imeshindwa na haiwezi tena kuiangamiza Tplf ni bora wazungumze tu.
 
Waziri Mkuu wa Ethiopia,Abiy Ahmed ametangaza Hali ya hatari nchini kote Ethiopia, hii Ni baada ya wapiganaji wa Jimbo la Tigray wa TPLF kuteka miji miwili ya Dessie na Kombolcha iliyoko Katika Jimbo jirani la Ahmara.

Waasi hao wa Kaskazini mwa Ethiopia ambao wamekuwa wakipigana na vikosi vya SERIKALI kuu ya Addis Ababa kwa mwaka Mmoja Sasa, wanaonesha Nia ya dhati ya kuanza kuushambulia mji mkuu wa Nchi hiyo wa Addis Ababa. Lakini SERIKALI ya Ethipia imesema kuwa bado vikosi vyake vinapambana na wapiganaji hao.

Waziri Mkuu huyo amewataka Raia wote wa Nchi hiyo ambao wanamiliki Siraha Kinyume Cha sheria wazisajiri Siraha zao ndani ya mda wa siku mbili ili kujiandaa kuulinda mji mkuu wa Addis Ababa.

Waasi hao wa TPLF wameungwa mkono na Wapiganaji wa jimbo la Oromo ambao wameonesha Nia ya kumuondoa Waziri Mkuu huyo Madarakani

Msemaji wa TPLF amesema kuwa,Nia yao haikuwa kupigana na vikosi vya SERIKALI nje ya Jimbo lao la Tigray,lakini kutokana na Mzingiro uliwekwa na Serikali ya Addis Ababa dhidi ya Jimbo Hilo umesababisha Ukosefu wa huduma mhimu za kijamii Katika Jimbo Hilo kitu ambao TPLF haiwezi kukubali kuona Wananchi wa Jimbo Hilo wakihangaika kwa kukosa Chakula,Maji na Madawa.
Vita hii inamkono wa Egypt na mabeberu(Ref: bwawa la umeme) na si rahisi kwa PM kusalia madarakani.
 
Back
Top Bottom