Exclusive: Njoolay mrahishie Kikwete kazi; jiuzulu mwenyewe!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
NImesikia juzi ati Mkuu wa Mkoa wa Rukwa amesema kuwa yuko tayari kujiuzulu endapo uongozi ulio juu yake utaamua afanye hivyo kufuatia wizi wa vocha za mbolea zenye thamani ya Tsh bilioni 6 kuibwa. Habari hii imeandikwa kwenye Habari Leo vile vile:

Nimeamua kujitolea kuelezea hili vizuri zaidi baada ya "ka nzi" kupita mitaa ya Rukwa (thanks ka-nzi.. you are becoming a pin in ccm's you know what!). Ifuatayo ni ripoti ya katoto ka "nzi"

 
What worth. Having another one doesn't mean any thing
 
Haya sijui PM atasema nini, na sera zake za kilomo kwanza. Mbolea zenyewe zinaibiwa nje ya mlango wake. Kawafukuza watu majuzi huko dar kwa uzembe, labda mi nadhani mwanakijiji ungemuuliza Mh.Pinda kwamba jamaa yuko tayari kuwajibishwa kwa uzembe wake.

Tukimuona anayo kazi hadi wiki ijayo huyu jamaa PM atakua ni msanii tu vile vile. Asilete mambo ya double standard fire the 'bozzo' who is responsible.
 
Kikwete hana la Kufanya juu ya hili kuna ambaye hamjui Mr Prezident katika kufanya maamuzi ..
 
tumewatajia hadi mambo mengine ambayo walidhani hayajulikani; natumaini Pinda huko Singida ataamua kuchukua uamuzi wa kumshauri Rais kuchukua uamuzi unaostahili..
 
kwa kuwa mkuu wa mkoa huo haivani na presidaa wetu basi huenda maamuzi flan yakafanyika.

karibu kila mkoa mbolea hii imeibiwa sana tu labda huko kwa njolay kumezid!
 
kwa presidaa huyu hilo mzee MM haliwezekani, labda atamhamishia Njoolay Dar aje kula kuku
 
Sijui nianzeje kwenye hili nalo... huo ni mkoa mmoja tu watu wanalamba bil. 6, kesho tukiambiwa hela ya kilimo kwanza imeisha then tunaanza kupiga kelele

hali iko hivyo kwa vitu vingi tu na mbole peke yake, mikoa yetu yote iliyo na borders iko porous na sielewi kwanini wanaweka viongozi dhaifu

Kuna wakati nilipost kuhusu our governance structure is not functional basing the quality of people we have onboard na geography yetu

decentralization may not be the best idea kwa baadhi ya vitu simply because we are very lenient to criminals
 
JK hawezi kuwawajibisha wasaidizi wake on the spot, labda kama kelele za kumtaka afanye hivyo zikiendelea....yeye yuko bariidi pale mjengoni.
 
tumewatajia hadi mambo mengine ambayo walidhani hayajulikani; natumaini Pinda huko Singida ataamua kuchukua uamuzi wa kumshauri Rais kuchukua uamuzi unaostahili..

Yo know what mkuu, haya maswala ya ruzuku ya Mbolea yapo pia Malawi. Na infact mbolea inayouzwa mfuko wa 50kg in Tz around 100,000 TZS, kwa Malawi ni kama 6000TZS. Lakini You will never ever find hiyo mbolea ya Malawi in Tz. Ila sisi tulipoanza tu mambo ya Ruzuku kabla ya Malawi anywayz, mbolea ilikuwa inavushwa usiku na mchana and was one of the hot cake biz by then.

SO WHY? It is all about consequences, Mr Bingu is very serious on the matter and he mean it. Ukikamatwa na mbolea mfukop mmoja unauvusha ni 1yr jail sentence bila kona kona. The same kwa mifuko 100 ni miaka 100 jela. Gari, mkokoteni, pikpiki itakayokamatwa kwa ajili ya kuvusha is seized right away by the govt.

Sisi tumekaa kifisadi fisadi as such hakuna agizo wala utaratibu unaoweza kuendeshwa bila ufisadi..Na hili pendekezo la wahalifu wapelekwe kwenye vyama vyao wakashiughulikiwe huko , Is TZ serious?????????
 
Ni habari ya kusikitisha sana,ubinafsi na tamaa za maisha bado ni ugonjwa kwa viongozi wetu.....sasa sijui KILIMO KWANZA ndio kina shika kasi ya kwenda nyuma au ni changamoto kama wasemavyo.........!
 
tumewatajia hadi mambo mengine ambayo walidhani hayajulikani; natumaini Pinda huko Singida ataamua kuchukua uamuzi wa kumshauri Rais kuchukua uamuzi unaostahili..
Kauli ya Njolay ni ya kujikosha kisiasa na mtego kwa Raisi..Anatambua uhusiano wake na Mkuu ukoje na angependa kuondoka kwa style ya kuachiana maswali hasa kwa umma..Ni nadra viongozi wakuu hasa hawa wa kisiasa wanapokosea hutoa kauli kama hizooo..naona TUNASONGA Mbele taratibuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu....

Nategemea PM amwite huyoo Njolay wajadili kwa maelekezo ya Raisi na hatimayee achiee ngazi..Itatusaidiaa kwa Maeneo mengine ambayo viongozii wamezoeaa kukosea na kubaki madarakanii..
 
lakini hawa watu wanataka tuwafanyie kazi zote kweli? tumewaambia kuhusu kuuzwa mbezi Beach wanakubali kuwa kumefanyika makosa.. lakini wanataka kuunda timu kuchunguza; zimeibwa voucha huko wanafanya nini? wanaunda tume kuchunguza; wamejenga majumba ya bilioni mbili na nusu hivi badala ya kuchukua hatua wanaunda tume!!
 

Njoolay na mafisadi wenzake hawatakiwi kujiuzulu bali washitakiwe na warudishe pesa zote walizoiba na kufungwa.

MM si mbolea tu:
-Mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami sumbawanga mjini kama ilivyo katika mji wa panda nao umekufa (inasemekana Njoolay na mafisadi wenzake wamekula pesa)
-Hata Nusu ya Uwanja wa saba saba sumbawanga Njoolay amemuuzia mmiliki wa kampuni ya Tawaqal.

NI BAHATI MBAYA KWA WATANZANIA NA BAHATI NZURI KWA MAFISADI KWAMBA HATUNA RAIS ANAYEJUA WAJIBU WAKE
 
CCM na serikali yake ni uozo tu there is nothing to expect from them.
 
MWanakijiji, your role no informal/formal... whether you like it or not, upo hapa for a reason, na kamwe usisikitike ni namna mambo yalivyo

endelea kuwa kiungo muhimu ila pia recruit system yako ya vi-nzi mara dufu kwani UWT wanaonekana kujua yanayoendelea lakini wanakuwa mute
 

Mkuu,

Hiyo ndio namna pekee Wanayoona kazi zinafanyika ambazo Watanzania wengi bado wana wanaona...IGP naye aliunda Tume kuchunguza kifungu cha Sheria kuhusu raia kumiliki pingu. Can you imagine...??!!

Hawa viongozi wetu hawana fikra mbadala za kusukuma maendeleo wao wanafuata taratibu walizozikuta tu..kama Robots.
 
Hao maafisa watakuwa ni watu wenye akili nzuri sana. Wanajifunza kwa urahisi sana.

Nasema hivyo kwa kuamini kwamba wameona jinsi nchi inavyoendeshwa na kujifunza nini kitatokea kama wakiamua kuiba. Wanfahamu. Hakuna kitakachotokea.

Nani achukuwe hatua?
 
Kwani yeye hawezi kuamu mpaka uongozi wa juu utake?kama anaona amekosea anapaswa kufanya hivyo kabla hata hajaambiwa kufanya hivyo.Viongozi wetu bwana wamezoea kushinikizwa tu..aargh!
 
Hili suala nililipata kijuu juu mwaka jana nikiwa Sumbawanga, sijaamini kwamba limeenda deep kiasi hiki. Kimsingi kwa stori nilizopata, huu 'Wizi Mtupu' wa mbolea ya ruzuku una mizizi mirefu sana, kiasi kwamba kama ni kuwajibisha watendaji basi huenda uongozi mzima wa mkoa wa Rukwa utawajibika.
Kuna bwana mmoja ambaye katajirika ghafla na mbolea hii ya wizi, yeye yuko kijiji cha Matai, ana guest houses kadhaa Matai na Sumbawanga mjini, ana malori kadhaa na mashamba makubwa ya mahindi ambapo kapata vitu vyote hivi 'within no time'. Kwa stori nilizopewa pale ni kwamba naye ni mfaidika wa mbolea hii ya wizi, kwa mgongo wa mkubwa fulani, kwamba mkubwa huyu anamtumia mfanyabiashara huyu kama 'Pen name'. Kijiji cha Matai kiko karibu kabisa na Kongo na Zambia, pamoja na bandari ya Kasanga.
Kuna kiungo cha stori hii natafuta ili tuunganishe, be back later.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…