Apps-tz
New Member
- Apr 10, 2020
- 4
- 4
Katika kipindi hiki cha ugonjwa wa corona, ambapo wengi wetu tupo nyumbani, moja ya changamoto kubwa tunayokutana nayo kununua mahitaji ya kila siku ya nyumbani kama vile vyakula, mboga mboga na vinywaji. Kwa kulijua hili kampuni ya Selcom wametuletea application inayoitwa Dukadirect inayokuwezesha kuagiza mahitaji yako ukiwa nyumbani na kuletewa hadi mlangoni kwako tena bure kabisa bila kulipia gharama za usafiri.
Uzuri wa application hii ni kwamba,
1. Wanafanya free delivery (kwa sasa ni kwa mkoa wa Dar es salaam tu).
2. Unaweza kulipa pale tu oda yako inapofika yaani (Cash on delivery) pia unaweza kulipia kwa Masterpass QR (Kwa kutumia Mpesa, Tigopesa, Airtel , Halopesa, Ezypesa na Tpesa) pamoja na kadi za Visa na Mastercard.
3. Kama bidhaa unayohitaji bado haipo unaweza kurequest bidhaa yako na wao wakaiweka kwenye orodha ya bidhaa zao .
4. Hakuna minimum order amout. Hivyo unaweza kuagiza kitu hata kimoja unachohitaji.
Unaweza kwenda Google play store au app store kupata na kujaribu kutumia ni huduma nzuri sana.