Fahamu baadhi ya sheria za kijamii zitakazokusaidia kuishi na watu vizuri

Fahamu baadhi ya sheria za kijamii zitakazokusaidia kuishi na watu vizuri

Ben Zen Tarot

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2014
Posts
4,298
Reaction score
7,612
1. Usimpigie mtu simu zaidi ya mara mbili mfululizo. Ikiwa hapokea simu yako, chukulia kuwa ana jambo muhimu yuko analifanya.

2. Rudisha pesa ulizokopa hata kabla mtu aliyekukopa hajakukumbusha au kukuomba. Kufanya hivi kunaonyesha ni jinsi gani ulivyo mwaminifu, na kutakufanya uaminike zaidi.

3. Usiagize chakula kingi usichoweza kukimaliza unapokuwa mgahawani au hotel. Agiza chakula kinachokutosha na utakachokimaliza, hii itakufanya uonekane ni jinsi gani unavyothamini chakula na kuheshimu juhudi za wakulima.

4. Usimuulize mtu maswali ya aibu mbele ya watu kama ‘Oh kwa hiyo bado hujaolewa?’ .au ‘Je, huna watoto’ au ‘Kwa nini hujanunua nyumba?’ Au kwa nini hununui gari?. Hilo sio jukumu lako, ni jukumu lake mhusika pamoja na MUNGU wake.

5. Ikiwa unapawe ofa na rafiki yako katika kulipia mambo tofauti tofauti wakati wa matembezi, Jitahidi na wewe umlipie wakati ujao, ili asikuchoke au kukudharau maana binadamu hawana dogo.

6. Heshimu maoni au mawazo ya mtu kwa kumsikiliza wakati anapoongea. Kumbuka kile ambacho ni 6 kwako kitaonekana 9 kwa mtu mwingine, usidharau maoni au mawazo ya mtu hata kama unajua kaongea pumba.

7. Usimkatishe mtu katika kipindi ambacho anazungumza, sikiliza kwanza akimaliza kuongea na wewe ongea, hii itasaidia kuepuka ugomvi au mabishano wakati wa mazungumzo yenu.

8. Usimseme mtu vibaya au kuongea mabaya yake mbele ya watu wengine, ikiwa una mabaya yake mtafute na zungumza nae kwa upendo ili ayatambue madhaifu yake na ajisahihishe. kumbuka hakuna binadamu mkamilifu.

9..Usisahau kusema asante katika kipindi ambacho unapokea kitu chochote kutoka kwa mtu au kusaidiwa jambo fulani. Hii itaonyesha ni jinsi gani unavyothamini.

10. Jifunze kumsifia mtu hadharani.na mkosoe mtu faraghani, hii itaonyshesha ni jinsi gani ulivyo muungwana. Usimkosoe mtu hadharani.

11.Mtu anapokuonyesha picha kwenye simu yake, usitelezeshe kidole chako kushoto au kulia. Huwezi kujua nini kinafuata, Jenga tabia ya kufanya kile ulichoelekezwa kufanya, tena kifanye kwa uaminifu.

12. Mwenzako akikuambia anajisikia vibaya kuwa mwelewa, usitake kujua sababu za kwanini anajisikia vibaya ikiwa hajakuambia.

13. Mtende na kumfanyia mfanyakazi wako wa ndani mambo unayowafanyia watoto wako, ikiwa ni upendo muonyeshe upendo kwa kumtimizia mahitaji yake yote. Kumbuka wewe umezaa tuu, ila yeye anakulelea watoto wako.

14. Ikiwa mtu anazungumza moja kwa moja na wewe, huku ukitazama simu yako au unacharti ni kukosa adabu. Jifunze kuweka umakini wako katika jambo moja.

15. Usitoe ushauri kamwe hadi uombwe; ili usije onekana umejipendekeza kwa kutoa ushauri usiohitajika.

16. Ondoa miwani yako ya jua ikiwa unazungumza na mtu yeyote barabarani. Ni ishara ya heshima.

17. Usizungumze kamwe kuhusu utajiri wako katikati ya watu maskini. Vivyo hivyo, usizungumze juu ya watoto wako katikati ya mtu tasa. Usizungumze kuhusu wazazi wako katikati ya mayatima.
Natumai umenielewa.
 
Ogopa sana mahakama ya jamii hii unakufa taratibu taratibu, ukisimama jukwaani, ukiingia kwenye media unakumbana na hatia wanasema ulimuua fulani huku wewe ulifanya siri.
 
Ukienda ofisi yoyote mpe heshima zote Secretary.mlinzi, wafanya usafi. Ikiwezekana mpooze hata na buku 5 tu. Hawa watu huwa wana mchango mkubwa sana katika kufanikiwa katika shughuli inayokupeleka hapo ofisini.

Mtaani kwako wape 500 au 200 za sigara hawa vijana wahuni wahuni. Hawa madogo huwa wana uelewa sana mtaa.kuna baadhi ya sehem watakusaidia.

Kuwa na namba ya bodaboda, police, mwanasheria, daktari kondakta wa mabus ya mikoani, mchungaji au ustadhi au padri. Wakala wa mpesa au nmb au crdb.

Jenga urafiki na wastaafu. Hawa wazee wana story nyingi sana za kufundisha. Wastaafu wana ushauri wao ambao umebase kwenye experience.

Mwenyezi Mungu amekujalia umejenga basi pale nje hebu weka kaduka karejareja. Badala ya kununua sukari mfuko uuweke ndani tu.nunua hiyo sukari weka dukani na wewe ujiuzie rejareja. Mchele,tambi,mafuta.


Ukiwa unaishi mjini hakikisha UMEJIUNGA KIKUNDI CHA KUSAIDIA na unashirikiana kwenye misiba na harusi. Pindi uwapo kwa matatizo upate wa kusaidiana na wewe. Hivi ndivyo wachaga wanafanya na makabila mengine.usikae mjini kwa kujitenga ilhali una familia tayari.


Hakikisha una mawasiliano na mtaalamu wa tiba asili. Kwenye huu ulimwengu kuna tatizo halitibiki kanisani wa hospital.

Mtu unamdai au amekudhulumu msamehe. Kupitia madeni watu wanauana na kujenga chuki isiyokuwa na maana yoyote.

Usimseme vibaya mfanyakazi mwenzako. Jitahidi mno usikae ukaanza kumsema vibaya workmate wako. Maneno hayohayo ndo yatakayotumika kukupima wewe. Mfano ukimsema kuwa siyo muaminifu automatically ukiyumba kidogo tu utaitwa mwizi.

Usigombanie Mali urithi.
Ugomvi wa mali za urithi ni mbaya sana.kama mwanaume pambana upate chako. Ndugu wakiona unawasumbua kwenye urithi kwa vile ni ndugu yao hawakuui wanakufanya kichaa. Vichaa wengi wamegeuzwa hivyo na ndugu zao.

Say less than necessary. Jitahidi sana usiwe muongeaji wa hovyo hovyo. The more you talk the more common you appear.
Usipige kura. Achana kabisa na haya maigizo. Anayechagua kiongozi sio mwananchi ila ni mhesabu kura ambaye ni tume ya uchaguzi iliyoteuliwa na rais ambaye ni mgombea katika uchaguzi huo.

Wekeza kwenye ardhi.
Ardhi hupanda thamani mida wote.

una mchepuko?
si dhambi kuwa na sidechick lakini hakikisha anafahamu uwepo wa nyumba kubwa. Kuna wanawake wameumbwa ili wawe sidechick na wanajua hilo. Wala hatakupa tabu.

wewe ni mnywaji?
Achana na bia hizi zitakupa hang over. Gonga k vant, Gordon yako moja na ka castle milk kako kamoja kakupooza uende nyumban ukapumzike.
Bia inanenepesha
Spirit inachoma mafuta.
Muhimu ni kunywa kwa kiasi. Na uhakikishe umeshiba. Spirit inaendana na nyama choma.

Karma ipo.heshimu sana hii sheria usimtendee mtu ubaya kwani utalipwa ubaya.
Mifano mizuri ipo kwa Sabaya na Makonda. Leo hakuna mwenye furaha kutokana na matendo yao.

Usiache ibada.
Usikubali wiki ipite bila kwenda kuongea na Mungu wako.
Dini ndo imesababisha tuka civilized.
Unapokuwa katika ibada tunakumbushwa namna ya kuwa watu wema.
Usiue
Usizini
Usiibe etc.
Ibada ni uwanja mzuri wa kukumbusha namna ya kuishi vyema na jamii yako.

Wape watoto wako elimu bora.
Wazazi wako walikusomesha st kayumba.
Pambana wanao wasome english medium.
Shule bora inatengeneza future nzuri ya kizazi chako.

Wewe na partner wako,mke wako,mama watoto wako hebu mjitahidi at least kila mwezi muende sehemu mkapate dinner na familia au nyie wawili mpige story 2 au tatu then mrudi home.
Tusiwasahau hawa wake zetu. Tusiwasahau.umuhimu wao upo milele.

Soma vitabu
Usikae tu bila kuupa ubongo chakula.
Vitabu hivi ni recommended
48 laws of power by Robert Greene
Subtle arts of not giving a f*ck.
Ego is an enemy.

Vitabu hivi vinaitwa self help book.


Last but most, BE YOU.
usiishi maisha fake. Ishi katika uhalisia wako. Jamii inapenda real people.

Na wewe mwana JF hebu tupatie sheria yoyote au ujuzi wowote ambao ni muhimu kuufahamu ili tuweze kukaa vizuri katika jamii yetu bila tabu yoyote!
 
Ukienda ofisi yoyote mpe heshima zote PS.mlinzi, wafanya usafi. Ikiwezekana mpooze hata na buku 5 tu. Hawa watu huwa wana mchango mkubwa sana katika kufanikiwa katika shughuli inayokupeleka hapo ofisini.

Mtaani kwako wape 500 au 200 za sigara hawa vijana wahuni wahuni. Hawa madogo huwa wana uelewa sana mtaa.kuna baadhi ya sehem watakusaidia.

Kuwa na namba ya bodaboda, police, mwanasheria, daktari kondakta wa mabus ya mikoani.

Jenga urafiki na wastaafu. Hawa wazee wana story nyingi sana za kufundisha. Wastaafu wana ushauri wao ambao umebase kwenye experience.


Ukiwa unaishi mjini hakikisha UMEJIUNGA KIKUNDI CHA KUSAIDIA na unashirikiana kwenye misiba na harusi. Pindi uwapo kwa matatizo upate wa kusaidiana na wewe.

Hakikisha una mawasiliano na mtaalamu wa tiba asili. Kwenye huu ulimwengu kuna tatizo halitibiki kanisani wa hospital.

Mtu unamdai au amekudhulumu msamehe. Kupitia madeni watu wanauana na kujenga chuki isiyokuwa na maana yoyote.

Usimseme vibaya mfanyakazi mwenzako. Jitahidi mno usikae ukaanza kumsema vibaya workmate wako. Maneno hayohayo ndo yatakayotumika kukupima wewe. Mfano ukimsema kuwa siyo muaminifu automatically ukiyumba kidogo tu utaitwa mwizi.

Say less than necessary. Jitahidi sana usiwe muongeaji wa hovyo hovyo. The more you talk the more common you appear.

una mchepuko?
si dhambi kuwa na sidechick lakini hakikisha anafahamu uwepo wa nyumba kubwa. Kuna wanawake wameumbwa ili wawe sidechick na wanajua hilo. Wala hatakupa tabu.

wewe ni mnywaji?
Achana na bia hizi zitakupa hang over. Gonga k vant, yako moja na ka castle milk kako kamoja kakupooza uende nyumban ukapumzike.
Bia inanenepesha
Spirit inachoma mafuta.
Muhimu ni kunywa kwa kiasi.

Usiache ibada.
Usikubali wiki ipite bila kwenda kuongea na Mungu wako.
Dini ndo imesababisha tuka civilized.
Unapokuwa katika ibada tunakumbushwa namna ya kuwa watu wema.
Usiue
Usizini
Usiibe etc.
Ibada ni uwanja mzuri wa kukumbusha namna ya kuishi vyema na jamii yako.

Wape watoto wako elimu bora.
Wazazi wako walikusomesha st kayumba.
Pambana wanao wasome english medium.
Shule bora inatengeneza future nzuri ya kizazi chako.

Wewe na partner wako,mke wako,mama watoto wako hebu mjitahidi at least kila mwezi muende sehemu mkapate dinner na familia au nyie wawili mpige story 2 au tatu then mrudi home.
Tusiwasahau hawa wake zetu.

Soma vitabu
Usikae tu bila kuupa ubongo chakula.
Vitabu hivi ni recommended
48 laws of power by Robert Greene
Subtle arts of not giving a JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala.
Ego is an enemy.

Vitabu hivi vinaitwa self help book.


Last but most, BE YOU.
usiishi maisha fake. Ishi katika uhalisia wako. Jamii inapenda real people.
Thank you so much mike2k

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Ukienda ofisi yoyote mpe heshima zote PS.mlinzi, wafanya usafi. Ikiwezekana mpooze hata na buku 5 tu. Hawa watu huwa wana mchango mkubwa sana katika kufanikiwa katika shughuli inayokupeleka hapo ofisini.

Mtaani kwako wape 500 au 200 za sigara hawa vijana wahuni wahuni. Hawa madogo huwa wana uelewa sana mtaa.kuna baadhi ya sehem watakusaidia.

Kuwa na namba ya bodaboda, police, mwanasheria, daktari kondakta wa mabus ya mikoani.

Jenga urafiki na wastaafu. Hawa wazee wana story nyingi sana za kufundisha. Wastaafu wana ushauri wao ambao umebase kwenye experience.


Ukiwa unaishi mjini hakikisha UMEJIUNGA KIKUNDI CHA KUSAIDIA na unashirikiana kwenye misiba na harusi. Pindi uwapo kwa matatizo upate wa kusaidiana na wewe.

Hakikisha una mawasiliano na mtaalamu wa tiba asili. Kwenye huu ulimwengu kuna tatizo halitibiki kanisani wa hospital.

Mtu unamdai au amekudhulumu msamehe. Kupitia madeni watu wanauana na kujenga chuki isiyokuwa na maana yoyote.

Usimseme vibaya mfanyakazi mwenzako. Jitahidi mno usikae ukaanza kumsema vibaya workmate wako. Maneno hayohayo ndo yatakayotumika kukupima wewe. Mfano ukimsema kuwa siyo muaminifu automatically ukiyumba kidogo tu utaitwa mwizi.

Say less than necessary. Jitahidi sana usiwe muongeaji wa hovyo hovyo. The more you talk the more common you appear.

una mchepuko?
si dhambi kuwa na sidechick lakini hakikisha anafahamu uwepo wa nyumba kubwa. Kuna wanawake wameumbwa ili wawe sidechick na wanajua hilo. Wala hatakupa tabu.

wewe ni mnywaji?
Achana na bia hizi zitakupa hang over. Gonga k vant, yako moja na ka castle milk kako kamoja kakupooza uende nyumban ukapumzike.
Bia inanenepesha
Spirit inachoma mafuta.
Muhimu ni kunywa kwa kiasi.

Usiache ibada.
Usikubali wiki ipite bila kwenda kuongea na Mungu wako.
Dini ndo imesababisha tuka civilized.
Unapokuwa katika ibada tunakumbushwa namna ya kuwa watu wema.
Usiue
Usizini
Usiibe etc.
Ibada ni uwanja mzuri wa kukumbusha namna ya kuishi vyema na jamii yako.

Wape watoto wako elimu bora.
Wazazi wako walikusomesha st kayumba.
Pambana wanao wasome english medium.
Shule bora inatengeneza future nzuri ya kizazi chako.

Wewe na partner wako,mke wako,mama watoto wako hebu mjitahidi at least kila mwezi muende sehemu mkapate dinner na familia au nyie wawili mpige story 2 au tatu then mrudi home.
Tusiwasahau hawa wake zetu.

Soma vitabu
Usikae tu bila kuupa ubongo chakula.
Vitabu hivi ni recommended
48 laws of power by Robert Greene
Subtle arts of not giving a JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala.
Ego is an enemy.

Vitabu hivi vinaitwa self help book.


Last but most, BE YOU.
usiishi maisha fake. Ishi katika uhalisia wako. Jamii inapenda real people.
Point
 
Umemaliza vibaya kwa kusema "be you"
Wengine hawawezi kuwa "them" at the same time wakaacha uzinzi, uwizi, ulevi, kuwaheshimu watu.. in short some of us are always evil 😈 kuwa good people is living someone's life.. 😁😁

Ni mtazamo.
 
Umemaliza vibaya kwa kusema "be you"
Wengine hawawezi kuwa "them" at the same time wakaacha uzinzi, uwizi, ulevi, kuwaheshimu watu.. in short some of us are always evil 😈 kuwa good people is living someone's life.. 😁😁

Ni mtazamo.
Be you katika ulevi ndo unywe kwa kiasi.
Ukipretend ndo unapitiliza sasa.🤣
 
1. Usimpigie mtu simu zaidi ya mara mbili mfululizo. Ikiwa hapokea simu yako, chukulia kuwa ana jambo muhimu yuko analifanya.

2. Rudisha pesa ulizokopa hata kabla mtu aliyekukopa hajakukumbusha au kukuomba. Kufanya hivi kunaonyesha ni jinsi gani ulivyo mwaminifu, na kutakufanya uaminike zaidi.

3. Usiagize chakula kingi usichoweza kukimaliza unapokuwa mgahawani au hotel. Agiza chakula kinachokutosha na utakachokimaliza, hii itakufanya uonekane ni jinsi gani unavyothamini chakula na kuheshimu juhudi za wakulima.

4. Usimuulize mtu maswali ya aibu mbele ya watu kama ‘Oh kwa hiyo bado hujaolewa?’ .au ‘Je, huna watoto’ au ‘Kwa nini hujanunua nyumba?’ Au kwa nini hununui gari?. Hilo sio jukumu lako, ni jukumu lake mhusika pamoja na MUNGU wake.

5. Ikiwa unapawe ofa na rafiki yako katika kulipia mambo tofauti tofauti wakati wa matembezi, Jitahidi na wewe umlipie wakati ujao, ili asikuchoke au kukudharau maana binadamu hawana dogo.

6. Heshimu maoni au mawazo ya mtu kwa kumsikiliza wakati anapoongea. Kumbuka kile ambacho ni 6 kwako kitaonekana 9 kwa mtu mwingine, usidharau maoni au mawazo ya mtu hata kama unajua kaongea pumba.

7. Usimkatishe mtu katika kipindi ambacho anazungumza, sikiliza kwanza akimaliza kuongea na wewe ongea, hii itasaidia kuepuka ugomvi au mabishano wakati wa mazungumzo yenu.

8. Usimseme mtu vibaya au kuongea mabaya yake mbele ya watu wengine, ikiwa una mabaya yake mtafute na zungumza nae kwa upendo ili ayatambue madhaifu yake na ajisahihishe. kumbuka hakuna binadamu mkamilifu.

9..Usisahau kusema asante katika kipindi ambacho unapokea kitu chochote kutoka kwa mtu au kusaidiwa jambo fulani. Hii itaonyesha ni jinsi gani unavyothamini.

10. Jifunze kumsifia mtu hadharani.na mkosoe mtu faraghani, hii itaonyshesha ni jinsi gani ulivyo muungwana. Usimkosoe mtu hadharani.

11.Mtu anapokuonyesha picha kwenye simu yake, usitelezeshe kidole chako kushoto au kulia. Huwezi kujua nini kinafuata, Jenga tabia ya kufanya kile ulichoelekezwa kufanya, tena kifanye kwa uaminifu.

12. Mwenzako akikuambia anajisikia vibaya kuwa mwelewa, usitake kujua sababu za kwanini anajisikia vibaya ikiwa hajakuambia.

13. Mtende na kumfanyia mfanyakazi wako wa ndani mambo unayowafanyia watoto wako, ikiwa ni upendo muonyeshe upendo kwa kumtimizia mahitaji yake yote. Kumbuka wewe umezaa tuu, ila yeye anakulelea watoto wako.

14. Ikiwa mtu anazungumza moja kwa moja na wewe, huku ukitazama siku yako au unacharti ni kukosa adabu. Jifunze kuweka umakini wako katika jambo moja.

15. Usitoe ushauri kamwe hadi uombwe; ili usije onekana umejipendekeza kwa kutoa ushauri usiohitajika.

16. Ondoa miwani yako ya jua ikiwa unazungumza na mtu yeyote barabarani. Ni ishara ya heshima.

17. Usizungumze kamwe kuhusu utajiri wako katikati ya watu maskini. Vivyo hivyo, usizungumze juu ya watoto wako katikati ya mtu tasa. Usizungumze kuhusu wazazi wako katika ya mayatima.
Natumia umenielewa.

18.Baada ya kusoma ujumbe mzuri kama huu jifunze kusema "Asante kwa ujumbe". hii itaonyesha ni jinsi gani unavyohitaji na kuyathamini maarifa

MWISHO.....
 
Back
Top Bottom