Fahamu mbinu ya kugawa makundi ya nyuki uliyonayo kujaza mizinga mipya isiyo na nyuki

Fahamu mbinu ya kugawa makundi ya nyuki uliyonayo kujaza mizinga mipya isiyo na nyuki

Fred Katulanda

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2011
Posts
380
Reaction score
550
Habari wadau;

Leo naomba nidokeze namna ya kugawa Mzinga wenye nyuki ili kujaza mizinga yako mipya isiyo nyuki kwa njia ya haraka badala ya kutumia njia ya awali ya kuwatega na kungoja waingie jambo ambalo linaweza kukuchelewesha na kuchukua muda mrefu.

Kwa mnaofuga au mnaotarajia kuanza ufugaji njia hii inaweza kufanywa yeyote ilimradi aelewe maelekezo haya kwa usahihi na kuzingatia ili aepuke kuwafanya nyuki kukimbia ndani ya Mzinga waliokuwemo.

Mbinu hii ya kugawa makundi itawasaidia kujaza mizinga mipya kwa kasi na inaweza kabisa kujaza mizinga 3 kutokana na mzinga mmoja wenye nyuki, ingawa kupata idadi kubwa ya mizinga utakayoijaza hutegemea na uimara wa Koloni au ukubwa wake lakini na idadi ya viunzi au fremu zenye majana ambayo hayajafikia kuwa nyuki kamili.

Sasa ili kufanikisha jambo hilo hakikisha nyuki ndani ya Mzinga wako wamekaa muda mrefu na Koloni lako lina nguvu na kubwa, kisha fanya yafuatayo;
1. Hakikisha una mizinga yenye nyuki tayari hivyo chagua mzinga Bora wenye Koloni zuri ikiwezekana kuliko na uzalishaji mkubwa wa asali ili utumie kuwagawa.

2. Hakikisha mizinga mipya ambayo unataka igawia nyuki inafanana au inaingiliana zile (Fremu za ndani au viunzi) ili utakapohamisha kutoka mzinga mmoja kwenda mwingine isiwe shida ziweze kuingiliana.

3. Zoezi hili lifanyike jioni au usiku wakati nyuki wote wakiwa wamerejea ndani ya Mzinga na siyo mchana.

4. Fungua mzinga wenye nyuki (Hapa lazima uzingatie ubora wa Koloni kama nilivyoeleza kwenye namba 1.), pulizia moshi kuwafanya nyuki wako watulie na.....;

5. Chukua au toa Fremu ndani ya mzinga yenye Majana (Watoto wa nyuki walio katika hatua ya Lava na Pupa), kisha kaziweke kwenye mzinga mpya na sehemu ya nyuki wakubwa.

6. Pamoja na Fremu zenye Majana ahakikisha unakuwa na fremu yenye Majana na kiasi cha asali na kama haipo weka fremu yenye asali sanjari na zile zenye majana ndani ya mzinga mpya.

7. Eneo ulipotoa Fremu au viunzi kwenye mzinga uliokuwa na nyuki rejesha au weka fremu mpya tupu zisizo na masega ili nyuki waanze kuzijenga upya.

8. Fukinika mzinga yako yote miwili na itundike juu ya mti au kibandani maana utakuwa na mzinga mpya wenye nyuki pia.

9. Kumbuka mzinga mmoja unaweza kuugawa kwa kuweka fremu hizo zenye majana hadi ukapata mizinga 2 au 3 lakini itategemea na ukubwa ama wingi wa fremu zenye majana nada wake.

10. Kumbuka kuacha pia fremu zingine zenye majana katika mzinga uliokuwa na nyuki ili nao kuuacha jai nai.

11. Hakikisha hatua yako hiyo haitaamuaisha Malkia kwenye mzinga uliokuwa na nyuki, kwani wao wataandaa Malkia mpya kutokana na majana. Maana Malkia hurutubishwa na nyuki wafanyakazi kutokana na majana ya.nyuki kike ambayo wao huyatambua.

NB: Kwa ajili ya kusaidia wasioelewa zaidi naweka picha kuonesha aina ya masega ambayo unapaswa kuchukua fremu zake ili kugawa Mzinga ili kukupa picha ya jinsi utakavyo ziona na kuzichukua.

IMG_20210829_135310_885.jpg
Ukiangalia picha hii kuna, Pollen ambayo NI chakuka huonekana hivyo ndani ya masega angalia nilipozungusha Rani ya blue.


IMG_20210829_135306_676.jpg
Nimeeleza majana ambayo ukiyaona ndani ya Mzinga wako katika fremu ni hayo ambayo yapo katika hatua mbili, hapo nilipozungusha rangi ya kijani yakiwa katika hatua ya Lava na kwenye rangi nyekundu yakiwa hatua ya Pupa. Fremu au kiunzi kikiwa na muonekano huo ichukue kwa ajili ya kugawa.


honeybeelifecycle.jpg
Na picha hii itakusaidia kutambua, hatua za nyuki kujua na kupatikana kwa Majana wakiwa katika hatua za Lava na Pupa. Lakini namna nyuki anavyoanza hatua za yai mpaka kukamilika kuruka.

Unaweza kujisomea makala zingine za Nyuki;
Uvunaji wa Sumu ya NyukiUtegaji

Nyuki waingie kwenye mzinga


Asanteni naomba kuwasilisha, kwa msaada zaidi tupigie +255622 642620.
 
Tuchambulie Kuhusu ufugaji wa kisasa inaonekana ukiwa na robo heka unaweza jaza mizinga zaidi ya 450 na minimum harvest ya asali ni kg 2 kwa mzinga,niliona maelezo fulani huko Uganda.

Kama una utaalam zaidi tupeane.
 
Tuchambulie Kuhusu ufugaji wa kisasa inaonekana ukiwa na robo heka unaweza jaza mizinga zaidi ya 450 na minimum harvest ya asali ni kg 2 kwa mzinga,niliona maelezo fulani huko Uganda.

Kama una utaalam zaidi tupeane.
Kujaza mizinga siyo tatizo, tatizo ni hiyo robo heka itakuwa na malisho ya kutosha kuwalisha nyuki wa mizinga 450.

Ufugaji wa kisasa Kwa robo heka mizinga 450 utapaswa kuiweka kwenye kubanda na siyo kuning'iniza kwenye miti.

Sasa ikiwa eneo lako hakuna malisho utalazimika kuwalisha. Japo tunaweza kuangalia nje ya eneo lako hilo la robo heka umbali wa Mita 200-300 kama kuna malipo maana nyuki hutembea umbali huo. Kama hakuna basi robo heka haitofaa kwa idadi ya mizinga 450.

bee-shelter-slider.jpg

Mfano wa Kibanda ambacho unaweza kujenga na kuiweka mizinga yako mingi katika eneo dogo. Hii ni moja ya njia za ufugaji wa kisasa.
 
Kujaza mizinga siyo tatizo, tatizo ni hiyo robo heka itakuwa na malisho ya kutosha kuwalisha nyuki wa mizinga 450.

Ufugaji wa kisasa Kwa robo heka mizinga 450 utapaswa kuiweka kwenye kubanda na siyo kuning'iniza kwenye miti.

Sasa ikiwa eneo lako hakuna malisho utalazimika kuwalisha. Japo tunaweza kuangalia nje ya eneo lako hilo la robo heka umbali wa Mita 200-300 kama kuna malipo maana nyuki hutembea umbali huo. Kama hakuna basi robo heka haitofaa kwa idadi ya mizinga 450.

View attachment 1923218
Ndani wa Kubanda ambacho unaweza kujenga nankuiweka mizinga yako eneo dogo na mingi. Hii ni Moja ya njia zabufugaji wa kisasa.
Hii njia kwangu naona ni nzuri kuliko kuning'iniza kwenye miti kwa sababu Eneo dogo lakini tija kubwa.

Nafikiria kwa mfano kama una Eneo la shamba jirani na misitu na maji huenda ikafaa zaidi
 
Hii njia kwangu naona ni nzuri kuliko kuning'iniza kwenye miti kwa sababu Eneo dogo lakini tija kubwa.

Nafikiria kwa mfano kama una Eneo la shamba jirani na misitu na maji huenda ikafaa zaidi
Yes, tunapoangalia eneo linalofaa ni lazima kuwa na uhakika wa malisho ya nyuki. Hivyo kama wewe unashamba na lipo jirani na msitu isiwe mbali sana (walau Mita 200-300) shamba lako litafaa kufuga maana nyuki watenda msitunikupata malisho yao.

Umegusia la maji, hili ni muhimu sana kwa nyuki. Ni vyema eneo liwe na maji, lakini hili siyo tatizo sana maana ni rahisi kujenga mabakuli ya kunywesha maji nyuki wako. Lakini lazima.ndani kuwe na both vitakavyoelea ili nyuki wakanyage kunywa maji maana nyuki hawajui kuogelea.

150613-bee-pond-hives1.jpg

Unaweza kuchimbia beseni, au kujenga kibwawa cha saruji Kwa ajili ya nyuki kunywa maji na ukahakikisha kinakuwa na maji msimu wa kiangazi zaidi. Ila ni lazima uweke vya vya kuelewa ili nyuki wakanyage kunywa maji.


8160fe16c2fee848a3393f4073c6b5ff-1.jpg

Mfano wa vitu unavyoweza kuweka nyuki wakanyage kunywa maji.
 
Yes, tunapoangalia eneo linalofaa ni lazima kuwa na uhakika wa malisho ya nyuki. Hivyo kama wewe unashamba na lipo jirani na msitu isiwe mbali sana (walau Mita 200-300) shamba lako litafaa kufuga maana nyuki watenda msitunikupata malisho yao.

Umegusia la maji, hili ni muhimu sana kwa nyuki. Ni vyema eneo liwe na maji, lakini hili siyo tatizo sana maana ni rahisi kujenga mabakuli ya kunywesha maji nyuki wako. Lakini lazima.ndani kuwe na both vitakavyoelea ili nyuki wakanyage kunywa maji maana nyuki hawajui kuogelea.

View attachment 1924100
Unaweza kuchimbia beseni, au kujenga kibwawa cha saruji Kwa ajili ya nyuki kunywa maji na ukahakikisha kinakuwa na maji msimu wa kiangazi zaidi. Ila ni lazima uweke vya vya kuelewa ili nyuki wakanyage kunywa maji.


View attachment 1924101
Mfano wa vitu unavyoweza kuweka nyuki wakanyage kunywa maji.
🙏🙏
 
Yes, tunapoangalia eneo linalofaa ni lazima kuwa na uhakika wa malisho ya nyuki. Hivyo kama wewe unashamba na lipo jirani na msitu isiwe mbali sana (walau Mita 200-300) shamba lako litafaa kufuga maana nyuki watenda msitunikupata malisho yao.

Umegusia la maji, hili ni muhimu sana kwa nyuki. Ni vyema eneo liwe na maji, lakini hili siyo tatizo sana maana ni rahisi kujenga mabakuli ya kunywesha maji nyuki wako. Lakini lazima.ndani kuwe na both vitakavyoelea ili nyuki wakanyage kunywa maji maana nyuki hawajui kuogelea.

View attachment 1924100
Unaweza kuchimbia beseni, au kujenga kibwawa cha saruji Kwa ajili ya nyuki kunywa maji na ukahakikisha kinakuwa na maji msimu wa kiangazi zaidi. Ila ni lazima uweke vya vya kuelewa ili nyuki wakanyage kunywa maji.


View attachment 1924101
Mfano wa vitu unavyoweza kuweka nyuki wakanyage kunywa maji.
Mkuu upo vizuri sana aisee
 
Karibu kwa mnaofuga au mnaotarajia kuanza, ulizeni tupeane ujuzi kwa kiasi nilichonacho.
Ahsante.

Biashara ya asali na bidhaa nyinginezo zitokanazo na nyuki ni biashara ya pesa nyingi sana kwenye nchi za wenzetu mfano Uingereza [emoji636], kuna hadi cases za watu kuibiwa mizinga ya nyuki UK.

Sekta hii haipo exploited to its full potential kwa nchi yetu, kama mtaalamu unahisi tunakwama wapi kama taifa?
 
Ahsante.

Biashara ya asali na bidhaa nyinginezo zitokanazo na nyuki ni biashara ya pesa nyingi sana kwenye nchi za wenzetu mfano Uingereza [emoji636], kuna hadi cases za watu kuibiwa mizinga ya nyuki UK.

Sekta hii haipo exploited to its full potential kwa nchi yetu, kama mtaalamu unahisi tunakwama wapi kama taifa?
Nchi hii tumekwama vitu vingi sana na zaidi ni pale tuliposema Kilimo ni utu wa Mgongo halafu hatukuwekeza kwenye hicho Kilimo kama Taifa.

Watalam wetu wa sekta hii, wanaohusika na utungaji wa sera hawajaichukua kama fursa kubwa. Natambua ipo mikakati mingi imeelezwa na kuandikwa kama Taifa na ikisimamiwa inaweza kutupatia fedha za kigeni , ila hatujaamua kwenda kwenye uhalisia hapo ndipo mambo ni tofauti.
i
Wakati nimeamua kuingia kwenye ufugaji nilitembelea wafugaji akini zaidi ya 95% ya wafugaji hao na ambao niliambiwa ni wafugaji wakubwa nilikuta anayeitwa mkubwa ana mzinga 50-100 kwenye mzinga zaidi ya 300 anayo ya kienyeji ambayo tija yake ndogo. Lakini ukiwauliza wanavuna nini asilimia kubwa hawajui mazao mwingine zaidi ya Asali na Nta.

Zao la Sumu ya Nyuki ni msamiati mpya kwa wafugaji hata baadhi ya maofisa nyuki wa Halmashauri na wachache wanaojua wanadai hawajui linavunwaje. Hapa utaona tunakisaje fedha za kigeni.

Hata hivyo bado wafugaji wetu wengi wanafuga bila tija uzalishaji mdogo na serikali haijamulika ufugaji huu kama moja ya fursa kubwa pia.

Naeeza kusema hayo.
 
Nchi hii tumekwama vitu vingi sana na zaidi ni pale tuliposema Kilimo ni utu wa Mgongo halafu hatukuwekeza kwenye hicho Kilimo kama Taifa.

Watalam wetu wa sekta hii, wanaohusika na utungaji wa sera hawajaichukua kama fursa kubwa. Natambua ipo mikakati mingi imeelezwa na kuandikwa kama Taifa na ikisimamiwa inaweza kutupatia fedha za kigeni , ila hatujaamua kwenda kwenye uhalisia hapo ndipo mambo ni tofauti.
i
Wakati nimeamua kuingia kwenye ufugaji nilitembelea wafugaji akini zaidi ya 95% ya wafugaji hao na ambao niliambiwa ni wafugaji wakubwa nilikuta anayeitwa mkubwa ana mzinga 50-100 kwenye mzinga zaidi ya 300 anayo ya kienyeji ambayo tija yake ndogo. Lakini ukiwauliza wanavuna nini asilimia kubwa hawajui mazao mwingine zaidi ya Asali na Nta.

Zao la Sumu ya Nyuki ni msamiati mpya kwa wafugaji hata baadhi ya maofisa nyuki wa Halmashauri na wachache wanaojua wanadai hawajui linavunwaje. Hapa utaona tunakisaje fedha za kigeni.

Hata hivyo bado wafugaji wetu wengi wanafuga bila tija uzalishaji mdogo na serikali haijamulika ufugaji huu kama moja ya fursa kubwa pia.

Naeeza kusema hayo.
Ahsante kwa majibu mujarab.
 
Very enlightening..👍
Asante kwa maarifa...
Sasa kama mtu anata kuwekeza kwenye hii biashara, kwa kufuata hizi njia za kisayansi na kisasa
Je ni kiasi gani cha mtaji kinahitajika?
 
Very enlightening..👍
Asante kwa maarifa...
Sasa kama mtu anata kuwekeza kwenye hii biashara, kwa kufuata hizi njia za kisayansi na kisasa
Je ni kiasi gani cha mtaji kinahitajika?
Hili swali wengi huuliza, siwezi kukupa jibu la moja kwa moja sababu kuna mahitaji itakubidi uyajue katika eneo lako yana gharama gani ndiyo yakupe gharama halisi. Mfano;
1. Utafugia mstuni au shambani, sasa kama ni msitu au shamba utanunua kiasi gani au utahitaji kibali.

2. Aina ya mizinga ambayo utafugia itakugharimu kiasi gani kwa kila mmoja. Maana mbao zinatofautiana bei eneo hadi eneo.
Unaweza kuanza na mizinga mingapi ili ujue gharama ya mizinga husika.

Binafsi huwa nawashauri kwanza kuanza na kujifunza, ili wafanye ufugaji anaojua ajue aina za mizinga na kutengeneza pia au kuwatega nyuki waingie.

Sasa ili ujue unaweza kuwekeza Kwa kiasi gani fanya hivi:
1. Bei ya eneo unalotaka kufugia.
2. Mizinga Sh 170,000 X 50=
3. Ujenzi wa kibanda (unaweza kuiweka katika miti)
4. Vifaa kama;
Bee suite 2X 150,000
Smoker Sh 50,000
Chujii Sh 60,000
Brash ya Nyuki Sh 20,000
Batasi Sh 20,000
Gambuti Sh 20,000

Kwa kifupi siwezi kuiweka gharama halisi hapa zikamfaa kila mmoja lakini nimekupa picha ndogo ikusaidie kuelewa. Na gharama zinapanda zaidi kulingana na mamna unavyotaka kuwekeza au kuanza mradi.
Gharama za uendeshaji itategemea umbali wa eneo la mradi na Aina ya ukaguzi unayofanya na kama ni wewe au utamuweka mtalaamu akufanyie.

Ila ukitupa kazi ya kukuchambulia na gharama zako binafsi na eneo unalotaka tunaweza kukuandalia kwa uzuri zaidi ikiwa ni pamoja na kukushauri mbinu za kuanza nazo kulingana na mtaji ulio nao.
 
Ni muda sasa umepita;
Swali:
1. Je, kuna mfugaji yeyote amejaribu njia hii?
2. Umefanikiwa au?
3. Umepata changamoto gani?

Nitafurahi iwapo mfugaji aliyefanyia kazi njia hii atatuelezea hapa ili Kama alipata changamoto tuweze kumsaidia zaidi maarifa. Lengo kuwajengea uwezo na utalaamu wa kujihudumia Wenger wafugaji.
 
Hili swali wengi huuliza, siwezi kukupa jibu la moja kwa moja sababu kuna mahitaji itakubidi uyajue katika eneo lako yana gharama gani ndiyo yakupe gharama halisi. Mfano;
1. Utafugia mstuni au shambani, sasa kama ni msitu au shamba utanunua kiasi gani au utahitaji kibali.

2. Aina ya mizinga ambayo utafugia itakugharimu kiasi gani kwa kila mmoja. Maana mbao zinatofautiana bei eneo hadi eneo.
Unaweza kuanza na mizinga mingapi ili ujue gharama ya mizinga husika.

Binafsi huwa nawashauri kwanza kuanza na kujifunza, ili wafanye ufugaji anaojua ajue aina za mizinga na kutengeneza pia au kuwatega nyuki waingie.

Sasa ili ujue unaweza kuwekeza Kwa kiasi gani fanya hivi:
1. Bei ya eneo unalotaka kufugia.
2. Mizinga Sh 170,000 X 50=
3. Ujenzi wa kibanda (unaweza kuiweka katika miti)
4. Vifaa kama;
Bee suite 2X 150,000
Smoker Sh 50,000
Chujii Sh 60,000
Brash ya Nyuki Sh 20,000
Batasi Sh 20,000
Gambuti Sh 20,000

Kwa kifupi siwezi kuiweka gharama halisi hapa zikamfaa kila mmoja lakini nimekupa picha ndogo ikusaidie kuelewa. Na gharama zinapanda zaidi kulingana na mamna unavyotaka kuwekeza au kuanza mradi.
Gharama za uendeshaji itategemea umbali wa eneo la mradi na Aina ya ukaguzi unayofanya na kama ni wewe au utamuweka mtalaamu akufanyie.

Ila ukitupa kazi ya kukuchambulia na gharama zako binafsi na eneo unalotaka tunaweza kukuandalia kwa uzuri zaidi ikiwa ni pamoja na kukushauri mbinu za kuanza nazo kulingana na mtaji ulio nao.
Mkuu mimi nilikua na swali hapo kwenye kibanda unaweza kutuelezea kidogo?
Nimewahi kuona mizinga ikiwekwa sehemu moja kwenye banda inapangwa kama makabati kwanzia chini hadi juu,na juu kibanda kimeezekwa kwa bati/bati kukinga na jua,mvua.

Pili,kuhusu nyuki wadogo je ufugaji wao wanaweza kuingia kwenye mizinga ya kuchonga kienyeji/yakisasa?au wao wanaishia kutengeneza asali yao kwenye miti,mapango tu?
 
Mkuu mimi nilikua na swali hapo kwenye kibanda unaweza kutuelezea kidogo?
Nimewahi kuona mizinga ikiwekwa sehemu moja kwenye banda inapangwa kama makabati kwanzia chini hadi juu,na juu kibanda kimeezekwa kwa bati/bati kukinga na jua,mvua.

Pili,kuhusu nyuki wadogo je ufugaji wao wanaweza kuingia kwenye mizinga ya kuchonga kienyeji/yakisasa?au wao wanaishia kutengeneza asali yao kwenye miti,mapango tu?
Pole Kwa kuchelewa kujibu, ngoja nikujibu.

Kuhusu kibanda: Nadhani picha unazoona zina uhalisia, katika kibanda mizinga upangwa lakini Kwa nafasi na kitalaam. Katika kibanda mizinga inapaswa kupanga kitalaamu.

Nyuki Wadogo: Hawa pia hufugwa na kuweka kwenye mizinga ya kienyeji au ya kisasa. Ila lazima mfugaji atambue nyuki Wadogo wanachangamoto kubwa kufugwa kuliko hao wengine.
Nitaweka tofauti zao kidogo hapa,
1. Nyuki Wadogo upatikanaji wao siyo Sawa na nyuki wakubwa ambao unatega wanakula, lazima ukanunue mbegu ili uwafuge.
2. Ni wepesi kuhama au kukuambia wanapokabiliana na changamoto kidogo. Hii ndiyo sababu waliowafuga wengi wamebaki na mizinga na nyuki hao (Wadogo) wakubwa hawapo wameondoka.

Siku tukijali niaandika Kwa kifefu na kufanya zaidi. Kwa sasa mfugaji anayetaka kufugwa kibiashara tunamshukuru kufugwa nyuki wakubwa maana ndiyo wanatoa pia asali nyingi kuliko Wadogo.
 
  • Thanks
Reactions: PYD
Mkuu nashukuru nimepata wafugaji wenzangu humu, nina mizinga ya top bar 10 tayari lengo ifike 150 mwakani 2022
IMG-20211111-WA0000.jpg
IMG-20211105-WA0002.jpg
 
Mkuu nashukuru nimepata wafugaji wenzangu humu, nina mizinga ya top bar 10 tayari lengo ifike 150 mwakani 2022 View attachment 2057225View attachment 2057234
Siwajibu;
Binafsi nafurahi kuona mfugaji aliyeanza kazi ya ufugaji tayari. Mimi nipo Mkoa wa Mwanza tunaweza kuwasiliana na kubadilishana zaidi mawazo na ujuzi.

Kwa post hii unaweza kuendelea kuongeza mizinga mipya na kuijaza Kwa njia ya kugawa makundi badala ya kutega kugonja nyuki wingie wenyewe jambo ambalo litakuchukua muda mrefu.

Wasiliana nami; +255 622 642620
 
Back
Top Bottom