Fahamu Vivinjari (Browsers) maarufu zaidi duniani

Fahamu Vivinjari (Browsers) maarufu zaidi duniani

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Browsers.png


- Kivinjari (Browser) ni programu ya Kompyuta au Simu ambayo hufanya kazi ya kupangilia, kuleta na kuonesha maudhui kutoka kwenye tovuti. Unapobonyeza kiungo (link), unatumia kivinjari kutembelea tovuti hiyo.


- Takwimu kutoka tovuti ya Global Stats Counter zinaonesha kuwa kivinjari cha Chrome kinachomilikiwa na Kampuni ya Google ndicho kivinjari kinachotumiwa na watu wengi zaidi, kikitumiwa na zaidi ya asilimia 64 ya watumiaji wote wa intaneti duniani, ikifuatiwa na kivinjari cha Safari kinachomilikiwa na kampuni ya Apple, zote za nchini Marekani.


- Hata hivyo, si vivinjari vyote vinavyotumiwa na watu wengi ni salama. Baadhi ya vivinjari salama zaidi ni pamoja na Firefox, Iridium Browser, Tor Browser nk.


- Kufahamu zaidi kuhusu vivinjari salama, soma:
 
Uc mini ukidownload video afu in case bundle limekata or whatever connection ikaanza kuloose ukiplay mzigo unaplay mpaka pale ilipoishia ila Chrome haiwez kuplay na ukikaa muda mrefu (hours) ukisema uje ku-resume the download mzigo unayeyuka, unajikuta unaanza upyaaa, it sucks to me that way! Nadhan watu wanaitumia kwasababu ni default browser kwenye android devices na labda ina features nyingine ambazo sizijui but for me Nah!
 
Hawa JamiiForums nao chenga Kwa kweli Huko walikotoa statistics Mozilla ina watumiaji 3.66% halafu kwenye chart haipo.

Ni kitu gani kimeikuta Mozilla maana ndio ilitoa kwenye soko IE ya windows? Mwaka 2009 market share ya Mozilla ilifika 32%.
 
Tatizo mnatupiga na kitu kizito halafu hamtaki tukiugulia... huo uzi wako ulioambatisha jamaa katuchoma na kitu chenye ncha kali halafu tukitaka kureply... "The thread is locked by moderator"
 
Chrome leo naitoa kupitia system ya kutoa bloatware nibaki na kivinjari nikipendacho haina inshu aisee, ina ads sana ila kwa kua ni built in kila nikitaka kucomand uc min au mi browrse iwe default search ingine inakataa Chief-Mkwawa msaada plz device n Mojitoi
 
Back
Top Bottom