Fahamu mbinu mbalimbali za kuongeza mauzo ya biashara yako

Fahamu mbinu mbalimbali za kuongeza mauzo ya biashara yako

Dr, namba moja ndio ina maana tu, namba mbili na tatu zinakuja automatic! Hivyo, endelea kututafutia njia zingine hizo mbili! Mpaka sasa umetaja njia moja tu!

Kama namba moja ina maana kuliko hizo nyengine, unamaanisha kuwa ukitaka kufanikiwa katika biashara yako ni ku focus katika kupata wateja wapya tu jambo ambalo sio kweli.

Ukitaka kutengeneza shilingi milioni 10 kwa mwezi kwa kuuza bidhaa za Laki 1 unahitaji wateja 100 wapya kila mwezi.

Kupata wateja hao unahitaji kumiliki mfumo mzuri wa masoko (marketing system) yenye kukuletea wateja 100 kila mwezi.

Lakini kama uta leverage wateja 100 wa mwanzo na kuwafanya wa spend pesa zaidi kwako na wawe wanakuja kwako mara kwa mara basi kipato kinaweza kuongezeka mara 2,3, 5 au hata mara 10.
 
Kama wewe ni mfanyabiashara au mjasiriamali unayehangaika kuongeza kipato cha biashara yako basi baada ya kufahamu njia tatu hizi utaona kuongeza kipato kwenye biashara yako ni rahisi kuliko kumsukuma mlevi.

Bila ya kupoteza muda tuanze mara moja


1. Ongeza Idadi Ya Wateja (Increase the Number of Customers)
Kipato cha biashara yako inatokana na wateja wanaonunua bidhaa au huduma unayotoa. Bila ya wateja huna biashara.

Na kila ukiwa na wateja wengi ndivyo kipato chako kinakuwa kikubwa.

Je Wateja Wako Utawapata Vipi?
Wateja hupatikana kwa kutangaza (wewe au watu wengine) uwepo wa biashara (au bidhaa/huduma) yako pamoja na kufanya mauzo (sales) baada ya wateja kuja kwako.

Bila ya matangazo watu wapya watakuwa hawafahamu biashara (au bidhaa/huduma) zako.

Kwa hivyo ni muhimu kuwa na formula ya matangazo yenye kuhakikisha wateja wapya wanakuja kila siku katika biashara yako.

Na matangazo unaweza kufanya kwa njia mbili.
  1. BURE – Kuwa na duka au ofisi sehemu iliyo mbele za nyuso za watu, kuongea na watu ana kwa ana, kutumia mitandao ya kijamii n.k

  2. Kulipia matangazo – Hii itakusaidia kuwafikia maelfu ya watu kwa mpigo na kwa haraka kwa kuwekeza pesa kwenye jukwaa lenye watu wengi.
Japokuwa njia hii ya kwanza (kuoneza idadi ya wateja) ni muhimu kwa kila biashara, njia hii sio rahisi na inaweza ikakugharimu kwa kiasi kikubwa kama utakuwa unalipia matangazo.

Na ndio maana kutegemea njia hiyo pekee biashara yako itakuwa hatariani, na ndio maana unahitaji kutumia na njia ya pili ambayo ni ku…..


2. Ongeza Idadi Ya Mauzo Ya Kila Mteja (Increase the Unit of Sales)
Kama kila mteja anakuingizia wastani wa shilingi elfu kumi kwa kila manunuzi, inabidi ujitahidi kumshawishi mteja huyo kununua bidhaa za ziada zitakazokufanya uongeza mapato kwa kila manunuzi.

Kama utaweza kuongeza wastani wa mauzo kutoka Tshs. 10,000 hadi Tshs. 20,000 kwa kila mteja, utakuwa ushaikuz biashara yako kwa 200% bila ya kuongeza idadi ya wateja.

Na uzuri ni kuwa wateja hawa tayari wanakujua, wanakupenda na wanakuamini. Kazi yako kubwa ya kufanya ni kuwapatia bidhaa za ziada na wewe unaongeza kipato kwa urahisi.

Swala la kujiuliza ni bidhaa gani ya ziada unayoweza kuwauzia wateja wako juu ya kile kitu wanachonunu kila siku?

Kama wewe upo katika biashara ya kuwatengenezea wateja wako tovuti, basi watahitaji kusajiliwa domain name na kurushiwa tovuti yao hewani au watahitaji kutengenezewa logo.

Kwa hivyo badala ya kumuuzia huduma ya kuwatengenezea tovuti ambayo pengine itakuingizia $500 peke yake, unaweza ukaingiza $20 ya usajili wa jina la tovuti hilo na $160 ya urushaji na $50 ya logo.

Kwa hivyo badala ya kuingiza $500 kwa kila mteja utakuwa unaingiza $730.

Unaweza hata ku ofa kuwatengenezea kurasa za mitandao ya kijamii ya Facebook, Twitter na Instagram kwa $100.

Kwa hivyo badala ya kutengeza $500 ya awali kipato chako kimekuwa ni $830 ambayo ni ongezeko la kipato chako cha awali kwa 66%.

Na uzuri ni kuwa haikugharimu pesa yoyote kuongeza kipato hicho na hutumii nguvu kubwa kumshawishi mteja huyo kwani alikuwa yupo tayari kufanya manunuzi kwako (yaani keshakuamini tayari).

Na hii unaweza kufanya katika biashara yoyote hata kama una kiduka kidogo cha kuuza vitu vya kuhitajika majumbani.

Kwa mfano ukiuza siagi unaweza kutoa ofa kwa mteja wako anunue na jam kwa bei pungufu.

KFC na McDonalds ni mahodari sana katika hili.

Ukiweka oda ya burger, wanakuuliza “je utapenda tukuwekee na chipsi katika hiyo burger?” ukisema ndio wanakuuliza tena “utapenda tukuwekee na kinywaji gani?”

Wewe na yako ilikuwa ni burger pekee yake lakini umejikuta unanunua na chipsi na soda.

3. Ongeza Idadi Ya Mauzo Endelevu (Increase the Frequency of Sales)
Jambo la tatu la muhimu kufanya ni kuhakikisha wateja wako wanarudi kwako mara kwa mara kununua bidhaa au huduma unayotoa.

Unaweza kufanya hivi kwa:
  1. Kuuza bidhaa au huduma zinayopendwa na wateja wako
  2. Kuwasiliana na wateja wako mara kwa mara kuwajulisha kuhusu OFA ya bidhaa au huduma mpya unayotoa.
Nikitoa mfano wa mteja wako aliyetaka umtengenezee tovuti, kipato endelevu kwako hapo ni
  1. Domain Registration - $20/mwaka
  2. Hosting - $160/mwaka
Vile vile unaweza ukampa OFA ya kumanage social media account zake kwa yeye kukulipa $200 au zaidi kwa mwezi.

Asikwambie mtu,

Hakuna kipato kitamu kama kipato endelevu

Unaweza kuwa na wateja 10 na ukaishi kama mfalme kwa sababu una kipato endelevu.

Chukulia mfano huduma hiyo ya social media marketing ambayo unawatoza wateja wako $200 kwa mwezi.

Ukiwa na wateja 10 tayari unaingiza $2000 ambayo ni Milioni 4.5 kwa hela zetu za madafu kila mwezi.

Japokuwa sio kila biashara inakuruhusu kuingiza kipato endelevu kama mfano niliotoa lakini unaweza kuwa mbunifu na kuhakikisha biashara yako inakupa kipato endelevu kwa wateja wako.

Mfano mzuri ni kuwasiliana na wateja wako wanaopenda kununua kwako mara kwa mara kila unapoleta mzigo mpya na kuwapa kwa bei ya OFA kama watachukua idadi fulani.

Ukifanya hivyo utakuja kugundua kuwa 80% ya mafanikio ya biashara yako inatokana na wateja wako wachache mno.

Hizo ndizo njia 3 pekee za kufanya kukuza biashara yako.

Je wewe unafanya njia ngapi?

Comment chini.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako,

Dr. Said Said
Utakuta hata duka huna, lkn unajifanya kushauri.

Biashara haipo simple kama unavyoelezea broo.
Ww ni sawa na wale inspirational speakers, wanayafnya maisha yanaonekana simple lkn ukiingia mtaani uloambiwa yte uyafanye ndo utafanikiwa yanabuma.
Au maprofesa na madokta wa vyuoni wanafundisha uchumi wakat wao hata duka hawajawah kufungua au kuuza.

Biashara sio rahis kama ulivyoelezea.
 
MMEELEZEA TU ADVANTAGES ZA ONLINE ADVERTS AND SERVICES. SA ELEZEENI NA DISADVANTAGES ZAKE ILI WA2 WAPIME FAIDA NA CHANGAMOTO/HASARA ZA ONLINE DEALS.

OVA
 
Ningependelea unifafanulie jinsi ya kumkatalia mteja wako kumpa mkopo, tatizo ukitoa mkopo na mteja kapotea. Je kuna njia gani za kuepusha hilo
MIMI NAUZA SPARE ZA PIKIPIKI WATEJA WANGU WA KUBWA N BODABODA KWAIYO KIUKWELI NAENDA KWA WATEJA KUONGEA NAO LAKINI UKIFIKA WANAKWAMBIA WANATAKA MKOPO NAFANYE HAPO KAKA..
 
Utakuta hata duka huna, lkn unajifanya kushauri.

Biashara haipo simple kama unavyoelezea broo.
Ww ni sawa na wale inspirational speakers, wanayafnya maisha yanaonekana simple lkn ukiingia mtaani uloambiwa yte uyafanye ndo utafanikiwa yanabuma.
Au maprofesa na madokta wa vyuoni wanafundisha uchumi wakat wao hata duka hawajawah kufungua au kuuza.

Biashara sio rahis kama ulivyoelezea.

Umetoa jibu as if tumezaliwa tumbo moja na unanifahamu vizuri.

Ungeaza angalau kuni google to get a background story yangu kwanza.

Biashara is simple. Na wanaohangaika ni wenye kutaka ku complicate.

Oh! And yes, I do run my own business. And no mimi sio motivational speaker.
 
MIMI NAUZA SPARE ZA PIKIPIKI WATEJA WANGU WA KUBWA N BODABODA KWAIYO KIUKWELI NAENDA KWA WATEJA KUONGEA NAO LAKINI UKIFIKA WANAKWAMBIA WANATAKA MKOPO NAFANYE HAPO KAKA..

Nani anamuhitaji mwenzake zaidi?

Wewe unamuhitaji huyo mteja au huyo mteja anakuhitaji wewe zaidi.

Kama wewe unamuhitaji mteja zaidi kuliko yeye anavyokuhitaji wewe inamaanisha kuna kasoro katika biashara yako.

Swali la kujiuliza ni je usipotoa huo mkopo watanunua kutoka kwako au wataenda kwa washindani wako?

Kama hawatonunua kutoka kwako basi angalia unakosea wapi na ujaribu kuboresha bidhaa/huduma zako.
 
*OFFICE/KIGOLI INAUZWA WAPENDWA IPO MTAA WA MAFIA NA SKUKUU NI KIGOLI CHA PEMPARS NA VITU VYA WATOTO INAUZWA NA KILA KITU KILICHOMO MWENYEWE KAHAMISHWA KIKAZI HIVYO WANAHAMA NDO AKAAMUA AUZE KWA MAELEZO ZAIDI 0688008799 NO YA MUHUSIKA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom