Exclusive: Njoolay mrahishie Kikwete kazi; jiuzulu mwenyewe!

Exclusive: Njoolay mrahishie Kikwete kazi; jiuzulu mwenyewe!

Hope this turns out to be true. I am in a very awkward position, sometimes optimistic, and sometimes (actually most of the time) very pessimistic about the direction these guys are taking our country. I hope these are just worries!!

Kitila.. watch out for something very dramatic to occur within these two months (up to the end of april).
 
Naomba kuuliza yafuatayo;
  1. Je fedha hizi zimepotea lini na kutoka fungu gani?
  2. Je fedha hizi ni kutoka bajeti ya mwaka gani?
  3. Je Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na hata Idara ya Kilimo, zilikuwa zinaratibu vipi mchakato mzima wa kugawa mbolea na maombi ya ruzuku?
  4. Je Serikali za vijiji ambazo kitakwimu zilijulikana zimeagiza vocha kupita idadi ya watu au kuomba mbolea kuliko mahotaji, ni nani alihakiki maombi hayo na kufanya ufuatiliaji?
  5. Je Wakaguzi wa mahesabu wa Idara ya Kilimo, Mkoa wa Rukwa, Wizara ya Kilimo, Wizara Tamisemi na hata Mkaguzi Mkuu wa mahesabu, walipitia vitabu hivi na mchakato mzima kuuhakiki?
  6. Je baada ya mbolea kutolewa na shangwe na vigeregere kupigwa, Mkuu wa Mkoa alifanya juhudi gani kwenda kukagua mashamba na maeneo yaliyonufaika na mbolea hizi?
  7. Je Waandishi wa habari waliokuwa kwenye mkutano huu, walishindwa nini kumuuliza Mkuu wa Mkoa maswali ya msingi au hata kumhoji kwa nini asubiri amri kutoka Ikulu na asijiuzulu mwenyewe kama sehemu ya uwajibikaji?
Ni hayo tuu, ndugu zanguni!
 
Mchungaji.. hayo maswali hiyo umetumwa mkuu? Nani atayajibu.. Tanzania tukiendelea kuuliza maswali hivi tunaweza kujikuta tunaanza kufikiria!
 
Mzee Mwanakijiji,

Kwa dakika hii, naomba mnikubalie maombi yangu nipigie kelele kitu kinaitwa Uzembe, wala sitaki kufikiria kuwa ni Ufisadi fulani kama ule wa EPA.

Swali la nyongeza, je Mikoa mingine ambayo ilishiriki katika mpango huu wa vocha wao walifanyaje kazi zao? ni mafanikio gani wameyaona na ni matatizo gani yaliyowakumba?

Je waliokuwa wakiratibu fungu hili la fedha kutoka Hazina, Tamisemi na Wizara ya kilimo, walipitiwaje kuona uhujumu uliotokea Rukwa kama watadai mikoa mingine hapakutokea uzembe kama huu uliosababisha uhujumu?
 
JUMLA ya vocha za pembejeo za kilimo 1,114 zenye thamani ya zaidi Sh 21 milioni kati ya vocha 34100 zilizogawiwa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro zimepotea katika mazingira mbalimbali kwa mawakala wa kata tatu za Manispaa ya Morogoro.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini hapa, ofisa kilimo, mifugo na ushirika, Dk Issack Khama alisema Januari 14 mwaka huu, ofisa mtendaji wa mtaa wa Lukobe kata ya Kihonda, Salma Mbandu alitoa taarifa juu ya kupotea kwa vocha 300 ambazo alikabidhiwa.


Alisema katika taarifa ya ofisa mtendaji huyo juu ya upotevu wa vocha hizo alidai kuwa baada ya kukabidhiwa vocha hizo akiwa njiani kwenda katika ofisi yake kuendelea na ugawaji wa vocha , alitumia usafiri wa pikipiki ambapo alizifunga nyuma ya pikipiki vocha hizo ambapo zilidondoka njiani na yeye kutoziona wakati zilipoanguka


Dk Khama alimtaja wakala mwingine kuwa ni ofisa mtendaji wa Ngerengere Mkangwa ambaye aliibiwa vocha 300 katika mtaa huo, baada ya kuziacha ofisini Januari 22 na aliporejea ofisini Januari 25 hakuzikuta na katika mtaa wa Mindu, zilipotea vocha 514 baada ya Mwenyekiti wa kamati za vocha za mtaa, Iddi Kassimu kuzihifadhi nyumbani kwake na kuvunjiwa nyumba na hivyo kuibiwa vitu mbalimbali zikiwemo vocha hizo.


Hata hivyo Dk Khama alisema baada ya kupokea taarifa za wizi huo, ofisi yake iliripoti kwenye vyombo husika ikiwemo ofisi ya katibu tawala wa mkoa, kamati ya vocha ya wilaya ambayo inasimamiwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro ambapo mawakala hao walitoa taarifa polisi ambapo uchunguzi zaidi kuhusu upotevu huo unaendelea.


Dk Khama alisema kati ya vocha hizo zilizogawiwa, vocha 1,114 ziliibiwa ambazo ni 361 za mahindi aina ya chotara, 375 za mbolea ya kupandia na 378 za mbolea ya kukuzia aina ya urea ambapo Januari 14 mwaka huu ofisa mtendaji wa mtaa wa Lukobe kata ya Kihonda Salma Mbandu alitoa taarifa juu ya kupotea kwa vocha 300 ambazo alikabidhiwa.


Alisema kuwa awali halmashauri ilipokea vocha 10,500 za mbolea za kukuzia 10100 za kupandia 10,500 za mahindi aina ya chotara, za mahindi mchanganyiko 2000 na za mbegu za mpunga 1000 ambapo ofisi hiyo ilizigawa kwa wenyeviti wa kamati za mitaa, maafisa watendaji wa mitaa hiyo mitatu ndio walihusika katika kusaini na kupokea vocha hizo.
 
Duh, sasa kisingizio ni buti la Bajaj lilifunguka kutokana na barabara kuwa mbovu na vocha zikadondoka!
 
Duh, sasa kisingizio ni buti la Bajaj lilifunguka kutokana na barabara kuwa mbovu na vocha zikadondoka!

Ungekuwa wewe ndio kiongozi wa kutoa maamuzi juu ya uzembe wa huyu mtu aliyepoteza vocha, ungefanyaje Rev? Tuendelee na mjadala.
 
Mkuu Mwanakijiji, ahsante sana kwa taarifa hii, RC Rukwa ni mhusika kwenye ufisadi huo hawezi jinasua, hapa ndipo tunapojidhihirisha kuwa Tz maneno meeengi! vitendo hakuna, muungwana hawazi kumwajibisha Njolay hata kama si wa kambi yake, naye anafahamu hilo ndo maana ana beep kwa kudai akitakiwa kujiuzulu atajiuzulu.

Kilimo kwanza TZ ni porojo, Bingu hakusubiri kuandaa porojo za kilimo kwanza, aliitaa wadau na kutaka ushauri, wa kwanza akawa mwakilishi wa shirika la WFP, akiwa na picha ya vionzozi wa Kiafrika aina ya JK (omba omba) alimwambia chakula cha msaada kipo tele, Bingu akampa saa 24 kuondoka Malawi kwani aliona ushauri wake hauwezi isaidia Malawi.

Baada ya kikao hicho ukafuata utekelezaji, wakamwaga mbolea ya ruzuku na pembejeo zingine kama mbegu na zana za kilimo. Leo hii Malawi tuliowapa msaada wa tani 2000 za mahindi, wamepeleka Kenya tani 80,000 za mahindi, chakula sio tatizo tena nchini humo.

Malawi unaruhusiwa kuvusha bidhaa zingine lakini sio pembejeo za kilimo, hakuna urafiki katika hilo.

Waziri wa Kilimo nchini Malawi ni wa tatu katika daraja za viongozi, ni baada ya Rais, Makamu anafuata Waziri wa kilimo.
 
Anangoja nini? Huyu si yule aliyehamishwa kutoka kule kaskazini baada ya kuboronga vibaya? Kama sikosei alihusishwa na uchomaji nyumba za watu kwenye kijiji chao, sikumbuki mkoa, wilaya, n.k.

Sielewi kwa nini JK anaendelea kuwakumbatia viongozi wabovu namna hii! Sielewi kabisa!

Itatia hasira!
 
Back
Top Bottom