KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 32,529
- 76,691
Ilikuwa ni weekend tulivu na yenye kibaridi chepesi nilichoamua nikichangamshe kwa kurukia maeneo ya starehe!. Hakuna starehe niliyoipenda Kama ya kunywa!,naam kunywa kile kimiminika chenye rangi ya dhahabu ambacho hubadilisha akili kuwa katika uchangamfu.
Ilikuwa ni mida ya saa mbili usiku baada ya kuangalia saa yangu akili changamfu ikanituma nitembelee banda lengine la wanywa kimiminika Cha dhahabu!,ktk kufikiri niliona nisitoke patapu nikaamua nijichukulia zile tabia za uswahili za kutoka na chochote kitu!. Punde nilikuwa nje ya banda nililopo huku mkono wangu wakulia ukiwa umeshikilia bia aina ya Serengeti lager!,kabla ya kuchukua uelekeo wa wapi niende nilijipima kwa kujipepesa ili nijue bado nipo ngangari kiasi gani!.. pepeso bado lilinena nipo fiti japo macho yangu yalikuwa tayari yakiashiria ulevi ndani yangu.
Baada ya kupata uelekeo nilipiga hatua zangu kwa uangalifu huku nikijitahidi kutoonekana kama mlevi niliekithiri!,funda zangu kadhaa za bia yangu tamu zilinifikisha mpaka kwenye lango fulani la kioo huku kwa ndani nikiona watu na harakati zao,wahudumu na wateja huku wengine wakilisakata rumba kwa michezo ya kilevu huku wakicheka bila sababu! Hapohapo nami bila sababu nikaliangua tabasamu huku mkono wangu ukiwa mkabala kuufungua mlango.. chakwanza nilikaribishwa na muziki mzuri uliokita katika masikio yangu,pili ndo Sasa zilifuatia sauti za walevi ambazo sikuzielewa zikisema nini bali niliona kama zinashindana na muziki ule mzuri uliokuwa ukipigwa.
Baada ya kuifikia kaunta nilipokelewa na macho yawatu kadhaa mengi yakiuliza "wewe ni nani...??" Yote niliyapotezea lakini lipo jicho moja la mlevi lenyewe lilinena tofauti tukiacha na yale mengine yaliyoonyesha mguno wa "ohoo" ama "Toba". La mlevi huyu lilikuwa ni jicho lenye uangavu na usaliti! Nalo nikajifanya silioni nikageukia kaunta nikakutana na mwanadada kapakia wanja uliokolea mithiri ya usiku wa manane wa wachawi kuwanga!.. mdomo wake wenye lips nyekundu ulinikaribisha kwa bashasha ukinena "karibu,nikuhudumie nini?"
Swali lake ndio kama lilinigutua kuwa nina bia mkononi!,nikafanya kuiinua kumuonyesha kuwa ningependa anipatie kinywaji Kama kile. Lakini katika kufanya hivyo ni Kama alikuwa hanielewi ndipo nikaamua nimwambie kwa maneno "nipatie Kama hii" napo hakunisikia ikabidi nipaze sauti kwa kushinda sauti za muziki na za walevi wengine! "Nipatie kama hii" wakati nikitamka hayo ndio wakati huohuo muziki ulikuwa ukifika tamati!
Hivyo kulifanya sauti yangu isikike kwanguvu kupita walevi wengine kitu kilichofanya wapunguze minong'ono na kugeuzia macho yao yakilevi maeneo ya kaunta!. Ilipita sekunde kadhaa wakarudia kelele zao huku wengine wakicheka na wengine wakiupokea muziki mwengine ulioanza kupigwa.
Kurudisha jicho langu kwa muhudumu nilikuta akinisubiri nigeuke ili anijibu lakini kabla hajafanya hivyo alikatishwa baada ya kuona mtu nyuma yangu akunishika bega!. Niligeuka kwa pupa maana ilikuwa ghafla! Alikuwa na mmoja kati ya mlevi aliekuwa akilisakata rumba kama mtu anataka kukatika viungo vyake vyote!. Uso wake wa ulevi ulinilokea kwa tabasamu la kinafki nililoliona toka hapo awali lile jicho lake angavu na lenye usaliti ama uchochezi ndani!.. aliongea kwa pupa "we ndama umefata nini humu..?" Sauti yake ilikuwa kali iliyogutua baadhi ya watu.. kabla sijajibu aliiangalia chupa yangu ya bia huku akiisonta na kusema
"Hizi hazipo humu!" Akaongeza "huoni kila mtu anaglass?"
Ndipo jicho langu likaambaamba na kuangalia huku na huko nikagundua ayasemayo ni kweli! Niliporudisha macho yangu kwake akaendelea "wewe mtu mwenye sauti ya ndama umekuja kutufanyia fujo humu!"
Niliguna na kuitazama bia yangu kabla sijanena chochote Kisha nikapiga pafu nyengine nzito niliyogugumia huku nikimuangalia mlevi yule alienibatiza jina la ndama!
Nilipomaliza sikuonyesha kuwa na muda nae nikamgeukia mhudumu ambae alionyesha bayana alifatilia maongezi yale.. nilimtolea jicho kisha nikamuuliza
"Ayasemayo huyu mlevi mkorofi yanaukweli?" Kabla hajajibu mlevi yule alinivuta tena begani kwanguvu! Nilipomgeukia alitaka kunena lakini kigugumizi kikamzuia kwa sekunde mbili,punde akalipata neno alilotaka kunena. Kwa sauti kubwa alinena "Amekuja kutufanyia fujo huyu!" Walevi wengine wakanitumbulia macho kodo! Akaongezeka na mlevi mwengine nae akiunga hoja na kupiga zogo "mfanya fujo kaingia!"
Mfadhaiko ukanipata baada ya mlevi mwengine nilipomsikia akinena "Atatuua huyu!" Sikujua walinena hayo kwasababu gani bali kelele zao zilinitia hasira ndipo nikamshika yule mlevi wa awali na kumtia ngumi mbili nzito zilizompeleka chini akitapatapa na kupiga mayowe!,ilisikika sauti ikinena kwa nguvu "tobaaa" watu wote waligeuka na kuona mlevi mmoja yupo chini hapohapo yule alienena atatuua huyu akanena zaidi kwa mayowe "nilisema mimi!"
Macho yote yalinitazama na punde waliingia mabaunsa wawili wakinifata mgubegube! Tahamaki nimebebwa na kwenda kutupwa nje huku nikisindikizwa na matusi mazito!
Narudi..
Ilikuwa ni mida ya saa mbili usiku baada ya kuangalia saa yangu akili changamfu ikanituma nitembelee banda lengine la wanywa kimiminika Cha dhahabu!,ktk kufikiri niliona nisitoke patapu nikaamua nijichukulia zile tabia za uswahili za kutoka na chochote kitu!. Punde nilikuwa nje ya banda nililopo huku mkono wangu wakulia ukiwa umeshikilia bia aina ya Serengeti lager!,kabla ya kuchukua uelekeo wa wapi niende nilijipima kwa kujipepesa ili nijue bado nipo ngangari kiasi gani!.. pepeso bado lilinena nipo fiti japo macho yangu yalikuwa tayari yakiashiria ulevi ndani yangu.
Baada ya kupata uelekeo nilipiga hatua zangu kwa uangalifu huku nikijitahidi kutoonekana kama mlevi niliekithiri!,funda zangu kadhaa za bia yangu tamu zilinifikisha mpaka kwenye lango fulani la kioo huku kwa ndani nikiona watu na harakati zao,wahudumu na wateja huku wengine wakilisakata rumba kwa michezo ya kilevu huku wakicheka bila sababu! Hapohapo nami bila sababu nikaliangua tabasamu huku mkono wangu ukiwa mkabala kuufungua mlango.. chakwanza nilikaribishwa na muziki mzuri uliokita katika masikio yangu,pili ndo Sasa zilifuatia sauti za walevi ambazo sikuzielewa zikisema nini bali niliona kama zinashindana na muziki ule mzuri uliokuwa ukipigwa.
Baada ya kuifikia kaunta nilipokelewa na macho yawatu kadhaa mengi yakiuliza "wewe ni nani...??" Yote niliyapotezea lakini lipo jicho moja la mlevi lenyewe lilinena tofauti tukiacha na yale mengine yaliyoonyesha mguno wa "ohoo" ama "Toba". La mlevi huyu lilikuwa ni jicho lenye uangavu na usaliti! Nalo nikajifanya silioni nikageukia kaunta nikakutana na mwanadada kapakia wanja uliokolea mithiri ya usiku wa manane wa wachawi kuwanga!.. mdomo wake wenye lips nyekundu ulinikaribisha kwa bashasha ukinena "karibu,nikuhudumie nini?"
Swali lake ndio kama lilinigutua kuwa nina bia mkononi!,nikafanya kuiinua kumuonyesha kuwa ningependa anipatie kinywaji Kama kile. Lakini katika kufanya hivyo ni Kama alikuwa hanielewi ndipo nikaamua nimwambie kwa maneno "nipatie Kama hii" napo hakunisikia ikabidi nipaze sauti kwa kushinda sauti za muziki na za walevi wengine! "Nipatie kama hii" wakati nikitamka hayo ndio wakati huohuo muziki ulikuwa ukifika tamati!
Hivyo kulifanya sauti yangu isikike kwanguvu kupita walevi wengine kitu kilichofanya wapunguze minong'ono na kugeuzia macho yao yakilevi maeneo ya kaunta!. Ilipita sekunde kadhaa wakarudia kelele zao huku wengine wakicheka na wengine wakiupokea muziki mwengine ulioanza kupigwa.
Kurudisha jicho langu kwa muhudumu nilikuta akinisubiri nigeuke ili anijibu lakini kabla hajafanya hivyo alikatishwa baada ya kuona mtu nyuma yangu akunishika bega!. Niligeuka kwa pupa maana ilikuwa ghafla! Alikuwa na mmoja kati ya mlevi aliekuwa akilisakata rumba kama mtu anataka kukatika viungo vyake vyote!. Uso wake wa ulevi ulinilokea kwa tabasamu la kinafki nililoliona toka hapo awali lile jicho lake angavu na lenye usaliti ama uchochezi ndani!.. aliongea kwa pupa "we ndama umefata nini humu..?" Sauti yake ilikuwa kali iliyogutua baadhi ya watu.. kabla sijajibu aliiangalia chupa yangu ya bia huku akiisonta na kusema
"Hizi hazipo humu!" Akaongeza "huoni kila mtu anaglass?"
Ndipo jicho langu likaambaamba na kuangalia huku na huko nikagundua ayasemayo ni kweli! Niliporudisha macho yangu kwake akaendelea "wewe mtu mwenye sauti ya ndama umekuja kutufanyia fujo humu!"
Niliguna na kuitazama bia yangu kabla sijanena chochote Kisha nikapiga pafu nyengine nzito niliyogugumia huku nikimuangalia mlevi yule alienibatiza jina la ndama!
Nilipomaliza sikuonyesha kuwa na muda nae nikamgeukia mhudumu ambae alionyesha bayana alifatilia maongezi yale.. nilimtolea jicho kisha nikamuuliza
"Ayasemayo huyu mlevi mkorofi yanaukweli?" Kabla hajajibu mlevi yule alinivuta tena begani kwanguvu! Nilipomgeukia alitaka kunena lakini kigugumizi kikamzuia kwa sekunde mbili,punde akalipata neno alilotaka kunena. Kwa sauti kubwa alinena "Amekuja kutufanyia fujo huyu!" Walevi wengine wakanitumbulia macho kodo! Akaongezeka na mlevi mwengine nae akiunga hoja na kupiga zogo "mfanya fujo kaingia!"
Mfadhaiko ukanipata baada ya mlevi mwengine nilipomsikia akinena "Atatuua huyu!" Sikujua walinena hayo kwasababu gani bali kelele zao zilinitia hasira ndipo nikamshika yule mlevi wa awali na kumtia ngumi mbili nzito zilizompeleka chini akitapatapa na kupiga mayowe!,ilisikika sauti ikinena kwa nguvu "tobaaa" watu wote waligeuka na kuona mlevi mmoja yupo chini hapohapo yule alienena atatuua huyu akanena zaidi kwa mayowe "nilisema mimi!"
Macho yote yalinitazama na punde waliingia mabaunsa wawili wakinifata mgubegube! Tahamaki nimebebwa na kwenda kutupwa nje huku nikisindikizwa na matusi mazito!
Narudi..