Fahamu kuhusu matumizi ya OverDrive (OD) kwenye gari automatic

Mkuu iache on mda wote usichanganywe na habari za mjini na high way! Sababu ni kwamba ikiwa on haizuii gari kuwa katika low gear vile vile ukiwa high way itaruhusu gari kuwa katika high gear mfano 4/5. Ukiizima uwe na kumbukumbu ya kuiwasha
 
Jamani gari yangu haina hzo button za over drive ni toyota wish ila ikifika speed 90 na kuendelea huwa engine inabadili sauti na mvumo na inaanza kukimbia sana je mfumo wake ni tofauti?
Sio gari zote zina hiyo button, kama yako haina weka D tembea
 
Imenibidi kujiridhisha. Leo nilipoanza safari, hapa Dar,niliacha dash Board ikiwa haina kile kitaa,nikawa engage kile kitaa,kiukweli RPM inakua juu sana ile taa ikiwa kwenye Dash Board.

Hii tayari ikanipa indicator kuwa hapa wese litakua linaliwa kama jini,nikarudisha kwenye hali ya kawaida ya Dashboard kuwa clean,na kweli RPM ikashuka hadi 2 kutoka ike 3.

Hivyo, bila kuathiri maelezo na ufafanuzi wa wadau, sitathubutu kuruhusu taa pale isome OD/ OFF,maana hali hiyo huongeza RPM na milio ya ajabu na hivyo wese kuliwa kama maji.
 
Hahahaha umegundua kuwa kule kuvuma kwa gari ndiyo kulikuchanganya ukahisi gari iko speedy?
 
Hahahaha umegundua kuwa kule kuvuma kwa gari ndiyo kulikuchanganya ukahisi gari iko speedy?
Nilichojifunza,OD/OFF taa ikiwaka ni ON,na isipoonekana, hapo iko OFF. Na ukijichanganya ukaacha OD/OFF utajuta kwa mafuta yatakayoliwa. Ila ni nzuri kama unataka ku overtake kwa ghafla,inakua na nguvu ajabu.
 
Taa ya "ODD/OFF" inapowaka Overdrive inakuwa On au Off?
 
Taa ya "ODD/OFF" inapowaka Overdrive inakuwa On au Off?
Post Namba 526,nimejibu hilo,tena nilifanya jaribio na kikubwa nilikua naangalia mabadiliko katika RPM,kwa hakika,OD/OFF taa ikiwaka,inakua na muungurumo mkubwa na RPM inapanda kutoka normal 2 au 2.2 had 3-3.5, hicho ni kiashiria cha ulaji wa mafuta mengi,wala hutakiwi kwenda Chuo Kikuu kujua hilo.
 
So tutembee taa ikiwa inawaka? I mean taa ya ODD/OFF.
 
So tutembee taa ikiwa inawaka? I mean taa ya ODD/OFF.
Hapana, tembelea TAA IKIWA IMEZIMA,DASHBOARD ikiwa plain. Kadri ilivyo,taa yoyote kwenye Dashboard ni kuwa kuna matatizo(malfunctions) au kuna kitu Dereva umekiweka kwa sababu maalum.

Kwa mfano, hiyo ikiwa inawaka,na kuna mtu unataka kumpita,iweke kwa haraka halafu kanyaga mafuta kwa kasi uone gari linavyopaa, ndani ya sekunde 10 tu utaweza kum overtake na kuweza kukaa sehem salama kuepuka kugongana uso kwa uso na gari la mbele yako maana kuna madereva huko barabarani(highway) wana roho za ajabu sana
 
Simple formular
KilaTaa kwenye Dashboardya gari yako ni warnibgso hakikisha taa zimezima.exceptzileza gia tu yaani D n.k
 
Anacho kisema mdau ni kwamba tumia OD gear ukiwa na speed kuanzia 80
 
Mi juzi sijui nimefanyaje nikaona O/D OFF imewaka.. kidogo nipeleke kwa fundi eti gari mbovu bahati nzuri mtu mmoja akanielekeza ndio nikajua..
Mara nyingi magari haya ya Kijapani au penginepo tunaagiza yaliokwisha kutumika hivyo kupata complete set ya manuals au booklets ni vigumu. Vipo vi gadget vingine watu hawajajua matumizi yake. Better uwasiliane na manufacturrer.
 
Ukijichanganya ukaweka OD on wakati unatembea speed zaid ya 60km/hr maana yake unatumia gia no 1 na 2. Lazima wese lilike kwa sana. OD ni kama upo miji ya jams sana. Ila kama unatembea zaid ya km 60 toa od
 
Ukijichanganya ukaweka OD on wakati unatembea speed zaid ya 60km/hr maana yake unatumia gia no 1 na 2. Lazima wese lilike kwa sana. OD ni kama upo miji ya jams sana. Ila kama unatembea zaid ya km 60 toa od
mm sijaelewa maana ya Overdrive gear ni namba ngapi?
basi huko nyuma katika Mada nyingine tumedanganyana
 
Nadhani umeongea kinyume.. ukiwa below 60 toa OD.
Ukijichanganya ukaweka OD on wakati unatembea speed zaid ya 60km/hr maana yake unatumia gia no 1 na 2. Lazima wese lilike kwa sana. OD ni kama upo miji ya jams sana. Ila kama unatembea zaid ya km 60 toa od
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…