Fahamu kuhusu kilimo bora cha Hiliki

Wewe ni mtu Wa tatu kuona unatafuta hiriki.
Na picha inayoambatanishwa ni hiihii.
Tuelezeeni kuhusu hiyo fursa isije mkapigwa kimyakimya mkaja kulialia humu
 
mrangi, Mkuu nijuavyo, Kuna hiliki ambazo hata zikikauka zinabaki na ule u kijani wake na mara nyingi ndo zinazohitajika katika soko la dunia, Nina jamaa yangu ndo biashara yake so Sina ufahamu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mrangi,
Waangalie tu isije ikawa ni ule utapeli wa ''kununua'' na ''kuuza''. Unakuwaje? (najua watu wengi wameshausikia) Unakuwa hivi: Mtu unakuwa na mzigo wako ambao uliununua kwa bei kubwa baada ya kuingizwa mkenge kuwa una soko na faida kubwa. Mfano unaweza kuwa na tani moja ya hiliki ambayo umeshindwa kuuza kwa bei unayotaka. Unachofanya ni kwanza kutengeneza mazingira ya kuwa zinahitajika hiliki nyingi kwa bei kubwa eg kilo moja sh 30,000 na zinahitajika nyingi sana.

Hili unafanya kwa kumtumia rafiki yako. Baada ya hapo analengeshwa ''fala'' mmoja anaambiwa fulani ana hiliki jaribu kwenda kuulizia. Anakuja anazikuta kweli na anaweza kuchukuwa kidogo kwenda kujaribu zari na unazinunua kweli. Hapo anakolea anakwenda kuchukuwa mzigo wote kwa bei kubwa na matapeli wanapotea na kumwacha na hiliki zake. Kama ni mjanja na yeye inabidi atafute wajinga wake.
 
mrangi,
Sasa SI inakua hasara, Kama mbichi Bei hiyo kwa kilo na ikikauka inabaki gram 10,hii inaitwa monkey business
 
Kuna mwenzako mwingine nae atafuta,chekianeni mpeane ramani.


dodge
 
nae
atafuta
chekianeni
mpeane

[emoji121]haya maneno ni kiswahili au??

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…