Exclusive Interview: Tundu Lissu amwakia mwandishi kwa kutokujua maana ya "Tume Huru ya Uchaguzi". Bila mfumo mpya wa uchaguzi hakuna uchaguzi 2025

Exclusive Interview: Tundu Lissu amwakia mwandishi kwa kutokujua maana ya "Tume Huru ya Uchaguzi". Bila mfumo mpya wa uchaguzi hakuna uchaguzi 2025

The Palm Beach

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2015
Posts
1,967
Reaction score
4,267

Courtesy: Mwanahalisi online TV

In summary:

1. Amkemea mwandishi kwa kusisitiza kuwa, serikali ilishafanya mabadiliko waliyoyataka ya kuundwa "Tume Huru ya Uchaguzi". Yeye amkemea na kumwambia:

"....kama unaamini kuwa kilichopitishwa na Bunge mwanzoni mwa mwaka huu ni Tume Huru ya Uchaguzi, basi wewe (mwandishi) hujui maana ya Tume Huru ya Uchaguzi...!"

2. Atumia muda huo kutoa elimu ya maana na mantiki ya "TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI" na uhuru ni upi. Mfuatlie mwenyewe kwenye video hii fupi...

3. Mwaka 2019 na 2020 tulishuhudia uchafuzi wa chaguzi hizo. Mwaka huu tumethibitisha pasipo shaka kuwa CHADEMA na vyama vingine vya siasa vilivyo nje ya serikali (vya upinzani) havishindani na CCM kwenye uchaguzi....

Amesema; ".....Sisi CHADEMA tulikuwa tunashindana na Majeshi polisi, TISS, JWTZ, Wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi wa Halmashauri za majiji, manispaa, wilaya, miji na watumishi wote wa serikali. Tumeshindwa katika uchaguzi huu na dola. CCM haipo, imeshakufa, haiwezi kushindana ktk sanduku la kura...!!

4. Mwisho amemaliza kipande hiki cha mahojiano yake kwa kusema;

".......kama hakutakuwa na mabadiliko muhimu ya mfumo mzima wa uchaguzi wa nchi na taifa letu kwa kubadili sheria na katiba, basi HAKUNA UCHAGUZI MKUU MWAKANI, yaani mwaka 2025...!

Watafanyaje kuzuia uchaguzi huo? Weka MB na kisha Mtazame, msikilize na mfuatilie mwenyewe kwenye video hii fupi ya dakika 15 hivi....
 
Irregularities kwenye chaguzi mbalimbali haziwezi kutatuliwa kwa simply kuwa na tume huru. Tatizo linaanza chini kwa kuwa na wafanyakazi wenye weledi. Tume inaweza kuwa fair kwa kuwa na kanuni zilizo kubaliwa na vyama vyote
 
Tundu Lissu...,; Huyu Ndiye.

Msikilize ukiwa unataka kuelewa kinacho elezwa. Ukisha sikiliza na kuelewa kinacho elezwa; inatosha!

Tundu Lissu sasa anadhihirisha ukomavu wake wa kisiasa, na uwezo wake wa kujieleza na kueleweka kirahisi kabisa.
 
Irregularities kwenye chaguzi mbalimbali haziwezi kutatuliwa kwa simply kuwa na tume huru. Tatizo linaanza chini kwa kuwa na wafanyakazi wenye weledi. Tume inaweza kuwa fair kwa kuwa na kanuni zilizo kubaliwa na vyama vyote
Hata hili kalisemea, labda uwe umelisahau tu.
Maana ya Tume Huru ya Uchaguzi; kama ni huru kweli, ndiyo yenye mamlaka na hao wa chini unao wazungumzia wewe.
Hawa wa chini hawaezi kufanya kinyume na taratibu za uchaguzi ambazo zinasimamiwa na tume huru yenyewe. Anaye kiuka taratibu anawajibishwa na Tume Huru yenyewe; na siyo chombo kingine nje ya hiyo tume. Kila mtumishi wa hiyo Tume anawajibika kwa Tume yenyewe.
 
Tundu Lissu...,; Huyu Ndiye.

Msikilize ukiwa unataka kuelewa kinacho elezwa. Ukisha sikiliza na kuelewa kinacho elezwa; inatosha!

Tundu Lissu sasa anadhihirisha ukomavu wake wa kisiasa, na uwezo wake wa kujieleza na kueleweka kirahisi kabisa.
Jamaa Lissu yupo vizuri sana kichwani na anahoja hasa, ccm lazima wamuogope, ktk hili Lissu amekosea kidogo tu- kuremotiwa na Msigwa
 
Jamaa Lissu yupo vizuri sana kichwani na anahoja hasa, ccm lazima wamuogope, ktk hili Lissu amekosea kidogo tu- kuremotiwa na Msigwa
Huyo Msigwa hana uwezo kiakili au hata kwa mali kumrubuni Tundu Lissu. Naona huu ndio umekuwa wimbo wako usio kikomo!
 
Mwandishi kaenda Mjinga kapewa Darasa 😆😂
Kapewa darasa hasa.
Natamani sana wajinga wengi tulio nao humu waweze kupata darasa hili pia.

Njuwa wengi tatizo ni 'MB'; sasa sijui tufanyeje kuwasaidia hawa!

Hiyo 'interview' ni 'masterpiece' hasa! Utadhani Tundu Lissu alikuwa amejiandaa kujibu swali hilo moja kwa moja; maana hata namba, majina na mengine ya kumbukumbu, yote yanatoka kichwani mwake bila ya kutazama mahali.
 
Bunge lilishapitisha tume ya uchaguzi iitwe tume huru ya uchaguzi. Lissu acha ubishi.
 
Jamaa Lissu yupo vizuri sana kichwani na anahoja hasa, ccm lazima wamuogope, ktk hili Lissu amekosea kidogo tu- kuremotiwa na Msigwa
Hivi huyu Msigwa na bwanako wewe mccm? Ukishafakamia mchemsho wa nguruwe unakuja kupumulia humu kumsifia Msigwa.
 
Back
Top Bottom