Faida 10 za kumshukuru Mungu

Faida 10 za kumshukuru Mungu

Ni mahubiri yanayothibitisha uwepo wa Mungu.
Mungu muweza wa yote hayupo , hayo ni maneno ya kujifariji ambayo hayana uthibitisho wowote , ni maneno ya kiimani tu , ambapo dini mbalimbali wanayo na Mungu wao pia wapo tofauti kifikra.
 
N

Wakati wa mkesha wa mwaka mpya, watu wanatumia muda mwingi kumshukuru Mungu. Faida za kushukuru tayari zimedadavuliwa.
Mungu yupi unahisi anatakiwa ashukuriwe kwa sababu wapo zaidi ya 1000 wote wanajinadi ni waumba kila kitu?
 
Tarehe 31 Desemba ni siku ambayo watu wengi hukusanyika makanisani kumshukuru Mungu. Zifuatazo ni faida 10 za kumshukuru Mungu:

1. Huimarisha Imani: Kumshukuru Mungu hutufundisha kutambua uaminifu Wake na kuimarisha imani yetu, tukijua kwamba anafanya kazi kwa manufaa yetu.

2. Hutupa Amani ya Moyoni: Shukrani huondoa mawazo ya wasiwasi na huzuni, na kutuachia amani ya kiroho inayotokana na kumtegemea Mungu.

3. Huongeza Furaha: Watu wanaoshukuru wana furaha zaidi kwa sababu wanathamini hata mambo madogo ambayo Mungu amewatendea.

4. Hutuleta Karibu na Mungu: Shukrani huimarisha uhusiano wetu na Mungu kwa kutufanya tutambue ukuu na upendo Wake maishani mwetu.

5. Huinua Nafsi Zetu: Kumshukuru Mungu hutusaidia kuona maisha katika mtazamo chanya, hata katika changamoto, na hutufanya tujihisi wenye thamani.

6. Hulinda Moyo Usipotoshwe: Moyo wa shukrani hutusaidia kuepuka kiburi na kujiona kuwa sisi ndio chanzo cha mafanikio yetu, badala ya kumtambua Mungu.

7. Hufungua Milango ya Baraka: Shukrani ni kitendo cha imani kinachomfanya Mungu kufungua milango ya baraka zaidi maishani mwetu.

8. Hutuongezea Uvumilivu: Tunaposhukuru kwa yale tuliyonayo, tunapata nguvu za kustahimili majaribu huku tukisubiri Mungu kutimiza ahadi Zake.

9. Hutufundisha Roho ya Unyenyekevu: Shukrani hutufundisha kuwa wanyenyekevu kwa kutambua kwamba kila kitu tunachopata kinatoka kwa Mungu.

10. Ni Njia ya Kutoa Ushuhuda kwa Wengine: Tunapomshukuru Mungu hadharani, tunawashawishi wengine kumwamini na kumtumikia Mungu kwa kuona jinsi alivyotutendea mema.

"Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu." (1 Wathesalonike 5:18).

Baada ya kuzijua faida hizo, naamini kesho utajiunga na Wakristo wengine kumshukuru Mungu kwa mambo mengi aliyotutendea mwaka huu. Sio kesho tu, siku zote kumbuka kumshukuru Mungu, ujionee faida hizo.
Uzi mzuri sana mkuu
Barikiwa sana
 
Faida 1 ya kwanini uwashukuru watu wema badala ya Mungu.


1. Kuwashukuru watu wema huonesha umuhimu na kuheshimu kile walichofanya.

Uko Jangwani umebanwa na kiu kikali na hauna maji. Umejaribu kufanya kila linalowezekana upate maji imeshindikana.

Assume kuwa umefanya dua yako kwa imani yako kumuba Mungu akusaidie.

Ukiwa katika point ya kukata tamaa ghafla anajitokeza msamalia anakupa maji. Unakunywa na kukata kiu yako.

Unapiga kelele nyingi kumshukuru Mungu kwa kujibu dua yako na sifa kibao za upendo ukimwagia.

Wakati huo yule msamaria hujampa shukurani ya kuamini yeye ndio sababu ya wewe kupona kifo cha kusababishwa na kiu badala hake sifa zote zimeenda kwa Mungu.

Automatically utaanza kuvimba kichwa kujiona kama tayari una vinasaba vya kimalaika na unauwezo wa ku-communicate direct na Mungu.

Na pengine wazo la kwanza ukitoka hapo utahitaji kufungua Kanisa au kuwa Sheikh wa msikiti kwa kile ulichokiona kama muujiza.

Lakini baada ya muda utapohisi maumivu makali ya tumbo na kuanza kukosa nguvu ndio huo muda ambao yule msamaria anakuambia nimekupa maji yenye sumu.

At this time utaanza kumuona yule msamaria ni mtu katili asiyekuwa na utu. Wakati huu yale mawazo ya mwanzo kuwa Msamaria aliyekuja na maji katumwa na Mungu utaona ni mawazo ya kijinga.

Utamuona jamaa ni shetani mwenye roho mbaya. Hutatamani kujikumbusha kuwa ni majibu ya dua yako kwa Mungu.

Lakini akikupa maziwa kutibu sumu yako halafu ukapona. Utarudi tena kwenye ujinga wako wa mwanzo "Daaah Mungu alikuwa ananijaribu na hii mara ya mwisho aliifanya kwa Ayubu"
 
Mambo yanayothibitisha uwepo wa Mungu ni mengi sana. Nimekutajia hilo moja tu, kwamba aliyesema wanadamu tutakufa ni Mungu. Na tangu aseme hakuna aliyeweza kupinga
Kwenda bhana, wewe unanipotezea tu mda hapa.
 
Thibitisha uwepo wake , hili ni jukwaa huru na hapa sio kanisani sawa mkuu?
IMANI ni kuwa na uhakika bayana juu wa uwepo wa mambo yatarajiwayo pasipo uthibitisho.
Mfano kupanga mipango ya kesho kwa imani kuwa utaiona kesho ukiwa hai mzima ,lakini kabla ya kuiona hiyo kesho unaweza ukafa na usiione hiyo kesho.

Huu uzi ni wa Kumshukuru Mungu kwa watu kwa watu wanaoamini katika uwepo wa Mungu.
kama endapo mimi ningekuwa siamini katika Mungu nisingechangia huu uzi mana ungekuwa haunihusu.Ni sawa na budha au siku wakiamua kumtembeza sanamu la mungu wao wale wahindi wameomba na kibali wanamtembeza mungu wao kwa maandamano ya amani wakimshukuru mungu wao wa kuchonga ambaye ni sanamu..halafu mimi navamia nawaambia huyo siyo mungu na kuwataka wanithibitishie kuwa huyo ni mungu..ndicho unachokufanya hapa .
 
IMANI ni kuwa na uhakika bayana juu wa uwepo wa mambo yatarajiwayo pasipo uthibitisho.
Mfano kupanga mipango ya kesho kwa imani kuwa utaiona kesho ukiwa hai mzima ,lakini kabla ya kuiona hiyo kesho unaweza ukafa na usiione hiyo kesho.

Huu uzi ni wa Kumshukuru Mungu kwa watu kwa watu wanaoamini katika uwepo wa Mungu.
kama endapo mimi ningekuwa siamini katika Mungu nisingechangia huu uzi mana ungekuwa haunihusu.Ni sawa na budha au siku wakiamua kumtembeza sanamu la mungu wao wale wahindi wameomba na kibali wanamtembeza mungu wao kwa maandamano ya amani wakimshukuru mungu wao wa kuchonga ambaye ni sanamu..halafu mimi navamia nawaambia huyo siyo mungu na kuwataka wanithibitishie kuwa huyo ni mungu..ndicho unachokufanya hapa .
Nataka nimjue huyo Mungu ndio naomba uthibitisho , sijue kama unanielewa lakini🤔
 
Back
Top Bottom