Fahamu namna ya utegaji Nyuki ili waingie kwenye mzinga

Fahamu namna ya utegaji Nyuki ili waingie kwenye mzinga

Fred Katulanda

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2011
Posts
380
Reaction score
550
Kutega Mizinga ili iweze kuingia nyuki ni sehemu ya utalaamu unapaswa kufanyika kwa makini. Wafugaji wapya wengine wamekuwa wakitega bila kupata mafanikio kutokana na kukosa ujuzi, hapa ninawaletea namna ya kufanikisha utegaji na nyuki waweze kuingia ndani ya mzinga.

Hatua za kufuata;
1. Chukua Nta yako kisha iyeyushe kwenye moto ikiwa ndani ya chombo na uweke kwenye mchirizi ya viunzi (Fremu) ya mzinga wako,
2. Chukua majani aina ya Malumba (Nitakuwekea picha) sugua kuta za ndani ya mzinga wako.
3. Chukua kigaye au kipande cha bati na weka mkaa wa moto kicha chukua vipande vya Nta na Majani hayo (Malumba) na uyachome kufukiza ndani ya mzinga wako wa nyuki.
4. Funika vyema mzinga wako kisha kautundike kungoja nyuki waingie.
5. Hakikisha wakati wa kutundika mzinga wako mlango wa mzinga unakuwa mashariki au magharibi.
6. Tega mzinga wako kuanzia Miezi ya Agosti hadi April hasa (Machi na April ndivyo vipindi vizuri zaidi kwa upangaji makundi).


IMG_20210822_153135.jpg
Pichani juu ni mmea ambao unajulikana kwa jina la Malumba unaotumika kusungua na kuchona ndani ya Mzinga ili kuita nyuki.

Mara baada ya kutega nyuki wakaingia ndani ya Mzinga wako, mizinga mingine siyo lazima utege upya bali unaweza kugawa makundi ya nyuki uliyopata na kujaza mizinga mingine, ni Kwa namna gani, fuatilia hapa.

Makala nyingine za ufugaji nyuki hizi hapa;
Ni nini husababisha asali kuganda?
 
Kutega Mizinga ili iweze kuingia nyuki ni sehemu ya utalaamu unapaswa kufanyika kwa makini. Wafugaji wapya wengine wamekuwa wakitega bila kupata mafanikio kutokana na kukosa ujuzi, hapa ninawaletea namba ya kufanikisha utegaji na nyuki waweze kuingia ndani ya mzinga.
Mimi nazalisha kisha nawaweka ndani ya mizinga.unaweza subiri ata mwaka wasije
 
Mimi nazalisha kisha nawaweka ndani ya mizinga.unaweza subiri ata mwaka wasije
Kuzalisha natumaini unaelezea ufanyaji wa Grafting ya Malkia, hii ni njia bora ambayo inamuhitaji mfugaji awe mweledi na awe na grafting kit. Siyo wote wanamudu njia hiyo na kutumia watalaamu kunahitaji uwagharamikie.

Ni njia fupi lakini lazima use na nyuki wa kuanzia shambani kwako au Kwa anayekuzalishia na uchague makundi bora ya uzalishaji.
 
IMG_20210822_153008.jpg


Kwa wenzetu China wanaitumia dawa hii kupulizia ndani ya mzinga INA matokeo mazuri, nimeitumia na kufanikisha uingiaji wa nyuki katika mizinga yangu zaidi ya 45+ changamoto ninuoatikanaji wake hapa nchini mpaka kuiaguza Kwa njia ya mtandao.
 
View attachment 1903205

Kwa wenzetu China wanaitumia dawa hii kupulizia ndani ya mzinga INA matokeo mazuri, nimeitumia na kufanikisha uingiaji wa nyuki katika mizinga yangu zaidi ya 45+ changamoto ninuoatikanaji wake hapa nchini mpaka kuiaguza Kwa njia ya mtandao.
Sasa mkuu huko mtandaoni hii unaiagiza kwa jina gani mana hapo naona kichina tupu
 
Kutega Mizinga ili iweze kuingia nyuki ni sehemu ya utalaamu unapaswa kufanyika kwa makini. Wafugaji wapya wengine wamekuwa wakitega bila kupata mafanikio kutokana na kukosa ujuzi, hapa ninawaletea namna ya kufanikisha utegaji na nyuki waweze kuingia ndani ya mzinga.

Hatha za kufuata;
1. Chukua Nta yako kisha iyeyushe kwenye na uweke kwenye mchirizi ya viunzi (Fremu) ya mzinga wako,
2. Chukua majani aina ya Malumba (Nitakuwekea picha) sugua kuta za ndani ya mzinga wako.
3. Chukua kigaye au kipande cha bati na weka mkaa wa moto kicha chukua vipande vya Nta na Majani hayo (Malumba) na uyachome kufukiza ndani ya mzinga wako WA nyuki.
4. Funika vyema mzinga wako kisha kautundike kunoja nyuki waingie.
5. Hakikisha wakati wa kutunzika mzinga wako mlango wa mzinga unakuwa mashariki au magharibi.
6. Tega mzinga wako kuanzia Miezi ya Agosti hadi April hasa (Machi na April ndivyo vipindi vizuri zaidi kwa upangaji makundi).


Hongera sana Mwamba!

Kazi iendelee.
 
HODI WAFUGA NYUKI WA KILIMANJARO.

Hii ni taarifa kwa wafugaji wote wa nyuki waliopo Mkoa wa Kilimanjaro hususan Same na Mwanga, nitakuwa huko kianzia Oktoba 5 hadi 7 hivyo tunaweza kuonana na kushauriana kupena elimi kuhusu ufugaji nyuki kisasa na mazao yake sita.

Kwa wenye uhitaji tafadhari waasiliana nami kwa ratiba.
Call/What's App ±255 622642620
 
Mkuu Fred Katulanda nina swali,

Niliwah kuambiwa asali ya Africa sana sana Tanzania ina soko sana nje kutokana na taste yake. Hata hivyo nikaambiwa ni asali ya nyuki wa asili ndo ina soko sana.

Lakini pia nikajulishwa kuwa ni ngumu pia kwa watu kuwekeza kutokana na kwamba ile taste inayopendwa inatokana na nyuki asili kuzunguka na kuchukua virutubisho kwenye mapori jambo ambalo ni gumu kulifanikisha ukiwafuga,


Swali langu, hili jambo ni kweli?

Na je, kuna namna ya kuwafuga bado ukafanikiwa kuzalisha asali sawa na ya nyuki pori?
 
Mkuu Fred Katulanda nina swali,

Niliwah kuambiwa asali ya Africa sana sana Tanzania ina soko sana nje kutokana na taste yake. Hata hivyo nikaambiwa ni asali ya nyuki wa asili ndo ina soko sana.

Lakini pia nikajulishwa kuwa ni ngumu pia kwa watu kuwekeza kutokana na kwamba ile taste inayopendwa inatokana na nyuki asili kuzunguka na kuchukua virutubisho kwenye mapori jambo ambalo ni gumu kulifanikisha ukiwafuga,


Swali langu, hili jambo ni kweli?

Na je, kuna namna ya kuwafuga bado ukafanikiwa kuzalisha asali sawa na ya nyuki pori?
Nimesoma swali lako nikiwa safarini niruhusu nikujibu machache.

"Niliwah kuambiwa asali ya Africa sana sana Tanzania ina soko sana nje kutokana na taste yake. Hata hivyo nikaambiwa ni asali ya nyuki wa asili ndo ina soko sana".

Nyuki wengi tunaofuga ni nyuki wa asili, maana wao siyo kama kuku kwamba wapo wa kisasa na wakienyeji.

Kuhusu soko ni kweli asali kutoka Afrika ina soko kubwa Ulaya sababu nyuki wetu wanapata malisho kwenye misitu ya asili ambayo bado ni mingi.

Ulaya kutokana na kutokuwa na mapori ya kutoka wamekuwa wakiwalisha nyuki wao vyakula ambayo hutayarishwa viwandani. Lakini kwetu bado tunao utajiri wa mapori na Miti mingi ya Maya ambako nyuki hujipatia malisho.
 
Nimesoma swali lako nikiwa safarini niruhusu nikujibu machache.

"Niliwah kuambiwa asali ya Africa sana sana Tanzania ina soko sana nje kutokana na taste yake. Hata hivyo nikaambiwa ni asali ya nyuki wa asili ndo ina soko sana".

Nyuki wengi tunaofuga ni nyuki wa asili, maana wao siyo kama kuku kwamba wapo wa kisasa na wakienyeji.

Kuhusu soko ni kweli asali kutoka Afrika ina soko kubwa Ulaya sababu nyuki wetu wanapata malisho kwenye misitu ya asili ambayo bado ni mingi.

Ulaya kutokana na kutokuwa na mapori ya kutoka wamekuwa wakiwalisha nyuki wao vyakula ambayo hutayarishwa viwandani. Lakini kwetu bado tunao utajiri wa mapori na Miti mingi ya Maya ambako nyuki hujipatia malisho.
Ahsante mkuu
 
Hii ni kuwahi kuinunua kabla waswahili wajaibadilishia matumizi na kuwa silaha ya maangamizi. Waswahili hawana dogo.
Haina madhara yoyote zaidi ya harufu inayoweza kuwavitia nyuki, haiwashi hivyo sidhani kama unaweza kutumika kama silaha.
 
HODI WAFUGA NYUKI WA KILIMANJARO.

Hii ni taarifa kwa wafugaji wote wa nyuki waliopo Mkoa wa Kilimanjaro hususan Same na Mwanga, nitakuwa huko kianzia Oktoba 5 hadi 7 hivyo tunaweza kuonana na kushauriana kupena elimi kuhusu ufugaji nyuki kisasa na mazao yake sita.

Kwa wenye uhitaji tafadhari waasiliana nami kwa ratiba.
Call/What's App ±255 622642620
Umesema nyuki ana mazao sita, mbali na asali mengine ni yapi hayo? Soko lake likoje nalo?
 
Haina madhara yoyote zaidi ya harufu inayoweza kuwavitia nyuki, haiwashi hivyo sidhani kama unaweza kutumika kama silaha.
Bora nisiseme hapa inaweza kutumikaje kama silaha. Asante sana, mkuu kwa dokezo la matumizi sahini ya dawa hii.
 
Back
Top Bottom