Ezekiel Maige, Tour Guide wa Kizungu wamevamia Mbuga zetu

Ezekiel Maige, Tour Guide wa Kizungu wamevamia Mbuga zetu

Heshima kwako Mvumbuzi.

Mkuu ni kweli tour guide wageni wamevamia kazi za wazawa.Bahati mbaya serekali ya magamba haina habari na masuala kama haya UWT iko kwaajili ya kuidhibiti CHADEMA na chama chochote kitakachotishia maslahi ya CCM.Miezi kadhaa iliyopita nilikuwa nafanyakazi fulani na kampuni ya SOKWE ASILIA nilishangaa kuanzia muhasibu,Inventory,manager wa camps,IT manager na key posts zote zimekamatwa na wageni [Kenya,Zimbabwe na S/Africa wazungu].Mishahara ya wafanyakazi wa wageni ulipwa kwa US Dollar[$ 5,000 - 12,000] pia haikatwi SDL,PAYE na NSSF.Hesabu za SOKWE ASILIA zinafungwa Kenya na South Africa.Hii ni kampuni moja yenye wafanyakazi wazawa zaidi ya 300 lakini wenye kulipwa kiwango kidogo cha mishahara Tsh 100,000 - 500,000/=.

Ukienda SERENA utashangaa nafasi zote kubwa zimeshikwa aidha na wahindi au wakenya.Ukwepaji wa kodi za serekali SDL,PAYE na Corporate Tax ni mkubwa kupita maelezo.Maafisa wa TRA mkoa wa Arusha wengi wana maisha ya juu kwasababu ya kushirikiana na haya makampuni kuinyima serekali mapato.wengi wanamiliki majumba na magari ya kifahari yasiyolingana na vipato halali.

Nasikia kutokwa na machozi; wako wapi viongozi wazawa na wazalendo kwa nchi yao au tuseme walikuwepo tu wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.Watanzania tumebaki kama yatima tunanyanyaswa, tunadhulumiwa, tunaibiwa tukiona na tunapiga kelele na hakuna wa kutusaidia. Mawaziri na viongozi wetu wa sasa wamebaki watu wa kutaka sifa mbele ya wahisani, watu wa kujionyesha na wanaohisi lugha ya uzalendo aidha imepitwa na wakati na ni aibu kuitaja au inatakiwa itajwe katika mrengo wa kukipigania CCM ili waendelee kula nchi.

Nchi inatelekezwa na imekuwa mahame ya wageni na hata tunapoongea hivi wanatuona kama machizi. Lakini nakumbuka Baba wa taifa hakuwa tayari kuona nchi yake ikichezewa kama mdoli namna hii na alitetea kwa kiasi kikubwa heshima ya Tanzania na matokeo yake WAHISANI HAWA HAWA walimbatiza na kumwita DIKITETA. Bora dikteta anayependa watu wake na kuchukia wageni kuliko viongozi wanaojidai wema kwa wageni huku wakiwatoa kafara wananchi wao ili tu wageni wafurahi.
 
Heshima kwako Mvumbuzi.

Mkuu ni kweli tour guide wageni wamevamia kazi za wazawa.Bahati mbaya serekali ya magamba haina habari na masuala kama haya UWT iko kwaajili ya kuidhibiti CHADEMA na chama chochote kitakachotishia maslahi ya CCM.Miezi kadhaa iliyopita nilikuwa nafanyakazi fulani na kampuni ya SOKWE ASILIA nilishangaa kuanzia muhasibu,Inventory,manager wa camps,IT manager na key posts zote zimekamatwa na wageni [Kenya,Zimbabwe na S/Africa wazungu].Mishahara ya wafanyakazi wa wageni ulipwa kwa US Dollar[$ 5,000 - 12,000] pia haikatwi SDL,PAYE na NSSF.Hesabu za SOKWE ASILIA zinafungwa Kenya na South Africa.Hii ni kampuni moja yenye wafanyakazi wazawa zaidi ya 300 lakini wenye kulipwa kiwango kidogo cha mishahara Tsh 100,000 - 500,000/=.

Ukienda SERENA utashangaa nafasi zote kubwa zimeshikwa aidha na wahindi au wakenya.Ukwepaji wa kodi za serekali SDL,PAYE na Corporate Tax ni mkubwa kupita maelezo.Maafisa wa TRA mkoa wa Arusha wengi wana maisha ya juu kwasababu ya kushirikiana na haya makampuni kuinyima serekali mapato.wengi wanamiliki majumba na magari ya kifahari yasiyolingana na vipato halali.

Inasikitisha sana mkuu Ngongo heshima kwako pia. Kinachotokea TZ ni hiki kama baba amekosa adabu na kumleta hawara ndani ya nyumba yake mbele ya watoto bila kuona shida hebu tabiri watoto watafanya nini. Iko wazi kwamba na kesho watoto nao watakwenda mtaani na kuopoa hata machangudoa na kuwaleta ndani ya nyumba ile ile ya baba yao kwani wanaona kama baba amefanya basi na mimi naweza fanya kwa sababu si kosa.

Maafisa wa TRA wameona anachofanya baba yao serikali na wao wakaona maadam ni RUKSA basi nao wasifanye makosa wakaishia kuwa kicheko mbele za watu.

System nzima ya serikali inajua kinachoendelea lakini kwa bahati mbaya wanatumia upole wa waTZ ambao sio wafuatiliaji wa vitu ambvyo siyo immediate kwao. This time serikali inatakiwa iwasikilize watu wake kama kweli inasema iko pale kutusaidia ili haya mambo wageni wanayotufanyia yapate malipizo yake. Mgeni afuate sheria za nchi na ajue kwamba na hii nchi ina watu ambao nao wanastahili heshima na ujira mzuri pia waelewe kwamba wanatakiwa wachangie kodi kutokana na mavuno wanayopata kutokana na rasilimali za watanzania. Corporate Social Responsibility inatakiwa ilipwe na makampuni yote ya kigeni lakini hili inayabana makampuni machache tu yanayo operate mijini kama ya Bia, simu n.k. Tunaomba serikali iamke sasa watupe blanketi sisi tunaumia jamnani.
 
Huyu Waziri ni kama mshereheshaji tu,kubadili hii wizara ni sawa na kurekebisha mikataba ya uchimbaji wa madini ya shahabu,hawa wazungu walishaiteka hii wizara hasa Idara ya Wanyamapori hakuna litakalowezekana,nimemsikia akieleza kugawa vitalu upya,wimbo unaoimbwa toka 2009 hadi leo,hakuna wa kumvika paka kengele,mbaya zaidi amegeuka Waziri mtendaj,hata watendaji wanamsubiri yeye afanye maamuzi wakati hana taaluma hata chembe inayohusu Maliasili wapo wanamuangalia anavyoponda taaluma zao,siku akiporomoka ndiyo utasikia mengi,njaa wacha banaaaaaaaaaaausipime
 
Huyu Waziri ni kama mshereheshaji tu,kubadili hii wizara ni sawa na kurekebisha mikataba ya uchimbaji wa madini ya shahabu,hawa wazungu walishaiteka hii wizara hasa Idara ya Wanyamapori hakuna litakalowezekana,nimemsikia akieleza kugawa vitalu upya,wimbo unaoimbwa toka 2009 hadi leo,hakuna wa kumvika paka kengele,mbaya zaidi amegeuka Waziri mtendaj,hata watendaji wanamsubiri yeye afanye maamuzi wakati hana taaluma hata chembe inayohusu Maliasili wapo wanamuangalia anavyoponda taaluma zao,siku akiporomoka ndiyo utasikia mengi,njaa wacha banaaaaaaaaaaausipime

Mwenzake aliyepita Shamsa Mwangunga yeye alikuwa stakeholder kabisa wa haya makampuni ya utalii hasa ya kutoka nje pia ndivyo ilivyo kuwa kwa mama yetu Zakia Meghji. Kwa bahati mbaya miaka ya hivi karibuni hatujapata mawaziri makini katika wizara hii nyeti ya serikali kiasi kwamba atakapopatikana basi atakuta uharibifu mkubwa sana umefanywa.

Kama waTZ wanaohangaika kukesha na watalii mbuga za wanyama hawatasikilizwa basi itakuwa ni usaliti kwa wapiga kura na watanzania kwa ujumla. Wenzetu Kenya wanajitahidi sana kutunza rasilimali zao lakini sisi tunazigawa bure kwa wageni ilimradi umeahidiwa ka-VOGUE au au kanyumba ka Ghorofa moja au ka hoteli. Ni kweli kazi ikiisha ndo mtu anakumbuka alivyowasaliti wenzake na hapo anakuwa amepoteza heshima mbele ya waTZ na kila mmoja anamwona mjinga na msaliti tu. Pressue au kiharusi havichelewi kubisha hodi kudai ka uhai kalichobaki. Bora umalize kazi yako waTZ wakusifu kwa kuwapigania na kuwasaidia kuliko waseme akafie mbali!!!!!!
 
Wizara ikishirikiana na TANAPA, Ngorongoro Conservation Authority waunde TASK TEAM ya kurekebisha hii hali kwani itaboresha maisha ya waTZ haswa walioajiriwa katika haya makampuni ya utalii. Bila hivyo watanzania wataendelea kunyanyasika katika nchi yao huku wageni wakija na kuchukua hata kile kidogo kilichobaki.
 
Mi naomba watanzania wenzangu uvumilivu sasa utushinde. Tufikie mahali tuseme BASI!! Liwalo na liwe.... Wakati sirikali inaanda kusheherekea miaka 50 ya uhuru na umaskini, sisi tujipange kufanya maandamano nchi nzima kuwakosoa hawa mafisadi wasiojali utu. Kwa kweli inasikitisha sana. Hakuna nafuu kwa mtanzania yeyote popote. Duh!! Sielewi kwanini tupo slow kufanya maamuzi ya kuwafukuzia mbali hawa wakoloni weusi... Aaah!
 
jamani kama ni swala la kuchukuliana ajira tusiishie kwenye utalii tu, kuna sehemu mbalimbali hii kadhia ipo, kwenye ndege zetu zinazofanya safari za ndani kuna wazungu kibao, hebu anayejua shughuli za uwanja wa ndege wa Arusha, aniambie ni marubani wangapi wazawa wanarusha zile ndege, tuende na kwenye makampuni yanayomilikiwa na wenzetu wa Asia, mabosi wote wametoka India mfano,NSK OIl ipo njiro, kule sidhani kama wale wana permit ya kufanya kazi nchini na sehemu yenyewe imejificha sana, Leopard Tours, Mt Meru Petrolium, Aim Steel n.k. hapa nimejitahidi kutokutoka nje ya Arusha lakini uchunguzi ukifanyika rasmi nchi nzima,yatagundulika makampuni mengi sana, tunachoambulia watanzania ni manyanyaso na dharau.
 
Kweli inauma sana nchini kwako ila ajira zinachukuliwa na wageni tena bila serikali kuwa na taaria au kuchunguza na kuchukua hatua.
mvumbuzi asante kwa kufumbua macho! hebu Maige ashtuke na kufuatilia hili suala mana kama hajasoma lazima atahadithiwa hii thread..
vitu kama hivi vikiendekezwa vinashamiri na inakuwa too late ku-control..please serikali okoeni wazawa!
 
Mi naomba watanzania wenzangu uvumilivu sasa utushinde. Tufikie mahali tuseme BASI!! Liwalo na liwe.... Wakati sirikali inaanda kusheherekea miaka 50 ya uhuru na umaskini, sisi tujipange kufanya maandamano nchi nzima kuwakosoa hawa mafisadi wasiojali utu. Kwa kweli inasikitisha sana. Hakuna nafuu kwa mtanzania yeyote popote. Duh!! Sielewi kwanini tupo slow kufanya maamuzi ya kuwafukuzia mbali hawa wakoloni weusi... Aaah!

Ni kweli tunakokwenda kuna kila dalili ya mtanzania kutambua haki yake na hili ni bomu linalosubiri kulipuka kama serikali itaendelea kuwaona waTZ ni wale wa miaka 40 ambao staili yao ni kudanganywa. Miaka 50 ya kusheherekea uhuru tunataka washeherekee wale waliongangania madaraka tangu ujana wao hadi leo na ambao kukua na kuishi kwao ni CCM. Sisi tunaopambana ni vema watugawie hizo hela kidogo za maadhimisho tukakodishe mashamba tulime kuliko kwenda viwanjani kuchomwa na jua huku tukishuhudia watu wakijitengenezea ulaji.
 
jamani kama ni swala la kuchukuliana ajira tusiishie kwenye utalii tu, kuna sehemu mbalimbali hii kadhia ipo, kwenye ndege zetu zinazofanya safari za ndani kuna wazungu kibao, hebu anayejua shughuli za uwanja wa ndege wa Arusha, aniambie ni marubani wangapi wazawa wanarusha zile ndege, tuende na kwenye makampuni yanayomilikiwa na wenzetu wa Asia, mabosi wote wametoka India mfano,NSK OIl ipo njiro, kule sidhani kama wale wana permit ya kufanya kazi nchini na sehemu yenyewe imejificha sana, Leopard Tours, Mt Meru Petrolium, Aim Steel n.k. hapa nimejitahidi kutokutoka nje ya Arusha lakini uchunguzi ukifanyika rasmi nchi nzima,yatagundulika makampuni mengi sana, tunachoambulia watanzania ni manyanyaso na dharau.

Kwa ufupi Arusha imekuwa shamba la bibi haswa Wazungu ni wengi na ukitembea mjini wazungu wengi wako kwenye private cars zao kuonyesha tayari wamepiga kambi hapa na wanafanya kazi. Ukiwa una drive kwa mfano kutokea Njiro hadi Kisongo unaweza kufikiri Arusha imekuwa Ulaya kwa jinsi wazungu wazawa wanavyoongezeka siku hadi siku. wengine wananunua milima na wanauziwa kirahisi kabisa kama mlima wa pale Ngulelo amenunua yule mzungu aliyekuja nchini akijidai anatengezeza baiskeli kwa teknolojia ya bei rahisi maarufu kama baiskeli za Smart Hardy. Tindiga la Kijenge pale Kimandolu lipo mnadani na aliyeuza ni Meya wa Arusha aliyebwaga Ndugu Laurent Hedi. Hivi serikali inakuwa wapi wakati viongozi wake wa kuanzia ngazi za chini wanauza nchi na waTZ kubakia wapangaji. Hii ni zaidi ya ukoloni mambo leo
 
jamani kama ni swala la kuchukuliana ajira tusiishie kwenye utalii tu, kuna sehemu mbalimbali hii kadhia ipo, kwenye ndege zetu zinazofanya safari za ndani kuna wazungu kibao, hebu anayejua shughuli za uwanja wa ndege wa Arusha, aniambie ni marubani wangapi wazawa wanarusha zile ndege, tuende na kwenye makampuni yanayomilikiwa na wenzetu wa Asia, mabosi wote wametoka India mfano,NSK OIl ipo njiro, kule sidhani kama wale wana permit ya kufanya kazi nchini na sehemu yenyewe imejificha sana, Leopard Tours, Mt Meru Petrolium, Aim Steel n.k. hapa nimejitahidi kutokutoka nje ya Arusha lakini uchunguzi ukifanyika rasmi nchi nzima,yatagundulika makampuni mengi sana, tunachoambulia watanzania ni manyanyaso na dharau.

Ni kupitia hoteli zote za wageni ,makumpuni yote na NGOs za kimataifa serikali ikiamua kufuatilia haitaamini kinachoendelea Tanzania. Najiuliza ni nchi imekuwa kubwa kutoweza kufikika na kutawalika au ni uvivu wa viongozi kutojua wajibu wao au kupofushwa na tamaa za kujilimbikizia utajiri ? Mbona wakati wa awamu ya kwanza hii nchi kila mahali palifikika na hakuna hata mgeni mmoja aliweza kujificha popote leo hii katika maendeleo ya kiteknolojia namna hii inakuwaje eti wageni walioko nchini wasifahamike wanafanya nini? Hapa lazima kuna namna viongozi waliopewa dhamana ya uangalizi wa hizi wizara wananufaika na sintofahamu hii ambayo haitakiwi kuwa sintofahamu? kama Polisi wameweka mkakati wa kuanzisha ulinzi shirikishi kwa nini serikali isiweke mfumo huo kwenye ngazi za chini kabisa ili wananchi waweze kutoa taarifa moja kwa moja wanapoona kitu ambacho kinaweza haribu uchumi wa nchi au wa mtanzania?.
 
Kweli inauma sana nchini kwako ila ajira zinachukuliwa na wageni tena bila serikali kuwa na taaria au kuchunguza na kuchukua hatua.
mvumbuzi asante kwa kufumbua macho! hebu Maige ashtuke na kufuatilia hili suala mana kama hajasoma lazima atahadithiwa hii thread..
vitu kama hivi vikiendekezwa vinashamiri na inakuwa too late ku-control..please serikali okoeni wazawa!


Haya mambo ipo siku viongozi wetu watazibuka masikio na kama si hivyo basi Mungu atawezesha kupatikana viongozi wengine committed na kuondoa wale wanaoshindwa kusimamia rasilimali za nchi yao kama ilivyo hivi sasa.
 
Inabidi viongozi wafundishwe listening skills kwani inawezekana hawajui kwamba nao wanatakiwa wawasikilize wanaowaongoza.
 
Haya mambo ipo siku viongozi wetu watazibuka masikio na kama si hivyo basi Mungu atawezesha kupatikana viongozi wengine committed na kuondoa wale wanaoshindwa kusimamia rasilimali za nchi yao kama ilivyo hivi sasa.

Mwana kwetu unayosema hayako mbali
 
Namshukuru sana Mbunge wangu wa Arusha mjini Mh. Godbless Lema wakati wa kipindi cha Maswali kwa waziri Mkuu leo Alhamis asubuhi amemwuliza waziri Mkuu Mizengo Pinda swali linalohusiana na hii mada yaani " Serikali ina mkakati gani kutokomeza tabia ya baadhi ya makampuni hususani Mahoteli kuajiri wageni kwa kazi zinazoweza kufanywa na waTZ?

Waziri mkuu alisema idara ya utumishi imeshaanza mkakati wa kushughulikia hili jambo ila akatoa angalizo na kusema tatizo la waTZ ni watu wenye visingizio vingi mno wawapo kazini na hii huharibu kazi. Kutokana na tabia hiyo basi huwalazimu kuchukua watu wa nje ya nchi ambao wako kikazi zaidi
 
Alichojibu Waziri mkuu haki- apply katika kazi za tour guide kwani wao wako highly motivated na kazi yao kwani wanajua wakitoa visingizio na kutokwenda porini hawapati tip. Kwa hiyo nataka kumjibu waziri mkuu kwamba si kweli kila mahali sababu zinazosababisha wamiliki wa haya makampuni kuajiri watu kutoka nje bali kwa kiasi kikubwa ni ukiukaji wa sheria za nchi ambazo kwa kiasi kikubwa hazifuatiliwi.

Pia waziri mkuu ameshindwa kueleza kama kwa sababu waTZ wana visingizio basi ni ruksa kuajiri watu kutoka nje just simple like that? Nafikiri sheria ingewekwa tu ya kuthibiti hali hii ikiwa ni pamoja na kuruhusu summary dismissal kwa wenye tabia hii kuliko kuonyesha kwamba dawa ya wenye visingizio ndiyo hiyo ya kuajiri watu kutoka nje bila kufuata sheria za nchi
 
Back
Top Bottom