UshapigwaMimi mwanangu kafanana na mama yake....
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
UshapigwaMimi mwanangu kafanana na mama yake....
Umejitahidi sana kufafanua kuhusu binary. Hongera sanaNi kawaida sana kusikia mama akisifiwa kwa kuzaa photocopy ya mume wake, bila kujua kwamba ile process ya ‘photocopying’ haikufanyika tumboni kwa mama, bali ilianza kwenye ‘Gonads /(Korodani)’ za baba mtu na kwenda kukamilika tumboni kwa mama.
Kidijitali taarifa za kielektroniki zinatunzwa na kusafirishwa katika ‘Digits’, yaani tarakimu ‘1’ na tarakimu ‘0’, na hizi ndio taarifa za chini kabisa za msingi za kidijitali. Muunganiko wa hizo tarakimu (bits) zikawa 8, ndio tunaita ‘byte’; mfano [10110001] ni ‘byte’ moja (1B) ya taarifa. Muunganiko wa hizi ‘bytes’ zikawa elfu moja , ndio tunaita ‘Kilobyte’ moja (1Kb). Muunganika wa hizo ‘Kilobyte’ zikawa elfu moja, ndio tunaita ‘Megabyte’ moja ya ‘data’/(taarifa) yaani (1Mb).
Kwahiyo ukiambiwa umepata 100Mb maana yake ndio hiyo. Hizi data zinatafsirika na kusafirishika vipi? Mfano ukitumia whatsapp kutuma neno ‘Mama’, hilo neno lina herufi 4, katika lugha za kidijitali (mfano Android platform) kuna makubaliano au standard (lugha ni makubaliano yaletayo maelewano) ; mfano; kwamba herufi ‘m’ iwakilishwe na byte 3 zenye mpangilio fulani wa zile bits (1’s and 0’s), (Switch on/Switch off) na hivyo yule mpokeaji wa meseji simu yake inatafsiri huo mpangilio wa ‘bits’ katika kila ‘byte’ na kupata jibu kwamba mtumaji anamaanisha herufi ‘m’, na herufi ‘m’ hutokea kwenye screen, halikadhalika kwa herufi zote la neno mama. Hadi hapa naweza kusema kwamba mtumaji wa meseji yenye neno ‘mama’ ndio baba ambae amezituma mbegu zake kwenda tumboni kwa mama, na yule mama ndio mpokeaji wa meseji na akaitafsiri kuleta matokea tarajiwa. Nimetolea hii computer analogy ili niweze kueleweka kwenye hatu inayofuata ya vinasaba vya msingi.
Vinasaba vya msingi kwa viumbe vyote hai duniani ni vinne (analogous to digits/bits); ambavyo ni ADENINE, THYMINE, GUANINE, CYTOCINE. Na huu ndio msingi haswa wa kipimo cha DNA. (Deoxyrybonucleic acid) testing.
*Na reserve comment ya kwanza ili niweze kufafanua jinsi hivyo vinasaba vinavyofanya maajabu yenyewe sasa.Kuanzia kwenye ‘Meiosis’ kabisa.., pia tutajaribu kufanya mjadala katika msingi wa kudodosa kuona inawezekana vipi mtoto anafanana hadi kutembea na baba yake?
View attachment 1684441
Mtoto anaweza kurithi vinasaba vya babu, bibi, mjomba , Shangazi nk. , ndio maana unakuta jitu liko hovyo ila watoto ni wazuri balaa...,Kwa hiyo unawashauri binadamu wachaguane wazuri ili wazae watoto wazuri...
Mkuu kwanza hongera kwa huo ujuzi ulionao maana ni wachache sana hufahamu mambo hayo. Mimi naomba kufahamu kuhusu ugonjwa wa ukoma(leprosy) kwani nimekua nikibashana na watu sana kuhusu huu ugonjwa. Huu ugonjwa ni ugonjwa wa kurithi (genetic inherited) ama ni familial disease?Je, wajua chromosome 23 kati ya 46 za Yesu zilipotoka?
Nimewaza tu, binadamu wote huwa na chromosome 46 katika viini vya seli zote mwilini, katika hizo 46, 23 hutoka kwa baba yake na 23 zingine hutoka kwa mama yake; pale mbegu inapoungana na yai ndio huwa 46. Kila Chromosome huwa ina vinasaba (genes) ambazo ndio hutoa maelezo ya jinsi gani mwili...www.jamiiforums.com
Unakopi kutokea mtandao gani?Wengine hufanana na bibi zao au babu zao, tutadodosa hili pia, hasa hasa tukijikita kwenye ‘Recessive’ na ‘Dorminant’ genetic traits tukizingatia matokeo yake katika ‘Homogenous’ na ‘Heterogenous’ combinations...
Kwa haraka haraka, Ugonjwa unaoambukizwa baada ya mtu kuwa keshazaliwa huwa sio wa kurithiMkuu kwanza hongera kwa huo ujuzi ulionao maana ni wachache sana hufahamu mambo hayo. Mimi naomba kufahamu kuhusu ugonjwa wa ukoma(leprosy) kwani nimekua nikibashana na watu sana kuhusu huu ugonjwa. Huu ugonjwa ni ugonjwa wa kurithi (genetic inherited) ama ni familial disease?
Kucopy nini? Hii mimi nilifundishwa form 4 na muhindi mmoja anaitwa ‘Mr.Khatri’, 2006 huko...Unakopi kutokea mtandao gani?
Toa mfano na weka pichaBado mtoto anaweza akakufanania lakini akawa mrembo mno hata kama baba ana sura mbovu, mifano ipo 😂