Mwamundela
Member
- Aug 28, 2013
- 49
- 71
๐๐๐๐๐
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Karibu sanaKigoma mwisho wa reli๐.
Haya mambo yanatishaUvaaji wa mavazi maalumu ni kaniki za kuwangia, nyeupe, nyeusi na nyekundu hayo ndio mavazi maalum: Kuwanga ni unatakiwa kuwa uchi wa mnyama, wanaovalia kaniki ni wale wageni ambao bado hawajazoea na ndio wengi hukamatwa.
1-WanaKigoma kuzungumzia swala la uchawi (hatujidai nalo, na wala hatulipendi kulinganishwa nalo ispokuwa ni ile hali ya kua karibu nalo kimipaka, kwasababu nchi 4 zinazo ongoza kwa nguvu za giza Afrika ni pamoja na Sudan kusini, Jamhuri ya Afrika ya Kati, na Kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.1.Mkoa wa Kigoma unasifika kwa uchawi sana Tanzania kuliko mikoa mingine je kuna ukweli gani juu ya hili? Na kwa nini Kigoma kuwe na wachawi wengi kuliko mikoa mingine?
2.Wazungu ni wachawi? Uchawi upi una nguvu kati ya uchawi wa kizungu na uchawi wa kiafrika? Uchawi wa kizungu unatumia tunguli na (makorokoro mengine) kama Afrika?
Zero benefit zaidi ya umaskini na ujinga tu
Soma makala hiyo ukipata nafasi na muda
Hivi ndugu zangu mnaamini kuna uchawi? Mmeingia darasani, mnama degree yakutosha, hivi inawezkana binadamu akasafiri angani kwa kutumia hivyo vyombo vya kichawi, ukifikiria kwa undani utapata jibu kuwa ni uongo, hakuna connection.WAKATI baadhi ya watu wakiepuka kabisa mijadala kuhusu uchawi na kutilia shaka kuwepo kwake kwa sababu ya jamii zetu kupokea imani ya Kikristo, na imani ya Kiislamu, wengine tunaendelea kutafiti mambo hayo kinaga ubaga.
Huu ni Utafiti endelevu, lengo kuu ni kukujuza tu tasnia hii ya wachawi ilivyo, tunakujuza haya kutokana na matukio ya 'Kichawi yanavyo athiri maisha ya watu.
Moja ya rejea tunayotumia ni center ndogo ya kumbukumbu ya uchawi iliyopo 'Moto Moto Museum'
Miongoni mwa vielelezo vinavyopatikana huko ni kwamba uchawi ni elimu ya ushetani. Ukishakua mchawi maana yake wewe ni shetani na utatumia nguvu za shetani ambazo kamwe haziwezi kusimama katika ulimwengu wa nuru.
Vitu baadhi vinavyohitajika ili mchawi aweze kusafiri, leo tutazungumzia vitu viwili tu lakini vipo vingi sana.
1- 'Chishimba' (ni mafuta ya binadamu) mafuta haya anapaka usoni kila atakapo hitaji kuruka, akishapaka mafuta haya mchawi kamwe hawezi kuonekana wala hawezi kusikika wala hawezi kugusika.
2- Indeke (ndege ya kuruka) inayotumika kwa usafiri wa masafa marefu unaochochewa na damu ya binaadamu na majimaji ya sehemu za siri za mwanaadamu kama vile mbegu za kiume na maji ya ukeni (Huchanganywa kwa pamoja).
UCHAMBUZI WA MAFUTA YA BINAADAMU
Kwanini mchawi apake mafuta ya Binaadamu?
Kikawaida wao wanavyoeleza ni kwamba Mwanaadamu anamafuta aina mbili, moja ni mafuta mazito yanayopatika kwenye mishipa ya damu (Cholesterol) ni dutu ya nta inayopatikana katika damu ya mtu.
Mwili unahitaji Cholesterol ili kujenga seli zenye afya, lakini viwango vya juu vya kolesteroli vinaweza kuongeza hatari yako ya ugonjwa wa moyo. Katika uchawi inaaminika kwamba jini anayekuvaa mwilini ili akusafirishe katika giza, ataingia mwilini mwako pindi tu ukipaka hayo mafuta ya binaadamua ya 'Cholesterol' jini huyu atakusafirisha kwa kasi sana na atakufikisha popote unapotaka kwenda.
Mafuta mengine ni yale ambayo yapo nje ya mishipa ya damu ya mwanaadamu (Body Fatty) ambayo ni Mafuta ya mwili katika misuli ya mwanadamu, hivyo mchawi akipaka mafuta haya huingiwa na jini mwenye nguvu ambaye humsaidia kupata nguvu ya yeye kushiriki matendo yake ya kichawi. Cholesterol ni ya kusafiri, Body fatty ni ya kumpa mchawi nguvu. (Hayo ni masharti ya majini hao wawili).
Upatikanaji wa mafuta hayo?
Hayapatikani zaidi ya kuua mtu kisha kumbanika kwa kumchoma na kisha mafuta haya aina mbili huchujwa, na kugawanywa kila aina ya mafuta kwenye chupa lake.
Je! kama umeingia kwenye uchawi ni lazima uuwe ili upate hayo mafuta?
Hapana, sio lazima uuwe kwani yanapatika kwa kuuzwa kwenye vilinge vya wachawi ambapo gharama yake hufikia Tsh Milioni 8 hadi 10 kwa lita, ambayo yanaweza kudumu kwa miaka mingi kwa kadiri unavyotumia.
Pia sio binaadamu wote mafuta yao yanafaa kutumika, ni baadhi ya binaadamu ambao miili yao inasifa ambazo wao wanazijua. Mara nyingi wachawi wanaonekana ni masikini kwasababu pesa zao nyingi zinaishia huko.
Je! kama mchawi hana kiasi hicho cha pesa kwa ajili ya mafuta anafanyaje?
Ni rahisi sana, kwani anaweza kubebwa na wenzake wakaenda nae kuwanga pamoja. Huyu sasa atakua anapewa lifti na wenzake kwa kulipia gharama kidogo walau laki 1 hadi laki na nusu kwa safari.
Je! mafuta yakiniishia naweza kuuwa mtu nikambanika kama sitaki kununua?
Ndio, unaweza kuua mtu na ukamfanyia utaratibu huo kama unayo taaluma hiyo, hii ni kwasababu kuna kozi maalumu ya utengenezaji wa mafuta hayo, ambapo baadhi ya wachawi husomea namna ya kuchakata mafuta hayo, kama mchawi anaweza basi atafanya mwenyewe kwa kupata kibali maalumu kwa mkubwa wao, na kama hana taaluma hiyo basi atakwenda kununua kwenye kilinge cha mafuta.
UCHAMBUZI WA DAMU NA MAJIMAJI YA SEHEMU ZA SIRI
Kwanini sasa ndeke hiyo itumie damu ilihali tayari nimepaka mafuta ya binadamu na jini wa safari ameshanivaa?
Kwasababu ndeke ni chombo ambacho wewe utatumia kuwa juu yake baada ya jini kukuingi, jini anataka kukaa juu ya kitu ambacho kina uhai wa mwanaadamu ambayo ni damu, mbegu za uzazi na maji ya ukeni. Mchanganyiko huo ndio kama mafuta ya kafara ili jini aliyekuvaa aweze kukaa juu yake.
Napata wapi damu ya binaadamu?
Kwa kuua mtu ndio utaweza kupata damu ya binaadamu. Kwa namna gani? mchakato wake ni vilevile wakati wa kumbanika, basi damu hukusanywa kivyake.
Damu gani haswa inayohitajika?
Damu ya mtu yeyote inaweza kufanya kazi, lakini damu yenye kasi zaidi na inayopendwa zaidi na yenye gharama kubwa zaidi ni damu ya mtoto mchanga, ambayo huchanganywa na nyama ya kitovu cha mtoto mchanga pamoja na kondo la nyuma la uzazi baada ya kuzaliwa mtoto mchanga. Vinaweza kutoka kwa watoto tofauti au mtoto mmoja.
Damu hiyo ndio grade one, na yenye gharama kubwa sana haswa ikichanganywa na nywele za kwanza za mtoto mchanga alizo nyolewa na kucha zake za kwanza kukatwa.
Gharama ya damu iko vipi ikiwa nitahitaji kununua?
Kwakua damu inayohitajika huwa tayari imechanganywa na mbegu za uzazi na maji ya ukeni, gharama yake hufikia Tsh Milioni 3 - 4. Ikiwa ni damu ya mtoto mchanga ndio imetumika basi hufikia Tsh milioni 8-10 kwa lita1. Ambayo utaitumia kwa miaka mingi sana kulingana na matumizi yako.
Na vipi hayo majimaji ya uzazi na mbegu za kiume?
Majimaji hayo au mbegu hizo zinapatikana kwa wachawi kujamiina ya watu wakati wa usingizi. Nguvu hii ya wao kushiriki tendo na watu huipata kwa kutumia 'Mkanda wa ngozi wa chatu' ambao huvaliwa kiunoni na mchawi ambaye ana nia ya kufanya uzinzi na mke wa mtu mwingine au mume wa mtu wakati wanandoa wako kitandani. Mume au mke hupakwa mimea ili apate usingizi mzito huku mzinzi akilala kwa uhuru na mwenza wake. 'Ambapo kwa lugha ya sasa huitwa jini mahaba'
Hivyo ndivyo majimaji na mbegu huchukuliwa na kuchanganywa na damu ya binaadamu, na mafuta ya binaadamu hupakwa mwilini tayari kwa safari ya kuelekea popote.
Ufafanuzi wa picha;
picha na 1. hapa chini ni Helikopta nyeusi kwa chini kuna kopo leusi lenye mafuta ya mchanganyiko wa damu na majimaji ya uzazi.
View attachment 2787428
Picha na 2. helikopa nyingine utaona kabisa chupa lake la mafuta ya damu na majimaji ya uzazi liko pembeni.
View attachment 2787436
Sasa mchawi atakaa hapo juu baada ya jini wa safari kumvaa, kwa wale wanaotumia ungo zana hizo wanaziweka juu ya ungo.
Picha na 3. Hi ya duara ndio 'Mkanda wa ngozi wa chatu' hutumika kushiriki tendo la ndoa na watu wakiwa usingizini,
View attachment 2787441
Picha no 4, na hizo tube mbili ndio mafuta ya kupaka 'Body Fatty' na 'Cholesterol' huitwa 'Chishimba' kwa Pembeni ni nywele za mtoto.
View attachment 2787445
Utafiti unaendelea!
Sikuelewa kitu. 1 -0. Baadae ntarudi kusoma tena na tena, labda yataniingia.Mchawi ana dhuru na kuleta maafa kwa mtu, Mwanga hadhuru yeye hujifurahisha tu kuwachezea watu basi lakini hadhuru. Mtu anayeaminika kuwa na uwezo wa kuwaletea watu maafa kwa kutumia ushirikina huyo ndio mchwi. , Mwanga yeye anawangia watu, kuwanga ni kusambira (kuwanga kwa kuzunguka moto), ni michezo ya kichawi kwa kujifurahisha tu. Sio kila Mwanga ni Mchawi, lakini kila mchawi lazima awe mwanga.
Dini ipi?Kwann wanaojihusisha na haya mambo ya uchawi ni wa dini ileeeeee
Kwanini sijaiona?Afadhali FaizaFoxy hajaiiona hii comment ๐คฆ
WALE MASHEIKH WANGANGA WA KIENYEJI WAPIGA RAMLI CYO WACHAWIKwanini sijaiona?
Uchawi wenyewe nchi za nje nilizowahi kuishi wanauchukulia kuwa ni "dini na imani" pia.
Kiislam uchawi wa aina yeyote ile ni ushirikina, na kila mshirikina hana msamaha. Makao yake ni motoni tu na maulamaa wengi wanaamini mchawi anaanza kuuona moto kabla hajafa.
Mchawi Kiislam ni mfanya kufuru, kukufuru maana yake ni kuupinga Uislam (kujitoa katika Uislam). Ukimuona mtu anafanya uchawi au wanga anasema yeye ni Muislam huyo anacheza na akili za wajinga tu, siyo Muislam huyo.
Nadhani wewe ni miongoni mwa wachawi maana mchawi hata siku moja hapendi na hataki kujulikana kabisa maana uchawi ni uovu kama ulivyo uovu mwingine kwenye jamii. Hata jina lako tu hapa JF (Kikinga) limekaa/linathibitisha pasi na shaka kwamba yu mkini u-mchawi.Hivi ndugu zangu mnaamini kuna uchawi? Mmeingia darasani, mnama degree yakutosha, hivi inawezkana binadamu akasafiri angani kwa kutumia hivyo vyombo vya kichawi, ukifikiria kwa undani utapata jibu kuwa ni uongo, hakuna connection.
Wengi wetu tunasikia tu kuwa kuna uchawi lakini hatujawahi shuhudia live.
I stand to be corrected.
IleeeeeeeeDini ipi?