Fahamu kuhusu Biashara ya bisi (popcorn)

Salamu kwenu wakuu, jana kwenye matembezi tembezi yangu hapa jijini arusha mida ya jioni mimi na ndungu yangu mmoja tulipita maeneo ya (eneo siwezi kulitaja ili kulinda biashara ya watu) tulikutana na mjasiliamali mmoja ana miaka kama 22-26 kwa kumuangalia. Pasi na shaka tukaona bora tukaribie eneo ilo. Eneo lenyewe lipo karibia na barabara (pembeni ya barabara upande wa kushoto) eneo analouzia popcorn kuna mashine ya popcorn na benchi la kukaa. Nikiwa nimekaa kwenye benchi nakula popcorn zangu nikaanza kumuuliza maswali madogo madogo tu.
Sw 1. Upo smart, una degree nn kaka?
Jb. (Akacheka) ninayo nimesoma accounting
Sw 2. Mbona umeacha uhasibu?
Jb. Sijaacha ila niliona ajira saivi ni ngumu bora nikiwa natafuta niendelee kujihusisha kwenye biashara ndogo ndogo
sw 3. Hahaa ok, mbona popcorn?, si ungefanya biashara nyingine labda kuuza mashati
jb. (Akacheka)mwaka jana nilivyo maliza chuo nilikua na kama 340000 cash mm nae nilikuta na muuza popcorn nikaipenda hii biashara
sw 4. Aise sasa biashara ulianzaje mkuu?
Jb. Nilipata hii mashine used kwa 270000 ilo benchi nilichukua nyumbani na ela iliyo baki nikanunua vifungashio, mahindi na mahitaji mengine. Siku ya kwanza niliuza popcorn za sukari mifuko 7 na za chumvi 12
MIMI: na saivi biashara inaendaje mzee bb?
jb. Yani hapa kwa siku naweza kuuza popcorn za chumvi mifuko 45 na sukari 20 minmum, maxmum popcorn za chumvi kama 55-60 na sukari 30-40
NOTE:
Popcorn za sukari mfuko mmoja 1000 na popcorn za chumvi 500
ukichukua minmum yake ya 45 X 500=22500 X 30= 675000,, 20 X 1000= 20000 X 30 =600000
TOTAL:1275000
(tuliongea mengi lakini ya muhimu ni hayo hata na ivyo popcorn zangu zilikua zimeisha)
 
Tatizo watu wengi wanaogopa "uthubutu" na hasa wasomi. Ziko biashara zinaonekana kama za mchezo mchezo vile lakini, zina faida ni balaaa.,.....
 
UMETOA GHARAMA ZA UENDESHAJI AU UMEFANYA CALCULATION ZA KIBUSH?
kiongozi izi ndio hesabu zinazopigwa mitandaoni na kwenye magroup ya whatapps zinaweka matarajio makubwa yasiyo na uhalisia ndio wanachofanya wahamasishaji wetu. tukipiga minimum cost ya 40% ya mauzo faida inakuwa 765,000/= na maximum cost ya 60% ya mauzo faida inakuwa 510,000/= bado yupo vizuri.
 
Hizo hesabu hazina uhalisia
Ukitaka kafanye weer
 
hizi popcorn zinaliwa sana kiivyo nlijua ni watoto tu ndio wanakula maana nikila hata si shibi naamua kuacha maana unachoka kutafuna
 
Bora yeye amethubutu maana wasomi wengi hujivunia vyet vyao huku mfukon nothing
 
Mm nilishangaa mtu ananiambia amenunua kiwanja ana jenga kwa kuuza maji tu niliona biashara ya kijinga kumbe
 


HABARI,
Nkweli kabisa hao wamejaa wengi sana mapaka waendesha bodaboda wako wengi sana wamemaliza vyuo.Ila pale wote mlichemka samahani lakini sina maana mbaya ulipo muuliza mbona aliacha uhasibu naye alipo kujibu haajaacha il ajira ngi ngumu hiyo inaonyesha bado mawazo ya watu wengi wakimaliza shule ni kuajiriwa wakati pale ndio sahihi anatumia shule yake vizuri kama alivyo someshwa.Tena hata kama alisoma kwa mkopa anaweza akawa analipa hata laki moja kila mwezi ili na wengine wakakopeshe najua sio wote wanaopata mikopo ila haao hao watakao bahatika.
Pia namshauri na ninatarajia hilo kwa kutimia elimu yake kwa sasa anaweza kusajili kampuni kabisa akakopesheka akafungua ofisi kubwa ya kutengeneza hipo na akawa anasambaza kwenye maduka madogo kwa bei ya chini hilo atafanikiwa sana nakupongeza sana mjasiliamali.Ajira tayali unayo fikiria kuajiri sasa.

LUMUMBA
 
Hiv kuna uhusiano wowote kati ya kuangalia movie na kula popcorn??
Mnamo mwaka 1885 mashine ya kwanza ya kutengeneza popcorn ilianzishwa.

Na wakaanza kuuzia sehemu za starehe kwa hiyo watu wakawa wanalia kwenye majumba ya cinema.

Ni rahisi kuitengeneza popcorn na harufu pia ni nzuri kwa hiyo haimbughudhi mtu.

Yaani uingie na dagaa kwenye jumba la cinema tutakimbia (just kidding)
 
Bado mauzo si constant...
Huwa nacheka sana na hizo hesabu za sijui sh ngal mara siku 30 mara 365...

Mi mwenyewe ninayo hiyo mashine dukani, hesabu sio nyepesi hivyo!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…