Hili suala nililipata kijuu juu mwaka jana nikiwa Sumbawanga, sijaamini kwamba limeenda deep kiasi hiki. Kimsingi kwa stori nilizopata, huu 'Wizi Mtupu' wa mbolea ya ruzuku una mizizi mirefu sana, kiasi kwamba kama ni kuwajibisha watendaji basi huenda uongozi mzima wa mkoa wa Rukwa utawajibika.
Kuna bwana mmoja ambaye katajirika ghafla na mbolea hii ya wizi, yeye yuko kijiji cha Matai, ana guest houses kadhaa Matai na Sumbawanga mjini, ana malori kadhaa na mashamba makubwa ya mahindi ambapo kapata vitu vyote hivi 'within no time'. Kwa stori nilizopewa pale ni kwamba naye ni mfaidika wa mbolea hii ya wizi, kwa mgongo wa mkubwa fulani, kwamba mkubwa huyu anamtumia mfanyabiashara huyu kama 'Pen name'. Kijiji cha Matai kiko karibu kabisa na Kongo na Zambia, pamoja na bandari ya Kasanga.
Kuna kiungo cha stori hii natafuta ili tuunganishe, be back later.