Evelyn wa chumvi...

Evelyn wa chumvi...

Baada ya kupaki gari alishuka na kwenda kuchukua vile alivyovihitaji katika supermarket ile,ilikuwa ni mifuko miwili tu ambayo ndani yake ilionekana kuwepo Kama box ambazo sikuzielewa ndani yake kulikuwa na nini. Baada ya kuingia garini alitoa tena samahani nami nikamtoa wasiwasi. Miguu yake mizuri iliirudia pedeli za Moto na breki huku mikono yake ikiikamatia usukani tayari kwa kuirudi safari yetu..

Baada ya kona mbili sauti yake ikakita Tena maskioni pangu kwa kusema "Eve" nami bila hiana nikamuuliza hilo ndo jina lako..? Akajibu ndio, hapohapo nikatupia kwa utani kiswali "uliongea nini na nyoka mpaka ukala tunda..?"
Aliangua kicheko huku akinitazama Kama mtu mwenye masihara sana! Kisha akajibu kwa kuuliza "Nawe Adam kwanini uliniacha peke yangu na nyoka..?"
Nilimuangalia huku nikitabasam na kugundua alikuwa akiniangalia kwa tuo huku akiuma mdomo wake wa chini!,Jambo hilo nililiona na kustaajabu mpaka kudhani kama naota ama ni pombe ama pepo limenivaa! Niliyapoteza mawazo hayo baada ya kurejesha umakini wangu na kumgutua aache kuniangalia bali aangalie mbele gari linapoelekea!.
Kama mtu mwenye hofu alinena "ooh! Sorry nafikiri wine ndo zimeanza kunilevya!"
Alinena hayo huku akiyarudisha macho yake katika umakini wa kuendesha.

Kimya kidogo akaniuliza "unaishi wapi..?" Nikamjibu ni baada ya mitaa miwili baada ya huu tuliopo.
"Okay mi naishi mtaa huu unaofuata" aliongezea Kisha nikasema "basi utaniacha hapo utakapofikia"
Baada ya kukata Kona na kuchukua barabara ya changalawe akaniangalia na kuongeza "Hapana nitakufikisha mpaka unapokaa baada ya hapo nitarudi"
Nikaguna na kumshukuru kwa huduma yake hii ya kutaka kunifikisha hadi ninapokaa!. Ilituchukua mwendo wa Kama dakika kumi tu mpaka kufika ninapokaa.
Tuliagana na kisha eve alirejea kwake nami nikaingia ktk gheto langu ambalo kwa kuliona tu hakukuwa na haja ya kuuliza kuwa alieishi humu alikuwa ni bachela!.
Baada ya kuwasha taa niliyarudisha macho yangu kwenye saa yangu nakugundua bado ni mapema mno kwa mimi kulala!,ndipo hapohapo nikakumbuka kuwa nimesahau kuchukua vilevi ambavyo ningenywea gheto!.
Hatua niliyoichukua ilikuwa ni kutembea tena mpaka mtaa wapili ambapo kulikuwa namaduka kadhaa ya pombe.
Dakika tano tu zilitosha kufikia maduka hayo na kuchagua moja wapo,Mara hii nilibadili mawazo nakuamua kuchukua kinywaji kikali zaidi! Kilikuwa ni kinywaji mithiri ya maji lakini hayakuwa maji! Chupa yake ya bapa na picha ya nembo ilitosha kuhubiri kimiminika kile kilikuwa ni kinywaji cha aina gani!..
Tamaa na husuda la kutungua lepe moja zilinitamalaki hata kuona tabu kufika kwanza gheto kabla ya kufungua kifuniko cha bapa lile!,nilijiambia "kote huko nikubebe tu nikikutana na vibaka wakanipora!" Sentensi hiyo ilimaliziwa huku tayari mdomo wangu ukiduguda mafunda kadhaa ya kilevi hichi chenye nembo ya mwanaume alieweka mikono juu!!..
Uchachu na ukali ulitamalaki kinywani nakusikia kilevi hichi kilivyokuwa kikishuka kwa tashtiti ktk koo langu ambapo hapo awali lilifanya niitwe ndama kutokana na sauti niliyoitoa!.. baada ya kujikuta nikikumbuka mkasa huo niliropoka tusi zito lawama zote nikizipeleka kwa yule mlevi mkorofi!.
Lakini punde mawazo hayo yakamezwa na taswira iliyojirudia ya mrembo eve!!.. hapohapo nikakumbuka na lile swali lake ambalo lilikuwa Kama jibu baada ya swali langu kuhusu yeye na nyoka!,nikajikuta nikiikumbuka taswira ya muonekano wake mzuri uliosheheni sifa kedekede mpaka kufikia hatua ya kujiapiza kuwa nitampata tena na awe wangu!!..
Hilo wazo nalo likapigwa kumbo baada ya kuufikiria umaskini wangu nakujikuta nikijihoji "utampata kwa lipi..? Nikajiuliza mwenyewe,Kisha nikajijibu!
"Au kwa kile kibaskeli chako kisichoisha pancha!"
Nikabaki kujicheka huku nikisema neno kwa kulirudiarudia "ndama ndama ndama!.
Nilinyanyua bapa yangu nakuduguda funda jengine kubwa Kisha nikafunika na kifuniko tayari kwa kutafuta uelekeo wa kuirudisha roho yangu ghetoni!.

Wenge la kimiminika bapa lilikuwa limeanza kunitamalaki wakati huo nikiwa mbele ya mlango wangu nikihangaikia funguo nyingi ambazo nyengine sikuwahi kujua niliziweka zakazi gani!!,kila funguo iliyoshindwa kufungua niliisindikiza na tusi!,ulevi nao kichwani ulichangia kutokujua funguo ipi ilikuwa ni sahihi mpaka kujikuta nikianza upya tena kufungua mpaka mara tatu ndipo kufuli likapata mfumbuzi wake! Nilifyonza huku nikiongea maneno ambayo hata mimi sikuyaelewa!.
Niliingia mpaka ndani huku nikiwa na bapa yangu nimeikumbatia kwapani kwenye mkono wakushoto!.

Narudi vumilieni itaisha msichokijua naandika ila sijui nini kitatokea..🤣🤣
 
Hiyu Msenger anajua kuandika vizuriii asee
Unasoma kitu ukivuta hisia za tungi inakuja kabisa kode...

Hii chumvi ntaisoma tena nikiwa na bia 9 kichwani niburudike kwa uwandish mtaam hivii

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Mkuu unahabari naandika halafu sijui uelekeo wa hichi ninachoandika..😂
Ila itaisha tu japo sijui itaishaje
 
Kwani Kisandu ak.a Don Nalimison ameshakula mzigo?

Huyu mtoto basi atakuwa na utamu wa ziada aisee au nyota imesafishwa na bahari ya Pacific.
 
Ulivoniita dada ndio umeharibu sasa
Baby nitumie namba niwafundishe namna ya kutongoza hawa vijana.

Muhamara utakavyosoma ndio full details zangu hizo.

Achana na watoto hawa wanataka kukuletea mapenzi ya kihindi.

Nguvu zote hizi zilizotumika kwenye keyboard solution yake ni cash tu.

Watoto wa mjini wanaojitambuwa na walioelimika hawauzi K na wala hawatoi bure.
 
Baby nitumie namba niwafundishe namna ya kutongoza hawa vijana.

Muhamara utakavyosoma ndio full details zangu hizo.

Achana na watoto hawa wanataka kukuletea mapenzi ya kihindi.

Nguvu zote hizi zilizotumika kwenye keyboard solution yake ni cash tu.

Watoto wa mjini wanaojitambuwa na walioelimika hawauzi K na wala hawatoi bure.
Umemaliza yote baba S tukutane jioni kwa ajili ya k vant 😁
 
Niliingia mpaka ndani huku nikiwa na bapa yangu nimeikumbatia kwapani kwenye mkono wakushoto,niliivuta nakuisogeza tena Kisha nikaiweka usawa wa macho yangu nikiiangalia kwa lile jicho la tamaa mbele mauti nyuma!.. Wala hata sikungoja niliduguda tena kwa pigo moja nakujikuta nikifumba macho huku nikikunja sura Kisha nikaiangalia tena nakujikuta nikijisemea "machozi ya mamba haya!"

Kabla hata sijakaa sawa ndipo punde hiyohiyo nikaona mwanga kwa nje ukijitahidi kutaka kupita ktk mlango wa chumba changu!,kikapita kimya masikio yangu yakanasa muunguro wa gari Kisha hapohapo nikasikia honi ya gari hilo ikihanikiza mara kadhaa!.
Nilijua huu ulikuwa ni ugeni wangu lakini haukuwa na taarifa kwa mara nyengine tena nikaitazama saa yangu ilionyesha ni saa tano nadakika hamsini na tano!,nikajikuta nikiropoka nani tena huyu..? Honi nazo ziliendelea kufikia masikio yangu nakuleta kero ambayo sikupenda kuisikia!.

Kwauchovu wakilevi nilijivuta na kuufungua mlango wangu napo nikalakiwa na mwanga wa taa za gari lile!,nikalifata na ndipo nilipogundua garini alikuwa ni Eve!

Kwasauti yakilevi niliyojitahidi kuificha nilimuuliza "mbona umerudi mrembo..?"
Alinitazama na kisha akafungua mlango wa gari nakunifata niliposimama.. "I need your company jonas!" Alijibu huku akinikaribia.

"Company..?" Nilihoji kwa mshangao huku nikimtupia macho ya maswali.. Mara hii alikuwa ameshanikaribia zaidi mpk niliyasikia marashi yake mazuri aliyokuwa amejipulizia,marashi yaliyoonekana kuwa ya gharama yaliyoishinda harufu yangu ya vimiminika vya vilevi nilivyovitungua usiku huo!.

Eve akaongeza "yes company ningeomba unisindikize kwenye birthday party ya rafiki yangu!"
Niliguna na kisha nikaitazama saa yangu nakuonyesha Kama mtu mwenye wasiwasi juu ya ombi lake,nikabaki kutafakari kidogo nilipomtazama kwa mara nyengine nilikuta macho yake yakiangaliana na macho yangu!,nilimtazama kwa tuo nakugundua alikuwa akinitazama kwa hamu kama mtoto alieona sukari ikipitapita mbele ya uso wake!. Kabla sijanena chochote akaongeza kwa sauti ya kudeka
"Please Jonas I need your company!"

Mara hii nikaliangua usoni kwangu tabasam hafifu nakujikuta nikimezwa na uzuri wake hapohapo mawazo yangu yakaanza kunilaumu kwa kuchelewa kuchukua maamuzi! Niliwaza "Hii bahati yako!" Wazo jengine likatamalaki "Mbuzi kafia kwa muuza supu!".
Mpaka hapo sikuwa napingamizi nilimuangalia Eve nakumjibu "sawa!" Alifurahi na kunijibu "ahsante"

Punde nilikuwa ghetoni nikiangalia nini chakuvaa usiku ule ili nimsindikize mrembo yule mahali ambako sikupajua!,Kuna muda niliona Kama nimemkubalia kirahisi ombi lake Tena mtu ambae nimemfahamu hivi punde tu! Nilijishangaa!! Lakini tena nikajiuliza "kwa uzuri ule naachaje kuwa company yake..?" Wazo jengine lakijinga likanijia "Kama unaenda kunyonywa damu je..?"

Niliguna nakulitupia mbali wazo hilo,hapohapo ikanijia na twasira yake vile alivyokuwa amevalia, kigauni cheusi kifupi chenye marumaru yang'aayo kwa mbali huku chini akiwa ametupia viatu vyeusi vya mchuchumio!. Nilitafakari nakuamua nami nivalie vipi ili niendanenae.

Ilinichukua dakika sita nikawa tayari nimeshatupia jeans nyeusi na tisheti ya kijivu huku nikisindiikiza na mkoti mweusi ambao niliuachia wazi bila kufunga zipu yake,chini nikavalia raba nyeusi zenye mistari myeupe kwa chini.

Nilipotoka alinipokea kwa macho yake mazuri nakutupia neno fupi tu "Nice" nami sikuwa nyuma hapohapo nikamsindikiza na usemi "hiyo marumaru yako yanitia kihoro!" Aliangua kicheko huku akiwa mkabala na mlango wa gari tayari kwaajili ya safari...

Ilituchukua Kama dakika kadhaa tu mpk kufika ktk moja ya hotel kubwa iliyofahamika kwa jina la king's hotel,baada ya kupaki tuliingia mpaka kwenye ukumbi tuliokuta watu kedekede waliovaa nadhifu huku wengine wakionekana tayari ktk hali za macho remburembu.. eve alinivuta hadi upande wa kushoto kulipokuwa namakochi mawili yaliyopangiliwa huku katikati kukiwa na meza ndogo ya kioo!. Aliniomba niketi Kisha akaniambia anarudi hivi punde.

Nilitulia huku nikitupia macho huku na kule nakuona watu kadha wa kadha wakiwa ktk makundi wakipiga stori mbili tatu. Mbele yangu niliiona maneno makubwa yakinakshiwa vizuri huku yakiwa yameandikwa "HAPPY BIRTHDAY MARRY" mapambo mengine yalihanikiza huku taa za marumaru nazo zikiwa hazipo nyuma ktk kufanya manjonjo yake!.

Mawazo yakaikumbuka ile bapa yangu niliyoiacha gheto nakujikuta nikijiona kama msaliti wa kinyaji changu ambapo mpaka sasa midugudo ile kadhaa bado iliendelea kutamalaki ktk viungo vya mwili wangu!. Kelele hafifu za maongezi ya watu zilinigutua Tena kurudisha fikra zangu ktk ukumbi ule! Dj aliukamata umakini wangu baada ya kucheza nyimbo moja wapo ya msanii wangu pendwa aliefahamika kama mfalme wa pop!

Alikuwa ni Michael Jackson na kibao chake cha "you rock my world" taratibu mguu wangu wakulia ulianza kwenda namapigo ya wimbo ule huku napo mkono wangu wakuume niliouegemeza kochini ulianza kutikisika vidole vyake!.. punde Eva alinigutua huku akitupia sentensi "samahani kwa kukuacha mpweke" aliyanena hayo huku akiniangalia kwa kitabasam chokonozi!.

Nilimuambia kuwa haina shaka..
Tofauti ya ujio wake huu alikuja na mgeni mmoja wapo!,mgeni ambae alikuwa amemshikilia kwa mkono wake wa kulia huku mkono wake wa kushoto akiwa na glass mbili ndogo!.

Alimtua mgeni yule mezani kisha akaziweka glass zile karibu na mgeni wetu mpya aliesomeka kwa majina "saint addo!" Kwa bashasha Eva alinikaribisha "karibu tujitibu" wakati akiyanena hayo mikono yake ilikuwa bayana ikiifugua kifuniko cha kinywaji kile kilichokuwa na rangi nyeusi! Alimimina katika glass zote mbili Kisha akanishikisha yangu nae akaishika yake!.. wakati akiyafanya hayo alikuwa amesimama ila baada ya kuishika glass yake alikuja kukaa mkabala namimi nakujikuta miili yetu ikigusana kwa namna ya watu ya kinamna!..

Baada ya kupiga funda moja ya kinywaji kile radha nisiyoielewa ilinienea ktk kinywa changu! Eva akaniangalia kwa tuo na kuniambia "hichi ni kinywaji changu pendwa" nami nikamuitika kwa kumwambia "sijazoea Mambo ya hivi" alicheka na kutupia utani "we umezoea yale ya kuitwa ndama..?" Mara hii tulijikuta tukicheka kwa pamoja!.

Ilikuwa ni taswira nzuri katika ukumbi ule ambao ulisheheni watu kadri muda ulivyozidi kwenda lakini ktk punde hii tuligutuliwa na sauti ya kiume iliyosikika katika spika ikituomba watu wote tusimame kwaajili ya kufanya kile kilichotuleta maeneo yale.. Alionekana binti aliependeza haswaa akiwa amevalia gauni la blue lenye kufunika miguu yake, taratibu huku akisindikizwa aliikaribia meza kubwa iliyokuwa imepambwa kwa marumaru na mioto iliyoonekana ikiwaka juu ya keki kubwa iliyovutia machoni.. ni wakati huu mc wa sherehe alimkaribisha mrembo huyu akakate keki yake huku akituomba tuimbe ile nyimbo ya happy birthday.. ukumbi ulilipuka kwa shangwe na bashasha Eva nae hakuwa nyuma mara hii akiwa amesimama pembeni yangu huku akiikamatilia glass yake alionekana kuwa mwenye shangwe na uchangamfu ambao sikumuona nao hapo kabla!.

Keki ilikatwa, champagne ikafunguliwa wenye Kunywa tukanywa na wenye zawadi wakatunuku,ilikuwa ni sherehe ambayo haikuchukua muda mwingi sana bali ilikuwa ni Kama starehe ya muda tu ndipo Sasa ukafika ule wakati wa dj kuzichangamsha nafsi za watu kwa kutumia ujuzi wake maridadi!.. santuri ziliitika na kufanya kila mmoja katika ukumbi ule kutokuwa mvumilivu nakujikuta sote tukinengulika kwa kufuata midundo ya muziki.. dj alirukia wimbo huu na ule na zote zilipokelewa kwa mayowe Kama si vifijo!.
Eve niliemfahamu muda mfupi hakuwa tena yule!,eve wasasa alikuwa mchangamfu kupita kipimo hakuna wimbo ulimpita!,kwa viungo vyake laini alicheza kwa madaha huku akinengua kwa pozi zilizokuwa zikionyesha dhahiri kile kinywaji cha "saint oddo" kilikuwa kimefika hatua za majinuni!.
Si kiuono chake tu bali mwili wake wote ulionyesha umaridadi katika kulisakata! Nilibaki nikimtumbulia macho nisijue niangalie kiungo kipi katika viungo vyake maana vyote vilionekana kucheza vizuri!.. eve alinitupia jicho nakuchanua tabasam alinisogelea nakunivuta huku akitupia maneno "acha ushamba"
Tulijikuta tumeshikana yeye mbele mimi nyuma yake tukilisakata kama wapenzi tuliobakiza siku chache tu tufunge ndoa!,mikito ya muziki ilizidi kunoga huku kila mmoja akijitahidi kuonyesha ufundi kwa mwenzake. Hakuna alietaka kushindwa! Kwa mikono yangu nilishika kiuno Cha eve kilichokuwa hakitulii kwa dansi za huku na huko! Niliona kama naenda kuzidiwa kete na kugawa ushindi kwa binti huyu niliyemfahamu kwa machache tu!.
Sikutaka iwe hivyo nami nikabadili namna ya uchezaji kwa kumgeuza anigeukie Kisha nikamsogeza karibu zaidi nakushika kiuno chake laini nae bila hiana akaweka mikono yake mabegani kwangu huku akinitazama kwa kurembua na kunikonyeza aliendeleza dansi ambapo mara hii aliniachia nafasi ya kuupapasa mwili wake,kitu kilichofanya nione nimepewa nafasi ya upendeleo hivyo hata kete za ushindi ziliegamia upande wangu!. Hakuna pigo la wimbo lililotushinda kucheza!,kila staili ilifana nakujikuta tukifika mbali na kuangaliana machoni kwa tamaa zilizowika zaidi na zaidi!..
Niliiangalia saa yangu nakugundua ilikuwa yapata saa tisa za usiku! Nilijinasua kwa eve nakumshika mkono wake wakulia Kisha nikamvuta pembeni,ndo kwanza alibaki akinitumbulia macho kwa kuona nikikatisha dansi aliyopenda kuona ikiendelea zaidi na zaidi!. Sikuyajali macho yake bali nilimkalibia kwenye sikio lake lakulia na kumwambia "turudi nyumbani!" Alinishangaa nakutupia neno huku akitoa sauti ya kilevi yenye deko
"mi nilijua tunakesha!"
Niliguna na kumtazama tena nikauona uso wake ulivyona husuda ya kutaka dansi tena na tena lakini majinuni mimi kwa minyweso niliyoichanganya leo mwili ulikuwa ushachoka na kibofu kuchoka kujaza vimiminika mbalimbali!.

"Hapana hatuwezi kukesha mi najihisi kuchoka!" Nilimwambia eve ambapo wakati huu alikuwa akiniangalia jicho la ushawashi zaidi akinitaka tuendelee kubaki!,nilijifanya kuangalia pembeni kwa sekunde kadhaa na kulipilotezea jicho lake chokozi kisha nikamvuta huku nikiongozananae kuelekea mlango wa kutoka nje! Ghafla kwa sauti ya deko akang'aka "tubaki bhana mi sijatosheka" nilipogeuka alionekana Kama mwenye huzuni kutokana na uamuzi wangu,lakini punde hii sikutaka kupelekwa kikondoo kama hapo awali!.. niliendelea kumvuta mpaka tukatoka nje!..

"Sasa ndo nini..?" Aliuliza huku akiuvuta mdomo wake!
"Imetosha eve" nilijibu
Kilipita kimya huku mwenzangu akionyesha Hali ya kununa! Ilikuwa ni picha ambayo waliyopita walituoa kama wapenzi tuliokwazana lakini bado tuliendelea kuhitajiana!.

Hatimae eve alinikubalia kishingo upande huku akinikabidhi funguo za gari na kuniomba mimi ndo niendeshe,tulijivuta mpaka kwenye parking ya magari nakuchukua gari yetu tukatokomea gizani kwa kuishika rami iliyotupeleka ktk njia tulitokujia lakini punde....

Narudi..😀
 
Kwani Kisandu ak.a Don Nalimison ameshakula mzigo?

Huyu mtoto basi atakuwa na utamu wa ziada aisee au nyota imesafishwa na bahari ya Pacific.
Hivi nalimi alikuwa anafatilia hili zigo..?
 
Baby nitumie namba niwafundishe namna ya kutongoza hawa vijana.

Muhamara utakavyosoma ndio full details zangu hizo.

Achana na watoto hawa wanataka kukuletea mapenzi ya kihindi.

Nguvu zote hizi zilizotumika kwenye keyboard solution yake ni cash tu.

Watoto wa mjini wanaojitambuwa na walioelimika hawauzi K na wala hawatoi bure.
Dah! Mkuu umeamua kutuchambua sasa mi naandika stori tu Wala Sina nae lolote dada wa watu.. we tumia miamala yako lakini jua watoto wake mjini tukimuamulia huyu analiwa tu..😂 joke hiyo msijekumind.
 
Back
Top Bottom