Face 2 Face with Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo: "Tunafanya Politics of Engagement kwa kuwa Pragmatic on What is Possible"

Ruzuku ilikuwa haki yao, kuipokea haliwezi kuwa kosa, vipi huyo anayeona bandari zetu Tanganyika zinatolewa kwa waarabu milele anaamua kunyamaza kimya? Au ni mrundi?!
 
ACT sio kama wako engaging ila hawana choice pona Yao ni maridhiano na CCM otherwise hawawezi pambana na CCM head-on kulinganisha na CHADEMA ambayo haihitaji endorsement ya CCM ili kushinda chaguzi yoyote au kuongeza ushawishi kwa wananchi.
Hayo mnayofanya Chadema sasa Cuf/Act walishayanya kwa miaka mingi kule Zanzibar na hawakupata chochote, hata nyinyi cdm hamtapata chochote Ccm ni ile ile. Mtamtakuja gundua hilo baadae sana, hata nyinyi hamuwezi pambana na ccm mnajitekenya tu na kucheka wenyewe. Zitto ni mwalimu kwenu amewatangulia sana uelewa kwenye siasa.
 
Paskali, nimekupata vzr - hope hata wabwekaji watakuelewa ingawa ni wagumu Kama jiwe la ziwa Victoria
 
Chadema ni sawa na mwanamke mwenye wivu ,mtu yeyote mwenye hoja nzuri kama hatoki chadema kwao ni mitusi tu
 

100%…. Paskali nakuelewa hapo uko sawa, ila usimwambini Zitto, huyo ni kinyonga, kama huamini subiri miaka kadhaa mbele.
 
Uko sahihi. Ni kwa vile tu ACT hawana uwezo na nguvu ya ushawishi Tanzania bara
Mayala,iko hiv
Mayala, haya masuala ya migongano(confrontations),mikutano,maandamano pamoja na majadiliano(engagements) ni sehemu ya mambo katika siasa...,na yote yanatumika kulingana na mazingira na wakati.

Zitto amesema kwamba ACT kwa sasa wanatumia majadiliano(engagement) kama njia pekee yenye uhalisia(pragmatic) katika kufanya siasa zao...na hivyo kuachana na njia nyingine za kufanya siasa. Labda kwa hilo yuko sahihi kwa namna yake ukichukulia wigo wa watu wachache wanaounga mkono ajenda za chama cha ACT hususan kwa Tanzania bara,hali ambayo inaleta ugumu wa kutumia yale masuala mengine kama mikutano yenye nguvu na maandamano..,njia ambazo zinahitaji upate mwitikio mkubwa toka kwa watu.

Lakini,njia ya kufanya engagements katika siasa ina ukomo au kasoro zake endapo huyo unayetaka kufanya naye engagement ana ushawishi na isitoshe anataka awe ana-dictate majadiliano yenu....kwa maana nyingine pande zote zilioingia katika engagement ni timu washindani lakini moja kati ya hizo timu inataka iwe refa.
Kwa mfano,Zitto amesema ,pamoja na mambo mengine wameiomba serikali iijumlishe rasimu ya tume ya Warioba katika miswada yake itakayopeleka bungeni.
Sasa serikali ikikataa ombi la ACT,watafanyaje ikiwa wanaona wazi kabisa rasimu hiyo ni muhimu? ACT wataacha kuchukua njia nyingine ili hoja yao hii muhimu yenye maslahi kwa taifa itekelezwe?
Hata CHADEMA nao siku za karibuni wametumia siasa za engagement kiasi cha kufikia watu kuwaita walamba asali.
Chadema wamesema wazi kwamba wameamua kutumia njia nyingine mikutano ya nguvu baada ya wenzao walioingia katika majadiliano kushindwa kutekeleza hata jambo moja walilokubaliana.
Sana sana tutamshangaa Zito kama kukubaliana na kila kitu refa anachoamua hata kama kinaipendelea timu waliyoingia uwanjani.
 
Mtamtakuja gundua hilo baadae sana, hata nyinyi hamuwezi pambana na ccm mnajitekenya tu na kucheka wenyewe. @Zitto ni mwalimu kwenu amewatangulia sana uelewa kwenye siasa.
Mwalimu? Be serious.... 2020 si alikua kwenye MoU na JPM aliambulia Nini kuzidi CHADEMA? Alisimamisha mgombea Urais vipi alizidiwa kura Hadi na Tundu Lissu huko huko Zanzibar ambayo ni ngome ya Maalim?

Baada ya 2020 vyama vimebaki viwili tu CCM na CHADEMA na Kwa Hilo nampongeza JPM alihakikisha wapinzani uchwara wote Wana quit siasa Sasa wamebaki serious politicians only and unfortunately ACT sio mojawapo na 2025 ndio itakua kaburi lao la milele maana Zanzibar hawana mtu wa calibre ya Maalim na huku bara ni non-existent na kama uchaguzi utakua huru na haki basi CHADEMA itazoa kura za kihistoria thus rendering ACT obsolete and casting them to the darkest pits of political oblivion.
 
Zanzibar unaijua Mzee au unazungumza tu unadhani Zanzbar tofauti kazileta Seif, Maalim kapokea tu kijiti soma historia tofauti ya Zanzibar ni zaidi ya Maalim Pemba hata kama kiongozi atakuwa nani misimamo yao haibadiliki kwa miaka michache hivyo hivyo Unguja tofauti zao ni za zaidi ya kisiasa.

Kitu kingine Zitto Junior CHADEMA ni kama hamjui siasa za Afrika Magu kawatuliza 2015 mpaka anaondoka viongozi wenu wote walikuwa wamekimbia hata Samia akiamua kuipa mkono ACT 2025 basi by 2030 CHADEMA itakuwa kama CUF au NCCR maana siasa za Afrika ni njaa tuu sasa ACT wakipewa resource kwanza hao CHADEMA kibao watakwenda huko ACT kwenye mtonyo na nafasi za uongozi.

La mwisho najua wewe mtu wa hoja ila CHADEMA imeharibiwa sana sijui ni impact ya siasa ya Magu imekuwa na kundi kubwa la watu ambao ni radical wao kutukana, uwongo, uzushi, ubaguzi kwao sio issue kabisa kikubwa wanapata engagement mitandaoni na majukwaani hii inawapa milage kwa muda mfupi ila in long run itawacost sana kwanza ndani ya chama na uungwaji mkono nje ya chama. Hili kundi linakipeleka chama kuwa kikundi cha harakati na sio chama mbadala kwa ajili ya kuchukua dola na kutoa majibu ya shida za wananchi.

Mie I fear CCM wakisema lets support ACT maana ACT atukane utakavyo ila wana wanasiasa kweli kweli push kidogo six year to 2030 wataifunika CHADEMA that one i can bet with you.
 
Sisi CHADEMA ngoja twende na "Confrontational Politics" mpaka kieleweke, hawa CCM hawana nia thabiti ya Reforms.
 
Ruzuku ilikuwa haki yao, kuipokea haliwezi kuwa kosa, vipi huyo anayeona bandari zetu Tanganyika zinatolewa kwa waarabu milele anaamua kunyamaza kimya? Au ni mrundi?!
Kwa hiyo kwa nini walisusia kama ni haki yao? Na kwa nini wasema mwanasiasa fulani ni fisadi hafai kuongoza kisha waje kumfanya mgombea wao?
 
Wangekuwa bora wangekuwa wanajiamini na kuweka mgombea wao wenyewe, unawa overrate sana CDM wa kipindi hicho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…