Fahamu hatari kubwa zinazozikabili nchi zinazotumia mifuko ya plastiki

Fahamu hatari kubwa zinazozikabili nchi zinazotumia mifuko ya plastiki

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
38,920
Reaction score
44,970
Matumizi ya mifuko ya plastiki inaweza kusababisha madhara yafuatayo;

1.) Kansa za aina mbali mbali
- Uchomaji wa mifuko ya plastiki majumbani, mabarabarani, mahospitalini pamoja na kwenye madampo husababisha kemikali za sumu aina ya carcinogens kusambaa hovyo kwenye hewa unayovuta. Mfano wa kemikali hizo ni 'Dioxins' na 'Furans' ambazo tafiti zimeonyesha kuwa na uhusiano mkubwa sana na magonjwa ya cancer na hata matatizo ya mifumo ya upumuaji kwa binadamu. Tupime kodi tunayokusanya kwenye mifuko hii vs hasara na mateso tunayopata kutibu watu kule hospital ya cancer ya ocean road, mamlaka zinazohusika zichukue hatua sasa.

2.) Matatizo ya homoni za jinsia (Ushoga na usagaji)
- Kemikali ya 'Dioxin' ambayo hupatikana kwenye moshi wa taka za plastiki zilizochomwa, endapo itavutwa kwa njia ya hewa na mtoto mchanga, utafiti umeonyesha kwamba inaweza ikasababisha mfarakano katika mfumo wa homoni za jinsia kwa mtoto huyo. Mtoto wa kiume anaweza akaja kuanza kuonyesha tabia za mtoto wa kike, na mtoto wa kike anaweza akaanza kuonyesha tabia za mtoto wa kiume hapo baadae, hivyo kupelekea kuongezeka kwa mashoga na wasagaji katika jamii. Waziri anaehusika apime haya na afanye maamuzi sahihi.

3.) Matatizo ya mfumo wa uzazi kwa wanaume wasio mashoga (Uhanithi na 'low sperm count')
-Utafiti umeonyesha pia, katika maeneo ambayo wanaume wake wamekuwa 'exposed' na kemikali za 'Dioxins' na 'Furans' kwa muda mrefu, pamekuwa na ongezeko la kushindwa kusimamisha viungo vya uzazi (usenge) pamoja na kuongezeka kwa matatizo ya wanaume kushindwa kurutubisha mayai (Low sperm count/weak sperm cells). Hili linahitaji kitabu kizima kuanza kufafanua, nashauri kila mtu akafanye research zaidi kwenye makala za kitabibu ili kupata undani wake. Pia katika maeneo hayo, imeonekana kwamba wasichana wanavunja ungo mapema mno. Hii hali naiona sana Tanzania, waziri unaehusika, waokoe wananchi wako.

4.) Athari za kiafya kwa wanyama, ndege na samaki

- Wanyama kama n'gombe hufananisha mifuko ya plastiki na chakula, hivyo huweza kuimeza na kusababisha kuziba kwa utumbo na hatimae kifo.

5.) Mifuko ya plastiki huweza kukaa hadi miaka 500 bila kuoza.
- Mifuko hii huwa haiozi bali huvunjika vunjika na kuwa vipande vidogo vidogo sana ambavyo huweza kujichanganya katika mifumo yetu ya maji na chakula na kusababisha watu kula na kunywa plastiki kwa kiwango kikubwa sana bila kujijua. Vipande hivyo vya pastiki ni sumu inayoua taratibu.

6.) Mifuko ya plastiki hupeperuka kirahisi na kuchafua mandhari

- Kutokana na kuwa miepesi sana, mifuko hii hupeperuka kirahisi kutoka kwenye vyombo vya kubebea taka na kwenye madampo, hivyo kusambaa hovyo kwenye makazi ya watu na kuharibu mandhari, pia huziba njia za maji na kusababisha mafuriko, pia mifuko hii hutumika kama mazalio ya vilui lui vya mbu waenezao malaria.
======================================

UPDATE:
Kamati ya Bunge ya viwanda na biashara yaagiza Serikali kupiga marufuku mifuko ya plastiki kutoka nje ya nchi
================================

UPDATE: 09/04/2019
Hatimae serikali kupitia waziri mkuu wamepiga marufuku, uzalishaji, uagizaji na matumizi ya mifuko ya plastiki nchi nzima, Tanzania inaelekea kuwa kama Rwanda sasa kwa usafi.


=====================================

Update: 24/05/2019

===============================

Update: 08/04/2021

================================
Nashukuru mpaka sasa tumefanikiwa kupata like 42 katika kampeni hii
 
1: Vifo kwa wingi wa viumbe wa baharini sea species pamoja na wanyama wanapoitumia mifuko ya plastic kama chakula.

2: Land pollution
Inapotupwa mifuko ya plastic kwa sababu haiozi, uoto wa asili hufa na huwezi kupanda chochote kikamea.

4: Kuziba kwa mifereji na madaraja na kusababisha mafuliko wakati wa mnvua. Ndiyo moja ya sababu kubwa ya kuziba kwa daraja la jangwani na maji ku overflow. Lakini sababu hii pamoja na kuwa basic, haizungumzwi na watendaji kwa ajili ya personal interest.

5: Uchafuzi wa mazingira yetu, makes our cities too dirty.

6: Economic threat:
Kuwauwa wanyama wanaofugwa na sea spices huharibu uchumi wa Watanzania
 
Hiyo namba 2 wakiisikia hao jamaa (mashoga) itakuwa ndio kisingizio chao na watachoma hiyo mifuko kupita maelezo ili watuambukize.

Hapo kwenye namba 3 kumefanya nitangaze vita rasmi na mifuko ya plastiki....shubaaaaamitt!
Sina hakika kama waziri wa mazingira anafahamu madhara haya kwa wananchi wake, vinginevyo angeshapiga marufuku walau uagizaji wa mifuko hiyo toka Kenya na nchi zingine ambazo kwao wamepiga marufuku ila wanatugeuza sisi ndio dampo la kutupa sumu zao
 
1: Vifo kwa wingi wa viumbe wa baharini sea species pamoja na wanyama wanapoitumia mifuko ya plastic kama chakula.

2: Land pollution
Inapotupwa mifuko ya plastic kwa sababu haiozi, uoto wa asili hufa na huwezi kupanda chochote kikamea.

4: Kuziba kwa mifereji na madaraja na kusababisha mafuliko wakati wa mnvua. Ndiyo moja ya sababu kubwa ya kuziba kwa daraja la jangwani na maji ku overflow. Lakini sababu hii pamoja na kuwa basic, haizungumzwi na watendaji kwa ajili ya personal interest.

5: Uchafuzi wa mazingira yetu, makes our cities too dirty.

6: Economic threat:
Kuwauwa wanyama wanaofugwa na sea spices huharibu uchumi wa Watanzania
Exactly, japo umetaja kwa namna nyingine, lakini ndicho hasa namaanisha.
 
Watendaji wetu kumbukumbu pekee kwa wananchi ni wakati uchaguzi unapokaribia. Na kwa vile hata wapige kura watu 10 mshindi atapatikana, huwafikiria kwa kiwango kidogo sana.
 
Na hata kama mtajifanya nimeandika kichina au maandishi hayaonekani ujumbe ndio huo, umefika tu
 
Inasikitisha kuona mada ya msingi na sensitive kama hii kukosa wachangiaji! Ila ingekuwa ni mada ya ngono, makalio, nguvu za kiume etc ingekuwa na page 30+ by now. So sad.
Sijui ni kwanini watu hawataki kusaidiana kushinikiza hili, bila shinikizo Makamba hatajali, atendelea kutuua kama ambavyo amekuwa akifanya muda wote huu
 
Pia hii mifuko pamoja na taka za plastic zinapoingia kwenye udongo na kushikamana nao huwa zinablock mfumo wa maji chini ya ardhi na kuharibu mifumo ya waterbed. Hii imepelekea hata mvua zinaponyesha kuna baadhi ya maeneo maji hayapenyi vizuri ardhini sababu ya kuwepo kwa kikwazo cha hii mifuko kwenye udongo
 
Yaaa ni kweli hata hapa Scandinavia,ulikua ukienda dukani kununua kitu chochote mfuko ulikua unaupata bure ila sasa maduka yote wameanza kuuza mifuko,ili watu washidwe kununua pia ndio mwanzo wa kuipiga marufuka na mwisho wa kuitumia ni mwaka huu itakua haipo kabisa,wanasema ni kwa ajiri ya mazingira.
 
Yaaa ni kweli hata hapa Scandinavia,ulikua ukienda dukani kununua kitu chochote mfuko ulikua unaupata bure ila sasa maduka yote wameanza kuuza mifuko,ili watu washidwe kununua pia ndio mwanzo wa kuipiga marufuka na mwisho wa kuitumia ni mwaka huu itakua haipo kabisa,wanasema ni kwa ajiri ya mazingira.
huku kwetu sijui mwisho liini
 
Katika hili bado viongozi wetu ni vipofu, wanazingatia tu at kuboresha huduma za afya pasipo kuangalia na kulinda afya za watu wao... Nani wa kuwapelekea viongozi wetu mawazo haya??... Nawasilisha.
 
Katika hili bado viongozi wetu ni vipofu, wanazingatia tu at kuboresha huduma za afya pasipo kuangalia na kulinda afya za watu wao... Nani wa kuwapelekea viongozi wetu mawazo haya??... Nawasilisha.
Ni vyema kupeana taarifa na mawazo mbadala
 
Ni vyema kupeana taarifa na mawazo mbadala
Hapa tuanze ss kwa kuwapa elimu watu juu ya athali za mifuko hii ya plastic hususani wale walio na elimu duni na ikiwezekana kuunda vikundi maalumu kupambana na tatizo hili Antiplastic combatants....... Hili group likiwa steady strong itakuwa rahisi kuungwa mkono na viongozi na watu wengne.. Tupeane mikakati namna ya kunusulu vijana hususani waishio mijini, vyuoni pamoja na uharibifu wa mazingira kwa ujumla. Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom